Kama haya mambo ya mikataba wataendelea kuachiwa CCM peke yao wayafanye, nina hakika kuna siku litatokea kubwa zaidi ndio akili zetu zitakaa sawa, nionavyo sasa hivi hii issue ya ripoti ya CAG imepokelewa kwa ushabiki zaidi watu badala wajadili namna ya kumaliza tatizo wanapoteza muda wote kumshambulia marehemu, wameshasahau system iliyomuweka marehemu madarakani bado tunayo mpaka sasa na ndio hiyo hiyo bado inatuwekea viongozi mpaka leo kwa sababu ya ubovu wa Katiba yetu.
Kila mwaka kila awamu CAG hutoa ripoti za aina hii, japo sasa wanajiliwaza huu ufisadi uliotokea haujawahi kutokea kabla, ni kama vile wanasema na wamekubali bora waibiwe kidogo kuliko kuibiwa sana, lakini hata kama hayo madudu hufuniliwa kila mwaka, wahusika huchukuliwa hatua gani? mara zote hulindana, ila bado tunapoteza muda mwingi kushangilia mambo ambayo hujirudia kila mwaka badala ya kutafuta solution ya tatizo angalau ya muda mfupi.
Nachojifunza kwenye hili sakata la ripoti ya CAG, ni kama vile watu walikuwa na chuki binafsi na mwendazake na sio chama chake au system iliyomuweka madarakani, na lakushangaza zaidi hao wapiga filimbi wengine ni "plastic opposition fans" wanaosikia mdundo wa ngoma lumumba, wao wanakata mauno mtaa wa tatu.
Nionavyo, ni bora sasa hii mikataba inayoingia serikali iwekwe wazi kila mwananchi aione, iwe ni kutangazwa kwenye magazeti ya serikali au pengine popote, muhimu mikataba iwekwe wazi watu waisome waichambue kabla ya kusaini na hayo makampuni, kuendelea kushangilia madudu yanayotangazwa na CAG kila mwaka tutadumaa kama taifa, ama sivyo tutaendelea kuchezeshwa ngoma na CCM kila wakati.