Kwa kweli inasikitisha sana tulipofikia

Kwa kweli inasikitisha sana tulipofikia

Kabisa mkuu future ya watt wetu ipo mikononi kwetu
Kabisa. Watawala wetu wanaotutawala hawafanyi makosa kabisa katika hili wanachonga njia kwa kizazi chake chote kisipite kwenye dhiki ila sisi wananchi wa kawaida tunasikitisha sana.
 
watoto wajue kujieleza kingereza fasaha, wajue kujumlisha, kutoa, kugawanya na kuzidisha hayo mengine ni mbwembwe....na ujue mtoto atafikia mahala ata branch out...hatakuwa kama utakavyo na jiandae na hiyo hali mapema mpe nafasi ya kujidhihirisha tokea akiwa mtoto wa primary
Usifikiri vijana hawajui hivyo vingereza na kujielezea usiishi katika nadharia tu juu ya maisha.

Vijana wanapitia msongo mkubwa wa mawazo huku mitaani na hivyo vingereza unavyo vizungumzia wewe wanavifahamu lakini hali zao zina sikitisha sana na hali inazidi kuwa mbaya mwaka kwa mwaka.
 
Una point

Lakini Lengo kuu la elimu ni kutoa ujinga kichwani

Elimu yetu ina shida kwa sababu haiwafundishi wanafunzi kuwa innovative

Mimi leo Swalehe kaniuliza we mzee hii solar ina 10v hatuwezi fanya izalishe 30v ?

Eeh nlishtuka ila nkajua ni kwa sababu ya elimu anayopata

More analytical and solving problems

Hata kama unasomesha mtoto wa kawaida jitahidi kumfanya akili yake iwe ya kufikiria

Mfundishe hata coding ina open mind

Lengo la shule sio kupata ajira

Kuna wengine watapata ajira wengine watatengenza wengine watatengenezewa

Sasa sisi tunatengeneza kundi moja

Ndio maana Tanzania ukiwa innovative in any way lazima ufanikiwe lots of stupid people with degree and PhD

Nasubiria Swalehe afike 14 nmwoneshe tenda za NEST
 
Ukitazama madogo asubuhi na mapema wanabeba mabegi mazito migongoni kuisaka elimu siku nzima wanakesha mashuleni kurudi mpaka jioni.

Wengine wanasomeshwa kwa lazima mpaka siku za weekend lengo ni kupata matokeo mazuri ya mitihani yao.

Wana sura zilizo na matumaini lakini moyoni mwangu kumejaa huzuni sana nikiwatazama kaka na dada zao mitaani kuna muda unatamani kuwaambia madogo kuwa wanapoteza muda na wanapotezewa muda wao huko wanakoenda asubuhi na mapema na kurejea majumbani kwao kiza kizito.

Ila unamua tu kukaa kimya na kuendelea na maisha yako lakini madogo hawana future yoyote kabisa wanajiendea tu sawa na kuku aliyekatwa kichwa.

Safari ya madogo na watoto wetu kwenye elimu ni sawa na safari ya kichaa ataenda umbali mrefu mwisho anarejea na takataka.

Kama familia haijiwezi ni vyema ndugu zangu hata kasi ya kuzaa tupunguze serikali zetu hizi hazijali lolote kuhusu umasikini wetu.

Kuzaa zaa hovyo tuachane na aina hii aina ya maisha.

Kwa ufupi taifa linazalisha rundo la masikini kwa kasi sana ndio maana kusifia viongozi na watu wenye pesa inaonekana ni kazi ya kujipatia pesa.

Hakuna future hapa taifani, hakikisha unazaa utakao weza walea na kuwatengenezea njia, viongozi wetu hawaishi kama tunavyoishi sisi wananchi wa kawaida wao wanawaandalia kesho yao bora watoto wao kielimu na kifedha.

Sisi wananchi wa kawaida tuna jiendea tu kama vichaa, tuna zaa masikini na tunaongeza rundo la masikini maana hata mifumo ya elimu yetu hai support kutukomboa na huu umasikini wetu.
tatzo wanaenda kusoma kitu kisicho na maana kwenye maisha yao ya baadae, me nafkiri ifikie wakati taifa litambue ya kwamba tayari tunao wasomi wengi kwenye nyanja za usimamiz na uendeshaji

Sas tuanze kutoa elimu zenye tija hasa kujikwamua kwenye harakati za kutafta maisha na ubunifu wa kutengeneza vitu vitakavyo uzwa na kutumika ndani
Ujue tanzania hatuna ushindani kabisa kwenye swala la izalishaji wa bizaa pamoja na malighafi za shambna alafu bado mtot anaenda kusoma au kisomea usimamiz wa biashara kwa pesa nyinga ambazo angezifanya mtaji kwa maisha yake ya kesho.
 
Inasikitisha sana kuona mlolongo wa elimu ulivyo mrefu kulingana na ajira zilizopo
 
Kwanza kwann watoto wanakaa zana shule huko? Tokea saa kumi na mbili alfajiri hadi saa kumi na moja jioni ili wagundue nini?
 
Mimi nilitakataa ,nikawambia Brokeside kama kufeli mwache afeli kwani nyie kinawauma nini? Na mtoto alikuja kupata A masomo yote
Kabisa, mzazi unatakiwa umlee mwanao sio uwaachie hilo jukumu shule, unachukua mtoto usiku akifika nyumbani analala, nyumbani kunakuwa kama bwenini.
 
Kwanza kwann watoto wanakaa zana shule huko? Tokea saa kumi na mbili alfajiri hadi saa kumi na moja jioni ili wagundue nini?
na ni mwanafunzi wa darasa la pili, mda wote huo anasoma nini huko?
 
Kwanza kwann watoto wanakaa zana shule huko? Tokea saa kumi na mbili alfajiri hadi saa kumi na moja jioni ili wagundue nini?
Yaani utaona very busy na elimu za kuwakariri kina kinjeketile ngwale na maujinga ya zinjanthropus!

This kind of education is fuckin wahead!
 
Yaani wanaenda shule kukariri ili wafaulu mitihani huku vichwani wakiwa watupu. Serikali nayo wala haijali, wanaacha shule zijifanyie watakavyo.
 
Back
Top Bottom