BUSHMEN 88
Member
- Sep 3, 2022
- 25
- 31
Habarin wanajukwaa
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada yapata mwezi mmoja na nusu uliopita nilipata ajali ya bodaboda na kuvunjika mguu wa kushoto mara mbili yani mfupa wa nyuma na mbele na daktari niliyeonana baada ya kumuonyesha picha ya mionzi akanishauri ili mguu uweze kukaa sawa ni lazima niwekewe chuma ingawa mimi nilimuomba niweke muogo ukizingatia kipato nilichonacho ni kidogo kulinganisha na bei yakuwekewa chuma.
Basi kulingana na ushauri wa kitabibu ikabidi nikubaliane nae kwamba nitaweka chuma ngoja nikajichange upya baada ya siku mbili kupita nikawa nimepata hiyo pesa na kufanyiwa operesheni.
Cha ajabu baada wiki tatu kufanyiwa operesheni nikawa nakanyagia mguu na wiki ya nne niliweza kutembea vizuri tu nakuweza kuvaa kiatu sasa swali langu linakuja je kuwekewa chuma ni njia salama zaid au ni mwili wa mtu na kinga alizonazo au vyakula ukizingatia wenzangu wengine tuliokuwa nao pamoja bado wapo kitandani na wengine bado awajaanza kukanyagia mguu.
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada yapata mwezi mmoja na nusu uliopita nilipata ajali ya bodaboda na kuvunjika mguu wa kushoto mara mbili yani mfupa wa nyuma na mbele na daktari niliyeonana baada ya kumuonyesha picha ya mionzi akanishauri ili mguu uweze kukaa sawa ni lazima niwekewe chuma ingawa mimi nilimuomba niweke muogo ukizingatia kipato nilichonacho ni kidogo kulinganisha na bei yakuwekewa chuma.
Basi kulingana na ushauri wa kitabibu ikabidi nikubaliane nae kwamba nitaweka chuma ngoja nikajichange upya baada ya siku mbili kupita nikawa nimepata hiyo pesa na kufanyiwa operesheni.
Cha ajabu baada wiki tatu kufanyiwa operesheni nikawa nakanyagia mguu na wiki ya nne niliweza kutembea vizuri tu nakuweza kuvaa kiatu sasa swali langu linakuja je kuwekewa chuma ni njia salama zaid au ni mwili wa mtu na kinga alizonazo au vyakula ukizingatia wenzangu wengine tuliokuwa nao pamoja bado wapo kitandani na wengine bado awajaanza kukanyagia mguu.