Kwa ‘madudu’ haya kwenye ripoti ya CAG, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa achia ngazi

Kwa ‘madudu’ haya kwenye ripoti ya CAG, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa achia ngazi

Kwa nini Majaliwa tu?? SAMIA SULUHU HASSAN inabidi naye ajiuzulu, tungekuwa na bunge msumeno lingepiga VOTE of No Convidence hawa wote waondoke, hata madudu yalilindwa na wao, waondoke Uchaguzi mwingine ufanyike. Au apewe Interim President tuweke katiba MPYA. Full spot.
Ukisema tupige kura tena, wagombea ni akina nani? Ni haohao waliopo kwenye system.
 
Unaonekana mwelewa na asante..

1. Hasara ya ATCL inatokana na Break Even point ama upya wa biashara yake na corona...

Unaweza kukubaliana na hilo?
 
Kwa nini Majaliwa tu?? SAMIA SULUHU HASSAN inabidi naye ajiuzulu, tungekuwa na bunge msumeno lingepiga VOTE of No Convidence hawa wote waondoke, hata madudu yalilindwa na wao, waondoke Uchaguzi mwingine ufanyike. Au apewe Interim President tuweke katiba MPYA. Full spot.

Siyo siri kuwa VP alikuwa marginalized na mwendazake.

Kazi zake zilikuwa kumwakilisha misibani na kufungua vyoo mashuleni.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Kwa nini Majaliwa tu?? SAMIA SULUHU HASSAN inabidi naye ajiuzulu, tungekuwa na bunge msumeno lingepiga VOTE of No Convidence hawa wote waondoke, hata madudu yalilindwa na wao, waondoke Uchaguzi mwingine ufanyike. Au apewe Interim President tuweke katiba MPYA. Full spot.

Siyo siri kuwa VP alikuwa marginalized na mwendazake.

Kazi zake zilikuwa kumwakilisha misibani na kufungua vyoo mashuleni.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Kujiuzulu hakutasaidia, bali wakiri udhaifu na wakubali kujirekebisha.
Mama aanzishe Mchakato wa katiba mpya itakayo towa mwanya kwa wakosefu kuchukuliwa hatua badala ya kulindwa na katiba, akiwemo Raisi mwenyewe.

Kujiuzulu ni dhana muafaka ya kuonyesha uwajibikaji.

Mzee ruksa aliwajibika kwa mapungufu ya waliokuwa chini yake.

Kujiuzulu ingempa heshima kuliko hali hii ya kuja kufurushwa unceremoniously.
 
Majaliwa anatakiwa kuachia ngazi haraka

Huyu kama haachii mwenyewe mama amsaidie kuondoka fasta tu.

1. Matumizi Jan - March
2. Ripoti ya tume ya ukimwi

Haviwezi kumwacha salama.

Ana jipya lipi la kutwambia?

Na akwende tu!
 
Rais wetu mwacheni inawezekana mwenda zake alikuwa hashauriki!

Mwache arekebishe yale aliyokuwa anashauri na kubakia kuzodolewa!

Huyu ndo anafahamu mapungufu yote! Nitamtetea mpaka pale itakapoonekana na yeye anaelekea mle.mle mwa mwandazake!

Msije kuishia kule kule mlipoanzia kumsema JK dhaifu then mkaletewa Dikteta ambaye kila mtu alikuwa analia na kusaga meno. Mara mtamzania kashasahau.

Tumwache arudishe nchi inapotakiwa kuwa! Huenda tukapata hata katiba mpya kipindi hiki!
Tatizo watanzania wengi ama hawasomibau ni wasahaulifu, mnasahau yeye alikuwa mwenyekiti mwenza wa bunge la katiba, mnataka Majaliwa ajiuzulu wakati huohuo mnasema rais alikuwa hashauriki hamuoni marai yenu yamebeba ajenda fulani
 
Ripoti hii ya CAG imeacha Serikali uchi na Waziri Mkuu kiongozi wa shughuli za kila siku za Serikali na msimamizi wa shughuli za Serikali za kila siku anapaswa aachie ngazi mara moja.

Ni aibu kwa madudu haya mpaka sasa upo ofisini, unafanya nini? Ona aibu mwenyewe uchukue hatua kwa heshima yako.

Nashangaa Mawaziri wanavyokuwa na makamera kuwajibisha vidagaa, wakuu wa shule kisa milioni 2 haikufanya manunuzi sahihi na huku mapapa wanakula watakavyo.

Kassim Majaliwa must go
"Kume kucha kume kucha, mambo ni moto"
 
makamu wa rais ni kivuli tu na ukizingatia aina ya rais tuliyekuwa nae huwezi kutoa lawama hata 0%..
Kuna watu wanataka waziri mkuu ajiuzulu kwa sababu alikuwepo wakati madudu yanafanyika lakini kwanini unamkimbilia waziri mkuu unaacha msaidizi wake wa karibu
 
Unaonekana mwelewa na asante..

1. Hasara ya ATCL inatokana na Break Even point ama upya wa biashara yake na corona...

Unaweza kukubaliana na hilo?
Asante sana mkuu, hakika una hoja za kuchangamsha kuchwa kuliko wengine. Sasa twende pamoja,

Sikatai kwamba, Corona Virusi ni sababu moja wapo ilioakisi hasara ya ATCL na mashirika mengine ya ndege duniani, ila Corona sio sababu ya kusababisha Beyond Margin Loss kutoka 2015 - 2021 kwa Air Tanzania.

1) Corona Virus ilianza mwaka 2019 (Covid-19). Hasara ya ATCL ilianza 2015 mpaka 2021. Kuna utofauti wa miaka 4 hapo ambayo Corona haikuwepo na haiwezi kutumika kama sababu kuu.

2) Air Tanzania route zake nyingi ni za ndani ya nchi, kila siku. Kwa Tanzania, Corona haijawahi kusababisha route za ndege kusimamishwa (Hakuna Lock Down) wala biashara kufungwa. - Ingekua Air Tanzania route zake zote ni za nje ya nchi, basi ningekubaliana na wewe.

3) Air Tanzania ndio ilikua kitovu cha serikali ya magufuli kuuwa mashirika ya FAST JET na PRECISION AIR ili shirika liweze kufanya MONOPOLY YA BIASHARA YA ANGA. Na ilifanikiwa kuwakandamiza mahasimu wake kibiashara.

4) Shirika la ndege la Air Tanzania lilianzishwa mnamo mwaka 1977 (Kama Sijakosea) baada ya kufa kwa EAC, hivo shirika la Air Tanzania sio GENI/JIPYA kibiashara ya maswala ya ndege na anga. Sikatai halikuwa na ndege na mengineyo mengi:

Maswali;

A) Swala la upya wa biashara kwa shirika lenye umri zaidi ya miaka 44 inakuja akilini kweli??? Kwa muda wote huo hawaijui biashara ya ndege na utendaji wake kazi???

B) Upya wa biashara au kufufua biashara unachukua zaidi ya miaka 5 tena kwa shirika lenye kukingiwa kifua na dola na lililo na msamaha wa kodi???

C) Corona imeathiri vipi biashara ya Air Tanzania, wakati shirika linategemea route za ndani ya nchi (Geita, Mwanza, Dar n.k) ambazo hazikufungwa kwasababu ya Corona???

KUMBUKA: Magufuli alituaminisha shirika la ATCL linaendeshwa kwa faida, na kufikia kutoa gawio kwa serikali la faida kwa kutumia vyombo vya habari - HII NAYO IMEKAAJE MKUU???
 
Professor Assad

Tuna BUNGE DHAIFU!! alikuwa sahihi kabisa na bado yupo sahihi mpaka sasa ndo maana alistaafishwa kwa lazima!!
 
Kuna watu wanataka waziri mkuu ajiuzulu kwa sababu alikuwepo wakati madudu yanafanyika lakini kwanini unamkimbilia waziri mkuu unaacha msaidizi wake wa karibu

Ina maana utakuwa umemsahau aliyekuwa karibu yake zaidi? Yule aliyekuwa anaongea naye mara kwa mara kiasi cha kutujulisha kuwa yuko busy na mafaili?

Yule aliyetufahamisha rais ana work plan yake isiyohojiwa na mtu?

Aliyetufahamisha kuwa rais si wa kuzurura magomeni au kariakoo?

Huyu ndiye aliyekuwa mtendaji mkuu pamoja na mwendazake.

Wajameni huyu angali bado ofisini anafanya nini?
 
Hata Rais wa sasa aachie ngazi maana alikuwa sehemu ya serikali, hilo jambo haliwezekani wote waliohusika na ubadhilifu washugulikiwe ikiwemo spika kwani alionywa muda mrefu kwa bunge kushindwa kuisimamia serikali.
Sasa mtapata akili, watu wanadai katiba mpya ili iongoze nchi hamkutaka
Leo haya ni maneno tu hakuna was kuwawajibisha viongozi, kwa Sheria ipi au katiba ipi?

Kwa mujibu wa katiba waziri mkuu siku alipofariki magufuli nae uwazi alikuwa hana uwaziri na Baraza lote kuvunjwa.

Watanzania wapumbavu Sana, kwenye masuala ya faida kwa taifa mnagawanyi.
 
Kama katiba ni hii inayomfanya Raid kuwa mungu mtu PM tunamuonea bure tu. Tuangalie tulipojikwaa so ltulipoangukia, katiba ni muhimu.

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
 
Qmmke labda wavuliwe kwa nguvu, Mwana CCM ajiuzulu we uliskia wapi ?
 
Hii ripoti ya CAG imetuonyesha,kutufundisha na kutuonya kuwa tunahitaji taasisi imara na siyo mtu mmoja mwizi na fisadi anayejidai na kujinadi imara.
Alikuwaa anasema Chagua Magufuli, mara Serikali yangu, Mara ccm ya Magufuli, blah blah kibao. Awamu zilizopita waliiba, ila hii ya jamaa wamekomba
 
Ripoti hii ya CAG imeacha Serikali uchi na Waziri Mkuu kiongozi wa shughuli za kila siku za Serikali na msimamizi wa shughuli za Serikali za kila siku anapaswa aachie ngazi mara moja.

Ni aibu kwa madudu haya mpaka sasa upo ofisini, unafanya nini? Ona aibu mwenyewe uchukue hatua kwa heshima yako.

Nashangaa Mawaziri wanavyokuwa na makamera kuwajibisha vidagaa, wakuu wa shule kisa milioni 2 haikufanya manunuzi sahihi na huku mapapa wanakula watakavyo.

Kassim Majaliwa must go
ni haibu, hadi kwenye ofisi yake kuna madudu. Tangu aseme uwongo akiwa msikitini kuhusu ugonjwa wa JPM, sina imani naye tena. Ogopa mtu anayesema uwongo msikitini...
 
Back
Top Bottom