Kwa lipi na kwanini Samwel J. Sitta aaminiwe?

Kwa lipi na kwanini Samwel J. Sitta aaminiwe?

SITTA ABADILI MSIMAMO, AKUBALI KATIBA YA CCM IJADILIWE
SITTA HAJALI NCHI TENA, SASA NI KIU YA URAIS NA 'BORA KATIBA'

Mswada wa sheria ya rasimu ulipopingwa bungeni, bunge la JMT liliupitisha kwa idadi ya wajumbe 100, chini ya 2/3 inayotakiwa. Hilo lilifanywa kwa nguvu ili kushinikiza mswada.
Mh Sitta akiwa mbunge na waziri alikuwepo ndani ya bunge.
Hakukemea kwasababu lilikuwa na mafao kwa CCM

Juzi wabunge wa UKAWA walipotoka nje ya ukumbi wa BMLK mh Sitta alisema majadiliano yataendelea kwavile akida imetimia ambayo ni 2/3 ya CCM na Mh Mrema.
Akidi ipi wakati kuanzia huko nyuma hakukuwa na suala la akidi mzee Sitta?

Ni sitta huyo huyo aliyeshindwa kukemea mswada uliopitishwa na watu 100 lakini akatumia wingi wa CCM bunge la katiba kuhalalisha kikao. Kwa wale msiomjua mzee huyu na undumila kuwili hya ni baadhi ya tu ya mambo ya mzee.

Mzee huyu alipofanya mbinu za kumnyanyasa Warioba kwa kumtanguliza mbele ili aadhibiwe na JK alisema busara zilimuongoza kwamba Rais azungumze baada ya Warioba.

Inashangaza kuona mzee huyo huyo ameshindwa kutumia busara kutambua kuwa katiba ni suala la nchi na si la chama.

Hadi sasa anachokifanya ni kuandika katiba ya CCM akitarajia kuwa katiba inayoandikwa itamwezesha kuteuliwa au kuwa Rais wa nchi hii.

Mzee Sitta anashindwa kutumia busara kubaini kuwa matatizo ya katiba anayoiandika na CCM si ya watu wa nje, ni ya watoto na wajukuu zake ambao huenda siku moja nyaraka hiyo hiyo ikaja kuwahukumu kama raia.

Na katika kuonyesha undumila kuwili na busara chache za mzee wetu, Sitta amependekeza muda zaidi wa kuchambua katiba.

Tunachojua ni kuwa anahitaji muda zaidi ili kuweza kufumua rasimu ya Warioba kwasababu muda uliopangwa hautoshi. Hilo mzee Sitta halioni kama gharama na upotezaji wa muda.

Ni upotezji wa muda kwasababu katiba ya CCM itafumuliwa pengine miaka chini ya 5 ijayo.
Je, hiyo ndio busara ya Sitta kwa kizazi hiki?

Katiba ya CCM inayoandaliwa inaweza kuzua vurugu nchini. Je, ndio busara za Rais mtarajiwa Sitta?

Ingawa anatumika kuhujumu wananchi kwa mategemeo ya Urais, Sitta atambue kuwa matendo, usaliti wa umma na undumila kuwili umeshahitimisha ndoto hizo kabla ya kuziota.

Tusemezane
 
SITTA AENDELEA KUIUZA TANGANYIKA, KWA URAIS

Tunakumbuka jinsi ambavyo Spika Sitta ima ametumika au ametumia kuvunja au kupindisha kanuni na sheria.
Historia ya Sitta kuhusu muungano ina mengi ya kujadili.

Hivi karibuni, Sitta amekaririwa akisema katiba mpya ya CCM inafikiria kutoa nafasi na mamlaka kwa Zanzibar ndani ya muungano. Na, kwamba, jambo la kuwa na 50-50 kati ya Tanganyika na Zanzibar lipo katika katiba hiyo.
Hayo ni mawazo yake ambayo kwa mzee anayetumika kama Sitta ni hatari kuyapuuza.

Sitta aliwahi kusema hakuna sababu za Watanganyika kutaka ardhi znz kwasababu ipo ya kutosha, lakini ni haki wazanzibar kupata ndani ya Tanzania, haki ambayo Mtanganyika si lazima awe nayo znz

Maoni ya tume ya Warioba yameonyesha hasira za Watanganyika. Suala la ardhi halipaswi kutungiwa sheria za kumbagua Mtanganyika, linatakiwa liwe soko huru ili soko liamue nani anunue nini na wapi.

Kuwatenga Watanganyika na kuruhusu Waitaliaoni, Waoman na Wamombasa ni chuki ambayo majibu yanatakiwa yalingane nayo.

Hakuna sababu za kupigazana kelele na wazanzibar. Wana haki ya kulinda nchi yao kwa kadri watakavyo.
Haki tunayotaka wala si ya kushindana na Zanzibar.
Haki yetu ni uwezo wa kuamua hatima ya taifa letu tukiwa na fiscal autonomy bila kuingiliwa na Znz nasi kutowaningilia.

Wakati znz inaandika katiba ya 2010 ambayo imevunja muungano na misingi ya undugu wa nchi mbili, Sitta alikuwa Spika.
Hakuwahi kukemea utovu huo wa nidhamu na hata sasa hajaweza kukemea.
Leo Sitta hawezi kuamua wznz wapate nini katika muugano.

Muungano ulishavunjwa na wznz, kinachofanyika ni kutafuta njia ya kushirikiana ili kutomaliza undugu uliopo.

Tume ya Warioba imependekeza mambo 7 ambayo Tanganyika itawasaidia wazanzibar.
Endapo 7 hayawezekani, wznz wanaweza chagua hali ya hewa tu tukaunda tume ya pamoja kila mmoja akakaa kwa amani kwakwe.

Tunamwambia Sitta kuwa hakuna suala la 50-50 na znz kwasababu, Tanganyika hailingani na znz hata 1/100 kwa jambo lolote lile. Kiutamaduni, uchumi au kisiasa. Ni matusi kuwaweka katika daraja moja na Tanganyika.
Hiki ni kisiwa ambacho ni kidogo sana, ambacho impact yake kwa Tanganyika haipo .

Kwasasa, Sitta atambue kuwa kujipenedekeza kwake akidhani anaweza kuwatumia waznz kwenye Urais ni kujidanganya.

Hakuna namna ambayo znz imejitangaza kama nchi na taifa ikawa na maamuzi yanayohusu Tanganyika.
Na wala hakuna uwezekano wa Tanganyika kukubali tena kuongozwa na kiongozi kutoka Zanzibar.
Kukubali ni kukaribisha mamaluki wa nchi jirani, ni kukabidhi nchi kwa raia wa kigeni! hilo halitatokea tena.

Sitta asahau ushawaishi wa zamani wa wznz ndani ya vikao vya maamuzi ya Tanganyika.
Pengine awaeleze wznz ukweli kuwa, wao kupitia katiba yao ya 2010 ni nchi, yenye utaifa na serikali yake.

Hakuna uwezekano mzanzibar akaja kutawala Tanganyika tena. Hakuna huo uwezekano hata siku moja.

Upo uwezekano wa mznz kuwa kiongozi wa Tanzania pale tu Tanganyika itakapozinduka na kuwa na uongozi wake.
Kupitia S2, znz isahau kabisa suala la kutoa uongozi wa nchi, 50-50 na amani waliyozoea kuipata Tanganyika.

Tusemezane
 
SITTA ALIPOTEZA UMUHIMU WAKE SIKU NYINGI

UBABE UNAMTOKEA PUANI, KIKAO CHA USULUHISHI CHAVUNJIKA


Kuna taarifa za kikao cha usuuhishi kati ya UKAWA na CCM kilichokuwa chini ya Jaji Mutungi kushindwa kupata muafaka.

Kwetu sisi duru, haukuona sababu za UKAWA kuhudhuria kikao hicho kwa namna yoyote.
Jaji Mutungi alianza kutumiwa kuleta mtafaruku CDM kwa kuchagua viongozi, nani agombee nani asigombee.
Huyu ni mamluki na hakuna uwezekano angekuja na jambo la maana.

Wakati huo huo kikao cha usuluhishi cha kamati ya BMK chini ya Samwel Sitta kilikuwa kifanyike leo.
Wajumbe walitumiwa taarifa, wengine wakisema hawatahudhuri na wengi hawakuwepo kabisa.
Kikao hicho nacho kimesusiwa na UKAWA.

Spika Sitta hana moral authority ya kuita kikao cha usuluhishi.
Ukifuatilia uzi huu tangu mwanzo, tumeeleza mzee huyu kama mmoja wa wanafiki.

Lakini pia ni Samwel Sitta aliyepindisha kanuni za BMK ili kumruhusu Kikwete kuhutubia baada ya Jaji Warioba.

Sitta alifa hivyo kwa kudharau wajumbe wa kamati ya uongozi na ile iliyoandika kanuni ambazo ndizo zilitumika kumchagua yeye.

Sitta alitoa utetezi wa kitoto kwa kusema hakukuwa na agenda na hivyo Rais asingeweza kuhutubia bunge.
Ni utoto kwasababu alipofungua Bunge la kwanza la JMT katika utawala wa JK, Sitta alikuwa Spika na siku ya kwanza hakukuwa na agenda lakini JK alihutubia.

Samwel Sitta aliwadhalilisha wenzake kwa kuwafanya majuha na wendawazimu.
Akaenda mbali na kutishia kutumia usalama wa taifa na vyombo vya dola ili kuzuia wabunge wasitoke katika bunge.

Hayo aliyafanya akitumaini kuwafurahisha CCM ili kujifagilia njia ya Urais.
Alichoshindwa kutambua ni kupotea kwa heshima yake, kudhalilika na sasa anadhalilishwa zaidi.

Anadhalilishwa kwasababu hakuna kikao anachoweza kuitisha watu wakaja kwa kutambua ni yule yule aliyezua tafrani na kuliyumbisha Bunge.

Hakuna shaka ndio maana anajibiwa hovyo na wabunge.
Hilo halitokei kwa bahati mbaya, ni Sitta mwenyewe aliyelitafuta.

Unapopewa dhamana ya taifa lazima uiheshimu. Samwel Sitta tuliyemtilia mashaka hata kabla ya kuchaguliwa, ameshindwa kutumia 'benefit of doubt' aliyopewa na wajumbe kulinda heshima yake na heshima ya taifa.

Kwasasa, Sitta amepoteza sifa za kuwa mwenyekiti, au msuluhishi.
Anaonekana kibaraka na mtu asiye na msimamo.

Kushindwa kwa bunge la katiba kunatokana na ubabe na ulaghai wa Samwel Sitta.

Ni dalili kuwa Sitta hana uwezo wa kulileta taifa pamoja.
Huyu hafai kuwa kiongozi wa taifa hili.

Historia ya utendaji wake na hasa kama waziri EAC inaeleza wazi Sitta si kuwa haaminiki, bali anatumika kirahisi

Sitta akae kando katika usuluhishi, amepoteza hadhi, sifa na uaminifu.
 
SITTA AENDELEZA UPOTOSHAJI
MBINU ZAMWISHIA, SASA ANATAMANI UBABE

HAKUNA KATIBA ISIYO NA MARIDHIANO


Kikao cha kamati aiyoiteua Sitta kimemalizika .
Wajumbe wa UKAWA hawakuhudhuria licha ya vitisho vya Sitta kuhusu kile alichokisema kama vichwa ngumu.

Hakika wamekuwa vichwa ngumu na kichwa kinamuuma Sitta wala si wao.
Anguko lake na uwezo wake kwa mambo ya kitaifa sasa hakuna shaka vimefika mwisho.

Katika taarifa yake, Sitta ametoa mapendekezo kadhaa ili kukidhi haja zake na CCM katika kuandika katiba yao

1.Kikao cha bunge maalumu kiendelee kama kilivyopangwa.
Hoja yake ni kuwa kuna mambo kama uvuvi, kilimo ambayo ni muhimu kuliko muundo wa serikali.
Sitta haelewi kuwa hakuna nyumba inayokamilika ikiwa na furniture tu bila jengo.

2.Kwamba, kikao hicho kimefanyika kwasababu akidi ya theluthi mbili ilitimia.
Sitta anafahamu yeye ndiye alichagua kamati hiyo na kujiwekea wajumbe anaojua watakidhi akidi
Kusema akidi imetimia ni kujidanganya mwenyewe, hakuna akidi inayotengenezwa na mtu na kutimia.

3.Kwamba, kuwe na mabadiliko ya kanuni ili kudhibiti utoro na ukosefu wa nidhamu
Sitta alikuwepo wakati bunge la JMT linapitisha sheria ya kuundwa bunge la katiba kwa akidi ya watu 100.
Kwa unafiki hakukemea, leo anapata wapi nguvu za kukemea uzembe alioshiriki kuutengeneza kutoka bunge la JMT

Lakini pia, kudhibiti nidhamu anakokutaka ni ili wajumbe wakubaliane naye.
Wale watakaokataa maoni yake wafukuzwe ili abaki na kundi la ‘ndiyo' mzee.

Sitta hatambui kuwa katiba inayoandikwa si yake wala watoto wake ni ya taifa na kwamba, lazima kuwe na mawazo mbadala hata kama hayapendi.

Udikteta kama wa kufukiwa Richmond, Meremeta haukubaliki zama hizi na hilo Sitta aelewe bila kumuonea aibu.
Sitta alifunika uzembe uliolitia taifa aibu na sasa anataka kurudia tena.

4. Kwamba, UKAWA wameombwa warudi na makundi ya jamii nay ale ya dini.
Sitta anapotosha kwasababu makundi ya dini yalitaka matakwa ya wananchi yasikilizwe.

Huko nyuma tuliwaonya UKAWA kuwa lazima wajibu tuhuma za viongozi wa dini wanaotumiwa.
Leo kina Sitta wanatumia viongozi wa dini katika mambo ya kisiasa.

Halafu kwa unafiki wanarudi kusema watu wasichanganye dini na siasa.
BMK ni la kisiasa na hivyo maoni ya viongozi wa dini ni sawa na yale ya wakulima na wavuvi na BMK halichagui Askofu au Sheikh kama Sitta anavyopotosha.

5.Sitta anasema makundi yanayoleta tatizo ni UKAWA na Tanzania kwanza.
Hili la Tanzania kwanza ni la chama chake cha CCM.

Wakati linaundwa Sitta alikuwa kimya leo anawezaje kusema ni tatizo wakati yeye alikuwa mshiriki wa kundi hilo.
Ushiriki wa Sitta ni pale alipotumwa na Tanzania kwanza kuhakikisha JK anahutubia na kumvuruga Warioba.

Samwel alishiriki vema na ni mwanachama wa Tanzania kwanza.
Hana moral authority ya kunyooshea kidole kundi hilo

7. Sitta anasema, makundi halali ni yale ya wajumbe wa Tanzania bara na wajumbe wa Zanzibar
Tazama mzee Sitta anavyojidhalilisha.

Kwanza, hakuna kundi la Tanzania bara. Sheria ya kuunda bunge hilo la katiba haitaji wajumbe wa Tanzania bara.

Hivyo mzee Sitta atambue kuwa sheria haimruhusu kusema achilia mbali kufikiri.
Tuna kundi la Zanzibar dhidi ya JMT. Wabunge wa bunge la JMT ni kutoka Dodoma wakiwemo wa CUF.

Vipi aseme wabunge wa bunge la JMT ni kutoka Tanzania bara.
Huu ni uongo usiopaswa kufanya na mzee wa umri wake tena akiwa mwanasheria.
Hilo lazima aambiwe ili asiendelee kutengeneza mazingira ya machafuko nchini .

Sitta amepewa nafasi ya kuendelea na bunge lake mwenyewe.
Kitu anachopaswa kukumbuka ni kuwa katiba haipatikani bila muafaka.

UKAWA wanawakilisha sehemu ya jamii.
Ni vipi Sitta anaweza kuipuuza sehemu hiyo akijivunia kuwa katiba inayoandaliwa ina mema kwa wananchi.

Samwel Sitta, CCM na wewe mtaandika katiba yenu. Muda si mrefu wananchi wa Tanzania wataandika katiba yao.
Wakati huo utakuwa nje ya system na tutakuwa na uwezo wa kukuita popote ueleze upotevu wa pesa unaoendelea kuufanya na wenzako.

Kenya walijaribu lakini nguvu ya umma ikatamalaki.
Watanzania wa leo si wa mwaka 1973 .

Sitta atafakari kama analitakia mema taifa hili siku zijazo.
Tunajua hawezi kuwa rais wan nchi hii tena, je, kinga aliyonayo JK yeye anayo?

Tusemezane
 
Mbali na Kulaani vikali kauli ya Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba Ndugu Samweli Sitta na Pia agizo la Mkuu wa Mkoa Wa Dodoma Bi.Rehema Nchimbi natoa rai kwa watanzania tujiandae kuchukua hatua kali za kiraia na kisiasa

Ndugu Samweli Sitta ameliambia Bunge Maalumu la Katiba kuwa kuna chombo kimoja cha habari kimekua kikijifanya kuwa kinajua kuandaa midahalo na makongamano sana na kurusha moja kwa moja kwa watazamaji midahalo ambayo washiriki wake wamekua wakilishambulia bunge maalumu la katiba na pia washiriki wanaonekana kuwa wa upande mmoja hivyo akapendekeza serikali iangalie hatua za kuchukua na pia akamtaja waziri wa Habari kwa jina lake.

Kauli hii ya Samweli Sitta inaonekana kukilenga waziwazi kituo cha Televisheni cha ITV na Redio One Stereo.

Hivi ni vitisho si kwa chombo hiki tu bali kwa tasnia nzima ya habari inayoongozwa na sheria mbovu ikiwemo ile sheria ya magazeti ya mwaka 1976.

Ni kinyume cha katiba ya nchi ya mwaka 1977 ibara ya 18(1) inayotoa uhuru wa kutoa maoni,uhuru wa kutoa na kupokea habari. Mwenyekiti wa Bunge la katiba lililopewa jukumu la kuboresha rasimu ya sheria mama ya nchi(Katiba) anaongoza kwa kutoa matamshi yanayovunja sheria mama iliyopo(Katiba ya Sasa)?

Mathalani,Rasimu ya katiba mpya hasa ibara ya 30 imelinda uhuru wa Maoni,Ibara ya 31 imelinda uhuru wa Habari na vyombo vya habari na pia ibara ya 34 ya Rasimu imelinda Uhuru wa mikusanyiko na kushirikiana na wengine.Ibara zote hizi zimeshambuliwa na Mwenyekiti wa Bunge maalumu la katiba akiungwa mkono na baadhi ya wajumbe ambao wanatokea kwenye tasnia ya habari akiwemo Ndugu Hamis Dambaya.Ni jambo la kusikitisha na la aibu kwa taifa linalolenga ustawi wa kidemokrasia katika karne hii iliyostaarabika

Sitaki kuamini kuwa Ndugu Sitta amekua ignorant kiasi hiki kushindwa kuelewa kuwa midahalo hiyo imekua ikitangazwa kuhamasisha washiriki bila kujali itikadi za kisiasa na pia waandaaji wa midahalo hulipia muda wa matangazo(Air time) kwa vyombo hivi bila kuvunja sheria za nchi.Mtu aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (Tanzania Investment Center)Nchini ameonekana kuwa mbumbumbu wa kutisha kuhusu suala la uwekezaji kwenye vyombo vya habari ambavyo vina leseni ya kufanya biashara bila kuvunja sheria za nchi?Pengine kwa fikra zake finyu ndio maana enzi za uongozi wake katika kituo cha Uwekezaji nchi iliingia katika uwekezaji holela na wa kutisha unaoligharimu taifa hadi sasa

Vyombo vinavyomilikiwa na watu au taasisi binafsi kwa kiwango kikubwa vimejitahidi kutoa habari bila upendeleo tofauti na vile vya serikali vinavyotumika kama vyombo vya propaganda kwa serikali na chama tawala kama ilivyo kwa kituo cha Televisheni cha TBC1 kinachofadhiliwa kwa kodi za watanzania

Inasikitisha zaidi kuona mtu ambaye hivi karibuni amekua akijinasibu kuwa na matamanio /uwezo kuwa Rais wa Tanzania akigeuka kuwa adui namba moja wa haki za kiraia na uhuru wa vyombo vya habari.Dikteta anayejiandaa kuishambulia Demokrasia huyu(Assault on Democracy).

Ni katika mazingira haya haya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amepiga marufuku mijadala inayolenga kujadili lolote kuhusu bunge la katiba mjini Dodoma.Haya ni matumizi mabaya ya Madaraka na ukiukwaji wa sheria za nchi na uvunjaji wa katiba ya sasa na pia dhihaka kwa maudhui ya rasimu ya katiba

Madikteta hawapendi midahalo na mijadala inayoamsha fikra mpya za kimapambano katika mazingira ambayo uongo unaofadhiliwa na serikali(State Sponsored lies) umeshika hatamu.Madikteta wote duniani hutishwa na na mijadala ya kisomi kwa kuwa madikteta ni wavivu pia wa kufikiri kwa mapana(Critical Thinking).Ni katika mazingira haya ya woga sheria mbovu ya vyombo vya habari hutumika vibaya na watawala ikiwemo mbinu za kishetani za kuteka na hata kuua wanahabari,wanaharakati,wanasiasa na hata wasomi wasiopenda kuburuzwa na watawala.Rangi zao halisi tumeebdelea kuzishuhudia leo hii.Tusirudi nyuma,tushikilie hapa hapa

Na sasa Tujiandae kukabiliana vikali na utekelezwaji wowote wa kauli hizi za kiimla .Tujiandae kulinda katiba ya nchi na haki ya watanzania kwa njia zozote ikiwa ni pamoja na maandamano na migomo

Uhuru wa vyombo vya habari unawambwa msalabani,Haki za kirai na Demokrasia inanyongwa na maimla.Tujitetetee,tujilinde sasa.

Aluta continua,Victory Ascerta....!
 
Kuna watu wamejisahau ama kwa makusudi au kwa upofu na hivyo kujikuta wanashindwa kwenda na wakati; ni kama hawajui dunia iko kwenye karne gani kiteknolojia. Bado wanadhani tumo katika zile nyakati ambazo jengo la ofisi likiungua basi na nyaraka zote zimepotea, wanaamini kwamba, kwa kufunga tovuti ta Tume, hakuna rekodi ya maoni yao ama binafsi au kwa makundi waliyoyatoa mbele ya Tume. Hawaamini kuwa kilichowezesha Tume kukamilisha kazi yao kwa weledi ni kutotanguliza itikadi mbele ya maslahi ya Taifa na kutoruhusu unafiki kufunika ukweli...RIP Dr. Sengodo Mvungi.

Unafiki hufuta kumbukumbu, hudhoofisha fikra na hudumaza akili; unafiki ni kama rutuba kwenye shamba lililopandwa mazao ya uongo, ulaghai na udanganyifu. Watu aina ya Sitta ni mavuno kutoka shamba hilo; wako tayari kuita nyeupe nyeusi mradi tu maslahi binafsi waliyoyatanguliza hayapati msukosuko. Huko nyuma tuliwahi kushuhudia Sitta, akiwa Spika wa Bunge alivyotumia wadhifa wake kumtetea kwa nguvu mkewe (Waziri) baada ya kukamatwa na kuhojiwa na TAKUKURU kwa tuhuma za kutaka kuwapa rushwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT, mkoa wa Tabora mwaka 2010.

Ni huyu huyu Sitta mwaka 2012 alidai Dr. Mwakyembe kupewa sumu na kwamba ushahidi alishawakabidhi Polisi akimtuhumu Waziri wa Mambo ya Ndani wa wakati huo Nahodha kwa kukalia ushahidi, nanukuu;
Sitta said:
Waziri Nahodha anataka ushahidi gani ikiwa taarifa za madaktari zinazomhusu Dk Mwakyembe kuhusu sumu aliyopewa zilishapelekwa polisi, anataka mimi nitoe ushahidi gani.
Huyo ndiye Sitta ambaye mwanzo alikuwa ameapa kuanika mambo yote baada ya kutumia hela za walipa kodi kumtembelea Dr. Mwakyembe hospitalini India. Huyo ndiye Sitta ambaye sasa analiongoza Bunge Maalum La Katiba, huo weledi kautoa wapi! Kasababisha BMLK kususiwa na UKAWA kwa kupuuza maoni ya wananchi wa Taifa hili na kuamua kuwatukana waliokuwa wajumbe wa Tume ya Marekebisho ya Katiba.

Pamoja na kuidharau, kuidhihaki na kuipuuza rasimu iliyowakilishwa BMLK ikiwa imetokana na maoni ya wanachi, Sitta, kama kiongozi wa Bunge hilo ameamua kuwa wananchi hawana haki ya kupata habari ya kinachoendelea humo. Kama walivyoamua kuifungia tovuti ya Tume ili wananchi wasiweze kusoma wenyewe randama zilizotolewa na Tume hiyo, sasa wameamua kuvifungia na vyombo vya habari kuhabarisha wananchi yanayojiri Bungeni. Huu ni ufedhuli, ulevi wa madaraka na umangimeza usiovumilika hata kidogo. Kwa hatua hii ni wazi CCM imeingiwa woga, woga wa katiba bora; katiba ya wananchi...wanahangaika kuficha nini?

Watanzania wenzangu, vya bure ghali. Uhuru wa kupewa ni tofauti na ulioupigania; huo utaulinda na kuutetea kwa gharama zozote zile na anayetaka kuupokonya itabidi ajiulize mara mbili. Tumeiruhusu CCM kututawala kifikra kwa muda mrefu, tumeiruhusu CCM kutugeuza watumwa ndani ya taifa letu muda mrefu, tumeiruhusu CCM kutunyanyasa kwa muda mrefu, tumeiruhusu CCM kutuibia kwa muda mrefu...sasa lazima tupaze sauti na kusema hapana, imetosha. Mambo yanatendeka ndani ya nchi hii ya ajabu kabisa lakini ni kwa sababu tu sisi wananchi tumeruhusu hali hiyo; sasa yabidi tuamue kuyapiga stop...uwezo tunao!
 
Watanzania wenzangu, vya bure ghali. Uhuru wa kupewa ni tofauti na ulioupigania; huo utaulinda na kuutetea kwa gharama zozote zile na anayetaka kuupokonya itabidi ajiulize mara mbili. Tumeiruhusu CCM kututawala kifikra kwa muda mrefu, tumeiruhusu CCM kutugeuza watumwa ndani ya taifa letu muda mrefu, tumeiruhusu CCM kutunyanyasa kwa muda mrefu, tumeiruhusu CCM kutuibia kwa muda mrefu...sasa lazima tupaze sauti na kusema hapana, imetosha. Mambo yanatendeka ndani ya nchi hii ya ajabu kabisa lakini ni kwa sababu tu sisi wananchi tumeruhusu hali hiyo; sasa yabidi tuamue kuyapiga stop...uwezo tunao!
Eti tukae kimya watuibie nyaraka inayotuhukumu na kututetea sisi wenyewe.

Wanataka katiba iwe mwongozo wa mwalimu mkuu wa shule ya sekondari.

Wanataka kuficha haki zetu kwa kutumia neno uzalendo.
Mzalendo ni yupi,anayetuambia Ukweli au yule anayetaka kutuficha katika madema kama samaki.

Tumenyanyasika miaka nenda rudi, tukipaza sauti tunaambiwa tunataka kuvunja amani na utulivu.

Hawataki tusome au tusikie nyaraka zinazotuhusu. Wanachotaka tuwasikilize wakitudanganya.

Tumedanganywa eti TPDC ilianzishwa kuagiza mafuta nje ya nje. Kirefu cha TPDC kinawakana

Huwezi kuwa na development company ya kununua mafuta.
Wanataka tuamini TPDC ni sawa na GAPEX wakati ilianzishwa kuendeleza sekta ya mafuta. Wametuona majuha.

Hawatambui hii ni dunia ya digitali, kwamba, kila dakika habari zinaingia mitandaoni kama JF.

Hawajiulizi , iweje kauli ndani ya bunge zipingwe kabla ya ya bunge lao hawajapiga makofi.

Wamekosa mahali pa kushika sasa wanatafuta mchawi.
Eti TV ndiye mchawi kwasababu ana macho mekundu na nywele ndefu.

Wanamsingizia umri wake ni mkubwa na sasa wanataka kumchoma moto kama wanavyoachia vikongwe wachomwe moto Shinyanga.

Wanatafuta mchawi kwasababu ITV imevaa kaniki. Wamesahau mchawi wa taifa hili ni yule tunayemlipia kodi atuonyeshe za zecomedy, akinukia marashi kumbe ni jini.

Walijaribu mitandao wakashindwa, sasa wanatafuta mchawi mwingine.
Leo tuna rekodi za mikutano yao yote. Ukienda u-tube usiku wa manane unawasikia wakipanga mbinu za kutudhulumu na kutulaghai.

Wamelewa chakari hawajui ni duni ya digitali.
Ulevi si ndaza,chimpumu, pingu au mnazi. Ulevi wa kisasa ni digitali.

Wameaua mufindi paper mill magazeti yasichapishe habari wakidhani wanatukomoa.

Uhuni huu tuukatae. Kama UKAWA walivyoanza kuwaonyesha CCM muda wao wa kuelekea maktaba kusabahiana na KANU na UNIP umewadia, nasi tuna dhima ya kuwaambia, NENDENI, TANGULIENI. ENENDENI KWA AMANI.

Mkifika muwape salamu zetu KANU na UNIP. Waambieni Zambia ipo na Kenya ipo.

Tumechoka uhuni.
Tanzania ya leo si ya miaka 50. Tuwakatae na kuwaambia mubashara, mume noa!



 
SAMWEL SITTA AJIUNDIA TUME YAKE YA KATIBA NYUMBANI KWAKE

ATUMIA UONGO KUKIDHI KIU NA MATAMANIO YAKE

AGEUZA NCHI KAMA FAMILIA YAKE, SASA AANDIKA KATIBA ALIYOTUMWA

MAFISADI WAMWEKA MFUKONI, KILICHOBAKI NI HEWALA HEWALA.


Tulieleza mapema kabisa kuhusu mzee Sitta hulka na tabia yake ya ubabe ulioambatana na ubinafsi.

Kwa muda tumekaa kimya ili kuwapa wanaduru nafasi ya kumtahmini mzee huyu
Ni wazi sasa kila mmoja anamuona kwa sura yake halisi

Sitta anachokipigania sasa hivi ni masilahi yake ya milioni 150 baada ya bunge

Pili, Kuwapendeza mafisadi na wahafidhina ili kutafuta huruma ya kuungwa mkono katika harakati za Urais
Na upo uwezekano ameshatambua kuwa sasa ndio mwisho wake kisiasa, mwaga mboga nimwage ugali.

Katika hali ya uzee usio na busara, Samwel Sitta amejiundia tume yake ya kukusanya maoni.
Tume hiyo ya sitta haina mamlaka ya aina yoyote kwa mujibu wa sheria za nchi hii.

Ni utot unaomsumbua mzee huyu kwa kuwa hana la kufanya zaidi.
Sitta anafahamu bunge hilo si halina maana bali ni ufujaji wa fedha.

Bado ametumia na kuwatumia watu masikini katika kutafuta mafao yake na familia yake hata kama nchi itavurugika.
Kinachoonekana ni kuandaa mazingira ima ya kuhama nchi akiwa ''fit' nchi ikiingia machafukoni

Samwel Sitta anasema tume ya Warioba haikukusanya maoni ya wafugaji na wakulima hivo kutowatendea haki.
Hiki ni kituko kikubwa kwasababu hakujawahi kutokea kundi lolote kulalamika kutopata fursa ya kutoa maoni.

Anachokifanya Sitta ni kuijundia tume yake ambayo ni vema tukaiita 'TUME YA UANI YA SAMWEL SITTA''

Sheria ya kuandika katiba imeeleza muda na matukio.

Hakuna mwanadamu wa kawaida anayemwelewa Samwel pale anapoamua kutumia mamilioni ya fedha kukusanya maoni yasiyo na minutes na wala uhalali wa kisheria.

Mbinu hii ya Sitta ni kutaka kuungwa mkono na hao wanavijiji.

Asichokitambua mzee huyu ni kuwa nchi si wafugaji 10 au wakulima wa pamba 20.

Wapi anapata uhalali wa kusikiliza maoni ya wakulima ikiwa hao anaozungumza nao hawajulikani hata kwenye kata zao.

Mzee anasema wafugaji wamemuomba waje kuzungumza naye.

Kituko ni pale anapozungumza nao bila kuwa na katibu na haieleweki anafikishaje maoni ya wafugaji na wachuuzi katika kamati.

Maana yake, ameamua kusema uongo, wamekuja wenyewe, kuwaongopea anachukua maoni na kuongopa kuhusu fedha za umma anazotumia bila tija isipokuwa ufujaji.

Sheria gani inamruhusu akusanye maoni ya wananchi? lini atakutana na walimu, madaktari n.k.

Hiyo tume yake sample size ni kiasi gani ukilinganisha na ya Warioba

Mzee Sitta kachangikiwa maana hata wasomi na wanasheria wenzake wanabaki kujiuliza kama mzee ana uwezo wowote uliobaki.

Mzee Sitta anapaswa kufanyiwa uchunguzi wa kina kiafya hasa kutokana na msongo wa mawazo.

Tusemezane
 
Mkuu Nguruvi3 ilibaki dakika 10 tu Mzee Sitta kujiunga na CHADEMA, sababu moja kubwa iliyokuwa inamsukuma ilikuwa ni uozo ndani ya CCM. Lakini baada ya kuambiwa kuwa wana-dossier yake na wanaweza kummaliza kisiasa ndani ya dakika chache, yeye mwenyewe alinywea.

Anachikifanya sasa ni kijinusuru tu ili aonekane mmoja wao.

Kwa sasa sidhani kama kuna mtu yoyote hasa mwenye akili timamu, anayeweza kusema CCM na wanachama wake wako sahihi kwenye suala la katiba. Lakini ili waendelee kuwa salama inabidi wajifanye hawana akili timamu. That is what Mr Sitta is doing.
 
Mkuu Nguruvi3 ilibaki dakika 10 tu Mzee Sitta kujiunga na CHADEMA, sababu moja kubwa iliyokuwa inamsukuma ilikuwa ni uozo ndani ya CCM. Lakini baada ya kuambiwa kuwa wana-dossier yake na wanaweza kummaliza kisiasa ndani ya dakika chache, yeye mwenyewe alinywea.

Anachikifanya sasa ni kijinusuru tu ili aonekane mmoja wao.

Kwa sasa sidhani kama kuna mtu yoyote hasa mwenye akili timamu, anayeweza kusema CCM na wanachama wake wako sahihi kwenye suala la katiba. Lakini ili waendelee kuwa salama inabidi wajifanye hawana akili timamu. That is what Mr Sitta is doing.
Kila walilojaribu lilikuwa na majibu. Walizungumzia gharama kubwa, wakaulizwa kwani sasa hivi nani analipa gharama hizo na kwa kiasi gani?

Sula hilo limejirudi juzi katika moja ya kamati za Bunge la Sitta na CCM. Mfuko wa pamoja umeleta mjadala mzito sana.
Wazanzibar wakitaka tu kupewa bila kuchangia kwa kisigizio cha uchumi wao ni mdogo.
Katika kudai mgawanyo, wazanzibar wanataka mara 10 zaidi ya kile wasichochangia. Watanganyika wamekuja juu na suala limeachwa kiporo. Hili rasimu ililieleza vizuri sana, CCM wakadhani wana short cut.

Suala la bunge nalo limeleta kizaizai ndani ya kamati zao wenyewe.
Wazanzibar wanataka kuwa sehemu ya JMT wajadili hata kisichowahusu.
Watanganyika wametaka uwakilishi ndani ya BLW, wznz wamekuja juu.
Watanganyika wanauliza, wznz wanajadili mambo ya Tanganyika yanawahusu nini?

Samwel Sitta, ameunda tume yake ''TUME YA S.J.SITTA'' kukusanya maoni.
Tume haina mjumbe mwingine isipokuwa Shibuda na Suluhu, Samia
Tume ya Sitta inakutana na watu 15 wa makundi wanaojua wao.

CCM wanajikuta mahali pabaya sana. Ni wao walihoji sample size ya watu 17,000 wa tume ya Warioba kuwa haina maana kwasababu haikuchukua maoni kwa ukubwa wa jamii yetu. Leo CCM wanaulizwa sample size ya wafugaji 17 inawakilisha wafugaji wa nchi hii? Wanauliulizwa sample size ya wakulima wa Pamba 20 inawakilisha wakulima wa Kahawa, mkonge, Tumbaku na mazo mengine ya nchi hii? Hawana jibu.

Haya yote ynaua hoja ya sample size ya Warioba ilikuwa ndogo.
Ndio maana watu kama mama Anna Tibaijuka aliyesimama kidete kumnanga Warioba leo hawana mahali pa kujificha

Maskini, maprofesa wanafundishwa maoni aliyochukua Sitta bila minutes wala uhalali wa kisheria.
Wanalishwa la kusema na sasa akina mama Anna hawajui sample size ya wakulima 20 ni ya kata au ya nchi.

Smawel Sitta anasema wamekuja wenyewe. Mzee huyu ana maradhi ya kusahau ambayo huwakuta watu wa umri wake.
Baada ya UKAWA kutoka Sitta alikaririwa akisema anataka katiba inayowajali wafugaji na wakulima. Leo anasema wamekuja wenyewe.

Hata kwa akili za kawaida, Sitta alipswa kujiuliza, ni sheria gani inampa uwezo wa kujitungia tume yake mwenyewe, kujichagua na kukusanya maoni. CCM nao wanaulizwa hivi tume ya Warioba na tume ya Sitta ipi ina mantiki hata kwa mwendawazimu?

Mzee Sitta kakata tamaa na maisha ya baadaye ya kisiasa. Anachokifanya ni kutaka pesa za bunge tu.
Hata kama kufanya hivyo kutalitumbukiza taifa katika machafuko, Sitta hajali na hiyo ndio dalili ya mtu aliyekata tamaa.

Sitta kwasasa hivi ni hatari kuliko mafisadi. Mtu asiyejali sheria na taraibu za nchi, na anayegeuza mambo ya nchi kama familia hna nia njema na mustakabali wa taifa hili. Sitta anatengeneza mazingira hatari sana na duru haina uhakika yakitokea yasiyotarajiwa jina lake litasalimika vipi katika yale 3 makubwa yatakayotajwa. Duru haina uhakika na hilo
 
Wakuu it is a bit disturbing kusikia kuwa "bunge la Katiba lina mamlaka kuliko tume ya Warioba" nimesoma hii kauli kwenye post moja inayohusu katiba mpya. I wonder kama ndio kimya kimya maoni ya tume ya warioba yanafutwa, kwa "tume ya Sitta" kukusanya maoni yake. I wonder whether bunge la katiba sasa limeanza kufanya kazi ya tume kusanya "maoni" kutoka kwa wananchi na kuyatumia kama kigezo cha kutaka tuwe na serikali mbili. I wonder kama tunashuhudia kazi ya tume ya Warioba inafutwa na "tume ya Sitta".

CC: Mwalimu
, Ngongo,Tuko, crusingtz, timbilimu, TUJITEGEMEE, MARAGARASI, asigwa, nitonye, idawa, Swiper, hmjamii, mchambuzi, Pasco, nnauye, ben saanane, mag3, bak, invisible
 
Wakuu it is a bit disturbing kusikia kuwa "bunge la Katiba lina mamlaka kuliko tume ya Warioba" nimesoma hii kauli kwenye post moja inayohusu katiba mpya. I wonder kama ndio kimya kimya maoni ya tume ya warioba yanafutwa, kwa "tume ya Sitta" kukusanya maoni yake. I wonder whether bunge la katiba sasa limeanza kufanya kazi ya tume kusanya "maoni" kutoka kwa wananchi na kuyatumia kama kigezo cha kutaka tuwe na serikali mbili. I wonder kama tunashuhudia kazi ya tume ya Warioba inafutwa na "tume ya Sitta".


CC: Mwalimu
, Ngongo,Tuko, crusingtz, timbilimu, TUJITEGEMEE, MARAGARASI, asigwa, nitonye, idawa, Swiper, hmjamii, mchambuzi, Pasco, nnauye, ben saanane, mag3, bak, invisible

Huyu mzee kaingia kuongoza BMK aliwa bado amelewa sifa za wakati ule wa RICHMOND...walipopambwa na pambio za "Wapambanaji dhidi ya ufisadi". Ulevi ule bado uko kichwani mpaka sasa anaona kuwa yeye ana akili kuliko kila mtu. Aliingia mkenge toka mwanzo kumruhusu JK ahutubie baada ya Warioba kinyume na utaratibu na since then mambo yamekuwa yakienda mrama huku yeye akichekelea....Sasa anaona kuwa jahazi limezama anatafuta kila namna pa kutokea lakini hawezi kuikwepa fedheha hii!
 
Kwa mtazamo wangu, Sitta anatafuta ushujaa wa kuipatia CCM katiba inayoendana na maslahi ya chama chake akiamini Kwamba hiyo itamweka sehemu nzuri zaidi mwakani Kama mgombea au mwenye Nguvu Katika kutafuta mgombea. Lakini anasahau Kwamba Ndio, ki-CCM anaweza kuibuka favorite kutokana na alivyoendesha bunge kwa maslahi ya chama, lakini inaweza ikatokea Hali ya Kwamba - kwenye ushindani dhidi ya ukawa au chadema, CCM ikahitaji mgombea ambae hajachafuliwa na uchakachuaji wa rasimu ya tume ya warioba, hivyo hata Sitta kuwekwa pembeni na kuchukuliwa Watu Kama Mwandosya n.k.

Mazungumzo Kati ya rais na ukawa ni ya muhimu sana kuyafuatilia kwani ukawa wakiteleza tu kwa namna yoyote na kuishia kuleta tafsiri kwa wananchi Kwamba wameridhia katiba bora ije baada ya uchaguzi, na kwa sasa itumike katiba iliyofanyiwa marekebisho, Hapa Sitta anaweza Kabisa Tumia the loophole vizuri sana kuwa a strong contender ndani ya chama, na atakuwa na hoja nyingi tu Zenye mashiko Kujibu hoja za ukawa iwapo watakuja Tumia hoja ya katiba mpya kwenye kampeni za uchaguzi wa rais 2015.

All that said and done? As we speak, lawama juu ya kukwama kwa mchakato wa katiba mpya hazipo kwa rais Tena Bali kwa Sitta. Zitamuathiri vipi? Inategemeana na moves za ukawa.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
UKAWA wakikubali hoja ya marekebisho ya katiba kwaajili tu ya uchaguzi watakuwa wametuangusha sana.....nitashangaa kama bado wataendelea kutoa fursa za uaminifu kwa watu wachafu na wenye historia za kukana hata kauli zao.......Taifa linahitaji katiba bora sasa.......
 
Kwa mtazamo wangu, Sitta anatafuta ushujaa wa kuipatia CCM katiba inayoendana na maslahi ya chama chake akiamini Kwamba hiyo itamweka sehemu nzuri zaidi mwakani Kama mgombea au mwenye Nguvu Katika kutafuta mgombea. Lakini anasahau Kwamba Ndio, ki-CCM anaweza kuibuka favorite kutokana na alivyoendesha bunge kwa maslahi ya chama, lakini inaweza ikatokea Hali ya Kwamba - kwenye ushindani dhidi ya ukawa au chadema, CCM ikahitaji mgombea ambae hajachafuliwa na uchakachuaji wa rasimu ya tume ya warioba, hivyo hata Sitta kuwekwa pembeni na kuchukuliwa Watu Kama Mwandosya n.k.

Mazungumzo Kati ya rais na ukawa ni ya muhimu sana kuyafuatilia kwani ukawa wakiteleza tu kwa namna yoyote na kuishia kuleta tafsiri kwa wananchi Kwamba wameridhia katiba bora ije baada ya uchaguzi, na kwa sasa itumike katiba iliyofanyiwa marekebisho, Hapa Sitta anaweza Kabisa Tumia the loophole vizuri sana kuwa a strong contender ndani ya chama, na atakuwa na hoja nyingi tu Zenye mashiko Kujibu hoja za ukawa iwapo watakuja Tumia hoja ya katiba mpya kwenye kampeni za uchaguzi wa rais 2015.

All that said and done? As we speak, lawama juu ya kukwama kwa mchakato wa katiba mpya hazipo kwa rais Tena Bali kwa Sitta. Zitamuathiri vipi? Inategemeana na moves za ukawa.


Sent from my iPhone using JamiiForums

Let us suppose that UKAWA wanaingia mkenge na kusema wanakubali marekebisho kiasi ya katiba kuruhusu uchaguzi ufanyike..

Let us suppose hali hiyo inampa Samuel Sitta opportunity ya kuonekana Mesiah ndani ya CCM......

Does that really give him any chance of being a strong contender? Unajua kui-discredit tume ya Warioba tayari ni laana, Kuna wanaCCM wengi tu wanaoipinga hadharani rasimu ya tume ya Warioba, lakini nje wanaiona ni makini na yenye kutetea maslahi ya Tanzania.

So far kutokana na usaliti alioufanya SS sidhani ana fursa hata ndogo ya kuwa strong contender. And given aspiration of EL na force behind his bid, SS will be shattered in a sec.
 
Let us suppose that UKAWA wanaingia mkenge na kusema wanakubali marekebisho kiasi ya katiba kuruhusu uchaguzi ufanyike..

Let us suppose hali hiyo inampa Samuel Sitta opportunity ya kuonekana Mesiah ndani ya CCM......

Does that really give him any chance of being a strong contender? Unajua kui-discredit tume ya Warioba tayari ni laana, Kuna wanaCCM wengi tu wanaoipinga hadharani rasimu ya tume ya Warioba, lakini nje wanaiona ni makini na yenye kutetea maslahi ya Tanzania.

So far kutokana na usaliti alioufanya SS sidhani ana fursa hata ndogo ya kuwa strong contender. And given aspiration of EL na force behind his bid, SS will be shattered in a sec.
It's over kwa J.S.Sitta.
JK na CCM wamekwenda Dodoma kutafuta namna ya kutoka, wamemwacha Sitta nguo zikiteremka magotini.

Mzee kaadhirika vibaya, kapoteza meli na mzigo.
Huko CCM wapo wanaomuona kama msaliti dhidi ya tume, wanaomuona dhaifu sana katika uongozi n.k.
Hata akisimama na Lusinde, anaweza kushinda lakini kwa taabu.

Wapinzani wake wapo vijiweni wakichekelea maana moja ya jina ni off the list, na hilo ni la Sitta.

It's over kwa Sitta hata yeye amebaini. Msikilize akiongea ni kama simba aliyejeruhiwa vibaya.
 
SITTA AKAMILISHA SAFARI YAKE KISIASA
BORA TAIFA LIINGIE MATATUZONI YEYE APATE ULUWA WAKE

CCM YAPOTEZA DIRA, SASA NI GENGE LA WAHUNI
WENYE BUSARA WAKAA PEMBENI

Bunge la Sitta linamaliza kikao Dodoma. Kwa mtazamo wao katiba mpya itakayolivusha taifa kwa miongo mingi ijayo imekamilika.
Ni katiba iliyopendekezwa kwa mbinu hila na ulaghai

Wananchi wanaona vituko vya nchi hii. Nyaraka iliyotumia mamilioni ya fedha za umma na muda wa miaka 2, imeandikwa kwa siku chini ya 70 tena nyingine zikitumika katika maongezi na mipasho.

Rasimu ya Warioba ambayo ni msingi wa maoni ya wananchi imetupwa na ile ya CCM kuingizwa rasmi.

Miongoni mwa wanaCCM wapo wanaolaani uhuni uliohitimishwa Dodoma.
Ilikuwa ni bora liende, pesa zilizotolewa 'zitumike' kama alivyosema Sitta.

Sitta alipendekeza ya kuwashirikisha wazanzibar katika serikali ya muungano.
Tulieleza katika mabandiko ya duru kuwa, ilikuwa ni mbinu ya kuwavuta wazn ili kupata wanachokitaka.

Akaeleza kuhusu wafugaji na wakulima, jambo alilioliundia tume yake na kwa kutumia takwimu za watu 30.
Ni Sitta na CCM waliobeza takwimu za Warioba, leo wamepigia kura takwimu za watu 30 zilizotolewa na tume binafsi ya Sitta.

Ukitazama rasimu ya CCM, wznz wamepewa pipi na peremende ili kuendelea na mfumo husika.
Hilo Sitta amefanikiwa kama alivyotumwa na CCM

Wakati uozo ukiendelea, Rais wa nchi yupo kimya kwa fiuraha, mamilioni ya fedha za walipa kodi yakiteketea

Walichokiandika ni nyaraka isiyo na thamani. Walichopata ni allowance ikisemwa Sitta amekula 150 Milioni.

Kwa watu wanaoiangalia Tanzania kutoka nje, au kwa mtazamo tofauti, hili linaeleza kwanini sisi ni masikini.

Unapokuwa na mwenyekiti wa BMK kama Sitta ambaye ni waziri, kwa aliyofanya Dodoma utajiuliza kipi tofauti anachofanya katika majukumu yake mengine ndani ya serikali na nje anakotuwakilisha katika jumuiya ya EAC

Imefika mahali Sitta anaidhinisha kura kwa kutumia whatsupp, internet, facebook, fax na upuuzi wa aina hiyo

Ni upuuzi kwasababu nchi zenye wazee wanaotumia akili hili lisingejadiliwa.
Unawezaje ku verify kura ya mtu kwa kutumia whattsup au facebook.
Hadi hapo Rais Kikwete yupo sahihi anaposema '' hajui kwanini Tanzania ni masikini'' na hakika asingeweza kujua

Mbinu za Sitta ni kupata 2/3 na ametumia majina ya ''maruhani'' kuipata hiyo 2/3.
Hata kama ingepatika bila mbinu, zoezi zima limekosa uhalali wa kisiasa na utashi wa wananchi.

Lakini inapofikia mhali mzee kama Sitta anatengeneza nyaraka, majina bandia ya kura, na vimemo vya kununua kura, asitokee mtu akauliza kwanini Tanzania ni masikini.

Sitta ameshirikiana na mtu mwenye kuhusishwa na ufisadi katika nchi Chenge.
Kwa mazingira ya kawaida wenzetu wasingemfikiria Chenge hata kukanyaga Dodoma achilia mbali kuwa ndani ya bunge.

Leo ndie anaandika katiba ya kukabiliana na changamoto za ufisadi yeye akiwa mshiriki mzoefu.

Inawezekana madudu aliyofanya Sitta ya highschool yametokana na mchango wa maana wa akina Chenge.

Hawa wana uzoefu wa ''kuvunja'' maeneo kama benki kuu bila kukamatwa na ndio maana Sitta alitamba kimemo kimoja ni chake.

Naye kapewa experience ye wizi wa kura ambazo ni haramu hata bila kuiba. Kwanini Tanzania ni masikini, sijui.

Jambo moja tu ambalo litakumbukwa ni jinsi Sitta alivyotengeneza mazingira mazuri ya vurugu nchini.

Siku zaijazo tatizo, matatizo ya uhuni wa Dodoma ikiwemo vurugu za kupinga uhuni huo, mikono ya Sitta haitakuwa misafi.

Sitta amekamilisha safari ya kisiasa,akifutika katika vitabu, magazeti, majarida isipokuwa pale wahuni na wapuuzi watakapjadiliwa.

Safari yake imekamilika kwa aibu kubwa , tunampongeza kwa ushujaa wa kusimama mbele ya jamii bila haya,soni au majuto kutokana na upuuzi aliousimamia Dodoma.

Ingekuwa Japan, watu wanaolaaniwa na umma kama Sitta, jimaliza ili kuepuka aibu ya mbele ya jamii.
Sitta ni 'shujaa'' hana mtima wa aibu wala soni

Sitta ametumiwa na CCM na atabaki karatasi ya maliwato. Waliomtuma watamruka soon,atabaki peke yake
Wapinzani wake leo ni shangwe, wanajua katika majina wanayosikia, la Sitta halitakuwepo masikioni mwa wananchi tena

Kwa wananchi, Sitta ni tatizo kuliko umasikini wao.
Wakati wananchi wanapigana na adui ujinga, maradhi na umasikini,Sitta amesimama kusaidia maadui hao watatu dhidi ya wananchi.

Historia itamkumbuka Sitta kama inavyomkumbuka Chief Mangungo.

Akina Nyerere, Mkwawa,Mirambo, wanamapinduzi wa znz na wengi wanatisika kwa hasira huko makaburini walikopumzika.

Hii ndio Tanzania walioiota kwa miaka mingi? Hizi ndizo fadhila za waliotoa damu kuitafuta, kuitetea na kuilinda nchi hii?

Tusemezane
 
Back
Top Bottom