Wapinzani argument yao kuu JPM alificha takwimu lakini ukiwauliza JPM hayupo mbona hamtoi hizo takwimu za maelfu hao wanaokufa kwa corona kama kweli wanakufa hawana jibu.Suala la Corona. Mbona hatusikii Takwimu? Waliosema kuchanjwa iwe lazima kwa wote wapo wapi? Suala la kuvaa barakoa? Hata wapinzani hatuvai.
Kipindi kile wakati yupo tulikuwa tumavaa ku prove him wrong. Now hayupo hatuvai. Chanjo zina expire bila watumiaji. Mikusanyiko ipo bila barakoa. Maisha yapo kama alivyotaka. Ajenda ya Covid 19 imesha.
Wamebaki wabunge tu wa Covid 19. Tumwogope Mungu ndugu zanguni. Pamoja na kuwa kwa sisi unafiki ni kama ngozi.... Katika hili tumwogope Mungu. Tuombe msamaha. Magufuli was right 100 asilimia.
Wapo waliokufa kwa Corona kama ambavyo wapo wanaokufa kwa Malaria, Ukimwi, Kifua Kikuu n.k.
But approach yake ilikuwa sahihi kuwa maisha yaendelee. Na hata hatukuona maiti zimetapakaa mitaani kama ambavyo ilitabiriwa na kutakiwa.
Tumeenda pata mikopo kutokana na Corona ambayo imetumika kwenye ujenzi na malupulupu kwa wengine.
Katika mikusanyiko yote hata maofisini watu hawanawi hata mikono achilia mbali kuvaa barakoa, na social distance. Nenda mikusanyiko yote kuanzia daladala, mpirani, masokoni, nyumba za ibada na arusini mbanano ni kama kawa bila hivyo vitu.
JPM alikuwa na atabakia shujaa katika hili la corona dunia nzima ( niliwahi kuandika hili katika uzi siku zilizopita)