Pre GE2025 Kwa huu utitiri wa miradi aliyomwaga Rais Samia mkoa wa Mwanza, angekuwa anatokea kanda ya Ziwa wapinzani wangesema anapendelea kwao

Pre GE2025 Kwa huu utitiri wa miradi aliyomwaga Rais Samia mkoa wa Mwanza, angekuwa anatokea kanda ya Ziwa wapinzani wangesema anapendelea kwao

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Vyote ulivyotaja anyway vivuko si JPM alikua analalamikiwa kumpa tenda nyingi songolo au umejisahaulisha. Soko kuu Mwanza ujenzi ushaanza zamani ila umedhoofishwa weee kumbe ndo mmekuja kuunganisha hapa
Una uhakika au umekaririshwa ujinga? Nikupe data?
 
Mkoa wa Mwanza ni Kati ya Mikoa ambayo Rais Samia amewapendelea sana Kwa kuimiminia miradi lukuki tena ya mabilioni Kwa mabilioni.

Miradi hiyo imegawanyika katika mafungu Makuu 3 ambayo ni

1.)Miradi ya Urithi kutoka awamu ya 5,iliyokamilika na inayoendelea.

2.)Miradi Mipya iliyoanza awamu ya 6 iliyokamilika na inayoendelea.

3.)Na miradi ambayo Iko Mbioni kuanza wakati wowote .

Ifuatavyo ni miradi ambayo inatekelezwa na Rais Samia Mkoani Mwanza Kwa Kila kundi.

(a)MIRADI MIPYA
1.Ujenzi wa Barabara za Lami Mitaani mradi wa TACTIC Mwanza CC na Ilemela MC km 32 eg Buhongwa-Igoma

2.Ujenzi wa Soko La Kirumba na Soko la Samaki Mkuyuni Bilioni 25.
4.Ujenzi wa Soko Kuu la Jiji la Mwanza
5.Ujenzi wa Hospitali ya Jiji gorofa 6
7.Ujenzi wa Jengo jipya la Mwanza Airport na kukarabati wa uwanja kuwa wa Kimataifa
8.Ujenzi wa Jengo la Kitega Uchumi la TBA Ghana Kota gorofa 7
9.Ujenzi wa Tawi la Chuo Cha DIT Mwanza
10.Ujenzi wa Tawi la Chuo Kikuu Cha Ardhi Mwanza (Sengerema)
11.Ujenzi wa Barabara za Mitaani chini ya TARURA eg Kisesa-Bujora,kiyungi road nk
12.Ujenzi wa Vyumba vya madarasa na shule Mpya zikiwemo za gorofa eg Kisenga ,Igudija nk katika Wilaya zote.
13.Ujenzi wa Vituo vya Afya, Hospital za Wilaya na ununuzi wa vifaa tiba Wilaya zote za Mwanza.
14.Mradi wa Maji Misungwi
15.Ujenzi wa Barabara ya Hungumalwa-Ngudu-Magu
16.Ujenzi wa Hospitali Mpya ya Rufaa Ukerewe
17.Upanuzi wa Bandari za Mwanza South sanjali na ujenzi wa vivuko vipya.
18.Miradi Ya maji Kila Wilaya chini ya Ruwasa eg Misungwi,Magu nk
19.Ujenzi wa Barabara ya Mabuki-Ngudu
20.Ujenzi wa Barabara ya Mwanza Airport -Kayenze-Nyanguge
21.Ujenzi wa Barabara ya Nansio-Rugezi
22.Ujenzi wa Barabara ya Mwanangwa-Misasi-Salawe-Kahama
23.Ujenzi wa Barabara ya Bukokwa-Nyakalilo

View: https://youtu.be/Aq7AGgVXaxQ?si=fb9L7WED3YEdNVdb

(b)Miradi ya Urithi
1.Ujenzi wa daraja la JPM
2.Ujenzi wa Sgr ya Mwanza-Isaka
3.Ukamilishaji wa Stendi za Nyegezi na Nyamhongolo
4.Ukamilishaji wa mradi wa Maji Butimba
5.Ukamilishaji wa Jengo la OPD Sekou Toure gorofa 6
6.Ukarabati wa Meli kubwa ya MV Mwanza Hapa kazi tuu.

View: https://youtu.be/n97F4rAuoPs?si=tmTMNkcjX_nX7z3r

(c)Miradi ambayo Iko Mbioni kuanza ni
-Upanuzi wa Barabara ya njia 4 kutoka Airport Hadi JPM bridge (lot 1 km 25).
-Ujenzi wa mgodi mkubwa wa Madini ya Dhahabu Nyanzaga
-Upanuzi wa Barabara kuu ya Musoma kuwa njia 4


My Take
Hiyo ni Baadhi tuu ya miradi iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa na Samia huko Mwanza.

Kiufupi Samia ameiheshimisha Mwanza kushinda Shujaa waliyedai Anapendelea Kwao.

Kazi Iendelee.

Nyanya mbovu hakuna mradi wowote aliobuni zaidi ya kurudisha uchifu sawa sawa na maagizo ya wajomba zake wakina bushiri wa oman
 
Mipango Mwanza Campus

View: https://youtu.be/5cp7jMOZR0I?si=QbojUA_kUXDkDX3k
Screenshot_20241017-115721.jpg
 
Kupeleka maendeleo sehemu yoyote kiutawala na kulihitajika si vibaya.Lakini,wanasiasa hawaaminiki.Kuna lengo fiche.Population factor na sympathy ya eneo hilo vinahitajika kwa matumizi mema ya baaden.Hakuna mjinga hapo.Ni win-win situation,basi!
 
Leo nawapa Wananchi uhalisia wa Mwanza
Wee CHAWA unajitahidi kufanya kazi uliyotumwa kisayansi zaidi, maana unaweka na vielelezo kabisa, ingawa vingi ni vya mchongo!!

Angalau malipo wanayokupa unayatendea haki.

Umewazidi wale machawa wachovu wa maneno matupu ya uongo akina Tlaatlaah Lucas Mwashambwa, nk
 
Wee CHAWA unajitahidi kufanya kazi uliyotumwa kisayansi zaidi, maana unaweka na vielelezo kabisa, ingawa vingi ni vya mchongo!!

Angalau malipo wanayokupa unayatendea haki.

Umewazidi wale machawa wachovu wa maneno matupu akina Tlaatlaah Lucas Mwashambwa, nk
Wewe bwege Mimi sio chawa.

Huwa sifanyi vitu Kwa stori za vijiweni Bali Kwa weledi, takwimu na facts.
 
Dodoma ni Capital City Kila kitu kinajieleza ukienda pale.

Leo nawapa Wananchi uhalisia wa Mwanza inavyopigwa mbeleko na Serikali ya Samia kushinda waliotangulia.
Usingeizungumzia Dodoma hivyo....
Ningefuta comment yangu😄
 
Back
Top Bottom