Mwadilifu Mdhulumiwa
JF-Expert Member
- Jul 22, 2021
- 419
- 640
Siku ya jana Jumatatu April01, 2024, baadhi ya vyombo vya habari nchini Tanzania vimeripoti vikiwakariri baadhi ya viongozi wa serikali wakitoa taarifa ya kugharamia safari ya mashabiki wa club ya Yanga kwenda na kurudi nchini Afrika kusini ili kwenda kuishangilia timu hiyo itakapoumana na timu ya Mamelody Sundowns ya huko Afika ya kusini katika mchezo wa mkondo wa pili wa robo fainali ya ligi ya mabinwa Afrika unaotarajiwa kupigwa siku ya tarehe 5, April , mwaka huu.
Hapana shaka kitendo hiki cha serikali ni cha kupongeza, kwani kinaunga mkono maendeleo ya michezo na vilabu nchini.
Hata hivyo serikali ilipaswa kutafakari kwa kina kama kweli Yanga walistahili kupewa huo msaada!....Unatoaje msaada kwa mtu ambaye anaweza kufanya kazi na kutengeneza fedha kwa jasho lake lakini kaamua kutoa huduma bure alafu gharama zinapomfika anakuwa ombaomba?
Kwa ukubwa, msisimko na mvuto wa ile mechi kati ya Yanga na Mamelody ni Dhahiri hapakuwa na sababu ya kuweka kiingilio bure na Yanga ingeweza kutengeneza pesa ndefu ambayo leo hii ndio wangeitumia kugharamia hizo gharama badala ya kwenda kuomba msaada wa serikali.
Ni ajabu Serikali kila siku inazihamasisha taasisi zake kuweka mkazo kwenye kukusanya mapato na kuna viongozi wengi tu wametumbuliwa ama kwa kuzembea kukusanya mapato au kutumia vibaya fedha za makusanyo ya mapato, alafua leo hii serikali hiyohiyo inakuja kumgharamia mtu ambaye anaachia mapato yanapotea kizembe wakati angeweza kuyakusanya kirahisi kabisa kuna miradi kibao ya wananchi imekwama kwa kukosa fedha za kuiendesha.
Sikatai serikali kusaidia kugharamia michezo , hapana lakini kwa hili la Yanga kuna kitu hakipo sawa, sababu mechi hiyo ya mkondo wa pili sio ya kushtukiza, bali tangu mwanzo Yanga walifahamu fika kuwa baada ya mechi ya mkondo wa kwanza watakuwa na mechi nyingine ya mkondo wa pili hivyo walipaswa kuweka mkakati wa kukusanya fedha ili kuwezesha hilo.
Tena walikuwa na nafasi kubwa kabisa ya kulifanikisha hilo sababu kampeni yao ya uhamasishaji wa mashabiki kuja uwanjani ilifanikiwa vya kutosha, ajabu kumbe walikuwa wakitangaza kutoa huduma bure huku upande mwingine wanawaza kwenda kuikamua serikali!
Nihitimishe kwa kusema serikali ifanye tafakari upya, hapa itajibebesha mzigo wa gharama usiokuwa na sababu kwa uzembe wa watu wachache. Fedha hizo kama kweli serikali itazitoa basi tukubali tuna tatizo katika menejiment ya fedha za umma tunazozipata na hii ni mojawapo ya sababu zitakazotufanya tuendelee kukopa huko mataifa ya Magharibi mpaka mwisho wa dunia hii.
Hapana shaka kitendo hiki cha serikali ni cha kupongeza, kwani kinaunga mkono maendeleo ya michezo na vilabu nchini.
Hata hivyo serikali ilipaswa kutafakari kwa kina kama kweli Yanga walistahili kupewa huo msaada!....Unatoaje msaada kwa mtu ambaye anaweza kufanya kazi na kutengeneza fedha kwa jasho lake lakini kaamua kutoa huduma bure alafu gharama zinapomfika anakuwa ombaomba?
Kwa ukubwa, msisimko na mvuto wa ile mechi kati ya Yanga na Mamelody ni Dhahiri hapakuwa na sababu ya kuweka kiingilio bure na Yanga ingeweza kutengeneza pesa ndefu ambayo leo hii ndio wangeitumia kugharamia hizo gharama badala ya kwenda kuomba msaada wa serikali.
Ni ajabu Serikali kila siku inazihamasisha taasisi zake kuweka mkazo kwenye kukusanya mapato na kuna viongozi wengi tu wametumbuliwa ama kwa kuzembea kukusanya mapato au kutumia vibaya fedha za makusanyo ya mapato, alafua leo hii serikali hiyohiyo inakuja kumgharamia mtu ambaye anaachia mapato yanapotea kizembe wakati angeweza kuyakusanya kirahisi kabisa kuna miradi kibao ya wananchi imekwama kwa kukosa fedha za kuiendesha.
Sikatai serikali kusaidia kugharamia michezo , hapana lakini kwa hili la Yanga kuna kitu hakipo sawa, sababu mechi hiyo ya mkondo wa pili sio ya kushtukiza, bali tangu mwanzo Yanga walifahamu fika kuwa baada ya mechi ya mkondo wa kwanza watakuwa na mechi nyingine ya mkondo wa pili hivyo walipaswa kuweka mkakati wa kukusanya fedha ili kuwezesha hilo.
Tena walikuwa na nafasi kubwa kabisa ya kulifanikisha hilo sababu kampeni yao ya uhamasishaji wa mashabiki kuja uwanjani ilifanikiwa vya kutosha, ajabu kumbe walikuwa wakitangaza kutoa huduma bure huku upande mwingine wanawaza kwenda kuikamua serikali!
Nihitimishe kwa kusema serikali ifanye tafakari upya, hapa itajibebesha mzigo wa gharama usiokuwa na sababu kwa uzembe wa watu wachache. Fedha hizo kama kweli serikali itazitoa basi tukubali tuna tatizo katika menejiment ya fedha za umma tunazozipata na hii ni mojawapo ya sababu zitakazotufanya tuendelee kukopa huko mataifa ya Magharibi mpaka mwisho wa dunia hii.