Kwa huu ufisadi wa kutisha wa sukari na kushindwa kwa BBT Bashe bado yupo wizarani?

Jamaa kama msomi hupaswi kuwa na hizo mindset za kimasikini, hivi shule uliyonayo ulienda kusoma vitu gani? Nakushauri futa hii comment jamaa
Hii wala siifuti, ndio yale ya kuambiwa "Unaulizia makofi polisi" wala haina tofauti kabisa. Watu wanakula kama wanakula na kipofu vile bila kushikana mikono.
 
Sasa hivi ndio fungulia mbwa
Yani ile ya Jakaya ilikuwa Trailer, sahizi ndio movie kamili. Watu wanapiga mafungu kwa billions bila hiyana.

Kama mechi basi refa kalewa chakari hata filimbi hawezi piga. Anaangalia watu wanacheza rafu na kujifungia magoli watakavyo. Mabeki wote wamekaa kwenye benchi la sub wanajipigia mivinyo tu.
 
Huyu ndio alikuwa akipiga kelele kabla ya kuwa waziri , wanasiasa wote wezi.
 
Ex Spy Kaka ilikuwa ni hili, ama kuna lingine laja?
HIyo kashfa, hakutakiwa kubembelezwa kujiuzulu. Na hela arudishe.

Sukari ina hela hasa hao waagizaji wakubwa. Kuna kipindi nilikuwa nikiwalipa kikazi, nyie hee ni kama madini ila haya matamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…