Pre GE2025 Kwa huu utitiri wa miradi aliyomwaga Rais Samia mkoa wa Mwanza, angekuwa anatokea kanda ya Ziwa wapinzani wangesema anapendelea kwao

Pre GE2025 Kwa huu utitiri wa miradi aliyomwaga Rais Samia mkoa wa Mwanza, angekuwa anatokea kanda ya Ziwa wapinzani wangesema anapendelea kwao

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

View: https://youtu.be/SuywoRmoCoM?feature=shared
20250310_214343.jpg
 
Hii barabara ya Mwanangwa-Misasi-Salawe-Solwa-Kahama (150Km) imefikia wapi kwa mwenye infos.
 
Mkoa wa Mwanza ni Kati ya Mikoa ambayo Rais Samia amewapendelea sana Kwa kuimiminia miradi lukuki tena ya mabilioni Kwa mabilioni.

Miradi hiyo imegawanyika katika mafungu Makuu 3 ambayo ni

a)Miradi ya Urithi kutoka awamu ya 5,iliyokamilika na inayoendelea.

b)Miradi Mipya iliyoanza awamu ya 6 iliyokamilika na inayoendelea.

c)Na miradi ambayo Iko Mbioni kuanza wakati wowote .

Ifuatavyo ni miradi ambayo inatekelezwa na Rais Samia Mkoani Mwanza Kwa Kila kundi.

(a)MIRADI MIPYA
1.Ujenzi wa Barabara za Lami Mitaani mradi wa TACTIC Mwanza CC na Ilemela MC km 32 eg Buhongwa-Igoma

2.Ujenzi wa Soko La Kirumba na Soko la Samaki Mkuyuni Bilioni 25.

3.Ujenzi wa Kampasi ya TIA Usagara-Mwanza ,Bilioni 8

4.Ujenzi wa Soko Kuu la Jiji la Mwanza

5.Ujenzi wa Hospitali ya Jiji gorofa 6

6.Ujenzi wa Majengo Mapya ya Gorofa Chuo Cha Ufundi na Maendeleo Misungwi.

7.Ujenzi wa Jengo jipya la Mwanza Airport na kukarabati wa uwanja kuwa wa Kimataifa

8.Ujenzi wa Jengo la Kitega Uchumi la TBA Ghana Kota gorofa 7

10.Ujenzi wa Tawi la Chuo Kikuu Cha Ardhi Mwanza (Sengerema)

11.Ujenzi wa Barabara za Mitaani chini ya TARURA eg Kisesa-Bujora,kiyungi road nk

12.Ujenzi wa shule Mpya za msingi na sekondari zikiwemo za gorofa eg Mwanza girls High School(Magu) only for science ,Nyanza P/School etc.

13.Ujenzi wa Hospital za Wilaya eg Sengerema ,Ujenzi wa Vituo vya Afya na ununuzi wa vifaa tiba Wilaya zote za Mwanza.

14.Mradi wa Maji Ukiriguru-Sumve Wilayani Misungwi Bilioni 32.

15.Ujenzi wa Barabara ya Hungumalwa-Ngudu-Magu km 71

16.Ujenzi wa Hospitali Mpya ya Rufaa Ukerewe

17.Upanuzi wa Bandari za Mwanza South sanjali na ujenzi wa vivuko vipya.

18.Ujenzi wa Chuo Cha Michezo Malya (Malya Sports Complex and Training Centre).Zaidi ya Bilioni 40.

19.Ujenzi wa Barabara ya Mabuki-Jojiro-Ngudu

20.Ujenzi wa Barabara ya Mwanza Airport -Kayenze-Nyanguge

21.Ujenzi wa Barabara ya Nansio-Rugezi

22.Ujenzi wa Barabara ya Mwanangwa-Misasi-Salawe-Solwa-Kahama km 150.

23.Ujenzi wa Barabara ya Bukokwa-Nyakalilo

24.Ujenzi wa Barabara ya Ilalila-Shibula

25.Ujenzi wa Barabara ya Sengerema -Nyehunge km 54.4 (Bilioni 73).

26.Ujenzi wa Daraja Kubwa la Simiyu lenye mita 150 pamoja na Barabara Unganishi.

27.Ujenzi wa Daraja Kubwa la Sukuma lenye urefu wa mita 70 na barabara Unganishi km 4.

28.Ujenzi wa Kituo Cha Kanda Cha Uokoaji Ziwa Viktoria

29.Majengo ya Utawala ya Halmashauri eg Kwimba,Magu, Sengerema DC nk.

30.Ujenzi wa Uwanja Mpya wa Michezo "Tabasam" Sengerema pamoja na Kukarabati wa viwanja vya CCM kirumba na Nyamagana.

31.Mradi wa Maji Kisesa bln 49

media="media="instagram:C89677rNdfd"]
View: https://www.instagram.com/p/C89677rNdfd/?igsh=ZTdkNml4YTQwa2V0[/URL]

View: https://youtu.be/Aq7AGgVXaxQ?si=fb9L7WED3YEdNVdb

(b)Miradi ya Urithi
1.Ujenzi wa daraja la JPM
2.Ujenzi wa Sgr ya Mwanza-Isaka
3.Ukamilishaji wa Stendi za
Nyegezi na Nyamhongolo
4.Ukamilishaji wa mradi wa Maji Butimba
5.Ukamilishaji wa Jengo la OPD Sekou Toure gorofa 6
6.Ukarabati wa Meli kubwa ya MV Mwanza Hapa kazi tuu.
7.Ukamilishaji wa Chuo Cha Ufundi na Teknolojia DIT Mwanza Campus
8.Ukamiloshji wa Tawi la Chuo Cha Mipango Vijijini Mwanza Centre

View: https://youtu.be/n97F4rAuoPs?si=tmTMNkcjX_nX7z3r

(c)Miradi ambayo Iko Mbioni kuanza ni

-Upanuzi wa Barabara ya njia 4 kutoka Mwanza CBD Hadi JPM bridge (lot 1 km 25),CBD-Usagara Jnct km 25.
-Ujenzi wa mgodi mkubwa wa Madini ya Dhahabu Nyanzaga
-Upanuzi wa Barabara kuu ya Musoma kuwa njia 4
-Upanuzi wa Barabara kuwa njia 4 kutoka Usagara-Shinyanga Border
-Kamanga-Katunguru-Sengerema km 3.
-Upanuzi kuwa njia 4 wa Barabara ya Mwanza-Nyanguge km 35.
-Mwanza Airport-Igombe-Kayenze-Nyanguge km 46
-Mkuyuni-Mahina-Nyakato km 10
-Nyakato(VETA)-Buswelu-Mhonze km 18.
View attachment 3127876

My Take
Hiyo ni Baadhi tuu ya miradi iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa na Samia huko Mwanza.

Kiufupi Samia ameiheshimisha Mwanza kushinda Shujaa waliyedai Anapendelea Kwao.

Kazi Iendelee.CC Nyanduzy , @feke b kidume
[URL unfurl="true" media=

View attachment 3128482View attachment 3128483View attachment 3128484View attachment 3128485View attachment 3128486

Yaani wewe unaona watu wa Mwanza ni wajinga kiasi hiki. unajiandikia mambo ya kipuuzi tu.

Baada ya kusifia hayo tueleze na anavyoiba na kujenga viwanda vya familia.´Morogoro.
 
Back
Top Bottom