Kwa maelezo haya, kigogo wa Serikalini anayeikandamiza Yanga ikose ubingwa ni nani?

Kwa maelezo haya, kigogo wa Serikalini anayeikandamiza Yanga ikose ubingwa ni nani?

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Mtangazaji wa Wasafi FM, Ricardo Momo amenukuliwa katika session yake redio akidai kuwa wale wazee wa klabu waliozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa watashitaki kwa Rais Samia Suluhu kuhusu klabu yao kuonewa, wamefanya hivyo kwa kuwa kuna kiongozi wa Serikali ambaye yuko nyuma ya pazia.

Momo hajataja jina la klabu lakini wote tunajua kuwa anamaanisha Yanga, kwani hao ndiyo ambao walifanya ‘press’ mara mbili, kwanza na Haji Manara na Hassan Bumbuli pamoja na ile ya wazee wa Yanga, anadai kuwa kuna kiongozi mwenye nguvu Serikalini ndiyo anawakandamiza Yanga.

Momo amerukaruka katika maelezo yake pasipo kutaja majina, na inavyoonekana kuna huyo kigogo wa Serikalini ni shabiki au mdau wa upande wa pili (inawezekana anamaanisha Simba), ndiyo maana Yanga wameanza kuwa na wasiwasi kuwa wanaweza kukandamizwa katika mbio zao ubingwa wa Ligi Kuu na Kombe la Azam Federation msimu huu.

Unadhani Momo yuko sahihi na kwa nini Yanga wanakuwa na wasiwasi wakati wanaongoza ligi tena kwa pointi nane na cha mwisho unadhani huyo kiongozi anayemzungumzia Momo ni nani?

Tujadiliane ndugu zangu!

Screenshot-from-2020-04-27-22_35_35.png
 
Wakaona dua peke yake haitoshi wakahisi kunaweza kukawa na ucheleweshaji wa majibu kutoka kwa Sir God

Wakahisi Mungu angeweza kujibu kipindi ambacho Simba tayari kasha chukua ubingwa afu ikawa too late, wakaona hapana ngoja tuangalie na upande wapili
 
Akuna cha kiongozi walanini ni ujinga na propaganda.

uyo kiongozi alitoa pia maagizo Yanga wapigwe nje ndani na wanigeria kwenye mashindano ya CAF?

Embu mumtag kiongozi mmoja wa Utopolo aje hapa tumkaange!
 
Wewe ni shabiki mjinga sana ina maana huko simba hakuna waropokaji??mbona@mingtier ni wana hara kila siku na I'd zake ishirini ?
hata hiki ulichoandika kinaonyesha si mzima kichwani. Hakuna zuzu mwenye akili.
 
Sasa mkuu anaongea huyo Ricardo Mama, unakuja kutuuliza ss tumsemee, au unataka tupige ramli.
 
Akuna cha kiongozi walanini ni ujinga na propaganda.

uyo kiongozi alitoa pia maagizo Yanga wapigwe nje ndani na wanigeria kwenye mashindano ya CAF?

Embu mutag kiongozi mmoja wa Utopolo aje hapa tumkaange!
Mfano wako wala hauendani.
 
Back
Top Bottom