Kwa madereva: Tuliowahi kutokewa na mauzauza barabarani tupeane uzoefu

Kwa madereva: Tuliowahi kutokewa na mauzauza barabarani tupeane uzoefu

--ngoja nifupishe,

Nakumbuka kuna siku 2012 nimepanda basi ya kampuni ya Satelite kutoka tanga kuelekea dar nikiwa nimekaa siti za karibu na mbele niliona dereva amepiga mabreki mengi gari ikayumba na tukasikia mlio mkubwa kwenye eneo la engine,a ila akaimudu na kuiweka sawa na akaweza kupaki pembeni ya barabara.

Wadau tukamgeukia dereva , "kulikoni unataka kutumwaga ?"
Akatujibu kuwa alikua ameona Kanga (ndege jamii ya kuku) na akamgonga ndio yule tulisikia kwenye engine,
Tukashuka na eneo la mbele la engin likafunguliwa, hatukukuta damu, manyoya wala dalili zozote za kugongwa kitu ila kitu pekee tulichokikuta ni fan belt iliokatika.

Tukajaribu kukagua huku na kule hatukukuta kitu chochote na safari yetu ikawa ndio mwisho mpaka ilipoletwa basi nyingine kutuchukua.

Mpaka leo hii sijaweza kujua ni kitu gani kilitokea japo dereva alikomalia msimamo wake
Alishikwa na bumbuwazi , katika hali hiyo angeeleza nini ? Ni vitu visivyoelezeka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa yangu alikuwa kwenye spidi kubwa maneneo ya Mikumi,akatokea mtu anakuja kwa kasi kuelekea kwenye gari,alikuwa na mwenzake kwenye gari akamwambia mgonge usifunge beak,jamaa akanyoosha,walisikia kishindo na mtu alieogongwa amepita kwenye kioo cha mbele kuelekea nyuma,hawakusimama walipofika Mikumi kwenye mji wakasimama na kuchukua chumba,kesho yake wanaangalia gari halina mchubuko wala taa iliovunjika,kufika Dar jamaa akaamua kuuza gari...
Kama una roho nyepesi ndio mwisho wa kuendesha masafa marefu [emoji851][emoji851]


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna siku ilikuwa 2007. Nikitoka Arusha kwenda Dar saa Saba Nane usiku nilikuwa napita maeneo ya kwedikwazu. Kuna mahala Barbara imenyooka Sana Basi nikawa natembea speed 100-120.
Kuna mrembo mmoja mdada akawa anasimamisha gari akiomba lift. Nikapiga taa kubwa kumwona vizuri mrembo haswaa, sikusimama nikanuoosha goti, huku najiuliza huyu anaenda Wapi saa hizi,. Bwana ile nampita kwa speed ile alinipiga busu Mara tatu hapo dirishani. Maana sikuwa nimefunga madirisha ili nipigwe upepo nisilale. Nilifika dar Sina raha kutwa nzima.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa sisi tunaoenda safari ndefu, tunaambiwa hao ni majini wasumbufu tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nishakutana na mwanamama,anatembea katikati ya barabara saa 7 usiku ukipita chalinze mjini kama km 15 kwendea dar,nilimkwepa na nilikua zaidi speed 120,niliokua nao kwenye gari wakanilaumu sana kwann sikumgonga eti yule ni jini,nikawaambia mbona nimemkwepa na tunaendelea na safari,kuna wengine wanakua wamerukwa akili tu,unamgonga then unafupisha maisha ya binadamu mwenzio kwa ajili ya kuamini imani za ajabu ajabu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna siku ilikuwa 2007. Nikitoka Arusha kwenda Dar saa Saba Nane usiku nilikuwa napita maeneo ya kwedikwazu. Kuna mahala Barbara imenyooka Sana Basi nikawa natembea speed 100-120.
Kuna mrembo mmoja mdada akawa anasimamisha gari akiomba lift. Nikapiga taa kubwa kumwona vizuri mrembo haswaa, sikusimama nikanuoosha goti, huku najiuliza huyu anaenda Wapi saa hizi,. Bwana ile nampita kwa speed ile alinipiga busu Mara tatu hapo dirishani. Maana sikuwa nimefunga madirisha ili nipigwe upepo nisilale. Nilifika dar Sina raha kutwa nzima.

Sent using Jamii Forums mobile app
Duuh mkuu aliweza kuja dirishani huku upo speed hyoo?

mndamba kutoka Ifakara
 
M

Mimi huwa nanyoosha goti tu sikwepi kitu mwaka 1993 nilimkwepa mbuzi nikajikuta niko mtaroni hata mbuzi simuoni tena LEYLAND la watu likiwa chakari cabin imebonyea ila sikuumia
Mkuu, now ushakuwa mzoefu

mndamba kutoka Ifakara
 
Ndoto, usingizi na imani za kishirikina.

Hakuna kitu. Why usiku na si mchana??

Why barabarani tu na si njia ya train, Angani au Majini??.

Story za abunwasi na changamsha genge.

Nishasafiri Barabara nyingi, masaa yote kuspan 24 hours sijashuhudia hayo.

Ulongo tu na kutiana woga, kuwapa ulaji waganga wa kienyeji wafanye zindiko.
 
Back
Top Bottom