Kwa jinsi Simba wanavyobebwa nashauri wapewe kombe

Hawa marefa wanatuharibia mpira... Offside kama ya leo sio ya visingizio.
Ujinga kama huu ulikuwepo mechi ya juzi ya Yanga na Mtibwa.. yaani nafasi ambayo sio offside ndio wanapuliza kipenga.. Upuuzi tupu.
TFF na Bodi ya Ligi acheni kutuvurugia mpira.. MAREFA WA HOVYO SANA.


Mimi Simba Sc mpaka nakufa.. ILA UKWELI USEMWE
 
Watu wa yanga hawasemi ukweli ndo shida kwa simba likitokea kabebwa ila wengine wanakausha na simba akinyimwa goli ambalo sio offside makosa hayaonekani yanayoonekana ni yale yanayoonesha feva kwa simba, kama tunakemea makosa tukemee tuweke usimba na yanga pembene sema refa amefanya makosa na sio kabeba timu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mechi mmebebwa,Yanga (Penalty na Mchimbi hakuwa offiside),Mwadui ,Namungo na leo polisi.Mnasajili kwa hela kubwa,mnalipa mishahara mikubwa lkn bado mechi mnanunua.
Waamuzi wetu wanashida sehemu haiwezekani makosa yaleyale kila siku,
 

Makosa aliyofanya refa yameibeba timu. Goli lile ndio lililoamsha morali ya Simba huku ikiishusha morali ya Polisi Tanzania. Tuje kwenye upande wa maamuzi yaliyoionea Simba, je ukiacha mechi dhidi ya coastal Union je ni mechi ipi nyingine simba walionewa? Maamuzi ya kuwabeba simba yamekuwa mengi sana kuliko maamuzi ya kuonewa.

Turudi kwa upande wa Yanga:

Yanga pia wameathirika na maamuzi mabovu ya waamuzi. Kuna maamuzi yaliyoyabeba na kuna maamuzi yaliyowaonea. Mechi dhidi ya Mtibwa kuna filimbi nyingi walizopigiwa mtibwa kuashiria kuwa wameotea wakati hawakuwa kwenye offside position. Lakini pia kuna filimbi iliyopigwa kwa Yanga kuashiria ni offside wakati haikuwa offside na mchezaji alikuwa kwenye position ya kufunga na kuna penati ya wazi walinyimwa baada ya kipa kumchezea vibaya Sibomana.

Wote Yanga na Mtibwa waliathirika kwa maamuzi mabovu ya marefa japo mtibwa walioneshwa filimbi nyingi za offside. Mechi dhidi ya Prison yanga alipata penati iliyokuwa na utata hasa baada ya tukio kama hilo lilifanywa na beki wa Yanga (Jafarry Mohamed) lakini tukio alilolifanya Jafarry Mohamed lilikuwa nje ya box hivyo ingekuwa ni faulo ya kawaida. Kuibadilisha nafasi kuwa goli nii asilimia 50 kushuka chini.

Ukichukua idadi ya mechi ambazo yanga yamenufaika kutokana na maamuzi yasiyo halali ni ndogo kulinganisha na maamuzi yasiyo halali yaliyoionea Yanga.

Simba anaongoza kwa kupata magoli yasiyo halali yanayopelekea kuamua matokeo ya mechi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha mkuu. Kunywa coke ya baridi uli relax.


Siku zote mwenye nacho huongezewa zaidi.

Kipindi cha manji tulipata shida sana

Mpaka goli za mkono tulikuwa tukifungwa na kina tambweeee.


Kutesa kwa zamu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…