Kwa Kichagga zinaitwa "ngoda" sijawahi kuziona popote zaidi ya Moshi. Zinaitwaje kwa kiswahili?

Kwa Kichagga zinaitwa "ngoda" sijawahi kuziona popote zaidi ya Moshi. Zinaitwaje kwa kiswahili?

Kibosho1

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2017
Posts
2,621
Reaction score
4,293
Hizi ni tunda zinaitwa Ngoda,miiti yake ni mikubwa kama miparachichi tu. Kwa mwaka zinatoka mara 1 tu misimu ya miezi ya 12 mpka mwezi wa kwanza mwanzoni.

Ladha yake ni chachu kwa umbali kama embe dodo ambalo halijaiva vizuri yani ina ugwadu kwa mbali. Ukila nyingi sana hutaweza kutafuna kitu sababu meno yatauma. Ila ni nzuri sana.
Zina umbo kama la zambarau

Je kwenu zipo? Zinaitwaje?
IMG_20201002_123311.jpg
 
Hizi ni tunda zinaitwa Ngoda,miiti yake ni mikubwa kama miparachichi tu. Kwa mwaka zinatoka mara 1 tu misimu ya miezi ya 12 mpka mwezi wa kwanza mwanzoni.
Ladha yake ni chachu kwa umbali kama embe dodo ambalo halijaiva vizuri yani ina ugwadu kwa mbali. Ukila nyingi sana hutaweza kutafuna kitu sababu meno yatauma. Ila ni nzuri sana.
Zina umbo kama la zambarau

Je kwenu zipo? Zinaitwaje?
View attachment 1587998
Hizi ni ndaraho au ndarao zipo kwa wingi Moshi Kilema, Marangu, Kirua, nk. Ni tamu sana zikiwa mbivu.
 
Back
Top Bottom