Kwa ‘madudu’ haya kwenye ripoti ya CAG, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa achia ngazi

Kwa ‘madudu’ haya kwenye ripoti ya CAG, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa achia ngazi

Ripoti hii ya CAG imeacha Serikali uchi na Waziri Mkuu kiongozi wa shughuli za kila siku za Serikali na msimamizi wa shughuli za Serikali za kila siku anapaswa aachie ngazi mara moja....
Kwa hicho ulichokiandika unamwonea waziri mkuu.
Waziri wa fedha kwa kipindi husika, Tamisemi, Mwenyekiti kamati PAC/Local governmanet, makamu wa Rais kipindi husika, mwanasheria mkuu wa serikali kipindi husika, mawaziri na makatibu wakuu katika wizara na idara kwa kipindi husika na ripoti ya kukaguliwa CAG nayo iwekwe bayana.

Wote waliowahi kuhudumu katika serikali na mashirika ya umma kwa kipindi husika kwenye nafasi ya utangaji sera na maamuzi.

WAJIUZULU
1. Wanasiasa-Uchaguzi mpya uitishwe.

2.Watendaji-ajira zisitishwe na uchunguzi wa kijinai ufanyike kisha hatua za kisheria zichukue mkondo wake;

3. Ipigwe kura ya kutokuwa na imani na serikali iliyopo kwa kuanza kuwalaghai wananchi kana kwamba hawakuwemo kama sehemu ya ubadhirifu na upotevu wa mali ya umma.

4. Rais iliyepo anaonesha kwa uwazi kabisa alikuwa na nongwa na hayati ila wakati wa uhai wake aliifichakwa sababu anazozijua mwenyewe.

Wananchi wanafahamu vizuri hatua kwa hatua ni kilitokea baada ya kutoka kufungua mradi wa polisi huko Kurasini, kujisikia vibaya, kukimbizwa muhimbili kisha kuhamishiwa hospitali ya Mzena hadi mauti.

Viongozi wa kisiasa, watendaji wa serikali, mashirika ya umma, wafanyabiashara na viongozi wa kidini (sio wa kiroho) ACHENI kuonesha chuki na VISASI vyenu dhahiri kwa umma dhidi ya hayati na wateule wake huku mkijua milkuwa sehemu ya hali hiyo. Kwa sasa hata mkichafua namna gani hayati Magufuli hao wananchi wa chini ambao ndio wapiga kura hawawezi kuwaelewa kwa vyovyote vile. Mlitakiwa msubiri muanze kuonesha mabadiliko halisi badala ya maneno matupu.

Kwa sa Tanzania itakuwa na historia ya uongozi wa kisiasa kwa ngazi ya Rais kwa kipindi kimoja tu kutoka ichama tawala hadi cha upinzani hata kama hakuna katiba mpya. Mnaweza kuleta ubishi kwamba watumia dola, hilo haliwezekani na somo halisi mtafundishwa muda mchache ujao.

Kuna chama cha upinzani kitashika madaraka pamoja na kwamba walikuwa wakosoaji wakubwa na kuzusha hofu kwamba wanaweza kuhatarisha amani ya nchi, itakuwa kinyume chake, hatafanya visasi, hatadharau jitihadi za viongozi waliotangulia na watachochea maendeleo ya kweli na kuaminiwa sana.

Kesho inaijua Mungu pekee hakuna mwenye hati na dhamana ya pumziko la wajibu.
 
Watu wazima wanaongea... Asante.
1. Upya ni kuanzia ndege mpya ambapo hasara ilikuwa 113B na sasa tuna 60B ambapo faida ipo ila inaliwa na running cost.

Projection ya BEP ilikuwa 5yrs tukakwama kwa corona.

2. Ndege kubwa hazikuwa intended kwa usafiri wa ndani ambapo tayari tunaenda ndani kwa sasa na nchi kama 5 za jirani.

Tayari tulipewa route ya UK tukakwama kutokana na restrictions za corona. Pia tunakamilisha route ya France nayo corona kikwazo.

3. Ndege zinatengeneza faida ila faida yake inamezwa na running cost katika upya wake. Hivyo kusema kuwa ndege haziingizi faida na kuamini kuwa hasara ya ATCL ni uzembe ama ufisadi sio kweli.

4. Biashara ya ndege ililenga kukuza utalii kwa maana ya wengi walikuwa wakienda Kenya then wanavuka kwa gharama nafuu kuingia TZ hivyo kuifaidisha Kenya na kwa sasa baada ya ndege utalii umekuwa sana. Hivyo ni kama matunda ya ndege yameonekana kwenye utalii.

Sio mjuaji ila najaribu ku share kidogo ninachokijua..

Kosoa na nipe mtazamo wako

Asante
View attachment 1747395
Naam mkuu, asante kwa kuniumiza kichwa,

Kwa upande wangu, lawama hizi ni za serikali na hawazikwepi. Kwanini lawama za serikali;

Shirika la ndege ATCL lilikua na ndege moja iliokua ikihudumu kuanzia mwaka 2011, ndege hio ilikua BOMBARDIER DASH-8 Q 300. Shirika lilikua linajivuta vuta kama mgonjwa mahututi (Wa leo au Wa Kesho).

Baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani mwaka 2015, alionesha nia nzuri sana ya kulifufua shirika hilo la ATCL jambo ambalo sisi raia tungefurahi sana kama angefanikiwa kulifufua shirika hilo. Ila alipokuja kupotea njia ni kwenye utekelezaji wa jinsi ya kulifufua;

Kwanini nasema hivo,

1) Mwaka 2016 alinunua ndege tatu BOMBARDIER DASH-8 Q 400

2) Mwaka 2018 (Kati ya Mwezi Julai au June) alinunua ndege tatu tena, BOMBARDIER CS300 mbili na BOENG 787 DREAMLINER.

3) Baada ya hapo akanunua ndege moja nyingine, AIRBUS A220-300.

Ndege hizo alinunua kwa hela taslimu (Cash), kwa muda mfupi sana hata kabla ya;

A) Hakuweka mazingira mazuri kwanza katika uongozi wa shirika la ATCL na matawi yake (Alichofanya ni kuwafunga waliokua viongozi wa shirika kwa kesi za uhujumu uchumi).

B) Hakuandaa mazingira mazuri ya kibiashara kwaajili ya shirika la ATCL, wala route za kibiashara kuandaliwa za ndani na nje ya nchi (Alichofanya ni kuzifungia kampuni ndogo za ndege kama FAST JET na PRECISION AIR - Akihisi wateja watahamia tu kwa ATCL watake au wasitake).

C) Alikurupuka kununua ndege nyingi kwa muda mfupi na kwa hela taslimu, kabla hata shirika halijaweza kuendesha ndege chache zile 3 za mwanzo kwa faida (Hata kabla route ya ndege 3 za mwanzo kupata, zikaletwa nyingine). Na matarajio yake hela zile zirudi ndani ya muda mfupi wa awamu yake ya kwanza ya utawala.

D) Hakujiandaa na maswala ya maamuzi ya mungu (Act Of God), mfano Ajali na Corona, mambo ambayo hayapo katika uwezo wa binaadamu kuyatarajia au kuyaepuka.

Swala la kufufua ATCL kwa kasi ile haikuwa na mantiki, lilifufuliwa bila kufanyika kwa RESEARCH wala kuandaliwa kwa STRUCTURE YA BIASHARA, lilifufuliwa kwa speed kubwa sana hata kabla ya shirika kuweza kusimama lenyewe.

Wajuzi wa biashara ya anga, walitarajia shirika kuendeshwa kwa hasara kubwa na mwisho wake baadhi ya ndege kuuzwa kwa bei ya hasara.

Nawasilisha,
 
Kuitaja hata hio milioni 2 naona aibu ...milioni 2 kwa hao mapapa waliopiga nchi mabilioni, ni kama hela ya chai tu au kununua boksa au soksi zao
 
Uzalendo wa sasa ni sawa na ujambazi, unyang'anyi, uporaji, unafiki, ujangili na unyang'au. Ukiambiwa wewe sio mzalendo kafanye sherehe na toa sadaka ya shukrani.
 
Sasa mtapata akili, watu wanadai katiba mpya ili iongoze nchi hamkutaka
Leo haya ni maneno tu hakuna was kuwawajibisha viongozi, kwa Sheria ipi au katiba ipi?...
Wewe ndio mpumbavu frustration zako tafuta pa kuzitolea haya mambo hayakuanza leo cag Assad alipotoa ripoti ya mwisho alizunfumzia udhaifu wa bunge na akaitwa na Ndugai leo Ndugai anapingana na hayati mnamshangilia
 
Mama kaamua kumuumbua, alikuwa na uwezo wa riport kuificha kama zile za miaka ya nyuma
 
Sijiuzuru mkuu nenda kanishtaki mahakama ya Dunia ya uhalifu.
 
Kuna watu wanataka waziri mkuu ajiuzulu kwa sababu alikuwepo wakati madudu yanafanyika lakini kwanini unamkimbilia waziri mkuu unaacha msaidizi wake wa karibu
waziri mkuu ni mtendaji na kiongozi wa mawaziri mkuu.....sio sawa na msaidizi na makamu wa rais..
 
Hahaha Kama unadhani kujiuzuru kwa mwanasiasa ni rahisi, muulize Wassira kwani toka enzi za Nyerere hadi leo anasumbuana na 'binti' yake Bulaya ubunge.
 
Habari wakuu! Habari kubwa iliyozima mambo ya Asas na Tanga fresh jana na leo ni reports ya CAG,huku tukiendelea kupata MADUDU mbalimbali yaliyomo humo ndani je tutegemee hatua gani zitachukuliwa au zinapaswa kuchukuliwa?! Je waliotajwa kweny mambo mbalimbali yahusio ubadilifu was a pesa watakamatwa au report hii huwa haitoi uhalali wa kuhoji kitu? Au mpaka Rais aseme wakamatwe ?
Kwa anaejua atupe ufafanuzi wa kisheria au kikatiba.
 
Nakili kuwa sio mtaalam wa mambo ya ndege hivyo sintabisha chochote..

Badala yake umeniongezea uelewa.

Thanks bro
Naam mkuu, asante kwa kuniumiza kichwa,

Kwa upande wangu, lawama hizi ni za serikali na hawazikwepi. Kwanini lawama za serikali;

Shirika la ndege ATCL lilikua na ndege moja iliokua ikihudumu kuanzia mwaka 2011, ndege hio ilikua BOMBARDIER DASH-8 Q 300. Shirika lilikua linajivuta vuta kama mgonjwa mahututi (Wa leo au Wa Kesho).

Baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani mwaka 2015, alionesha nia nzuri sana ya kulifufua shirika hilo la ATCL jambo ambalo sisi raia tungefurahi sana kama angefanikiwa kulifufua shirika hilo. Ila alipokuja kupotea njia ni kwenye utekelezaji wa jinsi ya kulifufua;

Kwanini nasema hivo,

1) Mwaka 2016 alinunua ndege tatu BOMBARDIER DASH-8 Q 400

2) Mwaka 2018 (Kati ya Mwezi Julai au June) alinunua ndege tatu tena, BOMBARDIER CS300 mbili na BOENG 787 DREAMLINER.

3) Baada ya hapo akanunua ndege moja nyingine, AIRBUS A220-300.

Ndege hizo alinunua kwa hela taslimu (Cash), kwa muda mfupi sana hata kabla ya;

A) Hakuweka mazingira mazuri kwanza katika uongozi wa shirika la ATCL na matawi yake (Alichofanya ni kuwafunga waliokua viongozi wa shirika kwa kesi za uhujumu uchumi).

B) Hakuandaa mazingira mazuri ya kibiashara kwaajili ya shirika la ATCL, wala route za kibiashara kuandaliwa za ndani na nje ya nchi (Alichofanya ni kuzifungia kampuni ndogo za ndege kama FAST JET na PRECISION AIR - Akihisi wateja watahamia tu kwa ATCL watake au wasitake).

C) Alikurupuka kununua ndege nyingi kwa muda mfupi na kwa hela taslimu, kabla hata shirika halijaweza kuendesha ndege chache zile 3 za mwanzo kwa faida (Hata kabla route ya ndege 3 za mwanzo kupata, zikaletwa nyingine). Na matarajio yake hela zile zirudi ndani ya muda mfupi wa awamu yake ya kwanza ya utawala.

D) Hakujiandaa na maswala ya maamuzi ya mungu (Act Of God), mfano Ajali na Corona, mambo ambayo hayapo katika uwezo wa binaadamu kuyatarajia au kuyaepuka.

Swala la kufufua ATCL kwa kasi ile haikuwa na mantiki, lilifufuliwa bila kufanyika kwa RESEARCH wala kuandaliwa kwa STRUCTURE YA BIASHARA, lilifufuliwa kwa speed kubwa sana hata kabla ya shirika kuweza kusimama lenyewe.

Wajuzi wa biashara ya anga, walitarajia shirika kuendeshwa kwa hasara kubwa na mwisho wake baadhi ya ndege kuuzwa kwa bei ya hasara.

Nawasilisha,
 
Sio huyo tu hata spika Ndugai kwa kutoishauri serikali vizuri. Mama Samia apange Safu yake vizuri
Hata mama SAMIA nae atoke zake hafai kuendelea kuwepo pale na yeye ni jizi tu kama majizi mengine. Utanishangaza kwamba mtuhumiwa namba mbili unamruka kwenda kuwajibisha mtuhumiwa namba tatu. Since mtuhumiwa namba moja hayupo tunamshukia namba mbili na wengine chini yake wote timua ofisini tuanze upya
 
Hawa wahe. Mawaziri, Manaibu waziri, Makatibu wakuu na wakuu wa Idara mbalimbali wanapaswa watizamwe kwa JICHO KUBWA LA TATU. lkn pia BUNGE LETU linapaswa lifanye kazi yake kikamilifu kuisimamia serikali.
 
Hata mama SAMIA nae atoke zake hafai kuendelea kuwepo pale na yeye ni jizi tu kama majizi mengine. Utanishangaza kwamba mtuhumiwa namba mbili unamruka kwenda kuwajibisha mtuhumiwa namba tatu. Since mtuhumiwa namba moja hayupo tunamshukia namba mbili na wengine chini yake wote timua ofisini tuanze upya
Endelea kusema hafai ,ngoja atupangie nchi.
 
Rais wetu mwacheni inawezekana mwenda zake alikuwa hashauriki!

Mwache arekebishe yale aliyokuwa anashauri na kubakia kuzodolewa!

Huyu ndo anafahamu mapungufu yote! Nitamtetea mpaka pale itakapoonekana na yeye anaelekea mle.mle mwa mwandazake!

Msije kuishia kule kule mlipoanzia kumsema JK dhaifu then mkaletewa Dikteta ambaye kila mtu alikuwa analia na kusaga meno. Mara mtamzania kashasahau.

Tumwache arudishe nchi inapotakiwa kuwa! Huenda tukapata hata katiba mpya kipindi hiki!
nakuapia hakuna cha Samia wala nani wa kuweka nchi sawa ni yaleyale
 
Back
Top Bottom