Kwa lipi na kwanini Samwel J. Sitta aaminiwe?

Kwa lipi na kwanini Samwel J. Sitta aaminiwe?

Nguruvi3

Platinum Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
15,773
Reaction score
32,431
MZALENDO au NDUMILA KUWILI?

Tuwangalie kwa jicho angavu
Ni tatizo tusilolijua
Pande mbili za mheshimiwa na tusiyoyakumbuka

Wanajamvi tutakuwa na sehemu I-III kuhusiana na mwenyekiti wa bunge la katiba, tukimwangalia alipotoka alipo na aendako.
Kwa mwenendo wake wengi tunajiuliza kama keshakata tamaa na sasa anahitimisha safari yake ya kiasiasa

Sehemu ya I

Mwenyekiti wa bunge la katiba(BMLK) Mh Samwel Sitta ni mwanasiasa asiyeleweka kwa wengi. Amejaliwa kipaji cha kuongea,busara na kujenga imani kama mmoja wa Wazelondo wa nchi hii.

Historia yake ni ndefu katika umri wa miaka 71. Sitta ni msomi wa sheria akiwa mhitimu kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaa. Alianza masomo yake mwaka 1964 na kumaliza mwaka 1971.
Miaka 7 chuoni UDSM haikuwa rahisi, naye kama walivyo wanasiasa wengine aliwahi kufukuzwa chuo mwaka 1966 katika ule mgomo wa kujiunga na JKT.

Mgomo huo uliitingisha nchi lakini si mwalimu Nyerere. Wanafunzi wa chuo kikuu walimpa mwalimu ‘ultimatum' kuhusu madai yao. Hatimaye wakajikuta uso kwa uso na mwalimu na ndipo walipokabiliana na nguvu ya hoja na nguvu za dola.
Wengine waliokuwepo ni akina Warioba na viongozi wengine.

Samwel Sitta amelihudumia taifa katika ngazi ya serikali na chama akiwa waziri, katibu wa chama, mkurugurenzi mtendaji wa mashirika ya umma n.k.
Hiyo pengine ni pamoja na kuwa na diploma katika mambo ya utawala kulikompa nafasi zaidi

Kwa haraka haraka Sitta anaonekana kama miongoni mwa wanafunzi watiifu wa Nyerere. Hata hivyo muda umetueleza bila kificho akina nani walikuwa watiifu na wepi walikuwa na woga wakiwa wanafunzi wanafaniki.

Sitta ilichomoza akiwa miongoni mwa wapiga debe wakubwa wa EL katika chaguzi za mwanzo. Tunakumbuka jinsi Mwalimu alivyomuangalia EL kwa jicho la hofu na uhalifu.
Pamoja na hayo sitta alikuwa mstari wa mbele kumuunga mkono

Sitta alikwenda mbali kupingana na Nyerere dhidi ya uteuzi wa mh EL.
Hata pale wenzake akina JK, Lukuvi, Seif khatibu walipoonekana kunywea, Samwel alisimama kidete na Swahiba yake EL.

Harakati zake zilifika mwisho ndani ya NEC pale mwalimu alipomtaka Sitta kama waziri wa sheria asome faili la EL na kuwaeleza wapi alikuwa anaonewa.
Hapo hakuwa na ujanja bali kuahirisha harakati zake.

Samwel Sitta ni mmoja wa wanamtandao ambao si tu walinyanyasa watu wengine bali pia waliwadhalilisha baadhi ya viongozi kwa kutumia nafasi zao. Mtandao huo uliundwa ili kuwabomoa wazee kama akina Malecela na wengine, Sitta akiwa mshiriki.

Matarajio ya Samwel Sitta kuchukua nafasi yalizidi pale Nyerere alipohitimisha safari ya EL. Ikumbukwe mtandao uliendelea na harakati hadi chaguzi zilziomwingiza JK magogoni.

Sitta akatumia fursa hiyo kunyemelea kiti cha uwaziri mkuu kwa vile tu EL alishachafuka na hivyo hakuwa chaguo tena siku za mbeleni.

Katika hali isiyotarajiwa na akiongozwa na vigogo wa mtandao wenye nazo, JK alijikuta akimchagua EL. Jambo hilo halikuwa habari njema kwa Sitta .
Hata hivyo Sitta akiwa mwanamtandao akatunukiwa nafasi ya Uspika.

Zipo habari za yeye kuomba msafara kama kiongozi mkuu.
Hilo likakataliwa ndipo nyongo na chuki zikaanza, mtandao ukaanza kumeguka kidogo kidogo.
Ilipotokea nafasi ya Richmond, Sitta hakusita kuitumia vema na mzee wa Monduli akajikuta kaangukia pua.

Sehemu itaendelea..........

Richmond na viporo alivyofunika
Posho za wabunge na alivyowageuka wananchi

n.k
 
Sehemu ya II

SITTA NA HISTORIA YA TANGANYIKA

Kabla hatujarudi bungeni alipokuwa Spika na sakata maarufu la Richmond, tungependa kuwakumbusha kuwa majuzi alipokuwa anawania nafasi ya uenyekiti, Sitta alisema yeye ni chura anarudi majini. Wengi hawakuelewa maana ya kauli hii. Hapa Sitta hakumaanisha kuwa alikuwa Spika anarudi kuwa Spika. Maana yake ina uhusiano na Tanganyika

Tumeeleza jinsi alivyokuwa sehemu ya Mtandao wa JK. Lakini si mara yake ya kwanza, Sitta alipokuwa waziri wa sheria na katiba lilikuwepo sakata la G55.

Tunachofahamu Sitta aliunga mkono kundi la G55 japo alikuwa waziri. Yupo katika kumbu kumbu akieleza maandalizi yalikuwepo kuwa na kura ya maoni(referendum) baada ya hoja za G55 kugonga mwamba kiufundi(On tech ground)

Katika bajeti ya wizara yake, mh Sitta aligusia suala hilo la kuwa na kura ya maoni (1995?).
Kilichomfanya asijitokeze wazi katika nafasi ya G55 ni nafasi yake ya uwaziri.
Hivyo anaposema chura anarudi majini ni wazi anajua kuwa ni suala la Tanganyika lanalolifahamu siku nyingi tu.

Kama ilivyokuwa huko nyuma, akiwa waziri wa sheria mh alishindwa kusimamia suala la kurudi kwa Tanganyika.
Uzalendo wake ukaishia katika chama zaidi ya imani yake juu ya uwepo wa Tanganyika.
Hivyo ni vema kabisa kusema suala la muungano loyality ya Sitta ni uwepo wa Tanganyika.
Tatizo ni kuwa, Sitta amefungwa na uchama zaidi ya uananchi.

Akiwa Spika wa bunge 2005-2010 mara nyingi amesikika akitoa kauli tata. Kwa mfano, ni sitta aliuliwauliza wznz kuhusu gharama za elimu ya juu n.k
Lakini ni Sitta huyo huyo alisema ni haki kwa wazanzibar kuwazuia Watanganyika kupata ardhi kwasababu kuna eneo kubwa Tanganyika. Kwamba Tanganyika kuwa na eneo ni shamba la bibi na muungano uliopo ni safi kabisa.

Misimamo ya Sitta inakuwa ya pande mbili na ni ngumu kuelewa anasimamia wapi.
Ni mtu anyejificha nyuma ya agenda na kuchagua upande baada ya kuona uelekeo.

Katika bunge la katiba Sitta amesikika akitetea kura ya siri lakini akichagiza kura ya uwazi.
Naye ni mtu anayependa kuchagua upande kutokana na mwelekeo na wala si maoni au maono yake binafasi.

Kwasasa hivi anaonekana kuwa ni muumini wa muungano wa serikali 2, kinachomsukuma zaidi ni nia yake ya kuwania Urais 2015. Sitta anafahamu kuwaudhi wahafidhina wa CCM ni kujitafutia madhara. Hilo alilionja wakati wa sakata la Richmond.

Sakata la Richmond lilitokana na hasira zake dhidi ya Mtandao uliomtupa na kumpa nafasi ya Spika.
Tunakumbuka iliwahi kutokea viongozi wengi walikuwa nje ya nchi na Spika akakaimu nafasi ya Urais na kupewa piki piki za kumsindikiza. Zote hizo zilikuwa ni jitihada za kumpooza. Na kila mara kiongozi mkuu wa serikali anapokuwa hayupo bungeni nafasi hiyo hupewa kwa vile ni sehemu ya mtandao.

Sakata la Richmond nalo halimuachi kama alivyo. Mara ya kwanza aliafiki kuwa hakukuwa na hujuma hadi kamati ndogo ya shelukindo iliposema kuna umuhimu wa kuchunguza zaidi.
Kwavile kamati ile ilikuwa ya bunge ikiwa na CCM wengi, mh alikubali. Nafasi ya kumfanyizia mh E ilipotimu akaitumia vema.

Kitu wengi wetu tusichokumbuka ni kuwa sakata lile halikuisha na ukweli wake ulifichwa.
Hata pale walipojitokeza watu kutaka kueleza ukweli na undani wake Spika Sitta alizima hoja hiyo.
Ndivyo alivyozima hoja za Meremeta na zinginezo kwa kigezo cha 'kiti' kimeamua

Kilichomsukuma kuzima hoja hizo ni ukweli kuwa bado alikuwa na matarajio ya Uspika na pengine nafasi ya juu zaidi.
Hata hivyo wahafidhina hawakumuacha, ndani ya CC uteuzi wake wa Uspika ukahitimishwa kwa sababu rahisi, ni zamu ya akina mama.

Hilo lilikuwa pigo kubwa kwa Sitta ambaye alikuwa anataraji kujenga mazingira ya Urais kupitia simple popularity kama Richmond. Ukweli unabaki kuwa Richmond na undani wake ulifichwa na kuzikwa na Sitta.

Ni kutokana na kutomwelewa, wengi waliona anafaa kuwa mwenyekiti wa bunge la katiba.
Sitta anatumia nafasi hiyo si kwa sababu ya kuipenda nchi yake, ni kutafuta umaarufu wa kujenga jukwaa (Platform) kwa ajili ya 2015. Ni kwa msingi huo tulishawahi kuonya mapema kuwa huyu si mtu wa kuaminika.
Anajali masilahi yake kuliko ya nchi, na ni mwepesi sana wa kuitumia nchi kufikia malengo yake.

Ingawa sasa hivi anaonekana kuwa CCM, Sitta ni muumini mzuri wa Tanganyika kutokana na historia yake. Kinachomsukuma ajali CCM katika mchakato ni ukweli kuwa alishawahi'kuumwa na nyoka' wakati wa kugombea Uspika.
Anafahamu kuwaudhi CCM kutahitimisha mbio zake haraka iwezekanavyo.

Ili kuwafurahisha CCM kwa kujenga mazingira ya baadaye na si ya nchi, Sitta amechukua uenyekiti na kwenda kinyume cha kanuni zilizoandikwa. Aliamua kumwita Warioba kwanza kabla ya JK ili kutoa nafasi ya kumbomoa, kumdhalilisha na kumfehdehesha jambo alilofanikiwa. Hakufanya hivyo kwa kukurupuka anafahamu umuhimu wa CCM na umhimu wa kutetea mtandao ambao anategemea utamwezesha kuelekea 2015.

Hatua ya pili ilikuwa kuwatisha wale wanaopinga muungano wa serikali 2.
Sitta amenukuliwa akisema atapamaba na wote wanaopinga muungano.
Hapa alimaanisha wanaopinga serikali 2 si kwasababu anaamini serikali 2 bali anataka kuwafurahisha CCM kwa gharama za mamilioni ya Watanganyika wanaodai serikali yao.

Hatua ya tatu ni kuunda kamati zitakazosukuma agenda ya serikali 2 kwa nguvu.
Kamati hizo zimesheheni na kupangwa CCM kuanzia mwanzo hadi mwisho.
Hilo ndilo alilotaka kwavile anaamini kupitia katib atakuwa amefungua milango ya kuelekea 2015.

Safari ya 2015 ameshainza, ingawa wengi hawafahamu, naye kama EL ametumia sehemu kama makanisa kuhakikisha anajiweka sawa. Hivyo kuunga mkono CCM kwa nguvu zote ni kuimarisha harakati zake hata kama kufanya hivyo ni kwa hasara ya nchi.

Je, move anayoifanya itamsaidia au itahitimisha safari yake mapema sana?
Bunge hili litamvumilia au litamvunjikia mikononi?

Tutaendelea........
 
Nguruvi3 nimekusoma vyema na mpaka sasa nimeelewa mwelekeo wa sitta. Pamoja na yote yanayoendelea nina uhakika kabisa na mambo yafuatayo pasina kuelezea:

1. BMLK halitamalizika salama
2. EL ni kigingi cha chuma kwa sitta
3. Sitta hatateuliwa kuwania urais 2015

Mkuu sasa endelea na mada sehemu uliyoiacha.
 
Last edited by a moderator:
Sehemu ya III

UNDUMILA KUWILI WA SITTA NI WA SIKU NYINGI


Wakati bunge linazinduliwa Spika Sitta akiwa katika kiti, jambo la kwanza lilikuwa kumwalika rais azindue.Hilo ni baada ya Wabunge kuapishwa. Ndio utaratibu umetumika miaka nenda rudi.
Ni nafasi ya Rais kueleza vipaumbele vya serikali yake.

Bunge maalumu la katiba linaloendelea liliandaa utaratibu kama huo tofauti ikiwa ni Rais kuzungumzia mambo ya kitaifa yanayohusiana na katiba.

Katika hali tuliotarajia wengine na tuliyowahi kuieleza Spika Sitta akaamua binafsi kwa kutumia 'busara zake' kumwalika Warioba kwanza ili Rais afuatie.
Busara anazozisema Sitta ni kuwa bunge lazima liwe na agenda kwanza ili Rais aje kulihutubia.

Licha ya wanasheria kuandaa kanuni hizo wakiwemo wenye busara zaidi, Sitta akatumia nguvu na ubabe wake kuhakikisha mkakati wa kuwadhalilisha wazee wenzake akina Salim Ahmed Salim, Jaji Warioba,Jaji Augustino Ramadhan, marofesa na madaktari unatimia kwa kupindisha kanuni.

Hilo amefanikiwa na JK kamvuruga mzee Warioba kama mtoto mdogo kwa kumzushia, kumzogoa na kumnyanyasa hata kwa asichokisema. Azma ya JK kupitia Samwel Sitta ikatimia.

Ni ngumu kuamini dhalili aliyopata mzee Warioba, alipaswa kupewa makamu wa Rais na waziri mkuu wa zamani. Samwel Sitta akaona ni bora amdhalilishe mzee mwenzake ili kufungua njia kuelekea 2015. Sijui kama mkakati huo utamsaidia maana historia ni mwalimu mzuri sana.

Huo ni undumila kuwili kwasababu alipokuwa anajinadi alisema anakwenda kutetea taifa na kwamba Tanzania kwanza.

Kinyume chake Tanzania pili, Sitta kwanza na CCM muhimu.
Ni undumila kuwili wa namna hiyo uliwahi kujitokeza katika bunge alililoongoza huko nyuma.

Baada ya wazee wa Dar es salaam kulalamikia posho na marupu rupu aliyoandaa Sitta, Rais alikubaliana nao hadharani.

Nyuma ya pazia Samwel Sitta akamshawishi rais kuhusu posho hizo na zikaongezwa kinyemela.
Hata alipoulizwa, Sitta alisema mshahara wa mbunge ni siri. Huyu mtu anayeitetea Tanzania hawezi kujadili mshahara wa mbunge ni mtetezi gani huyu.

Huyu ndiye anayepita makanisani na mashuleni akisema anapinga ufisadi na watu wanamwamwini. Ni jambo la kushangaza sana kwasababu Samwel Sitta ndiye aliyezika hoja ya pesa za radar isijadiliwe bungeni kwa nguvu za kiti cha Uspika.

Leo tunaaminishwaje kuwa Samwel anapiga vita ufisadi?
Kila kiporo cha tuhuma kisicho na majibu, Sitta ameshiriki kuficha.
Tunakumbuka matumizi mabaya ya fedha za ofisi. Leo tunaambiwa ni mwadilifu

Jana amesikika akisema uchaguzi wa wenyeviti hana lawama kwasababu CCM ni wengi na hata katika kura watashinda. Huyu ndiye mtu aliyeomba kiti kwa kauli mbiu ya Tanzania kwanza.

Leo hawezi kuliangalia bunge kama Tanzania bali CCM halafu tunaaminishwa ni mtu safi.
Anaongea jambo moja leo kesho anabadilika na msimamo tofauti.

Katika bunge aliloongoza kabla kama Spika, wenyeviti wa kamati za bunge baadhi hutoka vyama vya upinzani kwa kanuni ili kuleta sura ya bunge.

Mbona alipokuwa Spika hakuwahi kusema CCM ni wengi na hivyo waongoze kamati?
Huu kama si unafiki na undumila kuwili ni kitu gani wanajamvi?

Anachoshindwa kukielewa Sitta ni kuwa katiba ni agenda ya wananchi bila kujali CCM.Chadema/CUF au TLP. Mbinu anazotumia si kuwa zinawadhalilisha wananchi bali zinamweka mahali pagumu sana kiheshima,nafasi katika jamii, umri na matarajio ya baadaye.

Tutaendelea....
 
Sehemu IV

BUNGE LA KATIBA LITAVUNJIKA, SITTA ATAHITIMISHA SAFARI YA KISIASA

Bunge la katiba lina mvutano wa mudakuanzia mchakato hadi lilipofikia.
Kuna uvumilivu kwa mwanadamu na kipo kiwango.

Wapenda mabadiliko wamevumilia mengi ikiwemo la Sitta kubadilisha kanuni kwasababu ana 'busara sana' kuliko kamati zailizoandika kanuni hizo.

Chuki zilianza siku za nyuma, zikahamania bunge la katiba katika kanuni.
JK analaumiwa kwa hotuba ya kumfedhehesha Warioba. Hata kama yalikuwa maagizo yake, bado mzigo wa kukiuka kanuni na kuwasaliti wananchi upo begani kwa Sitta.
Lau angewasikiliza wanakamati wenzake leo asingekuwa anazungumziwa.

Sitta akaamua, kwanza kuitukana kamati iliyoandaa kanuni kwa kitendo cha kusema 'Yeye anabusara na ndizo zinamuongoza' tafsiri ya kwamba kamati haikuwa na busara katika maamuzi.

Pili, mzigo wa dhalili ya tume Warioba ni matokeo ya Samwel Sitta kupindisha taratibu

Tatu,kuunda kamati za CCM utakaopelekea machauko ni matokeo ya Sitta kuendekeza UCCM katika mambo ya kitaifa.

Wakati mswada wa kwanza unatolewa, Samwel Sitta alipangwa Zanzibar.
Huko alikumbana na nguvu ya wananchi kwa kuchoma mswada mbele kukiwa na vurugu kubwa.
Wananchi wa znz walimheshimu Sitta japo kwa kumsikiliza.
Ingekuwa akina Nap moto ungewaka zaidi.

Sitta akarudi kwa JK na kumshauri suala la muungano lijadiliwe kama masuala mengine.
Ni kwa kuona busara hizo na bila kumjua Sitta, wazanzibar walioko Dodoma wakampa uenyekiti

Huyu ni ndumila kuwili sasa anatumia upande wa pili kashughulikia wzn kama alivyo ahidi

Sitta kaweka wazi msimamo wa serikali 2 na kwamba muungano ni lazima.
Huu ni ujumbe maridhawa kwa wazanzibar, yale matumaini kuhusu malalamiko yanafikia hatima

Sitta keshasema atawashughulikia na salama ya wazanzibar ni ukimya.
Kama hiyo ndiyo njia waliyoamua, basi tunawatakia heri wznz na Sitta.

Mbele ya safari ni kweusi. Kama wapenda mabadiliko na nchi kwanza wataamua kwa dhati kusimama kidete wakiamini nchi na wananchi kwanza, hakuna sababu za kuwepo Dodoma.

Wananchi watawaelewa pale watakapoondoka Dodoma na kuzunguka nchi nzima wakieleza uhuni unaoendelea Dodoma chini ya uratibu na usaliti wa mzee wetu Sitta

CCM wataandika katiba, wakimaliza wananchi watakuwa wanaelewa nini kinatokea.
Tunakumbuka bajeti iliyoongeza bei za mafuta ya taa ilivyopingwa na wabunge wa upinzani chini ya Sitta. Ilimlazimu Spika atoe mawaziri bungeni kwenda kueleza uzuri wa bajeti ambako walikumbana na mawe na kila rabsha.

Wananchi wanafuatilia kwa umakini nini kinaendelea Dodoma. Kama lipo jambo wanalosubiri ni kusikia bunge maalumu la katiba la CCM na Samwel Sitta linafikia tamati haraka.

Sitta, kwa kujitoa 'mhanga' anakabiliwa na mambo mawili
1. Hasira za wabunge wa upinzani
2. Hasira za wazanzibar
3. Hasira za Watanganyika
4. Hasira za kamati ya kanuni
5. Hasira za umma dhidi ya dhalili kwa maoni yao kupitia Warioba.

Ingawa Sitta haonekani kujali kwa kuangalia masilahi yake 2015, bunge hili la katiba litahitimisha safari yake ya kisiasa. Hadi sasa hivi umma unafahamu kama msaliti wao na mtu anayeweza kutumika kama karatasi za maliwato, baada ya hapo hakuna thamani.

Itaendelea sehemu ya mwisho.....
 
Mkuu Nguruvi3, heshima mbele. Nimefuatilia huu uzi naona kama unatumia nguvu ya ziada kumpiga mawe SS kunani? Hata ka mwenyekiti wa BMLK angekuwa mtu mwingine unadhani ccm wangeacha kutumia wingi wao kushawishi matokeo ya mchakato huu?
Wapenda mabadiliko na demokrasia inabidi waangalie walipojikwaa na sio wanapoangukia, inabidi kujiuliza imekuwaje ccm wakawa wengi kwenye mabunge haya na iwapo wao ccm wanaona status quo inawapendelea kwa nini wasifanye kila hila mambo yabaki hivi yalivyo?
Kuna kambi fulani za wasaka uraisi ccm wamewekeza sana kiasi kwamba wasingependa katiba mpya kama ilivyoletwa kwenye rasimu na watafurahi zaidi iwapo mchakato huu utakwama. Tishio la wana-ukawa kujitoa, ni sawa na kumsusia ngedere shamba baadhi ya watu watasherehekea.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3, heshima mbele. Nimefuatilia huu uzi naona kama unatumia nguvu ya ziada kumpiga mawe SS kunani? Hata ka mwenyekiti wa BMLK angekuwa mtu mwingine unadhani ccm wangeacha kutumia wingi wao kushawishi matokeo ya mchakato huu?
Wapenda mabadiliko na demokrasia inabidi waangalie walipojikwaa na sio wanapoangukia, inabidi kujiuliza imekuwaje ccm wakawa wengi kwenye mabunge haya na iwapo wao ccm wanaona status quo inawapendelea kwa nini wasifanye kila hila mambo yabaki hivi yalivyo?
Kuna kambi fulani za wasaka uraisi ccm wamewekeza sana kiasi kwamba wasingependa katiba mpya kama ilivyoletwa kwenye rasimu na watafurahi zaidi iwapo mchakato huu utakwama. Tishio la wana-ukawa kujitoa, ni sawa na kumsusia ngedere shamba baadhi ya watu watasherehekea.
Kakalende , nipo katika rekodi ya kuonyesha bunge la katiba litakavyokuwa. Rejea nyuzi za duru.
Ni kama nilivyowaeleza wznz siku za nyuma na kama nilivyotahadhrisha kuhusu mchakato wa katiba n.k.

Hakika sasa hivi nathibitisha kila mstari nilioandika na kumbu kumbu zipo.

Kabla ya uteuzi wa Sitta nipo katika rekodi kuwatahadharisha wajumbe na Watanzania kuwa matumaini waliyo nayo kwake ni kujidanganya. Nipo katika rekodi na kumbukumbu zipo.

Ninachokifanya si kumpiga mawe Sitta, ni kuwaeleza wajumbe wa BMLK na Watanzania kuwa kwani hawakujua wanachagua mtu wa aina gani. Ndiyo maana naweka historia ya utendaji na matukio yanayomhusu.
Nawaeleza wajumbe wa BMLK kuwa waendelee kukamua mawe wakitaraji supu.

Lakini pia wapo wanaosema huyu ndiye mwenyewe kuelekea 2015. Kama mtanzania nawapa habari za sitta na wao wataamua kuchagua sura nzuri, kuchagua wanafiki au kuchagua viongozi.

Na mwisho ninamtahadharisha Sitta kuwa historia ya kuvunjika kwa bunge wiki hii haitakuwa na mkono mwingine bali mkono wake. Jina lake litakuwa limeandikwa katika historia kwa namna chafu sana.
Anaweza kuwa katika kundi moja na akina Bokassa na Milosovic katika vitabu kule library

Mkuu tunafanya taththmini tu na kila mtu anakaribishwa kueleza anachokijua.
 
Sehemu IV

BUNGE LA KATIBA LITAVUNJIKA, SITTA ATAHITIMISHA SAFARI YA KISIASA

Bunge la katiba lina mvutano wa mudakuanzia mchakato hadi lilipofikia.
Kuna uvumilivu kwa mwanadamu na kipo kiwango.

Wapenda mabadiliko wamevumilia mengi ikiwemo la Sitta kubadilisha kanuni kwasababu ana 'busara sana' kuliko kamati zailizoandika kanuni hizo.

Chuki zilianza siku za nyuma, zikahamania bunge la katiba katika kanuni.
JK analaumiwa kwa hotuba ya kumfedhehesha Warioba. Hata kama yalikuwa maagizo yake, bado mzigo wa kukiuka kanuni na kuwasaliti wananchi upo begani kwa Sitta.
Lau angewasikiliza wanakamati wenzake leo asingekuwa anazungumziwa.

Sitta akaamua, kwanza kuitukana kamati iliyoandaa kanuni kwa kitendo cha kusema 'Yeye anabusara na ndizo zinamuongoza' tafsiri ya kwamba kamati haikuwa na busara katika maamuzi.

Pili, mzigo wa dhalili ya tume Warioba ni matokeo ya Samwel Sitta kupindisha taratibu

Tatu,kuunda kamati za CCM utakaopelekea machauko ni matokeo ya Sitta kuendekeza UCCM katika mambo ya kitaifa.

Wakati mswada wa kwanza unatolewa, Samwel Sitta alipangwa Zanzibar.
Huko alikumbana na nguvu ya wananchi kwa kuchoma mswada mbele kukiwa na vurugu kubwa.
Wananchi wa znz walimheshimu Sitta japo kwa kumsikiliza.
Ingekuwa akina Nap moto ungewaka zaidi.

Sitta akarudi kwa JK na kumshauri suala la muungano lijadiliwe kama masuala mengine.
Ni kwa kuona busara hizo na bila kumjua Sitta, wazanzibar walioko Dodoma wakampa uenyekiti

Huyu ni ndumila kuwili sasa anatumia upande wa pili kashughulikia wzn kama alivyo ahidi

Sitta kaweka wazi msimamo wa serikali 2 na kwamba muungano ni lazima.
Huu ni ujumbe maridhawa kwa wazanzibar, yale matumaini kuhusu malalamiko yanafikia hatima

Sitta keshasema atawashughulikia na salama ya wazanzibar ni ukimya.
Kama hiyo ndiyo njia waliyoamua, basi tunawatakia heri wznz na Sitta.

Mbele ya safari ni kweusi. Kama wapenda mabadiliko na nchi kwanza wataamua kwa dhati kusimama kidete wakiamini nchi na wananchi kwanza, hakuna sababu za kuwepo Dodoma.

Wananchi watawaelewa pale watakapoondoka Dodoma na kuzunguka nchi nzima wakieleza uhuni unaoendelea Dodoma chini ya uratibu na usaliti wa mzee wetu Sitta

CCM wataandika katiba, wakimaliza wananchi watakuwa wanaelewa nini kinatokea.
Tunakumbuka bajeti iliyoongeza bei za mafuta ya taa ilivyopingwa na wabunge wa upinzani chini ya Sitta. Ilimlazimu Spika atoe mawaziri bungeni kwenda kueleza uzuri wa bajeti ambako walikumbana na mawe na kila rabsha.

Wananchi wanafuatilia kwa umakini nini kinaendelea Dodoma. Kama lipo jambo wanalosubiri ni kusikia bunge maalumu la katiba la CCM na Samwel Sitta linafikia tamati haraka.

Sitta, kwa kujitoa 'mhanga' anakabiliwa na mambo mawili
1. Hasira za wabunge wa upinzani
2. Hasira za wazanzibar
3. Hasira za Watanganyika
4. Hasira za kamati ya kanuni
5. Hasira za umma dhidi ya dhalili kwa maoni yao kupitia Warioba.

Ingawa Sitta haonekani kujali kwa kuangalia masilahi yake 2015, bunge hili la katiba litahitimisha safari yake ya kisiasa. Hadi sasa hivi umma unafahamu kama msaliti wao na mtu anayeweza kutumika kama karatasi za maliwato, baada ya hapo hakuna thamani.

Itaendelea sehemu ya mwisho.....

Big up mkuu kwa uchambuzi makini...
Niweke tu chorus kwa kusema hili BMK liko very delicate. Lakini pia CCM wameshaamua kuwa mchakato wa katiba unaishia hapa. Mbinu zao zote ni kuhakikisha uchaguzi mkuu ujao unafanyika chini ya katiba mbovu iliyopo. Wanajiaminisha kwamba watashinda uraisi. Then wanajua katiba mpya ikipatikana chini ya raisi mpya, huyo raisi atakuwa na maslahi kwenye kila muundo atakaoufanya. Kuanzia tume ya utumishi, jaji mkuu, Mwanasheria mkuu nk. JK sasa hivi anaelekea ukingoni. Katiba mpya ikipatikana chini ya JK hawana uhakika wa control kwenye tume ya utumishi wala tume ya uchaguzi.
Bila shaka hayo yalishaamuliwa katika vikao vyao kuwa hawaendi kwenye uchaguzi ujao na katiba mpya. Sitta anafahamu na yuko tu pale kuuza sura kwa maslahi ya uraisi 2015 CCM huku akifanya delaying techniques za kuahirisha bunge kila siku na kuvuruga kanuni ili mda uishe. Aliyosema Pinda kuwa huenda bunge la katiba likaahirishwa hadi mwakani kupisha mambi mengine ya kitaifa ni uthibitisho kuwa wamejiandaa katika hili...
 
Big up mkuu kwa uchambuzi makini...
Niweke tu chorus kwa kusema hili BMK liko very delicate. Lakini pia CCM wameshaamua kuwa mchakato wa katiba unaishia hapa. Mbinu zao zote ni kuhakikisha uchaguzi mkuu ujao unafanyika chini ya katiba mbovu iliyopo. Wanajiaminisha kwamba watashinda uraisi. Then wanajua katiba mpya ikipatikana chini ya raisi mpya, huyo raisi atakuwa na maslahi kwenye kila muundo atakaoufanya. Kuanzia tume ya utumishi, jaji mkuu, Mwanasheria mkuu nk. JK sasa hivi anaelekea ukingoni. Katiba mpya ikipatikana chini ya JK hawana uhakika wa control kwenye tume ya utumishi wala tume ya uchaguzi.
Bila shaka hayo yalishaamuliwa katika vikao vyao kuwa hawaendi kwenye uchaguzi ujao na katiba mpya. Sitta anafahamu na yuko tu pale kuuza sura kwa maslahi ya uraisi 2015 CCM huku akifanya delaying techniques za kuahirisha bunge kila siku na kuvuruga kanuni ili mda uishe. Aliyosema Pinda kuwa huenda bunge la katiba likaahirishwa hadi mwakani kupisha mambi mengine ya kitaifa ni uthibitisho kuwa wamejiandaa katika hili...
Ni kweli uyasemayo, sehemu ya V tutaeleza jinsi mkakati huo utakavyomuumiza Sitta personal na CCM kwa ujumla kama watatumia.
Ni silaha nzuri sana kama wapinzani wataibeba kwa uangalifu. Tutaendelea
 
Naunga mkono hoja ya Nguruvi3 kwamba sitta kusimamia mfumo wa serikali mbili kwa nia ya kuwa chaguo la CCM kama mgombea urais hakika hakutamsaidia. Hii ni kwa sababu hata wenzako wanaowania nafasi hiyo wana msimamo wa serikali mbili kwahiyo bado he won't stand out of the crowd; Busara kwake ni:

1. Kuunga mkono serikali tatu ambayo hata ndani ya ccm wamegawanyika, huku wale wa serikali tatu wakiwa ni viongozi wanaoheshimika ndani na nje ya chama (ukiachilia mbali wale ambao walikuwa ni wajumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba).

2. Kuunga mkono serikali tatu kwa vile agenda hiyo itasimamiwa na CUF na Chadema huko mbeleni na itakuwa ni moja ya vigezo vikubwa vya wananchi kupiga kura 2015. Kuwa mwana ccm anayesimamia upande wa wananchi (serikali tatu) is more a political asset to sitta than a liability.

Ajifunze huko nyuma jinsi gani wahusika walimgeuka. Hata mchakato wa ndani ya chama kupata mgombea urais 2015, Sitta ajue atageukwa dakika za mwisho. Ajue hilo. Kama kweli ana nia ya kuwa Rais 2015, asimamie upande wa wananchi (serikali tatu). Kwa kufanya hivyo, siasa za 2015 zitaweza hitaji mwana ccm mtetezi wa serikali tatu, na pia ataweza kuwa mtaji wa wapinzani iwapo atahamia chama kingine.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
SEHEMU YA V

SITTA NA KUHANGAIKA, SAFARI YA KISIASA IMEKWISHA

Tunafahamu mh Sitta alikuwa mwaanzilishi wa chama cha jamii (CCJ) baada ya kuona uwezekano wa kunyang'anywa kadi ya CCM ni mkubwa baada ya kukorofishana na wenzake wa mtandao.
Hata hivyo ilibidi apoozwe baada kuchaghuliwa kuwa waziri wa ushirikiano wa EAC.

Nafasi hiyo nayo kapwaya kwavile kumekuwa na matatizo mengi yasiyo na majibu hasa kuituhumu Tanzania ndani ya jumuiya pengine kutokana na uwakilishi hovyo wa Sitta na asivyoweza kutetea masilahi ya taifa.

Sitta kama waziri husika mara nyingi amekurupuka ima katika majibu yake au kusita kutoa ufafanuzi.Ndani ya EAC amekuwa akisisitiza demokrasia itumike si kwa wingi bali kwa hoja.

Inashangaza kuona akiwa ndani ya bunge la katiba demokrasia hiyo ameshindwa kuitumia.
Juzi kakubali iwepo kura ya wazi na siri kwa mbinu kama zile za kumwalika JK kuja kumshambulia na kumdhalilisha Warioba.

Jitihada za Sitta ni kuhakikisha anatimiza matakwa ya CCM ili aonekane kama mtu anayeweza kutoa na kusimamia maamuzi magumu ikiwemo mbinu za CCM za kila siku za kulaghai umma.

Sitta anachosahau ni kuwa ndani ya CCM ana makovu makubwa kutokana na majereha aliyosababisha kwa makundi mbali mbali akiwa Spika wa bunge hilo 2005-2010

1. Kundi la mtandao lenye mgombea wao anayepita makanisani na misikitini kwa udi na uvumba
2. Kundi linalomuona mtu aliyezuia jitihada za CCM kujisafisha kwa kufukia machafu akiwa Spika
3. Kundi linalomwona mnafiki, asiyeaminika na mwenye tabia za undumikuwili kama tunazoshuhudia

Katika bunge linaloendelea wapo wanaCCM wanaotaka ipatikane katiba ya wananchi kwa ajili ya nchi.Kundi hilo sasa limezimwa kwa kura ya wazi itakayolilazimisha lifanye hivyo kinyume na matakwa yao.

Ni kundi kubwa linalomuona Sitta kama kinara wa usaliti dhidi ya nchi na haliwezi kusimama naye siku za baadaye.

Sitta amebaki na kundi la wananchi lililompa heshima likidhani katika suala nyeti kama katiba, Sitta angeweza kurekebisha mapungufu yake ya siku za nyuma.
Hili nalo sasa limeshawishika bila kificho kuhusu unafiki na undumila kuwili wa Sitta.

Hivyo Sitta ameondoa uwezekano wa kuchaguliwa kubeba bendera ya chama kwa kutibua sehemu muhimu na nyeti zinazoweza kumpa fursa hiyo.

Sitta amepoteza heshima yake mbele ya jamii inayofuatilia bunge linaloendelea Dodoma kwa sasa.

CCM itatumia udhaifu uliopo Dodoma kuonyesha amepoteza mvuto na ushawishi tena katika jamii

Hiyo itakuwa njia rahisi sana kumweka pembeni kabla ya makundi hayatoa msimamo wao.

Kutokana na hali hiyo Sitta amehitimisha safari yake ya kisiasa.
Sitta hakubaliki tena ndani ya chama, kwa wananchi walioko upinzani waliompa benefit of doubt na jamii nzima kwa ujumla wake.

Upo uwezekano kuwa Sitta amekata tamaa ya kuwania Urais.
Anachokifanya sasa ni kumalizia muda wake wa kisiasa kwasababu hana cha kupoteza tena.

Laiti angelikuwa ana hofu na jambo lingine la badaye, Sitta asingeweza kusimama madudu na ujuha unaoendelea Dodoma.

Katika kutafuta jambo la kustaafu mh Sitta ameamua nafasi ya Uspika iwe ndiyo ya mwisho katika legacy yake.

Tatizo linaloonekana wazi ni bunge analoongoza lisimalizike kutokana na hali aliyojenga Sitta.

Wabunge watavutana na mwisho wa siku ni kuvunjika kwa bunge.
Sitta atabaki na wana CCM wenzake , maadui na mahasimu wake ndani ya CCM watatumia nafasi hiyo kummaliza kabisa.

Ndiyo maana tunasema Sitta hawezi kugombea tena nafasi katika nchi hii.
Amejimaliza kisiasa na atamalizwa muda si mrefu.

Kutokana na madudu yanayoendelea Dodoma chini ya usimamizi hafifu na hovyo wa Sitta usiozingatia utaifa au demokrasia leo Sitta akisimamishwa na Lowassa, Lowasa atamshinda licha ya makando kando ya ufisadi.

Hakuna jambo linalowatia wananchi maudhi kama utoto anaoendesha Sitta na jinsi alivyoamua kuwadharau wananchi.

Sitta anaonekana kinara wa mpango wa kumdhalilisha Warioba, Salim, Butiku, Augustino Ramadhani, prof Baregu, Prof Palamagamba na wasomi wengine.

Hili linamweka Sitta katika nafasi mbaya pengine kuliko ufisadi wa EL.
Hiyo haimaanishi EL ni mwema au ufisadi wake ni bora, kinachotokea ni kura ya chuki, kwamba huyu ni fisadi na mwingine ni mnafiki. Watalazimika kuchagua katia ya mashetani wawili 'between the two devils' na hapo Sitta hana lake.

Tumalizie kwa kusema nia ya bandiko hili ni kuwaondoa wananchi hofu waliokuwa nayo kwa Sitta.

Huko nyuma tuliwaonya wapinzani dhidi ya mtu huyu.
Ni mara nyingi tumeongelea kuhusu unafikia na undumila kuwili wake.

Tunashangaa wananchi wanapolalamila sasa hivi.
Huyo ndiye Samwel JohN Sitta, mzee mwenye sura mbili akijificha katika ngozi ya kondoo.

Tusemezane
 
Mkuu Nguvu nakubaliana na wewe lakini naona kama unashindwa kutazama picha kwa Uhalisia wake, kama utapata muda kuangaalia maandiko yangu kwa miaka takribani 7 niliyokuwa naandika humu nimekuwa nikisema kwamba Tanzania bado sana kufanya maamuzi. Nimekuwa nikisema kwamba maamuzi yanayotakiwa kufanyika kabla ya kuanza na haya ya katiba ni mapinduzi ya kifikra na kijamii social re-engineering.

Kikubwa lazima tukumbuke ya kwamba CCM ni chama chenye watu wenye ufahamu wa mfumo uliopo. CCM ni taasisi, na hakuna chama hata kimoja Tanzania narudia HATA kimoja chenye mfumo wa kitasisi zaidi ya CCM, hivyo kutokana na hilo CCM wana mkono ulio juu (upper hand). Na sababu wao wana ulewo wa mfumo ( not necessary knowledge of the current situation) inakuwa rahisi sana wao kuchakachua. Na kwa hili mimi siwalaumu CCM, ni mfumo wowote wa kichama, Obama na wafaidhina wenzie Democrat walipitisha bili ya Afya mwaka juzi, bila kujali kwamba itagharimi Marekani mabillioni ya dollar, lakini walipitisha bili hiyo saa sita usiku. This is how political party system works.

CCM walijua tangu mwanzo hili jambo litakwenda kwenye wire, hivyo walijipanga, wakijua fika bungeni wao wana uwiano mkubwa zaidi ya theluthi tatu, swala likawa kwenye hawa wabunge 201 wakuchagulia, lakini ukifanya uchambuzi wa harakaharaka ukiangalia Tanzania bara utaona mgawanyo ni 60% CCM na 40% wengine (Independent, CDM, CUF na kina mimi No Vote, No nothing). Hivyo kwenye kila watu 10, kuna watu 6 ambao wanavutiwa na CCM, hivyo kwenye wale wajumbe 201, kuna 121 ambao wanakuwa na CCM kutokana na itikadi bila hata CCM kuwaomba. Hivyo ukijumlisha hawa "wajumbe wa kuteuliwa" na CCM tayari utaona CCM wana 68% ya Bunge Zima, watakiwa kuiba wengine 20 or more kutimiza ahadi.

Ukiangalia kwa upande wa upinzani wao wameingia bungeni na 19% ya bunge lote, it is impossible wao kupata chochote wanachotetea, i mean ANYTHING. Ili wao washinde watatakiwa wapate wabunge wote 201 wa kuteuliwa Jumlisha 100 wa CCM.
This will never happened, tuna nafasi zaidi ya kumuona Yesu akirudi kuliko kuliona hili kutokea.

Mwisho wa siku Sitta atamaliza hili kwa kuonekana kwamba yeye ni hero ndani ya CCM, na CCM hawajali upinzani wanasema nini, wao wanajali kutekeleza ilani na katiba ya chama chao.
Nafahamu kuna wanaosema kwamba hili bunge ni chance kubwa sana ya kuvunjika, kusema kweli hiyo chance ya kufunjika ni ndogo sana. Sababu kama nilivyosema mwanzo CCM wameshakaa chini na wanafahamu kwamba namba zinawapendelea wao kuliko upinzani na wengine wote. Wabunge wa CCM kutoka ZNZ wataburuzwa tuu. Maaamuzi ya CCM ni kutoka kamati kuu, hata mkisema kura ziwe za siri, wana CCM wako royal sana na chama chao.
 
@Mtanganyika , niweke sawa kuwa suala la katiba si sera ya CCM na wala hawakushiriki kuanzisha mchakato. CCM wamedandia treni kwa mbele ndiyo maana wanahaingaka sana.

Pili, unaliangalia suala la namba kirahisi. Nipo katika rekodi nikawaonya wapinzani kuhusu juisi walizokunywa. Nilitahadharisha kuhusu CCM kutumia wingi wao.
Swali la kujiuliza, je katiba ni sawa na mswada wa bima ya afya?
Je kuna ushindani katika nyaraka ya taifa inayomuathiri kila mtu bila kujali itikadi zao?

Kuhusu namba, kitendo cha CCM kushinikiza na kuwaweka wabunge mahabusu kwa kura ya wazi ni ushahidi namba unayoisema haipatikani kidemokrasia.Jana, kamati zimeshindwa kupata 2/3 kwasasababu ya CCM. Ukifanya extrapolation utaona CCM bila kura ya wazi haiwezi kupata 2/3.

Kwamba, CCM ni taasisi kimfumo ni kweli, na ukweli kuwa upinzani haujawa kama taasisi vimechangia CCM kuonekana ni taasisi. Tumelizungumzia sana kuhusu udhaifu wa upinzani.
Laiti wangalikuwa makini pengine mchakato ungekuwa umechukua sura tofauti.

Kwa, mfano hakuna mbinu ya CCM waliokuwa haiwajui au kuisoma tukiwaeleza.
Tuliwaambia tume ya Warioba ni sehemu ya wajumbe, wakaridhia mswada baada ya kudanganywa kukutana na JK Juisi za mananasi ya kiwangwa, walipoondoka JK akasaini mswada uliopitishwa na wabunge 100.

Kuhusu Sitta, tuliwatahadharisha wapinzani kuwa historia inamsema vibaya.
Akachaguliwa kwa kishindo tena wapinzani wakishindwa kumuunga mkono mpinzani wa Sitta.

Sitta ana tatizo la kutaka kutumia bunge kwa masilahi binafsi. Anataka kuonyesha ndiye aliyeivusha nchi katika mchakato. Well, kuna sehemu mbili za shilingi.

CCM wanamtumia sana , wajanja wakiwa wamejificha. Sasa hivi Sitta anaonekana hovyo kwasababu ya kupokea maagizo bila kutumia busara za uzee wa miaka 71

Kamati zikichaguliwa alisimama na kusema kwa kiburi , ni demokrasia,wengi wape na hata kura ikipigwa CCM watashinda. Sitta amesahau kiti alichokalia si cha CCM ni cha Watanzania.
Kachagua kufurahisha watu 108 kwa gharama ya kupoteza watu milioni 35 ni kukosa busara.

Leo anarudi kuteua wapinzani kuingia katika kamati baada ya kung'amua kuna family feud na 2/3 haipatikani.Ni mtego ule uliomnasa J.J.Mnyika kwa kukubali kura ya wazi na ya siri.

Ndiyo kamba amemtupia Mbowe.
Hadi hapo utaona Sitta hana busara, ana kiburi, dharau, jeuri na kudhani ni mweledi sana.

Alitumia dharau kiburi na majivuno kusema lazima JK aje baada ya Warioba.
Akatumia vyombo vya usalama na kutisha watu. Kwa muda amefanikiwa, kwa kipindi kirefu amehitimisha safari yake kisiasa.

Hata ndani ya CCM hawakubalini na jinsi alivyosuka mipango ya kumdhalilisha Warioba, Salim, Butiku, maprofesa na wasomi. Matusi, dhihaka na kejeli zote anazotupiwa Warioba zina reflect kwa Sitta zaidi ya JK. Hapa alitangulizwa kama mbuzi wa kafara.

Kuvunjika kwa bunge kupo na kinachofanyika sasa hivi ni kuahirisha kwa sababu za kipuuzi.
Na upuuzi huo wa kuahirisha una reflect uwezo wa Sitta kuongoza mipango michafu ya CCM.
Hivi ina maana hawakujua kuna bunge la bajeti. Kwanini hakushauri bunge liahirishwe?

Jibu ni kuwa, alijua anaweza kuburuza wajumbe katiba ipitishwe kiubabe na kwa kiburi chake. Amegundua upinzani ndani ya CCM na anahitaji muda wa kuponya majeraha. Ataahirisha bunge.

Kuahirisha bunge hakujaondoa dhana ya kuvunjika.
Ngoja suala la mkataba,nchi au si nchi litakapozuka.

JK alikubali znz kuwa na mbadiliko ya katiba 2010, sasa hivi anamtupia zigo Sitta, na mzee huyu kwa upungufu wa busara atajikuta anabeba lawama zisizomhusu.

CCM kwa jinsi yoyote iwavyo wapo katika wakati mgumu, na Sitta anatumika kama chambo. Wajanja wenzake wanaowania 2015 wapo kimyaa.

Umeshamsikia EL au January Makamba. Wote wamejificha ili kulinda sura zao, Sitta kaamua kuhitimisha safari ya kisiasa na umri wa miaka 71. Hatakuwa kiongozi wa nchi hii tena baada ya JK

Sitta hafai, ni janga, aibu na fedheha nyingine inayokuja.
Keshatumiwa na CCM kama karatasi ya chooni, mwisho wake umetimia.
 
Mtanganyika,

Non-CCM walijua mchezo huu wakati wa kupitisha sheria lakini as you said CCM had the upper hand hivyo sheria ikapita na sasa, statistically, wana wajumbe wengi.

Lakini za mwizi arobaini, hitaji la 2/3 kwenye kupitisha vifungu inawarudisha kwenye ground zero. CUF na CCM zanzibar wako sawa. Yes Non-CCM hawawezi kupitisha vifungu lakini wana uwezo wa kukwamisha na kusambaratisha mambo.

Lakini mtihani mkubwa uko uraini Zanzibar. Hapa ndio CCM (kwa uelewa wangu) waliuziwa mbuzi kwenye gunia! Kati ya wana CCM Zanzibar wanaon-cooperate na CCM makao makuu hakuna hata mmoja mwenye ubavu wa kuzima moto uraiani.Hakuna.Watapayuka sana lakini mwisho wa siku watanyukwa vibaya na wananchi.

Kwa maoni yangu mchakato wote wa katiba mpya mwenye upper hand ni CUF Zanzibar.
 
Last edited by a moderator:
Mtanganyika,

Non-CCM walijua mchezo huu wakati wa kupitisha sheria lakini as you said CCM had the upper hand hivyo sheria ikapita na sasa, statistically, wana wajumbe wengi.

Lakini za mwizi arobaini, hitaji la 2/3 kwenye kupitisha vifungu inawarudisha kwenye ground zero. CUF na CCM zanzibar wako sawa. Yes Non-CCM hawawezi kupitisha vifungu lakini wana uwezo wa kukwamisha na kusambaratisha mambo.

Lakini mtihani mkubwa uko uraini Zanzibar. Hapa ndio CCM (kwa uelewa wangu) waliuziwa mbuzi kwenye gunia! Kati ya wana CCM Zanzibar wanaon-cooperate na CCM makao makuu hakuna hata mmoja mwenye ubavu wa kuzima moto uraiani.Hakuna.Watapayuka sana lakini mwisho wa siku watanyukwa vibaya na wananchi.

Kwa maoni yangu mchakato wote wa katiba mpya mwenye upper hand ni CUF Zanzibar.

Mkuu hata huko Zanzibar ni fact kwamba CCM wanajua kwamba kelele zitakuwepo for few days, watadeploy wanaume kutoka Tabora watakwenda huko na vibao vitatembea na mwisho wa siku kila mtu atabaki na mkewe chumbani. CCM wa Zanzibar au Tanzania Bara wanafanana, wanapenda madaraka na wanajua fika kabisa ukigeuza mkondo basi VX zinaamia kwa jirani. Ukweli CCM wamewakea mfukoni USA na EU (wapigaji kelele wa haki za binadamu) ambao wao wote wanataka muungano ubaki kama ulivyo kwa hofu zao kwamba Ukikatika tuu basi Vijana wenye mlengo wa kigaidi wataamia Visiwani. Na hii ni hofu na ujinga lakini ukweli upo palepale. Kwamba CCM wanafahamu kwamba karata zao ni madume na majike na Majokeli yote wanayo wao. Hivyo hili jambo la katiba kura za wazi za siri ni kutimiza hesabu na kusema mlitaka katiba mpya hii hapa na dunia imeona.

Mkuu jee unadhani Sitta alipogawa kamati ameweka CUF na CCM Zanzibar katika uwiano wa 50-50? I doubt, atakuwa ameweka hisabati zake akijua kamati 6 au zaidi zina ratio kubwa, then kama mbili zina chache, mwisho wa siku ukichanganya zote unakuta wao wapo juu. Hizi karata hata usichangenyeje hapati mtu dume, kwani CCM wametoa madume yote.
 
Mkuu hata huko Zanzibar ni fact kwamba CCM wanajua kwamba kelele zitakuwepo for few days, watadeploy wanaume kutoka Tabora watakwenda huko na vibao vitatembea na mwisho wa siku kila mtu atabaki na mkewe chumbani. CCM wa Zanzibar au Tanzania Bara wanafanana, wanapenda madaraka na wanajua fika kabisa ukigeuza mkondo basi VX zinaamia kwa jirani. Ukweli CCM wamewakea mfukoni USA na EU (wapigaji kelele wa haki za binadamu) ambao wao wote wanataka muungano ubaki kama ulivyo kwa hofu zao kwamba Ukikatika tuu basi Vijana wenye mlengo wa kigaidi wataamia Visiwani. Na hii ni hofu na ujinga lakini ukweli upo palepale. Kwamba CCM wanafahamu kwamba karata zao ni madume na majike na Majokeli yote wanayo wao. Hivyo hili jambo la katiba kura za wazi za siri ni kutimiza hesabu na kusema mlitaka katiba mpya hii hapa na dunia imeona.

Kwenye USA, EU etc uko sahihi maana hata press release ya No 10 juzi kuhusu maongezi ya Cameroon na mkulu walitaja "hatari ya kuongezeka kwa extremists!'

Kuhusu kubwaga vijana toka Tabora itakuwa kosa of historical proportion. CNN wataweza kutupa counts! Unajua success waliyokuwa wanapata vijana wa Tabora huko nyuma ilitokana na 'ushirikiano'. Sasa hakuna kitu cha namna hiyo, sasa hivi ni Zanzibar kwanza.

Na moja ya mapungufu ya Muungano wa sasa (sio ule wa Nyerere) ni kutofahamiana kati ya ccm Zanzibar na Bara. and post 2010 mambo ni mabaya zaidi.

Sitta alichaniwa makaratasi Bwawani, na kama angekuwa ni mtu wa kuona mbele angewaongoza ccm wenzake huko Dodoma ili waachane na 'cosmetic' thinking. So far ccm wanacheza mkanda ule ule wa zamani. kosa.
 
Kwenye USA, EU etc uko sahihi maana hata press release ya No 10 juzi kuhusu maongezi ya Cameroon na mkulu walitaja "hatari ya kuongezeka kwa extremists!'

Kuhusu kubwaga vijana toka Tabora itakuwa kosa of historical proportion. CNN wataweza kutupa counts! Unajua success waliyokuwa wanapata vijana wa Tabora huko nyuma ilitokana na 'ushirikiano'. Sasa hakuna kitu cha namna hiyo, sasa hivi ni Zanzibar kwanza.

Na moja ya mapungufu ya Muungano wa sasa (sio ule wa Nyerere) ni kutofahamiana kati ya ccm Zanzibar na Bara. and post 2010 mambo ni mabaya zaidi.

Sitta alichaniwa makaratasi Bwawani, na kama angekuwa ni mtu wa kuona mbele angewaongoza ccm wenzake huko Dodoma ili waachane na 'cosmetic' thinking. So far ccm wanacheza mkanda ule ule wa zamani. kosa.

CNN au BBC ni walewale kaka, yaani kama kuna jambo ambalo Wazanzibar watakosea ni kulianzisha, kwani watachapwa na hakuna atake ingilia. Ndio maana nimewai kusema Zanzibar hawana strategic, politicaal, economical au geographic advantage kwenye hili. Wanapigana mikono yao ikiwa imefungwa nyuma, kusema kwamba watoe macho hilo litafanyika kwa week tuu kama Mtwara, leo bomba la gesi lipo Kinyerezi.

Advantage ya CCM ni kwamba wanao wapa mkono ndio vilanja wa dunia and that is sad fact.
 
CNN au BBC ni walewale kaka, yaani kama kuna jambo ambalo Wazanzibar watakosea ni kulianzisha, kwani watachapwa na hakuna atake ingilia. Ndio maana nimewai kusema Zanzibar hawana strategic, politicaal, economical au geographic advantage kwenye hili. Wanapigana mikono yao ikiwa imefungwa nyuma, kusema kwamba watoe macho hilo litafanyika kwa week tuu kama Mtwara, leo bomba la gesi lipo Kinyerezi.

Advantage ya CCM ni kwamba wanao wapa mkono ndio vilanja wa dunia and that is sad fact.

Theoretically, ningeweza kusema uko sahihi. Ungovernable ndicho naweza kusema kwa sasa. plus vijana wa Tabora watakaa for how long?
 
FJM,

Sijui kwanini unapoteza muda kujadiliana na Mtanganyika wakati kimsingi yupo upande wako wa hoja. Mnapopishana ni kwamba "mlinzi wa kweli wa muuungano ni vifaru na mizinga, sio wananchi". Vinginevyo ukimsoma, anakiri kwamba umma wa zanzibar na Tanganyika una kiu kubwa sana ya Tanganyika. Sasa kujadiliana na mtu wa aina hii inakuwa haina maana, ingekuwa na maana pale tu angekuwa anasema kwamba wananchi hawataki Tanganyika, huku yeye na makada wenzake ndani ya chama wakiachia mchakato uwe fair and transparent to prove that.

Hawa watu wanaweweseka, serikali tatu itawaathiri sana kimadaraka na vibaraka wao waliopo ambao hawapo tu CCM bali Chadema. Tunavyozungumza, they are indecisive kuhusu kugombea urais wa Tanganyika au Muungano, na nilishamwambia Mtanganyika kwenye mjadala wetu ule wa gharama za muungano, kwanini serikali tatu inawapa wakati mgumu sana. Hawana nia yoyote njema kwa wananchi, ni madaraka yao tu ndio yanawasumbua kwani yatayumbishwa sana na serikali tatu. Isitoshe, serikali tatu inapeleka madaraka karibu zaidi na wananchi kuliko serikali mbili. Wao wanataka madaraka yakae mbali kabisa na wananchi, hata ikibidi wayazuie na vifaru na mizinga.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom