Kwa madereva: Tuliowahi kutokewa na mauzauza barabarani tupeane uzoefu

Kwa madereva: Tuliowahi kutokewa na mauzauza barabarani tupeane uzoefu

Zionist

JF-Expert Member
Joined
Dec 5, 2017
Posts
1,866
Reaction score
2,996
Habari wana JF,

Nimekua nikisikia kwamba barabarani Kuna vitimbwi vya mauza uza nikawa siamini, sasa ni juzi nilikua natoka Arusha kuelekea Kibaha. Nilifika sehemu jina silifahamu, ni kijiji baada ya kutoka Mombo.

Ni kwamba nikiwa kwenye mwendo alitokea mtu upande wa kushoto akawa anaingia barabarani Kama vile haioni gari nikapunguza mwendo na kupiga honi, nikitumaini jamaa atasimama ama kustuka, badala yake akaongeza spidi na kuliingia gari upande ule ule wa kushoto mimi na jamaa yangu tukasikia kishindo, side mirror ikavunjika ikaweka na kreki mbaya sana kwenye kioo cha mlango wa kushoto.

Nilisimamisha gari fasta tukashuka na kuangalia tunamuona yule mtu anakwenda tu kwa spidi ile ile, kama vile hakikutokea chochote. Tukawa tunashangaa basi yule mtu akaingia kama kwenye kichochoro Kati ya nyumba mbili, hii nyumba ya kulia Kuna jamaa alikua ameketi kibarazani amepaki pembeni gari aina ya vitz.

Tukamfuata jamaa yangu akamuuliza, Ndugu huyu mtu amekatiza hapa unamfahamu ? Maana tumemgonga na gari tumesimama ili tumtazame lakini cha kushangaza jamaa hakuanguka wala kuyumba ameelekea huku. Cha kushangaza tena, Jamaa akatuambia, nyie mpo salama? Tukamjibu ndio. Akasema basi shukuruni nyie endeleeni na safari. Nikamuuliza mbona hatuelewi?

Badala ya kujibu akabaki ametukazia macho jamaa yangu akanishika mkono na kunivuta tukaondoka. Lakini mpaka sasa hivi tumebaki na maswali vichwani mwetu.

Ni nini hasa kilitokea....

Asanteni
 
--ngoja nifupishe,

Nakumbuka kuna siku 2012 nimepanda basi ya kampuni ya Satelite kutoka tanga kuelekea dar nikiwa nimekaa siti za karibu na mbele niliona dereva amepiga mabreki mengi gari ikayumba na tukasikia mlio mkubwa kwenye eneo la engine,a ila akaimudu na kuiweka sawa na akaweza kupaki pembeni ya barabara.

Wadau tukamgeukia dereva , "kulikoni unataka kutumwaga ?"
Akatujibu kuwa alikua ameona Kanga (ndege jamii ya kuku) na akamgonga ndio yule tulisikia kwenye engine,
Tukashuka na eneo la mbele la engin likafunguliwa, hatukukuta damu, manyoya wala dalili zozote za kugongwa kitu ila kitu pekee tulichokikuta ni fan belt iliokatika.

Tukajaribu kukagua huku na kule hatukukuta kitu chochote na safari yetu ikawa ndio mwisho mpaka ilipoletwa basi nyingine kutuchukua.

Mpaka leo hii sijaweza kujua ni kitu gani kilitokea japo dereva alikomalia msimamo wake
 
Hiyo kawaida kabisa kwa sisi tunao safiri safari kila mkoa mara nyingine unamkuta bibi tena yule unaemfaham lakini alishakufa au mbabu na bakora mkononi wakati mwingine unaona picha ya jeneza kabisa limefunguliwa na sanda ipo au mtoto mdogo anatambaa yaani tushazoea wala hofu ile haipo tena.
Onyo.ukiona vitu kama hivyo usijaribu kukwepa au kushika break inakula kwako.
Mi kukna siku naenda dodoma niko na ford new model kuna kizee kilitokea vichakani kikasimama ghalfa barabarani haki ya (mungu mungu nisamehe)nilikaza mikono kushika steling vizuri nilimpa nikafumba macho ili nisione ninavyoua huwezi amini nilimpita na sikusikia kishindo chochote na nilienda mbele kama 4 klmtrs nikapaki gari kuangalia sikuona tatizo kwenye gari na niliendekea nabsafari yangu bila presure.
 
Jamaa yangu alikuwa kwenye spidi kubwa maeneo ya Mikumi,akatokea mtu anakuja kwa kasi kuelekea kwenye gari,alikuwa na mwenzake kwenye gari akamwambia mgonge usifunge break,jamaa akanyoosha,walisikia kishindo na mtu alieogongwa amepita kwenye kioo cha mbele kuelekea nyuma,hawakusimama walipofika Mikumi kwenye mji wakasimama na kuchukua chumba,kesho yake wanaangalia gari halina mchubuko wala taa iliovunjika,kufika Dar jamaa akaamua kuuza gari...
 
Kuna siku ilikuwa 2007. Nikitoka Arusha kwenda Dar saa Saba Nane usiku nilikuwa napita maeneo ya kwedikwazu. Kuna mahala Barbara imenyooka Sana Basi nikawa natembea speed 100-120.
Kuna mrembo mmoja mdada akawa anasimamisha gari akiomba lift. Nikapiga taa kubwa kumwona vizuri mrembo haswaa, sikusimama nikanuoosha goti, huku najiuliza huyu anaenda Wapi saa hizi,. Bwana ile nampita kwa speed ile alinipiga busu Mara tatu hapo dirishani. Maana sikuwa nimefunga madirisha ili nipigwe upepo nisilale. Nilifika dar Sina raha kutwa nzima.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna siku ilikuwa 2007. Nikitoka Arusha kwenda Dar saa Saba Nane usiku nilikuwa napita maeneo ya kwedikwazu. Kuna mahala Barbara imenyooka Sana Basi nikawa natembea speed 100-120.
Kuna mrembo mmoja mdada akawa anasimamisha gari akiomba lift. Nikapiga taa kubwa kumwona vizuri mrembo haswaa, sikusimama nikanuoosha goti, huku najiuliza huyu anaenda Wapi saa hizi,. Bwana ile nampita kwa speed ile alinipiga busu Mara tatu hapo dirishani. Maana sikuwa nimefunga madirisha ili nipigwe upepo nisilale. Nilifika dar Sina raha kutwa nzima.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hee mkuu alikupigaje mkuu daaaah???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna siku ilikuwa 2007. Nikitoka Arusha kwenda Dar saa Saba Nane usiku nilikuwa napita maeneo ya kwedikwazu. Kuna mahala Barbara imenyooka Sana Basi nikawa natembea speed 100-120.
Kuna mrembo mmoja mdada akawa anasimamisha gari akiomba lift. Nikapiga taa kubwa kumwona vizuri mrembo haswaa, sikusimama nikanuoosha goti, huku najiuliza huyu anaenda Wapi saa hizi,. Bwana ile nampita kwa speed ile alinipiga busu Mara tatu hapo dirishani. Maana sikuwa nimefunga madirisha ili nipigwe upepo nisilale. Nilifika dar Sina raha kutwa nzima.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mzee Ulikuwa Kwenye Bajaji Ama Gari Lenye Speed Ya Maana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
M
Mimi mwaka juzi nakumbuka natoka zangu club nilimuona mwanamke wa kizungu barabarani kavaa baibui mrefu mzuriiiii...ilikuwa kama saa tisa usiku kasimama peke yake. Naamini alikuwa jini
Mimi huwa nanyoosha goti tu sikwepi kitu mwaka 1993 nilimkwepa mbuzi nikajikuta niko mtaroni hata mbuzi simuoni tena LEYLAND la watu likiwa chakari cabin imebonyea ila sikuumia
 
Sijawahi kushuhudia though kuna ndugu yangu anaendesha magari makubwa ya mizigo anapiga route za congo, zambia , rwanda , burundi nk story kama hizo huwa anatuhadithia sana mauza uza wanayokutana nayo barabarani nyakati za usiku.
 
Mwaka huu nipo na Toyota Ipsum new model maeneo ya Gairo naitafuta Dodoma mida kama ya saa tano usiku hivi, ghafla naiona gari toyota carina SI imesimama mbele yangu.

Sijui nini kilitokea ila niliingia nzima nzima wala hakukuwa na kishindo cha magari kugongana ila tairi zilipiga kelele sana maana nilijaribu kuzuia brake na wala hakukuwa na uharibifu wa gari.

Mpaka leo sielewi ile gari ilitokea wapi na kama uchawi basi umeadvance.
 
Kuna siku ilikuwa 2007. Nikitoka Arusha kwenda Dar saa Saba Nane usiku nilikuwa napita maeneo ya kwedikwazu. Kuna mahala Barbara imenyooka Sana Basi nikawa natembea speed 100-120.
Kuna mrembo mmoja mdada akawa anasimamisha gari akiomba lift. Nikapiga taa kubwa kumwona vizuri mrembo haswaa, sikusimama nikanuoosha goti, huku najiuliza huyu anaenda Wapi saa hizi,. Bwana ile nampita kwa speed ile alinipiga busu Mara tatu hapo dirishani. Maana sikuwa nimefunga madirisha ili nipigwe upepo nisilale. Nilifika dar Sina raha kutwa nzima.

Sent using Jamii Forums mobile app
Trople Kiss!? Maimuna huyo!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom