Hii wala siifuti, ndio yale ya kuambiwa "Unaulizia makofi polisi" wala haina tofauti kabisa. Watu wanakula kama wanakula na kipofu vile bila kushikana mikono.
Yani ile ya Jakaya ilikuwa Trailer, sahizi ndio movie kamili. Watu wanapiga mafungu kwa billions bila hiyana.
Kama mechi basi refa kalewa chakari hata filimbi hawezi piga. Anaangalia watu wanacheza rafu na kujifungia magoli watakavyo. Mabeki wote wamekaa kwenye benchi la sub wanajipigia mivinyo tu.