Kwa hili alilolifanya Diamond, litamgharimu sana katika safari yake ya kimuziki

Kama ni kweli hata mim itabidi niwapunguze kina suge mcnight,dr dree,2pac nimpatie kanafas kidogo kwenye maktaba yngu ya music kuhusu bongo movie ntaendelea kuangali wakorea period
Kama ni kweli yuko UKAWA basi naahidi kuwa mshabiki wake from today ....
 
Diamond ni ccm acha kuleta habari zako za uongo na kashaanza kumpigia promo makufuli ukawa tuna wananchi wa kuisapoti harakati za kumtoa mkoloni mweusi kaya kwa kaya mtaa kwa mtaa kijiji kwa kijiji na wasanii wa kutosha usitake wanaukawa waanze kumsifia mccm wenu hapa
 

Ccm je? Mme,mke,mtoto- jk,salma,riziwani. Kaka ,mdogo mtu.: jk na membe. Nape na babake.
 
Ccm je? Mme,mke,mtoto- jk,salma,riziwani. Kaka ,mdogo mtu.: jk na membe. Nape na babake.

Kwahiyo hayo mabadiliko mnayohubiri ni yapi ikiwa wote ni wale wale.Tena CHAGGADEMA ni zaidi maana wao wameanzia kwenye chama siku wakishika nchi(God forbid) watu watalia tu......................
 
Kutokana na kushabikia ccm, upendo wangu na ushabiki wangu kwake umepoa kabisa. Nyimbo za diamond zikipigwa huwa nazima kama ni radio au tv, na kama niko na serebuka basi narudi kukaa kwenye kiti changu. ..Fafulukti!
 

Hivi jamani mbona nyinyi mnakuwa wanafiki sana? Diamond pia ana haki kama yako. Uchaguzi huja na kupita. Nani kakwambia wapenzi wa Sugu au Prof. J ni wa UKAWA tu? Kwa taarifa yako mimi hawa jamaa waili nawazimia pamoja nakuwa siko UKAWA. Mbona hukusema haya kwa Flora Mbasha ambaye ametoa album ya Lowasa? Mbona hamsemi kuhusu juma nature? Acha kuwa na mawazo mgando kisa tu Diamond yuko kwa magufuli. Acha unafiki wewe. Angemsupport lowasa haya maneno ungesema? Wakati mwingine kuweni na busara kidogo. Upenzi kama wako unakua kama ukoma sasa.
 


Naheshimu mawazo yako lakini huna point kabisa. Wewe unaleta mapenzi yako ya UKAWA kwenye profession za watu. Kitu kikubwa Diamond anachotafuta sasa hivi ni HELA na sio TUNZO. Simaanishi kuwa TUNZO si muhimu lakini kwa sasa ni fedha kwanza.
 

big up mkuu umeongea kweli tupu na nimependa vile umeonesha ukomavu kwenye mambo nyeti ya kitaifa bila kua mnafki. Tanzania tunahitaji kila mtu afikiri hivi kwani maendeleo yatakuja pale ambapo viongozi watajua wananchi hawataki upumbavu.
Kwa upande wa diamond yeye kakosea kwani sio kila kitu kinafaa kutumia fursa vitu vingine inabidi awaze maslahi ya taifa lake kwa ujumla kwani hiyo ita determine kipindi chote cha miaka 5 au 10 iwapo atashabikia kitu anbacho najua ata yeye roho inamsuta CCM haina sababu yoyote ya kuendelea kuwepo madarakani labda watakaoisupport ni wale wanayonufaika nayo ni one way or another.
Nikiwa pia ni team diamond naomba niseme hajafanya vizuri na yeye anajua kitu alichofanya ni kurudisha fadhila kwa kikwete alivyokua anamwita ikulu basi nae kaamua kumsupport magufuli ila kama binadamu kakosea basi tumkosoe na tuendelee kumsuppport najua ni hasira tu ila badae utakua sawa na tuendelee kumsupport msanii wetu.
ASANTE
 
Last edited by a moderator:
Kutokana na kushabikia ccm, upendo wangu na ushabiki wangu kwake umepoa kabisa. Nyimbo za diamond zikipigwa huwa nazima kama ni radio au tv, na kama niko na serebuka basi narudi kukaa kwenye kiti changu. ..Fafulukti!

Mwambieni na Mbowe aache kupiga nyimbo zake pale kwenye lile danguro lake BILICANUS,Na hilo danguro litakuwa linatoa huduma kwa CHAGGADEMA TU.....................
 
Nafikiri hakupata nafasi ya kuzungumza na Marow na mkewe besta
 
Kwahiyo hayo mabadiliko mnayohubiri ni yapi ikiwa wote ni wale wale.Tena CHAGGADEMA ni zaidi maana wao wameanzia kwenye chama siku wakishika nchi(God forbid) watu watalia tu......................

List ya wabunge viti maalumu UVCCM mwaka 2015:
1.Halima Bulembo -Mtoto wa Mwenyekiti Jumuia ya Wazazi Abdalah Bulembo
2.Zainab Katimba -Mtoto wa Maimuna Tarishi aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa wizara mbalimbali mbali
3,Juliana Masaburi-Mtoto wa Meya wa Jiji la Dar Masaburi Didas
4.Mariamu Ditopile-Mtoto wa aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM wilaya ya Sengerema Ditopile Mzuzuri aliyeua Dereve wa daladala
5.Maria Kangole-Mtoto wa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha Onesmo Kongole
6.Sophia Kizigo Mtoto wa Naibu katibu Mkuu UVCCM Taifa Bwana Mafume Kizigo
7.Jaquiline Mzindakya-Mtoto wa Chrisant Mzindakaya ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa jimbo la Kwale.
8.Margaret Sitt-Mke wa Samwel Sitta(Mbunge viti maalum 2010-2015)
9.Kawawa,Sokoine, (Watoto wa Mfaume KAwawa na Sokoine Moringe Marehemu)-Ubunge viti maalum2010-2015

Niambie kama CCM ina moroal authority ya kuwanyooshea vidole upinzani.

Kabla hujatoa kibanzi kwenye jicho la mwenzako toa kwanza BORITI kwenye jicho lako.

Siku njema.....
 

Uchambuzi murua kabisa huu,
Unatakiwa ujue Watanzania wamechoka na ccm kwa mambo kama haya, ndio maana wanataka kuona mbadala wa ccm ambae hatafanana na ccm kwa lolote,
Kama upinzani umeona haya kwa ccm na wao wanarudia na kupita njia ile ile ya ccm, kuna sababu ya kuwa na upinzani nchini?
 
Mkuu sijui kama utaeleweka hapa...........................
 
Mwambieni na Mbowe aache kupiga nyimbo zake pale kwenye lile danguro lake BILICANUS,Na hilo danguro litakuwa linatoa huduma kwa CHAGGADEMA TU.....................


Hivi kwani hapa tunamzungumzia mbowe?

Nimesema sisikilizi nyimbo za diamond, sababu diamond ni mtu wa kutengeneza siyo msanii mwenye kuheshimu taaluma na kipaji yake.
 
Hivi kwani hapa tunamzungumzia mbowe?

Nimesema sisikilizi nyimbo za diamond, sababu diamond ni mtu wa kutengeneza siyo msanii mwenye kuheshimu taaluma na kipaji yake.

kwasababu haamini chama na mtu unayemtaka wewe au??
 
WACHA NA MIE NIONEKANE KUWA NINA AKILI NDOGO NA FUPI NAMSAPOT DAI KWA ASILIMIA ZOTE. NI MAISHA YAKE NJE YA MUZIKI NA ANAUHURU HUO#Team magufuli forever
 

Mr.Hero,inategemea na njia halisi upinzani hasa kwa Tanzania ulivyoanza.Tujiulize sote ulianza kwa kasi?Ulipokelewaje na wanachama,wananchi,viongozi wa chama Tawala,serikali,polisi,jeshi na wanachi wa kawaida?

Je hatukuaminishwa kwamba upinzani ni uadui,upinzani utaleta vita,upinzani una ukabila,udini nk nk.Tuone vyama vilivyokuwa vikuu kabisa CUF,NCCR mageuzi vilikufaje hivi?Tena vikiwa kwenye PEAK.

Ilikuwa siyo rahisi kwa watanzania wakawaida kukubaliana na vyama vya upinzani,mikoa michache ya mipakani ndiyo ilikuwa ya kwanza kupokea upinzani labda sababu ya mazingira yaliyokuwepo.Na kwa sababu hiyo waliokubali kuingia kwenye harakati za upinzani ni Ndugu wa waliokubali kwa uharaka upinzani napo ilikuwa shughuli kuwabadilisha,familia na marafiki wa karibu.Hivyo kwangu mimi sioni kama tunatakiwa kuwalaumu kwa jinsi ya mengi hawa waliyoyapitia,na ndiyo maana wengi walipewa vyeo ili hasa kuviweka vyama kushikamana.

Wengi waliona CUF na NCCR zilivyokufa hivyo kuhofia hasa haya ya kununuliwa na chama tawala ndipo vyama hivi vilipokuwa na imani kwa wale wa karibu ambao wanaweza kuwa-control.hata JKN alivyoamua kuingia kwenye siasa nina uhakika alianza na waliokaribu naye hasa na aliowaamini.

Na ninachokifikiria baada ya miaka hii ishirini vyama hivi vitajitoa katika kuwapokea ndugu wa karibu na kuwaingiza wengine na kuwaaminisha kama wanaaminika.Nina imani hiyo.Lakini leo miaka 54 CCM imekuwa na tatizo lile lile la kubeba ndugu wa viongozi,kuwarithisha uongozi na kuwaacha watoto wasiyo na careoff kugwaya mtaani,kushindwa hata kuingia kwenye siasa.

Nadhani ningeiona CCM imeamua kubadilika kama haya majina ya watoto wa fulani yangepungua zaidi mwaka huu ili kuwaonyesha watu wanabadilika.

Picha ya watoto wa watawala kuwa ndiyo wenyewe kuingia kwenye SIASA kunanipa hofu kuu kwamba sasa serikali inatengeneza TABAKA LA WATAWALA na ndiyo maana tunasikia kila aina ya sauti.Kama CDM ingekuwa chama TAWALA na kama kina nia ya kuwa CHAMA tawala sitasita kukisema waziwazi kuondoa ile dhana ya WATAWALA wawe ndiyo wale wale na familia zao.

Leo Didas Masaburi anagombea Ubunge Ubungo tuseme anapata,BUNGENI tuna BABA na MTOTO ni wabunge ile hali ya NDIYOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO hata kwa sera mbovu hazitaisha.Ila kama assessment ikafanyika akapita mtu kwa quality na siyo kwa pesa yake au kuwa mtoto wa fulani nina uhakika tutajenga bunge lenye confidence kwa watawala.Lakini RUSHWA ni RUSHWA imekaa katika kutoa HONGO ya MWILI,PESA au UNDUGU wa mtu anayegombea.
Leo watoto zaidi ya kumi wanaingia kwa viti maalum au kugombea tunatengeneza UTAWALA wa kifalme taratibu huku tukijua lakini ndani ya CCM wenyewe wanachama mnashindwa kukemea sababu ya uwoga.

Watoto wa MKULIMA hawawezi kuwa watawala wala viongozi sababu ya ELIMU DUNI wanayopewa kwenye shule za kata aka St.KAYUMBA,na hili la kuua ELIMU liko very strategically ili kuendelea kuhodhi madaraka.

Watanzania tulikemee kote siyo tu CCM vyama vyote sasa tuseme basi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…