Kwa lipi na kwanini Samwel J. Sitta aaminiwe?

Kwa lipi na kwanini Samwel J. Sitta aaminiwe?

FJM,

Sijui kwanini unapoteza muda kujadiliana na Mtanganyika wakati kimsingi yupo upande wako wa hoja. Mnapopishana ni kwamba "mlinzi wa kweli wa muuungano ni vifaru na mizinga, sio wananchi". Vinginevyo ukimsoma, anakiri kwamba umma wa zanzibar na Tanganyika una kiu kubwa sana ya Tanganyika. Sasa kujadiliana na mtu wa aina hii inakuwa haina maana, ingekuwa na maana pale tu angekuwa anasema kwamba wananchi hawataki Tanganyika, huku yeye na makada wenzake ndani ya chama wakiachia mchakato uwe fair and transparent to prove that.

Hawa watu wanaweweseka, serikali tatu itawaathiri sana kimadaraka na vibaraka wao waliopo ambao hawapo tu CCM bali Chadema. Tunavyozungumza, they are indecisive kuhusu kugombea urais wa Tanganyika au Muungano, na nilishamwambia Mtanganyika kwenye mjadala wetu ule wa gharama za muungano, kwanini serikali tatu inawapa wakati mgumu sana. Hawana nia yoyote njema kwa wananchi, ni madaraka yao tu ndio yanawasumbua kwani yatayumbishwa sana na serikali tatu. Isitoshe, serikali tatu inapeleka madaraka karibu zaidi na wananchi kuliko serikali mbili. Wao wanataka madaraka yakae mbali kabisa na wananchi, hata ikibidi wayazuie na vifaru na mizinga.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mchambuzi mimi nadhani nitakuwa wa mwisho kuchukua kadi ya CCM baada ya Mboe kuchukua then mimi, mimi naangalia uhalisia na najikita kwenye kusoma wakati. Nadhani kufanya dhana kwamba tutaona serikali ya tatu, hilo jambo nadhani halina nafasi katika bunge hili. Hivyo mimi mpenda serikali moja tuu ama ya Tanganyika au Tanzania siwezi kupata ninachokitaka na Wewe, Warioba na wengine wapenda serikali tatu sidhani kama hilo litawezekana kwa sasa, labda 2015 "Labda". Hivyo, wote tupo kwenye boti moja.

Nimefanya mchanganuo kwenye post moja hapo awali kwamba CCM ni asilimia 48% ya Bunge, Upinzania ni 18% na hawa "undecided" ambao wamechaguliwa na CCM ni 35%. Ili hoja ya Tanganyika ipite inabidi upate 100% of undecided, 100% of Upinzani na 41% ya CCM. Umeona hapa jinsi tunavyotofautiana kwenye kuelewa uhalisia? Kuwapata CCM hata 10% inabidi usukume ardhi na mbingu, na hii ni sababu ya strategic advantage ambayo CCM wanayo. Ndio maana kwenye mandiko yangu nikasema kama mchezo ni Last Card, basi CCM wana majoka yote manne. Lakini ili CCM washinde na idea zao wanatakiwa kupata wabunge 130 tuu kutoka kwenye hawa undecided. Na ukitazama muundo wa Tanzania 60% ya wananchi wanaelemea CCM. Hivyo technical CCM inatakiwa kubadili mioyo ya wabunge 20 tuu kwenye wale undecided.

Mimi nadhani hapa umegeuza script kuhusu wanaotaka Tanganyika na serikali mbili zaidi hao ndio wapenda madaraka. Kaka kama unadhani kwamba tukiongeza Tanganyika basi ndio tutaondoa CCM kwenye madaraka basi nadhani kweli tunatofautiana imani. Ukiwapa CCM Tanganyika watachukua na kuongoza, wataweka bunge la watu 300 (sababu wao ndio wataandika Katiba ya Tanganyika), Wataongoza muungano sababu wao ndio majority na watajaza watoto wao kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Ni ukweli usio fichika kwamba kama miujiza ikatokea Tanganyika ikazaliwa basi ni walewale watakao ongoza Tanzania Muungano na Tanganyika, ila sasa wataweka watu wao kwenye either Tanzania au Tanganyika. Lakini, ukiacha hayo yote kwa nini tupoteze muda kuanzisha kitu ambacho mimi na wewe wote tunajua kitakufa? Wazanzibar watakuja na kusema wanachangia serikali ya tatu lakini hawawezi kupata raisi sababu ya population, hivyo watataka kujitoa moja kwa moja. why waste time?
Ndio maana mimi nasema bora tulirudie hili jambo wakati wananchi wa Tanzania wakiwa na ufahamu.
 
FJM,

Sijui kwanini unapoteza muda kujadiliana na Mtanganyika wakati kimsingi yupo upande wako wa hoja. Mnapopishana ni kwamba "mlinzi wa kweli wa muuungano ni vifaru na mizinga, sio wananchi". Vinginevyo ukimsoma, anakiri kwamba umma wa zanzibar na Tanganyika una kiu kubwa sana ya Tanganyika. Sasa kujadiliana na mtu wa aina hii inakuwa haina maana, ingekuwa na maana pale tu angekuwa anasema kwamba wananchi hawataki Tanganyika, huku yeye na makada wenzake ndani ya chama wakiachia mchakato uwe fair and transparent to prove that.

Hawa watu wanaweweseka, serikali tatu itawaathiri sana kimadaraka na vibaraka wao waliopo ambao hawapo tu CCM bali Chadema. Tunavyozungumza, they are indecisive kuhusu kugombea urais wa Tanganyika au Muungano, na nilishamwambia Mtanganyika kwenye mjadala wetu ule wa gharama za muungano, kwanini serikali tatu inawapa wakati mgumu sana. Hawana nia yoyote njema kwa wananchi, ni madaraka yao tu ndio yanawasumbua kwani yatayumbishwa sana na serikali tatu. Isitoshe, serikali tatu inapeleka madaraka karibu zaidi na wananchi kuliko serikali mbili. Wao wanataka madaraka yakae mbali kabisa na wananchi, hata ikibidi wayazuie na vifaru na mizinga.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mchambuzi

Siku moja baada Jaji Warioba kuwasilisha report bungeni, niliongea na MCCM mmoja huko Dodoma na ilibidi nichecke jibu la swali langu. Alisema "we are totally confused". Nadhani hiyo confession tumeiona jinsi walivyoitupia tume virago!
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi mimi nadhani nitakuwa wa mwisho kuchukua kadi ya CCM baada ya Mboe kuchukua then mimi, mimi naangalia uhalisia na najikita kwenye kusoma wakati. Nadhani kufanya dhana kwamba tutaona serikali ya tatu, hilo jambo nadhani halina nafasi katika bunge hili. Hivyo mimi mpenda serikali moja tuu ama ya Tanganyika au Tanzania siwezi kupata ninachokitaka na Wewe, Warioba na wengine wapenda serikali tatu sidhani kama hilo litawezekana kwa sasa, labda 2015 "Labda". Hivyo, wote tupo kwenye boti moja.

Hadidi za rejea zilisema nini kwa tume juu ya muungano? ULINDWE na UBORESHWE.
Ebu tuelezee hilo linafanyika vipi in practice (serikali mbili au moja).

Nimefanya mchanganuo kwenye post moja hapo awali kwamba CCM ni asilimia 48% ya Bunge, Upinzania ni 18% na hawa "undecided" ambao wamechaguliwa na CCM ni 35%. Ili hoja ya Tanganyika ipite inabidi upate 100% of undecided, 100% of Upinzani na 41% ya CCM. Umeona hapa jinsi tunavyotofautiana kwenye kuelewa uhalisia? Kuwapata CCM hata 10% inabidi usukume ardhi na mbingu, na hii ni sababu ya strategic advantage ambayo CCM wanayo. Ndio maana kwenye mandiko yangu nikasema kama mchezo ni Last Card, basi CCM wana majoka yote manne. Lakini ili CCM washinde na idea zao wanatakiwa kupata wabunge 130 tuu kutoka kwenye hawa undecided. Na ukitazama muundo wa Tanzania 60% ya wananchi wanaelemea CCM. Hivyo technical CCM inatakiwa kubadili mioyo ya wabunge 20 tuu kwenye wale undecided.

Ndio maana nimemwambia FJM kwamba kimsingi, unaelewa nguvu ya hoja ya Tanganyika kwenye umma wa Tanzania Bara na Zanzibar. Tunachotofautiana ni kwamba CCM wataizima hoja kwa wingi wao, tena sio wa kujiamini au hiyari bali kutishana kupitia kura ya wazi;pili, mfumo utalindwa na vifaru kwa vile sio matakwa ya wananchi; kitendo cha rais kutishia umma na vifaru maana yake ni kwamba bila ya kutishia umma, ccm itaumbuka kura ya maoni. That's the bottom line;

Mimi nadhani hapa umegeuza script kuhusu wanaotaka Tanganyika na serikali mbili zaidi hao ndio wapenda madaraka.

Nilikueleza kwenye uzi wa gharama za muungano kwanini serikali tatu inawapa shida wanaotaka urais 2015; haukujibu; na hizi ni taarifa za ndani ambazo nimezipata;hakuna nia ya dhati kwa wananchi bali madaraka;kugombea urais wa Tanganyika hautakuwa na maslahi muhimu, kugombea wa muungano pia hauutakuwa na maslahi muhimu - kwa wapenda madaraka na assets zinazokuja na imperial presidency;nilikueleza kule kwa undani, kazisome ukipata muda;

Kaka kama unadhani kwamba tukiongeza Tanganyika basi ndio tutaondoa CCM kwenye madaraka basi nadhani kweli tunatofautiana imani.

Hakuna sehemu nimesema tuitoe ccm kwa utanganyika. Usikwepe hoja; mkataba wa muungano haukutaja vyama vya siasa, TANU na baadae CCM ikaja kuteka mchakato mzima na ndio maaa tupo kwenye mgogoro;hata mwalimu alikiri hilo kiaina baada ya kugundua kwamba suala la makamu wa rais kutoka znz litaleta tatizo, ndio maana ikaja idea ya mgombea mwenza;

Kwa kifupi, CCM ilikuwa na fursa ya kumalizana na jinazimi la Tanganyika for good iwapo JK ange stick na uamuzi wake wa kuanzisha mchakato wa katiba huku akisema kwa mfano makosa ya kihistoria yanaeleweka, tuyasamehe etc etc na tungekuja na hoja nzuri tu za kusamehe ili mradi nia ni kuanza upya na kurekebisha uchakachuaji wa historia;umma ungeiunga mkono ccm kwa nguvu sana; instead, ccm inalazimisha kwamba kilichotokea katika historia ni halali hata kisheria na kidemokrasia, and it shouldn't be questioned;in other words, our union was God Ordained!

Wewe sio mwana ccm, fine, mimi ni mwana ccm;nachotamani ni wazee walioharibu historia wairekebishe ile watuachie chama na muungano usio na migogoro; mimi shida yangu ni hiyo tu;
Tunataka tuje shindana na upinzani kwa hoja nyingine ambazo zinajadilika pande zote mbili;sio hili la mfumo wa muungano;wazee wanatuachia mgogoro mkubwa sana wakijiandaa kustaafu kwa kukataa mfumo wa serikali tatu ndani ya muungano wa nchi moja kiasi kwamba wazanzibari nao wameleta nchi yao, yote ni kwa sababu ya kiburi cha CCM;rejea sakata la jumbe na tume za kina kisanga, nyalali etc;
Ukiwapa CCM Tanganyika watachukua na kuongoza, wataweka bunge la watu 300 (sababu wao ndio wataandika Katiba ya Tanganyika), Wataongoza muungano sababu wao ndio majority na watajaza watoto wao kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Ni ukweli usio fichika kwamba kama miujiza ikatokea Tanganyika ikazaliwa basi ni walewale watakao ongoza Tanzania Muungano na Tanganyika, ila sasa wataweka watu wao kwenye either Tanzania au Tanganyika.
Sasa kama ni hivyo, kwanini ccm inahangaika kuingilia mchakato wa katiba mpya kama kweli inajiamini?

Lakini ukiacha hayo yote kwa nini tupoteze muda kuanzisha kitu ambacho mimi na wewe wote tunajua kitakufa? Wazanzibar watakuja na kusema wanachangia serikali ya tatu lakini hawawezi kupata raisi sababu ya population, hivyo watataka kujitoa moja kwa moja. why waste time?

Umekimbia mjadala wetu ule wa gharama, rudi ujibu hoja zangu kule kwani majibu yapo kule;

Ndio maana mimi nasema bora tulirudie hili jambo wakati wananchi wa Tanzania wakiwa na ufahamu.

Kwa hiyo waliotoa maoni kwa tume juu ya serikali tatu walikuwa hawana ufahamu? Tafadhali jadili ufahamu kwa wananchi wa znz na wale wa Tanzania, kwamba wanahitaji ufahamu upi zaidi; ule wa ccm kusema wataleta baraza la wawakilishi la Tanzania bara ili pawe na mabunge matatu, serikali mbili? Kwa hili tu, hivyo sivyo walivyofundishwa kwenye civics sekondari kuhusu mihimili mikuu ya dola;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi

Siku moja baada Jaji Warioba kuwasilisha report bungeni, niliongea na MCCM mmoja huko Dodoma na ilibidi nichecke jibu la swali langu. Alisema "we are totally confused". Nadhani hiyo confession tumeiona jinsi walivyoitupia tume virago!
Huyo aliyesema hayo alijua kwanini wapo confused. Si umesikia serikali na Ikulu zimepeleka mkataba feki ulioghushiwa? Hapo kweli si confusion!

Kila mtu anasema lake kuhusu mkataba wa muungano. Wapo wanaosema upo New York, wengine wanasema Moscow, na baadhi kusema ulizama wakati unavushwa kwenda znz. Confusion haiishi hapo wapo wanaoamini mkataba ni furushi kubwa sana linahitaji kontena kulipleka Dodoma. Wengine wanasema unahitaji askari 1000 kulindwa na hakuna pesa za kuwalipa kuupeka Dodoma. Kwanini wasiwe confused.
 
Hadidi za rejea zilisema nini kwa tume juu ya muungano? ULINDWE na UBORESHWE.
Ebu tuelezee hilo linafanyika vipi in practice (serikali mbili au moja).

Mkuu hili tulishalichambua kwamba sawa Jaji Warioba alikusanya maoni ya Watanzania akaja na hoja muungano Ulindwe na Kuboreshwa, alichokosea yeye ni kuangalia uhalisia wa hoja hiyo. Mimi nitakwenda kaburini nikiamini kwamba tunaweza kuuboresha muungano huu kwenda kwenye serikali moja na kuipa Zanzibar identity yake. Nafahamu kwa sasa wengi tumeweka wazo kwamba 1+1=3. Tatizo linalosababisha tushindwe kuboresha hizi mbili tulizo nazo ( for disclosure nina support mbili kuliko tatu only sababu ya gharama) ni kushindwa kwa viongozi wetu kufikiria nje ya box na kufanya maamuzi magumu. Ukweli ni kwamba kilichotakiwa ni kuweka pande zote 3 za Zanzibar, najua utadhani nimekosea kusema pande tatu, lakini ukweli ni kwamba Zanzibar kuna Muungano wa Mkataba supporter, Muungano wa Serikali 3 na Muungano wa Serikali 2. Kilichotakiwa ni kukaa na pande hizi zote na kufunga chumba na kusema kwamba hapa tuta jadili mpaka kupata ufumbizi ambao wote tutaukubali.

[/QUOTE] Ndio maana nimemwambia FJM kwamba kimsingi, unaelewa nguvu ya hoja ya Tanganyika kwenye umma wa Tanzania Bara na Zanzibar. Tunachotofautiana ni kwamba CCM wataizima hoja kwa wingi wao, tena sio wa kujiamini au hiyari bali kutishana kupitia kura ya wazi;pili, mfumo utalindwa na vifaru kwa vile sio matakwa ya wananchi; kitendo cha rais kutishia umma na vifaru maana yake ni kwamba bila ya kutishia umma, ccm itaumbuka kura ya maoni. That's the bottom line;. [/QUOTE]

Mkuu kama kweli Watanzania Bara wengi wanataka Tanganyika basi tungeona msukumo huo kwenye michakato ya kampeni zinazoendelea za viti vya ubunge na udiwani kwamba CCM walitakiwa waadhibiwe kwa kuto sikiliza maoni ya Wananchi, lakini unaona trend inaonyesha kwamba bado Watanzania Bara wanaikumbatia CCM, na Kinana anajaza watu mpaka wanakosa pakusimama japokuwa ni CCM hiyohiyo inawasababishia watoto wao wasiende shule. Hii hoja ya Tanganyika ipo kwenye mitandao, magazeti na blogs, Mtanzania wakawaida sasa hivi anawaza atampelekaje Selemeni Form One wakati pesa ya ada hana, anawaza jee atavuna Heka yake mmoja ya Mpunga na Mvua hizi za masika? Mtanzania wa Bara akili yake haipo kwenye serikali ya tatu au ya nne. Anawaza jee ataweza kuyakabili maisha?

Nilikueleza kwenye uzi wa gharama za muungano kwanini serikali tatu inawapa shida wanaotaka urais 2015; haukujibu; na hizi ni taarifa za ndani ambazo nimezipata;hakuna nia ya dhati kwa wananchi bali madaraka;kugombea urais wa Tanganyika hautakuwa na maslahi muhimu, kugombea wa muungano pia hauutakuwa na maslahi muhimu - kwa wapenda madaraka na assets zinazokuja na imperial presidency;nilikueleza kule kwa undani, kazisome ukipata muda;

Mchambuzi, anaekwambia kwamba CCM wanaumiza kichwa kwamba serikali ya tatu itawasumbua kutoa raisi anachanganya dawa tuu. Ukweli ni kwamba kama tutaanzisha Tanganyika mwezi ujao, basi kwenye hiyo mitandao ya CCM watatoa raisi wa Tanganyika na Watanzania. Hii sio theoretically ni facts, sababu kwanza CCM wana more resources kushinda chama chochote, wana watu wakutosha, na wanaweza kucheza uwanja mzima dakika 90 peke yao. Leo mkianzisha Tanganyika na Tanzania basi jua Chadema hawana resources za kufanya kampeni ya nafasi zote mbili ni CCM peke yake mwenye hizo resources. Hivyo kusema kwamba CCM wanaumiza kichwa kwa 2015, labda kujua kwamba ni mtandao gani utachukua serikali zote mbili.

Hakuna sehemu nimesema tuitoe ccm kwa utanganyika. Usikwepe hoja; mkataba wa muungano haukutaja vyama vya siasa, TANU na baadae CCM ikaja kuteka mchakato mzima na ndio maaa tupo kwenye mgogoro;hata mwalimu alikiri hilo kiaina baada ya kugundua kwamba suala la makamu wa rais kutoka znz litaleta tatizo, ndio maana ikaja idea ya mgombea mwenza;

Kwa kifupi, CCM ilikuwa na fursa ya kumalizana na jinazimi la Tanganyika for good iwapo JK ange stick na uamuzi wake wa kuanzisha mchakato wa katiba huku akisema kwa mfano makosa ya kihistoria yanaeleweka, tuyasamehe etc etc na tungekuja na hoja nzuri tu za kusamehe ili mradi nia ni kuanza upya na kurekebisha uchakachuaji wa historia;umma ungeiunga mkono ccm kwa nguvu sana; instead, ccm inalazimisha kwamba kilichotokea katika historia ni halali hata kisheria na kidemokrasia, and it shouldn't be questioned;in other words, our union was God Ordained!

Mkuu lazima ukumbuke kwamba mzizi wa muungano huu umejikita zaidi ya CCM kushinda sehemu yoyote ile, sababu ya historia. Ni TANU na ASP ambao walikuja na mchakato wa Muungano, kipindi hicho hawakuwaza wala kufikiri kwamba kuna siku kutakuwa na vyama vingine ambavyo vitakuwa na wazo mbadala. Hivyo Muungano ni core thread inayonganisha CCM na niukweli usiofichika CCM will never abandoned mfumo huo sababu Mzimu wa Mwalimu bado uko hai ndani ya CCM. Na kwa sasa sababu CCM wao ndio majority hivyo hili lipo upande wao.

Sasa kama ni hivyo, kwanini ccm inahangaika kuingilia mchakato wa katiba mpya kama kweli inajiamini?

Utakumbuka kwa mara ya kwanza katika historia CCM waliadhibiwa mwaka 2010, japokuwa walishinda bunge kwa asilimia zaidi ya 75% lakini kwa wao ili ilikuwa simu ya kuwaamsha. CDM walianza kupiga mayoe ya katiba mpya, na JK na wenzie waliichukua na kusema hiyo niya kwao. Lakini jee unadhani kweli kabisa CCM wanataka kutoa katiba ambayo ina Ridhiwani na Juma Kajole nafasi moja? Unadhani kabisa watatengeneza katiba ya kusababisha siku moja VX ziendeshwe na jirani? Hilo halikuwepo ni against the nature of human.

Mwisho nimeshasema kwamba elimu ya uraia ya Watanzania wengi wa kizazi hichi cha yeboyebo imepunga wengi wapo busy kwenye BBM na whatsapp. Na wazee walio wengi wao wanaza kujiongezea mali. Hivyo ni wachache sana wenye uweleo wa jinsi serikali ya aina yoyote inavyofanya kazi, achilia hiyo ya tatu.

Kuhusu Zanzibar nimesema huko nyuma wengi hawajui tofauti ye mchele na chuya, wao wanafuata upepo tuu. Msukumo mkubwa unatoka kwa Afrabia ambao wapo Oman, Dubai, Yemen, Canada na UK. Hawa kama kina Harith Ghassany wamekuwa wakisukuma swala la kwamba Zanzibar yetu imeporwa mwaka 1964. Lakini ukweli ni kwamba watu hawa wana chuki na mapinduzi, na wanatumia kila njia kuhakikisha kwamba muungano unapasuka na wao wanarudi Zanzibar. Kelele za kina Sheikh Fareed na Uhamsho zote zinatokana na fedha inayotoka nje ya Zanzibar. Na hapa ndio nikasema kwamba USA na EU hawawezi hata siku moja kuacha Tanzania ipasuke, ndio nikawambia CCM wataleta watu kutoka Tabora ambao wataongeza nguvu.

Mimi nimejikita zaidi kwenye uhalisia. Kwa sasa tukubali kabisa hakuna jipya kutoka Dodoma. Labda CCM waamue.
kuhusu kura, kaka wana CCM wako royal sana na chama chao, wewe ni kada wa kwanza kukuona unakuja kwenye majukwaa na kuupinga mfumo huu. Lakini wenzio wote wameshikwa pabaya mfano hali ni Mzee Sitta na Wawakilishi kutoka Zanzibar ambao uliona Pindu alivyomkana Warioba mchana kweupe. Siwapendi CCM lakini nawakubali jinsi wanavyoweza kuendesha agenda.
 
Mkuu hili tulishalichambua kwamba sawa Jaji Warioba alikusanya maoni ya Watanzania akaja na hoja muungano Ulindwe na Kuboreshwa, alichokosea yeye ni kuangalia uhalisia wa hoja hiyo. Mimi nitakwenda kaburini nikiamini kwamba tunaweza kuuboresha muungano huu kwenda kwenye serikali moja na kuipa Zanzibar identity yake. Nafahamu kwa sasa wengi tumeweka wazo kwamba 1+1=3. Tatizo linalosababisha tushindwe kuboresha hizi mbili tulizo nazo ( for disclosure nina support mbili kuliko tatu only sababu ya gharama) ni kushindwa kwa viongozi wetu kufikiria nje ya box na kufanya maamuzi magumu. Ukweli ni kwamba kilichotakiwa ni kuweka pande zote 3 za Zanzibar, najua utadhani nimekosea kusema pande tatu, lakini ukweli ni kwamba Zanzibar kuna Muungano wa Mkataba supporter, Muungano wa Serikali 3 na Muungano wa Serikali 2. Kilichotakiwa ni kukaa na pande hizi zote na kufunga chumba na kusema kwamba hapa tuta jadili mpaka kupata ufumbizi ambao wote tutaukubali.
Ndio maana nimemwambia FJM kwamba kimsingi, unaelewa nguvu ya hoja ya Tanganyika kwenye umma wa Tanzania Bara na Zanzibar. Tunachotofautiana ni kwamba CCM wataizima hoja kwa wingi wao, tena sio wa kujiamini au hiyari bali kutishana kupitia kura ya wazi;pili, mfumo utalindwa na vifaru kwa vile sio matakwa ya wananchi; kitendo cha rais kutishia umma na vifaru maana yake ni kwamba bila ya kutishia umma, ccm itaumbuka kura ya maoni. That's the bottom line;.
Mkuu kama kweli Watanzania Bara wengi wanataka Tanganyika basi tungeona msukumo huo kwenye michakato ya kampeni zinazoendelea za viti vya ubunge na udiwani kwamba CCM walitakiwa waadhibiwe kwa kuto sikiliza maoni ya Wananchi, lakini unaona trend inaonyesha kwamba bado Watanzania Bara wanaikumbatia CCM, na Kinana anajaza watu mpaka wanakosa pakusimama japokuwa ni CCM hiyohiyo inawasababishia watoto wao wasiende shule. Hii hoja ya Tanganyika ipo kwenye mitandao, magazeti na blogs, Mtanzania wakawaida sasa hivi anawaza atampelekaje Selemeni Form One wakati pesa ya ada hana, anawaza jee atavuna Heka yake mmoja ya Mpunga na Mvua hizi za masika? Mtanzania wa Bara akili yake haipo kwenye serikali ya tatu au ya nne. Anawaza jee ataweza kuyakabili maisha?

Mchambuzi, anaekwambia kwamba CCM wanaumiza kichwa kwamba serikali ya tatu itawasumbua kutoa raisi anachanganya dawa tuu. Ukweli ni kwamba kama tutaanzisha Tanganyika mwezi ujao, basi kwenye hiyo mitandao ya CCM watatoa raisi wa Tanganyika na Watanzania. Hii sio theoretically ni facts, sababu kwanza CCM wana more resources kushinda chama chochote, wana watu wakutosha, na wanaweza kucheza uwanja mzima dakika 90 peke yao. Leo mkianzisha Tanganyika na Tanzania basi jua Chadema hawana resources za kufanya kampeni ya nafasi zote mbili ni CCM peke yake mwenye hizo resources. Hivyo kusema kwamba CCM wanaumiza kichwa kwa 2015, labda kujua kwamba ni mtandao gani utachukua serikali zote mbili.

Mkuu lazima ukumbuke kwamba mzizi wa muungano huu umejikita zaidi ya CCM kushinda sehemu yoyote ile, sababu ya historia. Ni TANU na ASP ambao walikuja na mchakato wa Muungano, kipindi hicho hawakuwaza wala kufikiri kwamba kuna siku kutakuwa na vyama vingine ambavyo vitakuwa na wazo mbadala. Hivyo Muungano ni core thread inayonganisha CCM na niukweli usiofichika CCM will never abandoned mfumo huo sababu Mzimu wa Mwalimu bado uko hai ndani ya CCM. Na kwa sasa sababu CCM wao ndio majority hivyo hili lipo upande wao.

Utakumbuka kwa mara ya kwanza katika historia CCM waliadhibiwa mwaka 2010, japokuwa walishinda bunge kwa asilimia zaidi ya 75% lakini kwa wao ili ilikuwa simu ya kuwaamsha. CDM walianza kupiga mayoe ya katiba mpya, na JK na wenzie waliichukua na kusema hiyo niya kwao. Lakini jee unadhani kweli kabisa CCM wanataka kutoa katiba ambayo ina Ridhiwani na Juma Kajole nafasi moja? Unadhani kabisa watatengeneza katiba ya kusababisha siku moja VX ziendeshwe na jirani? Hilo halikuwepo ni against the nature of human.

Mwisho nimeshasema kwamba elimu ya uraia ya Watanzania wengi wa kizazi hichi cha yeboyebo imepunga wengi wapo busy kwenye BBM na whatsapp. Na wazee walio wengi wao wanaza kujiongezea mali. Hivyo ni wachache sana wenye uweleo wa jinsi serikali ya aina yoyote inavyofanya kazi, achilia hiyo ya tatu.

Kuhusu Zanzibar nimesema huko nyuma wengi hawajui tofauti ye mchele na chuya, wao wanafuata upepo tuu. Msukumo mkubwa unatoka kwa Afrabia ambao wapo Oman, Dubai, Yemen, Canada na UK. Hawa kama kina Harith Ghassany wamekuwa wakisukuma swala la kwamba Zanzibar yetu imeporwa mwaka 1964. Lakini ukweli ni kwamba watu hawa wana chuki na mapinduzi, na wanatumia kila njia kuhakikisha kwamba muungano unapasuka na wao wanarudi Zanzibar. Kelele za kina Sheikh Fareed na Uhamsho zote zinatokana na fedha inayotoka nje ya Zanzibar. Na hapa ndio nikasema kwamba USA na EU hawawezi hata siku moja kuacha Tanzania ipasuke, ndio nikawambia CCM wataleta watu kutoka Tabora ambao wataongeza nguvu.

Mimi nimejikita zaidi kwenye uhalisia. Kwa sasa tukubali kabisa hakuna jipya kutoka Dodoma. Labda CCM waamue.
kuhusu kura, kaka wana CCM wako royal sana na chama chao, wewe ni kada wa kwanza kukuona unakuja kwenye majukwaa na kuupinga mfumo huu. Lakini wenzio wote wameshikwa pabaya mfano hali ni Mzee Sitta na Wawakilishi kutoka Zanzibar ambao uliona Pindu alivyomkana Warioba mchana kweupe. Siwapendi CCM lakini nawakubali jinsi wanavyoweza kuendesha agenda.

Sidhani kama upo nchini kwani kwa hoja zako, hauelewi jinsi gani wananchi wa kawaida wanavyozidi funguka juu ya Tanganyika na umuhimu wake licha ya ccm kutumia fedha nyingi sana kwenye mabaraza ya katiba kuwajaza wananchi woga na upotoshaji juu ya Tanganyika. Hoja ya msingi kuhusu Tanganyika kwa upande wangu ni serikali yake, nachojadili ni umuhimu wa devolution au federalism. Sijali sana nchi kuwa moja, nachojali ni serikali tatu, na hivyo ndivyo wananchi wengi wanavyopanuka sasa kiuelewa, huku wewe ukiongelea wananchi wa BBM na Whatsap. Unaposema kwamba hoja ya Tanganyika ni ya kwenye mitandao tu inazidi kudhihirisha kwamba haupo in touch na nini kinaendelea mitaani in urban areas right now; kwa kweli hauna uelewa na kinachoendelea;ccm na uongozi wake wanaelewa ndio maana kinana tayari yupo busy kuwaambia wananchi kwenye mikutano waikatae tanganyika wakati hata hicho kipengele hakijaguswa kwenye mijadala ya ya bunge as we speak;

Sio kweli kwamba EU na USA wanaulinda muungano, hizo ni porojo; ebu research kidogo tu mtazamo wa CIA na taasisi nyingine za mataifa haya wanasemaje kuhusu solution ya mgogoro wa sasa; you are not in touch with reality;soma wanazuoni wa nje;wote na taasisi zao wanaongelea maneno matatu - devolution, devolution, devolution; hoja zako za znz kuchochewa etc ni za kweli ila haya yalikuwepo even before the idea ya muungano, usitake potosha mambo;matatizo haya watayamaliza wazanzibari wenyewe; nitajadili hili kwa kirefi baadae;

Hivi unajua maana ya 1+1 equals 3 katika muktadha wa muungano wetu? Hoja zako nyingi ni za kisiasa, naomba uje kwenye uzi wangu titled "Tundu Lissu na Kiini Macho Cha Muungano", tujadili suala husika kwa facts, evidence na kwa mujibu wa sheria za katiba;nimekualika kule, haujaja;

Mwisho ni kuhusu mimi kuwa kada lakini nipo upande tofauti na kina sitta na kificho; seriously? Unataka kuniambia mimi kama kijana natakiwa kurithi ccm ya kina sitta na kificho? Siwezi, na nimejadili sana hilo;ukitaka kujua kwanini, tembelea profile yangu utakutana na topics nyingi on that;

Naomba uje kwenye uzi wangu wa Tundu Lissu, kule nitakujibu vizuri zaidi hoja zako nyingi humu kwani zina fit zaidi katika muktadha ule;

Nakusubiri kule;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Huyo aliyesema hayo alijua kwanini wapo confused. Si umesikia serikali na Ikulu zimepeleka mkataba feki ulioghushiwa? Hapo kweli si confusion!

Kila mtu anasema lake kuhusu mkataba wa muungano. Wapo wanaosema upo New York, wengine wanasema Moscow, na baadhi kusema ulizama wakati unavushwa kwenda znz. Confusion haiishi hapo wapo wanaoamini mkataba ni furushi kubwa sana linahitaji kontena kulipleka Dodoma. Wengine wanasema unahitaji askari 1000 kulindwa na hakuna pesa za kuwalipa kuupeka Dodoma. Kwanini wasiwe confused.
wameenda mbali zaidi na kusema eti umepotea na ile FLIGHT MH370 toka Malaysia, (just kidding)
wakuu bado tunapata darasa toka kwenu, tunaelimika na tunaona mazingaombwe bunge la katiba kama yalivyotabiriwa tangu mwanzo.
 
SITTA SASA NI AIBU
HANA SONI, KIZAZI KUMCHEKA.
AKATA TAMAA NA URAIS


Magazeti yamenukuu Samwel Sitta akisema sahihi za mkataba uliofikishwa zilikuwa na matatizo.
Akasema makosa ya herufi zilizoonekana zimeandikwa kwa computer yametokana na wafanyakazi wa bunge walioongeza herufi hizo kwa kuzikazia ili zisomeke vema na wajumbe.

Mh Sitta ni mwanasheria kitaaluma, ni waziri na mtu aliyekuwa anaheshimika.
Anafahamu vema maana ya nyaraka na taratibu zinazopaswa kufuata katika kubadili, kutoa nukushi (copy), kuondoa au kuongeza maneno.

Cheti cha mtoto au mjukuu wake hata kama kimekosewa kwa herufi moja, sita hana uwezo wala mamlaka ya kukazia nukushi isipokuwa kupitia mamlaka husika iliyotoa cheti au mahakama.
Katika taratibu za kiofisi sualahilo linaambatana na sahihi na tarehe ya aliyefanya mabadiliko hayo.

Mkataba wa muungano ni moja ya nyaraka nyeti sana katika taifa letu.
Imesainiwa na viongozi wa taifa hili kwa niaba ya mamilioni na hatima ya taifa.
Kutoa nukushi tu ni jaribio lisilokubalika kimaadili kwa kuzingatia uzito wa suala hilo.

Sitta anapotoa madai hayo,kwakweli ni kuidhalilisha taaluma ya sheria, wasomi na viongozi.
Kwa watu wa mataifa mengine hiki kinaweza kuwa 'ze comedy' na huko walipo hawana mbavu.
Kwa upande mwingine ni kielelezo cha kwanini sisi ni masikini.

Endapo kiongozi mkubwa kama Sitta ambaye si mwenyekiti tu bali waziri mwanadamizi anaweza kutoa utetezi tete,hafifu na hovyo kama huo, hapo kuna kila sababu ya Tanzania kuendelea kupokea mamilioni ya misaada.

Lakini pia ni ushahdi kuwa tuna safari ndefu kufikia ndoto za taifa hili.
Huyu ni waziri na mwenyekiti asiyejua maana ya nyaraka, vipi mvuvi na mkulima anaweza kujua hata maana ya kunawa mikono kabla ya kula ?

Mwanaduru. wala usidhani Sitta amefanya hivyo kwa bahati mbaya.
Baada ya serikali kuona inakabiliwa na tuhuma nzito, za kufedhehesha na kusikitisha, serikali ikaamua kumtumia Sitta kujiepusha na balaa hilo.

Kama ilivyo kawaida, Sitta hakawii 'kujifunga mabomu na kujilipua' ili watakaobaki ima wawe salama au ndio usemi wa nzi hufia kidondani.

Sitta kaamua kutoa utetezi ambao mtu mwenye malengo ya kisiasa ya baadaye asingethubutu. Wenzake wamekwepa mzigo na yeye kujitwisha zigo hilo.

Amejitwishwa kama alivyowahi kusema wapinzani hawakugombea nafasi.
Akapanga kamati zake za CCM ili kuwafurahisha wana CCM wenzake.
Mambo yalipobadilika wana CCM wakaona bunge linavunjikia mikononi mwao.

Wakaomba wapinzani waongezwe. Kwa aiibu mabadiliko hayo akatangaza makamu wa Sitta ili kumpa nafasi Sitta kuficha uso wake.

Hii ina maana moja tu, kuwa Sitta ameji expose katika mazingira mabaya sana ambayo yamemvunjia hadhi na heshima.

Hakuna tena anayemfikiria kama mtu makini wala kumfikiria katika nafasi yoyote ya uongozi

Sitta amepoteza umaarufu, mvuto. amepoteza uungwaji mkono na wanataaluma yake.
Ni jambo la fedheha mwanasheria kusimamia na kutetea uhalifu ambao katika misingi ya kawaida hauwezi kutetewa.

Sitta amefanya hivyo kwasababu ya kuelewa kuwa mbio zake za 2015 sasa zimefika ukiongoni. Hana cha kupoteza tena 'he has nothing to lose' na kwamba anaweza kuagizwa lolote na akafanya ilimradi tu malipo yaingie.

Pengine malipo ni bora kwa familia yake, ninachelea kusema ipo siku wajukuu watasoma habari zake na kubaki kujiuliza, hivi babu alikuwa anafikri nini.

Tusemezane
 
Samuel-Sita-April8-2014.jpg

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,Samuel Sitta

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, leo anatarajiwa kukutana na Kiongozi wa Kanisa Katoliki nchini, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, jijini Dar es Salaam.

Kadhalika, Sitta atakutana na Mufti wa Tanzania, Sheikh Shaaban bin Simba, makao makuu ya Baraza la Kiislamu Tanzania (Bakwata), yaliyopo Kinondoni.

Tangazo fupi lililotolewa kwa vyombo vya habari na Idara ya Habari (Maelezo), jana lilisema kuwa kiongozi huyo wa Bunge atakutana na Kardinali Pengo leo saa 3:00 asubuhi na kisha atakutana na Mufti Simba saa 6:00 mchana.

Tangazo hilo fupi halikufafanua nia hasa ya kiongozi huyo kukutana na viongozi hao wa dini.

"Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba anatarajia kukutana na Kardinali Pengo saa 3:OO asubuhi St. Joseph na baadaye saa 6:00 mchana Kinondoni kukutana na Mufti bin Simba. Mikutano itafanyika jijini Dar es salaam," lilieleza tango hilo fupi.

Hata hivyo, pamoja na kwamba tangazo hilo halikuweka bayana nia ya Sitta kukutana na Mufti pamoja na Kardinali Pengo; wadadisi wa masuala ya kisiasa wameeleza kuwa mwenendo wa Bunge la Katiba hasa mivutano isiyokwisha inayoendelea kwenye vikao bungeni itakuwa ajenda kuu ya kuwafuata viongozi hao.

Tangu kuanza kwa Bunge Maalum la Katiba, kumekuwa na mivutano isiyokwisha kuanzia ile ya kura ya siri au ya wazi, iliyoibuka wakati wa kupitisha Kanuni za Bunge hilo kiasi cha kuafikiana kwamba kura zote mbili zitumike wakati wa upitishaji wa vifungu mbalimbali vya rasimu ya Katiba.

Kadhalika, suala la kupitisha kifungu cha rasimu kwa theluthi mbili ya kura za wajumbe kutoka Zanzibar na Tanganyika pamoja na muundo wa serikali; ni masuala ambayo bado yanaleta mvutano mkubwa bungeni.

Mivutano hiyo imezaa makundi ndani ya Bunge; kundi moja likiundwa kama Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambalo linatetea muundo wa serikali tatu kwenye Katiba ijayo na lingine likijiita Tanzania Kwanza, linalotetea muundo wa serikali mbili.

Kundi la Ukawa linaundwa na wajumbe wa upinzani na kundi la Tanzania Kwanza linaundwa na wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); na yamekuwa yakilumbana ndani na nje ya Bunge, kiasi cha kuyumbisha kiti cha Mwenyekiti.



CHANZO: NIPASHE

Yeye amedai alipeleka taarifa za nini kinaendelea bungeni akadai ilikuwa ni mhimu kwa yeye mwenyewe kupeleka taarifa ili hawa wakubwa awaondolee wasiwasi
Hapa swali ni je kweli anapeleka taarifa za kinachoendelea bungeni au ndo anaenda kutafuta uungwaji mkono kuelekea 2015?? na kwa nini akutane na Pengo na Simba tu?
 
Yeye amedai alipeleka taarifa za nini kinaendelea bungeni akadai ilikuwa ni mhimu kwa yeye mwenyewe kupeleka taarifa ili hawa wakubwa awaondolee wasiwasi
Hapa swali ni je kweli anapeleka taarifa za kinachoendelea bungeni au ndo anaenda kutafuta uungwaji mkono kuelekea 2015?? na kwa nini akutane na Pengo na Simba tu?
Hii nayo ni hatari nyingine anayoteneneza Sitta.
Viongozi wa dini wana sehemu na maeneo yao. Kuwaingiza katika migogoro ya kisiasa ni kutafuta balaa.

Mzee Sitta busara zake zi wapi?
 
Hii nayo ni hatari nyingine anayoteneneza Sitta.
Viongozi wa dini wana sehemu na maeneo yao. Kuwaingiza katika migogoro ya kisiasa ni kutafuta balaa.

Mzee Sitta busara zake zi wapi?
Mkuu, Nguruvi3 , kosa la Mh. Sitta liko wapi?.

Kama nchi kupitia Marais wake imeishajenga utamadamu wa kufunga safari kutoka Ikulu kwenda kuwaona Viongozi wa dini kuwaeleza mambo yanavyoendelea nchini, kwa nini kwa Mh. Sitta iwe ni nong'wa wakati yeye kwa sasa ndiye dereva wa mwelekeo wa nchi kwa vizazi vijavyo baada ya 2015?.

Ninadhani kama tunakuwa tumeumwa na nyoka, kwa sasa hata unyasi ukitikisika tunashituka!

Hatuwezi kuzika vichwa na kujidanganya kama viongozi wa dini nchini hawana nguvu ya kutikisa nchi katika siasa zetu.

Maybe I'm missing a point!.
 
Mkuu, Nguruvi3 , kosa la Mh. Sitta liko wapi?.

Kama nchi kupitia Marais wake imeishajenga utamadamu wa kufunga safari kutoka Ikulu kwenda kuwaona Viongozi wa dini kuwaeleza mambo yanavyoendelea nchini, kwa nini kwa Mh. Sitta iwe ni nong'wa wakati yeye kwa sasa ndiye dereva wa mwelekeo wa nchi kwa vizazi vijavyo baada ya 2015?.

Ninadhani kama tunakuwa tumeumwa na nyoka, kwa sasa hata unyasi ukitikisika tunashituka!

Hatuwezi kuzika vichwa na kujidanganya kama viongozi wa dini nchini hawana nguvu ya kutikisa nchi katika siasa zetu.

Maybe I'm missing a point!.
Suala la katiba si la kisiasa ni suala la kitaifa. Tayari kuna viongozi wa taasisi za kidini ndani ya bunge. Kitendo cha kwenda kuwaona viongozi wa dini mbili ni ubaguzi mkubwa. Wapi kiongozi wa mabohara, Ismailia n.k.?

Ni kwanini wakati wa mgogoro wa kisiasa mwenyekiti aende kuomba msaada wa viongozi wa dini? Hivi watakapokuwa na maoni tofauti huoni kwamba hapo ndipo hoja za upendeleo zinaanza?
 
Suala la katiba si la kisiasa ni suala la kitaifa. Tayari kuna viongozi wa taasisi za kidini ndani ya bunge. Kitendo cha kwenda kuwaona viongozi wa dini mbili ni ubaguzi mkubwa. Wapi kiongozi wa mabohara, Ismailia n.k.?

Ni kwanini wakati wa mgogoro wa kisiasa mwenyekiti aende kuomba msaada wa viongozi wa dini? Hivi watakapokuwa na maoni tofauti huoni kwamba hapo ndipo hoja za upendeleo zinaanza?
ubaguzi huu hautamuacha 6 hata kidogo, Pengo anawakilisha RC, je wale waumini wa Rutheran, pentecoste, wasabato na wengine wote wanaongozwa na Pengo? mzee 6 amechemsha ubaguzi huu, kwanini hakumuona Askofu Malasusa na Shekh Simba? au kwanini hakwenda kwa Kakobe? basi ni bora angeenda kuwaona hao viongozi wa dini kimya kimya kuliko kutangaza na kwenye media....
 
“CCM isibaki kuwa kichwa ngumu kupinga serikali tatu."

Samuel Sitta.
------------------------------------------------


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
"CCM isibaki kuwa kichwa ngumu kupinga serikali tatu."

Samuel Sitta.
------------------------------------------------


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
mtu mzima kama Sita akionyesha unafiki wake wazi wazi bila aibu sijui akina mwigulu na January makmba watafanyaje....
 
mtu mzima kama Sita akionyesha unafiki wake wazi wazi bila aibu sijui akina mwigulu na January makmba watafanyaje....

Hao vijana uliowataja inaonekana walishaamua kurithi CCM ya wazee waliompokea Mwalimu, CCM ambayo sio ya kumpigania tena mnyonge, sio ya ushindani kwa hoja, sio inayoheshimu kanuni zake za kukaa mbali na fitina, unafiki na woga, sio CCM inayosimama na mwongozo wa Chama (1982) kwamba "kokosoa na kukosolewa ndio silaha ya mapinduzi". Kwa kufanya kosa hilo, wazee walioharibu CCM wakienda katika maisha ya ustaafu, vijana hawa watapata kazi sana ya kurudisha imani ya chama kwa wananchi kwani wameshirikiana na waharibifu wa chama kuifikisha CCM ilipo sasa. Ilitakiwa wasimame kidete kama kina Lugola, Filinkunjombe, Lembeli, Bulaya na wengine ambao ni wana CCM lakini wanasoma alama za nyakati mara nyingine.

Pengine watawadanganya wapiga kura wao huko majimboni kwao kwamba waliweka utaifa mbele. Hakika wananchi wengi maeneo mengine hawatawaelewa. Bado wana muda wa kubadilika, hasa January. Huyo mwenzake haiwezekani tena.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
mtu mzima kama Sita akionyesha unafiki wake wazi wazi bila aibu sijui akina mwigulu na January makmba watafanyaje....
Hao vijana uliowataja inaonekana walishaamua kurithi CCM ya wazee waliompokea Mwalimu, CCM ambayo sio ya kumpigania tena mnyonge, sio ya ushindani kwa hoja, sio inayoheshimu kanuni zake za kukaa mbali na fitina, unafiki na woga, sio CCM inayosimama na mwongozo wa Chama (1982) kwamba "kokosoa na kukosolewa ndio silaha ya mapinduzi". Kwa kufanya kosa hilo, wazee walioharibu CCM wakienda katika maisha ya ustaafu, vijana hawa watapata kazi sana ya kurudisha imani ya chama kwa wananchi kwani wameshirikiana na waharibifu wa chama kuifikisha CCM ilipo sasa. Ilitakiwa wasimame kidete kama kina Lugola, Filinkunjombe, Lembeli, Bulaya na wengine ambao ni wana CCM lakini wanasoma alama za nyakati mara nyingine.

Pengine watawadanganya wapiga kura wao huko majimboni kwao kwamba waliweka utaifa mbele. Hakika wananchi wengi maeneo mengine hawatawaelewa. Bado wana muda wa kubadilika, hasa January. Huyo mwenzake haiwezekani tena.
Wakubwa hapa lipo neno. Hawa vijana akina Nape, Mwigulu, January, Dr Faustine, Dr Kigwangalla wanaposhindwa na Mzee kama Warioba au Msekwa inaleta hofu, inatisha na inasikitisha.

Naomba uvumilivu kidogo, inabidi nao tuwaangalie kwa darubini katika eneo lao special. Hapa ni kwa sita,
Kuna uzi unaokuja wa kuangalia Impact ya vijana katika siasa na mabadiliko ya taifa hili.
Jina la uzi hio litakuwa '' Duru za Siasa: Vijana wameshindwa katiba, hawawezi uongozi'

Tutawaonyesha mmoja baada ya mwingine na jinsi gani walivyotanguliza CCM mbele ya taifa.
Ni jinsi walivyosaliti vijana na kizazi hiki
Jinsi gani hawapaswi kuaminiwa tena, na walivyoshindwa kwa maono na wazee wa 1947.

Coming soon
 
Suala la katiba si la kisiasa ni suala la kitaifa. Tayari kuna viongozi wa taasisi za kidini ndani ya bunge. Kitendo cha kwenda kuwaona viongozi wa dini mbili ni ubaguzi mkubwa. Wapi kiongozi wa mabohara, Ismailia n.k.
Ni kweli swala la Katiba ni suala la Kitaifa lakini vile vile hatuwezi kuukataa ukweli uliopo kuwa viongozi wa dini nchini ni sehemu ya nguzo kuu za kitaifa.

Kwa Tanzania, makanisa na misikiti inaendelea kuongozeka kila siku badala ya kupungua kama ilivyo katika nchi za Magharibi kwa maana kuwa, wananchi wengi nchini wanaendesha maisha yao kwa sasa katika misingi ya imani za dini (Kikiristo na Kiislamu). Kama wewe ni mwanasiasa unayetaka kuwaongoza wananchi wengi katika misingi wanayoitaka kwa faida ya mstakabali wa taifa lao, basi huwezi kujitenga na misingi hii ambayo inashikiliwa na viongozi wa dini hizo.

Tupende tusipende, Mafanikio ya upatikanaji wa Katiba yanategemea sana makundi makuu mawili nchini.
1) Vyama vya siasa
2) Madhehebu ya dini.

Ukiangalia katika kundi la kwanza utakuta kuwa Viongozi wake wakuu wa vyama vya siasa nchini wako kwenye Bunge moja kwa moja ambapo wengine wako mpaka kwenye Kamati ya Maridhiano ndani ya Bunge. Hii ina maana kuwa, kile kinachoendelea ndani ya bunge siyo kwamba wanakielewa pekee bali wao ndiyo wanakifanya. Kwa hiyo hili kundi linashiriki moja kwa moja likiwa na viongozi wake.

Ukiangalia kundi la pili utaona kuwa, lina wajumbe katika Bunge Maalum lakini halina viongozi wake wakuu kama lilivyo kundi la kwanza. Kwa maana hiyo, sioni tatizo hata kidogo kwa Mh. Sitta kwenda kuonana na viongozi wakuu wa kundi la pili muhimu ndani ya bunge Maalum ili kuwaeleza kile kinachoendelea ndani ya bunge. Kuwa na kundi katika bunge linalowakilisha madhehebu ya dini hakumfungi kiongozi wa mwenye hekima kupata mawaidha au kubadilisha mawazo na Kiongozi yoyote muhimu katika ufanikishaji wa shughuri anayokabiliana nayo.

Kusema kuwa Mh. Sitta ni mbaguzi naona kama umewahisha hitimisho na kwa maana hii, hujamtendea haki kwa sababu bado hajamaliza ziara ya kuwatembelea viongozi mbali mbali muhimu nchini na amebaisha zaidi kwa kusema hivi,
Ziara hiyo ambayo amesema ni utaratibu aliouanza kukutana na viongozi wa dini, pia ilimkutanisha na Mufti wa Baraza la WaislamU Tanzania (BAKWATA), Shekhe Issa Bin Shaaban Simba. Sitta alikutana na Rais Kikwete juzi.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Sitta, Rais Kikwete hajataja ni lini Bunge hilo litaanza tena kwa nyongeza ya siku 20 kwa mujibu wa sheria, baada ya siku 70 zinazomalizika mwezi huu, kuisha ili kufanya jumla ya siku 90. Lakini amesema uongozi wa Bunge umekusudia lianze tena Agosti mwaka huu.

Alisema lengo la kukutana na viongozi hao wa kidini ni kuwaeleza kinachoendelea Dodoma, kwa kile alichodai viongozi hao wana ushawishi na wafuasi wengi nyuma yao, hivyo si busara kusikia mitaani.

Katika mkutano huo Sitta alikanusha habari ya gazeti moja lililodai anakwenda kuwaangukia viongozi hao na kusema hana dhambi za kufanya hivyo.

“Leo (jana) nimepanga kukutana na viongozi wa dini zetu na si hawa tu nitakaokutana nao, nitaendelea na utaratibu huu kwa viongozi wengi hata wenye wafuasi wachache, hawa wana ushawishi japo hawahusiki sana na siasa lakini ni viongozi wa jamii, wanapaswa kupata taarifa sahihi ya nini kinachoendelea Dodoma,” alisema Sitta.

http://habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/23870-bunge-la-katiba-jk-akubali-muda-zaidi

Ni kwanini wakati wa mgogoro wa kisiasa mwenyekiti aende kuomba msaada wa viongozi wa dini? Hivi watakapokuwa na maoni tofauti huoni kwamba hapo ndipo hoja za upendeleo zinaanza?
Dhana nzima ya kiimani katika dini ni kuamini kuwa kuna "nguvu" ambayo ni zaidi ya nguvu tulizonazo kiakili katika kupambana na changamoto ambazo tunaamini ziko juu ya uwezo wetu.

Viongozi wakuu wa madhehebu ya dini wanawakilisha hiyo "nguvu" iliyo juu ya uwezo wetu kwa maana kuwa, huwezi kwenda kuomba ushauri kwa jambo ambalo liko chini ya uwezo wako.

Kama Mh. Sitta anaamini mgogoro ulioko mbele yake uko juu ya uwezo wa chombo kinachotaka kukabiliana nao, basi sioni tatizo la yeye kwenda kuomba ushauri kwa wawakilishi wa nguvu iliyo juu ya uwezo wake.
 
Ng'wamapalala
Nianze kwa kusema hakuna ushahidi kuwa Sitta alikwenda kuomba ushauri. Inawezekana alikwenda kuomba ushawishi.
Ushauri na ushawaishi vinaweza kuwa vitu viwili tofuati kabisa, na utetezi wako kuhusu hilo lazima uzingatie mazingira unless utuambie una ushahidi alikwenda kwa ushauri.

Pili, wawakilishi wam makundi wana maana moja, walishazungumza katika mikutano yao na kubaini kuwa kuna ya kuzungumziwa. Maoni hayo lazima yazingatiwe na wala si kuzingatia maoni ya mtu mmoja iwe Pengo au Simba.

Tatu, kulikuwa na nafasi ya kutoa maoni kuhusu muungano na katiba kupitia tume. Wakubwa hao walifikiwa na kutoa maoni yao, leo ushauri gani zaidi ya ule.

Nne, hivi maoni yao yakitofautiana tunawezaje kuondoa hisia za makundi ambazo zinajengeka kila uchao.

Tano, pamoja na kuwa na dini nchi haitakiwi kuongozwa katika misingi ya kidini. Wapo watu hawana dini, hawa walifikiwaje na Sitta katika kutafuta ushauri.

Sita, ni kweli kuwa ongezeko la wanasiasa makanisani na misikitini linazidi, huo ni uchafu kwasababu wanasiasa sehemu yao ni mwembeyanga na Jangwani. Tanyotokea Afrika ya kati, Nigeria na kwingineko ni matokeo ya kuwakaribisha viongozi wa dini kwatika uongozi wa nchi.

Vongozi wa dini wanapaswa kuongoza jamii kimaadili, kama wataingia katika mambo ya siasa, jambo lisiloepukika basi wafanye hivyo wakiangaliwa kama moral percepective na si kisiasa.

Saba, kuna uozo uliofanyika nyakati za Sitta kama spika wa bunge la JMT. Hakuna siku aliwahi kutafuta ushauri wa viongozi wa dini. Lipi leo linamkimbiza huko kama si unafiki.

Kwa vile amekwenda kwa wakuu wa dini mbili, vipi wale wasiofikiwa na ugeni wa Sitta, nafasi yao katika jamii ipoje na ni kwa msingi gani wao wadhani ni sehemu ya taifa na mchakato kwa ujumla.
 
Ng'wamapalala
Nianze kwa kusema hakuna ushahidi kuwa Sitta alikwenda kuomba ushauri. Inawezekana alikwenda kuomba ushawishi.
Ushauri na ushawaishi vinaweza kuwa vitu viwili tofuati kabisa, na utetezi wako kuhusu hilo lazima uzingatie mazingira unless utuambie una ushahidi alikwenda kwa ushauri.

Pili, wawakilishi wam makundi wana maana moja, walishazungumza katika mikutano yao na kubaini kuwa kuna ya kuzungumziwa. Maoni hayo lazima yazingatiwe na wala si kuzingatia maoni ya mtu mmoja iwe Pengo au Simba.

Tatu, kulikuwa na nafasi ya kutoa maoni kuhusu muungano na katiba kupitia tume. Wakubwa hao walifikiwa na kutoa maoni yao, leo ushauri gani zaidi ya ule.

Nne, hivi maoni yao yakitofautiana tunawezaje kuondoa hisia za makundi ambazo zinajengeka kila uchao.

Tano, pamoja na kuwa na dini nchi haitakiwi kuongozwa katika misingi ya kidini. Wapo watu hawana dini, hawa walifikiwaje na Sitta katika kutafuta ushauri.

Sita, ni kweli kuwa ongezeko la wanasiasa makanisani na misikitini linazidi, huo ni uchafu kwasababu wanasiasa sehemu yao ni mwembeyanga na Jangwani. Tanyotokea Afrika ya kati, Nigeria na kwingineko ni matokeo ya kuwakaribisha viongozi wa dini kwatika uongozi wa nchi.

Vongozi wa dini wanapaswa kuongoza jamii kimaadili, kama wataingia katika mambo ya siasa, jambo lisiloepukika basi wafanye hivyo wakiangaliwa kama moral percepective na si kisiasa.

Saba, kuna uozo uliofanyika nyakati za Sitta kama spika wa bunge la JMT. Hakuna siku aliwahi kutafuta ushauri wa viongozi wa dini. Lipi leo linamkimbiza huko kama si unafiki.

Kwa vile amekwenda kwa wakuu wa dini mbili, vipi wale wasiofikiwa na ugeni wa Sitta, nafasi yao katika jamii ipoje na ni kwa msingi gani wao wadhani ni sehemu ya taifa na mchakato kwa ujumla.

Ushauri ni ule aliopewa Kikwete na kiongozi mmoja wa dini aliyemtembelea Rais Kikwete kwenda kunywa nae chai na kumshauri dhidi ya serikali tatu. Haya ni maneno yake rais mwenyewe kwenye hotuba yake ndani ya BLK mwezi machi mwaka huu. Rais hakutaja jina wala dini ya mshauri husika.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom