Dada zangu mtanisamehe sana ila niwaambieni tu kuwa ni matendo yenu ndiyo yanatufanya Sisi Wanaume hasa Mimi GENTAMYCINE nizidi ' Kuwapuuza ' hasa kutokana na wengi wenu kuwa na uwezo mdogo wa Kuchanganua mambo, Kufikiri na Kujieleza ili ' Great Thinkers ' tunaowatizana tuone kuwa nanyi ' Vichwani ' mwenu mpo vizuri.
Kupitia Kipindi cha SHILAWADU kinachoendelea hewani sasa huyu Mwanadada Mpenzi wa Msanii wa Maigizo Ray Kigosi aitwae Chuchu Hans ametegwa swali dogo tu kuwa labda ni kwanini hadi hivi sasa haishi pamoja na Ray Kigosi na jibu lake alilotoa ndilo limenifanya nije na kuwaambia Wanawake kuwa bado wana safari ndefu katika kuweza kutumia vyema IQ's zao vinginevyo tutaendelea ' Kuwapuuza ' hadi Kiama kitakapokuja.
Huku akijua kabisa kuwa kwanza ameshatenda ' dhambi ' kubwa ya Kuzaa nje ya Ndoa na Ray Kigosi huku hapo hapo tena akiwa ' amemsaliti ' Mume wake wa Ndoa kabisa aishiye nchini Australia kwa sasa Mwanadada huyu Chuchu Hans alijibu kwamba hawezi kuishi pamoja na Ray Kigosi kwakuwa bado hajafuata Sheria za Dini ili awe nae na pia bado hawajakubaliana katika Dini kwamba ni nani kati yao amfuate mwenzake Kiimani kwani wote wawili ni Dini tofauti Chuchu akiwa ni Muislamu na Ray ni Mkristo.
Nawaombeni kuwaulizeni Members wa JamiiForums ambao nawakubali 100% kuwa wengi wenu ni Great Thinkers tena mliotukuka kabisa hivi hii ' Kauli ' ya ' Kipuuzi ' ya huyu Mwanadada Chuchu Hans alitakiwa aitoe akiwa bado hajazaa na Ray huku wakijua kabisa kuwa ' wanazini ' ili kumtumikia vyema Mwenyezi Mungu au hivi alivyoitoa sasa baada ya Kuzaa na Ray ndiyo yupo sahihi?
Hivi ili uonekane kuwa upo makini na unajua unachokifanya hadi Watu wasiwe na mashaka na uwezo wako wa Kufikiri kwa mfano ukishajua kwamba katika ' Kichaka ' fulani kuna Nyoka wakali mno tena wenye Sumu kubwa unapashwa uchukue tahadhari nao kabla hawajakuuma au unatakiwa ungojee Kwanza wakukong'oli / wakuume kisha udhurike ndipo sasa uwe nao makini pamoja na hicho Kichaka?
Dada zangu mnaniangusha sana hebu jitahidini mno kutumia IQ's zenu vyema ili tusiwadharau.
Nawasilisha.