Kwa hili la Inyala, Mbeya ninampinga Makamu wa Rais Dr. Mpango kwa agizo lake "quick fix" na kumsihi awe serious na maisha ya Watanzania

Kwa hili la Inyala, Mbeya ninampinga Makamu wa Rais Dr. Mpango kwa agizo lake "quick fix" na kumsihi awe serious na maisha ya Watanzania

Unalionaje agizo la Dr. Mpango?

  • Zuri linafaa sana

    Votes: 4 21.1%
  • Halifai kabisa

    Votes: 15 78.9%

  • Total voters
    19
Ila kweli kile kipande anzia ile barabara ya MPYA kutoka makambako inapoishia ni kibaya Sana na mbaya barabara ni ndogo Sana,

Labda KWa mda kuanzishwe utaratibu Kama ule wa pale kwenye mlima wa kushuka Mbalizi, magari yasubiliane KWa nusu saa Kama wafanyavyo pale
Kwa intervention ya mda ndicho wanafanya kwamba magari yanasubiriana hata sasa lakini pia wameambiwa wafanye ukaguzi wa brake za malori kabla ya kushuka ila haieleweki kama Polisi walikagua brake au laa maana tatizo la kufeli brake lilijirudia..

VP alichosema na ambacho ni plan ya mda ya TanRoads ni ku divert malori kwenye njia nyingine Wakati wanajiandaa na kujenga hiyo barabara yote ikiwemo bypass..
 
Miundombinu Inaruhusu kujihami? Unajihami vp kwenye single carriage road kwenye mteremko? Gari nyingine ikifeli break na kuja kwako unaenda wapi? Unapajua Inyala au?

Common sense isn't common hakika
Asante Mkuu, tumeliongelea sana humu swala la kuwa na 'Runaway trucks Ramp.
Malori Duniani kote huwa yanafeli breki kwenye miteremko mikali au mirefu.
 
Inasikitisha sana jinsi tusivyoweza kuwa na majawabu sahihi huku kuna lundo la Wataalamu
Chadomo mna matatizo Sana aisee,yaani zaidi ya kuropoka sidhani kama hata mnafuatiliaga hata mipango ya Serikali zaidi kukurupuka..

Hiyo barabara inaanza kujengwa yote kutoka Igawa hadi Tunduma kuwa njia 4 na inaanza mwaka huu sio hadithi ila wanaanza kwa vipande kama Uyole hadi Airport na Mlowo hadi Tunduma..

Interventions aliyoagiza VP ni ya mda na nzuri tuu,wakishachepusha malori njia yake hakuna ajali utasikia hapo..
 
Katika taarifa yake kuhusu ajali ya pale Inyala Mkoani Mbeya iliyoua watu kadhaa pamoja na DED wa Igunga, Gazeti la Mwananchi limetoa taarifa kwamba ajali hiyo imetokea ikiwa ni siku tatu zimepita baada ya Makamu wa Rais Dkt. Mpango kutoa maagizo kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kuanza ukaguzi wa magari ya mizigo katika eneo hili.

Sasa nashindwa kuelewa busara ya Makamu wetu wa Rais kwamba suluhisho la kuzuia ajali pale Inyala ni kuyakagua magari ya mizigo kabla hayajapita kile kipande cha barabara. Hili nalipinga kwa dhati. Nimeshindwa na hata kuchukizwa na jinsi watu walio na madaraka nchini kama Dkt. Mpango wanavyoyachukulia mambo mazito kirahisi namna hivi.

Hili ni eneo ambalo karibu kila wiki panatokea ajali mbaya sana, na Dkt. Mpango anasema kagueni magari kabla hayajapita hapa. Hii ni busara kweli?

Anapaswa kuelewa nini kinasababisha ajali pale kabla ya kutoa kile tunaita utatuzi wa kisiasa kwa tatizo la kisayansi.

Kwa kumsaidia tu na kumpa ushauri wa bure usio wa kisiasa, ni kwamba kuna sababu kubwa tatu zinazosababisha ajali pale;
  1. Barabara imeharibika sana na kuweka matuta ya lami kudidimia ambayo mara nyingi yanakulazimu kupita upande usio wako wa barabara au kupoteza control ya gari unapopanda tuta kwa sababu gari zinayumba sana kwenye haya matuta
  2. Hiyo sehemu ina mlima/mteremko wa umbali mrefu
  3. Hiyo sehemu ni ya solid line ambayo huwezi ku-overtake gari nyingine (japo madereva wa mabasi hawajali hili)
Sasa Dkt. Mpango anapaswa kutoa wazo la kuzuia ajali pale kwa kuangalia hizo sababu tatu. Na kwa mawazo tu, haya yanapaswa kufikiriwa na Serikali ili kuzuia vifo na ajali za kila wakati eneo hili;
  1. TANROAD waamrishwe kutengeneza hili eneo haraka sana. Matengenezo yanayotakiwa hapa ni kama yale yaliyofanyika mteremko wa Kitonga katika kuzuia barabara kuweka matuta kutokana na uzito wa malori.
  2. Kwa kuwa hili ni eneo la mlima/mteremko wa umbali mrefu, pawekwe climbing lane ili kuwepo na njia tatu na ambayo moja itatumiwa zaidi na malori yanayopanda taratibu sana eneo hili
  3. Zaidi ya kuweka climbing lanes, eneo hili liwekwe "lay-by" kadhaa (yaani michepuko katika barabara iliyo kama sehemu ya kituo cha basi) ili madereva wanaopanda au kuteremka wawe na eneo la kuingia pale wanapoona gari lao linaanza kuleta matatizo na kulifanyia marekebisho, badala ya kusimamisha lori barabarani eneo la hatari.
Mwisho, ninawaomba sana viongozi wetu jaribuni kuwa serious na matatizo yanayowakabili Wananchi, hasa yale yanayosababisha vifo. Msitangulize kukimbia gharama za kutatua matatizo kama haya na kupendekeza majibu ya kisiasa ambayo hayatatusaidia. Kama tatizo ni fedha, tunakatwa sana tozo, tumieni hizo pale Inyala kama suala la emergency.

Safi kabisa, umenena vyema , hizo ndo solution zinatakiwa kuletwa na viongozi wetu!! Siyo solution rahisi rahisi tu, inasikitisha sana,,
 
Katika taarifa yake kuhusu ajali ya pale Inyala Mkoani Mbeya iliyoua watu kadhaa pamoja na DED wa Igunga, Gazeti la Mwananchi limetoa taarifa kwamba ajali hiyo imetokea ikiwa ni siku tatu zimepita baada ya Makamu wa Rais Dkt. Mpango kutoa maagizo kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kuanza ukaguzi wa magari ya mizigo katika eneo hili.

Sasa nashindwa kuelewa busara ya Makamu wetu wa Rais kwamba suluhisho la kuzuia ajali pale Inyala ni kuyakagua magari ya mizigo kabla hayajapita kile kipande cha barabara. Hili nalipinga kwa dhati. Nimeshindwa na hata kuchukizwa na jinsi watu walio na madaraka nchini kama Dkt. Mpango wanavyoyachukulia mambo mazito kirahisi namna hivi.

Hili ni eneo ambalo karibu kila wiki panatokea ajali mbaya sana, na Dkt. Mpango anasema kagueni magari kabla hayajapita hapa. Hii ni busara kweli?

Anapaswa kuelewa nini kinasababisha ajali pale kabla ya kutoa kile tunaita utatuzi wa kisiasa kwa tatizo la kisayansi.

Kwa kumsaidia tu na kumpa ushauri wa bure usio wa kisiasa, ni kwamba kuna sababu kubwa tatu zinazosababisha ajali pale;
  1. Barabara imeharibika sana na kuweka matuta ya lami kudidimia ambayo mara nyingi yanakulazimu kupita upande usio wako wa barabara au kupoteza control ya gari unapopanda tuta kwa sababu gari zinayumba sana kwenye haya matuta
  2. Hiyo sehemu ina mlima/mteremko wa umbali mrefu
  3. Hiyo sehemu ni ya solid line ambayo huwezi ku-overtake gari nyingine (japo madereva wa mabasi hawajali hili)
Sasa Dkt. Mpango anapaswa kutoa wazo la kuzuia ajali pale kwa kuangalia hizo sababu tatu. Na kwa mawazo tu, haya yanapaswa kufikiriwa na Serikali ili kuzuia vifo na ajali za kila wakati eneo hili;
  1. TANROAD waamrishwe kutengeneza hili eneo haraka sana. Matengenezo yanayotakiwa hapa ni kama yale yaliyofanyika mteremko wa Kitonga katika kuzuia barabara kuweka matuta kutokana na uzito wa malori.
  2. Kwa kuwa hili ni eneo la mlima/mteremko wa umbali mrefu, pawekwe climbing lane ili kuwepo na njia tatu na ambayo moja itatumiwa zaidi na malori yanayopanda taratibu sana eneo hili
  3. Zaidi ya kuweka climbing lanes, eneo hili liwekwe "lay-by" kadhaa (yaani michepuko katika barabara iliyo kama sehemu ya kituo cha basi) ili madereva wanaopanda au kuteremka wawe na eneo la kuingia pale wanapoona gari lao linaanza kuleta matatizo na kulifanyia marekebisho, badala ya kusimamisha lori barabarani eneo la hatari.
Mwisho, ninawaomba sana viongozi wetu jaribuni kuwa serious na matatizo yanayowakabili Wananchi, hasa yale yanayosababisha vifo. Msitangulize kukimbia gharama za kutatua matatizo kama haya na kupendekeza majibu ya kisiasa ambayo hayatatusaidia. Kama tatizo ni fedha, tunakatwa sana tozo, tumieni hizo pale Inyala kama suala la emergency.
Pole ndugu afadhali umesema sasa haya matatu uliyoweka hapo yanafanya sasa gari kubwa kutumia brake nyingi ambazo zinamaliza reserve ya upepo katika mitungi matokeo yake ni kufail brake. Hawa wanasiasa na polisi likitokea janga wao cha kwanza kutengeneza mazingira ya wao sio chanzo cha ajari na hawahusiki.

Kuna mjinga mmoja anaweka foleni ya malory yafatane matokeo yake kwakuwa hayana mwendo na distance kati ya lorry na lorry ni ndogo yana mwaga upepo tu ngoma likifika down halina brake. Sie wananzengo tulifikiri wangeshauri trucks ziongeze ukubwa wa mitungi ya upepo, b. yake malorry yasiwekwe katika foleni na mwisho barabara iwe na parking anayemaliza upepo aingie kushoto kujaza upepo.

Yaani polisi wanasingizia marehemu wa watu bure wakati bado ajari zinazuilika, wenye mamlaka waache politike watimize wajibu wao sio majibu mepesi kila kukicha.
 
Marlezo yote haya ni hofu ya ukaguzi kwani mnabeba vitu gani?

Ukaguzi kwa weledi upi? Wa hawa ndugu?

IMG_20220915_083641_830.jpg


Kama ni hao apongezwe Mh. Kinana kwa kuwatolea uvivu.
 
Chadomo mna matatizo Sana aisee,yaani zaidi ya kuropoka sidhani kama hata mnafuatiliaga hata mipango ya Serikali zaidi kukurupuka..

Hiyo barabara inaanza kujengwa yote kutoka Igawa hadi Tunduma kuwa njia 4 na inaanza mwaka huu sio hadithi ila wanaanza kwa vipande kama Uyole hadi Airport na Mlowo hadi Tunduma..

Interventions aliyoagiza VP ni ya mda na nzuri tuu,wakishachepusha malori njia yake hakuna ajali utasikia hapo..
Si wangeanzia hapo kwenye shida na mauaji ya kila siku
 
Pole ndugu afadhali umesema sasa haya matatu uliyoweka hapo yanafanya sasa gari kubwa kutumia brake nyingi ambazo zinamaliza reserve ya upepo katika mitungi matokeo yake ni kufail brake. Hawa wanasiasa na polisi likitokea janga wao cha kwanza kutengeneza mazingira ya wao sio chanzo cha ajari na hawahusiki.

Kuna mjinga mmoja anaweka foleni ya malory yafatane matokeo yake kwakuwa hayana mwendo na distance kati ya lorry na lorry ni ndogo yana mwaga upepo tu ngoma likifika down halina brake. Sie wananzengo tulifikiri wangeshauri trucks ziongeze ukubwa wa mitungi ya upepo, b. yake malorry yasiwekwe katika foleni na mwisho barabara iwe na parking anayemaliza upepo aingie kushoto kujaza upepo.

Yaani polisi wanasingizia marehemu wa watu bure wakati bado ajari zinazuilika, wenye mamlaka waache politike watimize wajibu wao sio majibu mepesi kila kukicha.

Barabara ya kudumu iliyo katika matumizi, tangu lini kuwa operated kama single lane?

Single lane isiyokuwa katika matengenezo inaingia je akilini?

Barabara yenye mteremko mrefu, kulikoni kukosekana parking in between? Kulikoni kukosekana climbing lane?
 
Iko hivi hilo eneo ajali asilimia zaidi ya 90% husababishwa na ma lories ambayo huwa Yana fail brake! Moja ya kudhibiti ajali ni kuangalia brakes kama ziko sawa! Pia njia ziwe angalau tatu au nne ! Lkn bado swala la brake ni muhimu mno! Yaani unapopita hapo lazima uwe makini na rear view na mbele na uwe unatoa maamuzi ya haraka mno!
 
Si wangeanzia hapo kwenye shida na mauaji ya kila siku
Kwa hapo sijajua ila wamekuja na hiyo intervention ya ku divert malori..

Shida ziko Hapo mteremko wa Inyala na Mlima Mbalizi,hii njia ya kusubiria imefanya Kazi kule Mbalizi huku Inyala inaonekana mlima ni mrefu zaidi ndio maana wameamua kufanya diversion ya trucks..
 
Katika taarifa yake kuhusu ajali ya pale Inyala Mkoani Mbeya iliyoua watu kadhaa pamoja na DED wa Igunga, Gazeti la Mwananchi limetoa taarifa kwamba ajali hiyo imetokea ikiwa ni siku tatu zimepita baada ya Makamu wa Rais Dkt. Mpango kutoa maagizo kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kuanza ukaguzi wa magari ya mizigo katika eneo hili.

Sasa nashindwa kuelewa busara ya Makamu wetu wa Rais kwamba suluhisho la kuzuia ajali pale Inyala ni kuyakagua magari ya mizigo kabla hayajapita kile kipande cha barabara. Hili nalipinga kwa dhati. Nimeshindwa na hata kuchukizwa na jinsi watu walio na madaraka nchini kama Dkt. Mpango wanavyoyachukulia mambo mazito kirahisi namna hivi.

Hili ni eneo ambalo karibu kila wiki panatokea ajali mbaya sana, na Dkt. Mpango anasema kagueni magari kabla hayajapita hapa. Hii ni busara kweli?

Anapaswa kuelewa nini kinasababisha ajali pale kabla ya kutoa kile tunaita utatuzi wa kisiasa kwa tatizo la kisayansi.

Kwa kumsaidia tu na kumpa ushauri wa bure usio wa kisiasa, ni kwamba kuna sababu kubwa tatu zinazosababisha ajali pale;
  1. Barabara imeharibika sana na kuweka matuta ya lami kudidimia ambayo mara nyingi yanakulazimu kupita upande usio wako wa barabara au kupoteza control ya gari unapopanda tuta kwa sababu gari zinayumba sana kwenye haya matuta
  2. Hiyo sehemu ina mlima/mteremko wa umbali mrefu
  3. Hiyo sehemu ni ya solid line ambayo huwezi ku-overtake gari nyingine (japo madereva wa mabasi hawajali hili)
Sasa Dkt. Mpango anapaswa kutoa wazo la kuzuia ajali pale kwa kuangalia hizo sababu tatu. Na kwa mawazo tu, haya yanapaswa kufikiriwa na Serikali ili kuzuia vifo na ajali za kila wakati eneo hili;
  1. TANROAD waamrishwe kutengeneza hili eneo haraka sana. Matengenezo yanayotakiwa hapa ni kama yale yaliyofanyika mteremko wa Kitonga katika kuzuia barabara kuweka matuta kutokana na uzito wa malori.
  2. Kwa kuwa hili ni eneo la mlima/mteremko wa umbali mrefu, pawekwe climbing lane ili kuwepo na njia tatu na ambayo moja itatumiwa zaidi na malori yanayopanda taratibu sana eneo hili
  3. Zaidi ya kuweka climbing lanes, eneo hili liwekwe "lay-by" kadhaa (yaani michepuko katika barabara iliyo kama sehemu ya kituo cha basi) ili madereva wanaopanda au kuteremka wawe na eneo la kuingia pale wanapoona gari lao linaanza kuleta matatizo na kulifanyia marekebisho, badala ya kusimamisha lori barabarani eneo la hatari.
Mwisho, ninawaomba sana viongozi wetu jaribuni kuwa serious na matatizo yanayowakabili Wananchi, hasa yale yanayosababisha vifo. Msitangulize kukimbia gharama za kutatua matatizo kama haya na kupendekeza majibu ya kisiasa ambayo hayatatusaidia. Kama tatizo ni fedha, tunakatwa sana tozo, tumieni hizo pale Inyala kama suala la emergency.
Mkuu toka miaka ya Magufuli akiwa Wazirii wa Ujenzi na Rais, serikali imenyanyapaa barabara za mkoa wa Mbeya kwa kiwango kikubwa.
Matokeo ya dhambi hii sasa imeanza kuwala hata viongozi.
 
Ila kweli kile kipande anzia ile barabara ya MPYA kutoka makambako inapoishia ni kibaya Sana na mbaya barabara ni ndogo Sana,

Labda KWa mda kuanzishwe utaratibu Kama ule wa pale kwenye mlima wa kushuka Mbalizi, magari yasubiliane KWa nusu saa Kama wafanyavyo pale
Utaratibu kama wa Mbalizi upo pale Inyala.
Hawa wakubwa waliooata ajali walisimamishwa wakakaidi.
Wameyapata ya kuwapata.
Lakini kimsingi barabara ni mbaya mbaya mbaya mno kipande chote toka Igawa hadi Tunduma.
Serikali iko kimya kama haioni.
Wananchi wamekufa wengi hadi tumechoka kulia.
Sasa tusubiri viongozi waendelee kufa kwa wingi ili suala lieleweke.
 
Nimeona taarifa ya Mkuu wa Mkoa Mbeya, Homera, akisema DED na dereva wake waliambiwa na polisi wa usalama barabarani wasubiri kwanza, wao wakalazimisha kwenda wakisema walikuwa na haraka.

Naona hiyo haraka yao ndio iliyosababisha mwendo kasi ulioleta ile ajali, ndio maana ile gari ya DED imechakaa vibaya sana. Hawa viongozi wa serikali waache kutumia vyeo vyao kulazimisha mambo hadi kwenda kinyume na taratibu, wataisha.
Na wataisha kwelikweli haya mambo hayahitaji ujuaji...
Lakini apumzike kwa Amani.
 
wapumbavu tupo wengi sana aisee.

Yaani miaka yoooote tunapambana na vitu vidogo vidogo saaana, WaAfrica tuna matatizo lakini watanzania tuna matatizo zaidi.

Viongozi wanamatatizo, wananchi wanamatatizo, CHANZO KIKUU NI POOR BASIC EDUCATION KWA WATU WOOOOTE.
Unakwepa ukweli wa mambo.
Magufuli PhD, alijenga flyover hata ziwani L. Victoria , mbadala wa kivuko cha Busisi.
Hapo ni upendeleo kwa sehemu fulani na chuki kwa sehemu nyingine.
 
Ai
Utaratibu kama wa Mbalizi upo pale Inyala.
Hawa wakubwa waliooata ajali walisimamishwa wakakaidi.
Wameyapata ya kuwapata.
Lakini kimsingi barabara ni mbaya mbaya mbaya mno kipande chote toka Igawa hadi Tunduma.
Serikali iko kimya kama haioni.
Wananchi wamekufa wengi hadi tumechoka kulia.
Sasa tusubiri viongozi waendelee kufa kwa wingi ili suala lieleweke.
Aisee kumbe, tatizo nao wakisha KUWA kwenye v8 Basi mazalau Kama yote wanaboaga sana
 
Kwa intervention ya mda ndicho wanafanya kwamba magari yanasubiriana hata sasa lakini pia wameambiwa wafanye ukaguzi wa brake za malori kabla ya kushuka ila haieleweki kama Polisi walikagua brake au laa maana tatizo la kufeli brake lilijirudia..

VP alichosema na ambacho ni plan ya mda ya TanRoads ni ku divert malori kwenye njia nyingine Wakati wanajiandaa na kujenga hiyo barabara yote ikiwemo bypass..
Sawa ila Kuna member hapo juu anasema walisimamishwa wakakaidi ,so ni vyema pia watu kutii SHERIA , unasimamishwa hutaki kisa ni mtu flani,sio sawa
 
Back
Top Bottom