Kwa kinachoendelea huko Ukraine sasa nimeelewa kwanini viongozi wetu wa Afrika wameamua kuwa Vibaraka tu

Kwa kinachoendelea huko Ukraine sasa nimeelewa kwanini viongozi wetu wa Afrika wameamua kuwa Vibaraka tu

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Kwa yanayoendelea mataifa ya kiarabu na sasa habari inayovuma ni Uvamizi wa kijeshi wa taifa la Urusi Kwa Taifa la Ukraine ni dhahiri kuwa Waafrika hawana namna ya kufanya zaidi ya kuwa Vibaraka.

Sisi ambao hatujawahi kushika nafasi za juu katika nchi tunaweza kuwalaumu hawa ndugu zetu lakini nimrjaribu kufikiria Kwa upande wa pili nimegundua kuwa ndugu zetu hawana jinsi, hawana chaguo zaidi ya aidha kukubali kuwa kibaraka au kupokea vipigo ambavyo huwa vya Aina Aina.

Viongozi wote niliokuwa nawashambulia Kwa kweli mnisamehe tuu.
Nilifikiri kibinafsi bila kuvaa viatu vyenu. Sasa nimetambua jinsi msivyokuwa na chaguo zaidi ya kuwalamba Wababe wa Dunia viatu.

Ukweli ni kuwa usipomlamba viatu Mchina, basi utawalamba nchi za Magharibi na Marekani au Kanada.

Ubabe wa Dunia upo na utaendelea kuwepo,
Hakuna cha mzalendo wala ndugu yake uzalendo,
Tupo katika nyakati za kutawaliwa, inabidi tuwe wapole huku tukiwekeza kwenye elimu Kwa watoto wetu, hasa elimu ya kujitambua na elimu ya Mazingira.

Hii elimu ya kujifanya mzalendo ukiwa hauna Cheo ni uongo mtupu, wengi wakipewa uongozi hukuta kinyume na Yale waliyoyadhania.

Kwa mfano;
Tutafute mtu yeyote anayejiona mzalendo, alafu apewe nchi, utashangaa ndani ya miaka miwili mitatu ananyosha mikono na kujiunga katika kundi la Vibaraka.

Nini KIFANYIKE;

1. Elimu ya utambuzi na mazingira itolewe

2. Dini zote za kuja zifutwe na kama Hilo litakuwa gumu kutokana na kuwa Vibaraka bado ni wengi katika Dini hizo, basi elimu itolewe kuwa Dini ni elimu tuu ya maadili ya kumfanya mtu awe mwema ndani ya jamii.
Lakini hazina uhusiano wowote na MUNGU.

3. Neno Demokrasia lipatiwe maana nyingine kulingana na Mila na desturi ya taifa na jamii zetu.

4. Serikali iratibu mzunguko wa uzalishaji, na kuandaa matajiri wenye asili ya Tanzania ambao kwenye top 50 wawe zaidi ya Asilimia 80.

5. Serikali ianzishe Karakana kubwa kila kanda za kuzalisha Vijana wenye ubunifu na Teknolojia.

6. Serikali isiogope kuwa na Sera za Uvamizi na kutanua mipaka ya Nchi Kwa kuangalia maslahi ya watu wake. Hili kila siku nalisema.

Acha nipumzike kwanza
 
Ukweli ndiyo huo as long as bado tunaenda kuwatembezea bakuli kuombaomba basi lazima tu wataendelea kututawala huwezi kuleta ubabe kwa anayekulisha vinginevyo acha kumtegemea anza kujilisha mwenyewe kisha ndiyo ulete huo ubabe! Eti hatutaki watuingilie kisiasa ila kiuchumi pesa zao tunazitaka teh hakunaga huo undugu wala urafiki wa hivyo!
 
Ndo maana ukiingia kwenye anga za Putin unashushwa kaptura marinda yanatatuliwa
 
Kama wewe ungekuwa ndiye Rais Kwa mfumo wa Dunia ilivyo usingekuwa kibaraka??
Isingetokea sababu sahivi mimi ningewekeza kwenye science na technology, tatizo la africa kulipwa pesa ndefu wanasiasa ambao siyo wazalishaji na wazalishaji kulipwa kdg, ndiyo maana kila mtu anatamani kuwa mbunge, DC, DAS, DED, RC n.k
 
Ukweli ndiyo huo as long as bado tunaenda kuwatembezea bakuli kuombaomba basi lazima tu wataendelea kututawala huwezi kuleta ubabe kwa anayekulisha vinginevyo acha kumtegemea anza kujilisha mwenyewe kisha ndiyo ulete huo ubabe! Eti hatutaki watuingilie kisiasa ila kiuchumi pesa zao tunazitaka teh hakunaga huo undugu wala urafiki wa hivyo!
Mifumo mibovu na ufisadi ndiyo tatizo la africa
 
Kwa CCM hii utasubiri sn miaka 90 ijayo
Siyo suala la CCM, hivi unadhani leo hii tukimpa nchi Lissu ambavyo kawa Kibaraka wa Wazungu kiasi hicho, unategemea nini? Huo ndo ukweli japo ni mchungu. Afrika na nchi zingine hata zilizoko Ulaya tunaishi kwa kujipendekeza tu kwa Wababe wa Dunia
 
Angalau wewe umejitambua mapema sasa uanze kuwaelewesha wale wanaharakati uchwara wa Twitter,
Wengine wajanja wamewafuata huko huko kwenye Nchi zao kuwalamba Viatu huku kwenye Mitandao wakiliponda Taifa lao.
 
Siyo suala la CCM, hivi unadhani leo hii tukimpa nchi Lissu ambavyo kawa Kibaraka wa Wazungu kiasi hicho, unategemea nini? Huo ndo ukweli japo ni mchungu. Afrika na nchi zingine hata zilizoko Ulaya tunaishi kwa kujipendekeza tu kwa Wababe wa Dunia
Hahahaha mfumo mbovu, hata Ulaya walianza na mifumo mizuri, una mlipaje mbunge mgonga meza 340000 kwa siku kama siyo ujinga? unaacha kumlipa mwalimu au mtumishi mwingine mzalishaji alafu unategemea maendeleo, yaani unataka umkamue ng'ombe atoe maziwa mengi huku hutaki kumpa chakula cha kutosha una akili kweli?
 
Leo ndo umejua, hakun cha chadema wala nini ni bla bla tuu...sema nini kwenye concept ya Mungu hapo kama umechochora vibaya sana
Kajipakata pale nilifikili nimeona peke yangu
 
Back
Top Bottom