Kwa maisha wanayoishi ndugu zake Harmonize halafu nikimuona anatoa mil 9 kwa wengine, inaniuma sana

Hao jamaa zake wenyewe kuwa na ndugu mwenye jina kwao tayari ni fursa na msaada tosha.

Wajiongeze, wao wamechapa usingizi akajitokeza msela mmoja akajiita Harmorapa, kaitumia fursa.
 
Kusaidia mtu ni hiari, mbona hata rais ana ndugu zake wanasota tu huko vijijini.
Mtu mmoja hawezi kumaliza matatizo ya ukoo mzima.
 
Huo ushauri wako ni sawa na kumshauri anayetaka kufikia matunda juu ya mti kwamba asitumie kuni za wenzake za kupikia kutengeneza ngazi, wakiti akiweza kuangua Matunda wote watanufaika.

Pia kuna mengi huyajui kwenye hizi industry, kuna mbinu nyingi za kuimarisha brand kazi ziende mbele, hivyo jiongeze ndugu, usimeze tu kila kitu kama kilivyo.
 
Watanzania kwa kupangiana maisha tuna first class.kumsaidia mtu ni matakwa binafs.
 
Mwacheni na hela zake anazitafuta yeye, unajuaje labda ndugu zake hawakumsapoti kipindi chote.
Anyway usimpangie mtu maisha huwezi jua maisha gani kayapitia, ndugu zetu wengine pasua vichwa, kama wananchi wa Tanzania hawataki kazi ila wanapenda kugawiwa hela za bure na bado watakaa kando wakusemee wee , wakuchambee.
Nadhani kila mtu aishi maisha yake afanye atakavyo, naamini huyo jamaavangekuwa ndugu yako ungeenda kwa shilawadu umseme.
 
huwezi ukasaidia dunia nzima saidia pale panapowezekana
 
Ni kweli mkuu...Mimi mwenyewe huyo
"Mayonnaise" ni mtoto wa shangazi lakini hajawahi kunipa hata mia mie nateseka hapa kijijini na biashara yangu ya majeneza.! Nilishamwambia anisaidie japo kupata masoko ya bidhaa zangu huko Dar lakn wapi.!
ongeza ubunifu utengenezaji
Wew huna wazazi wako? Kawalilie huko
Kila mtu anawajibika kwanza wazazi ( mama+baba) then watoto + mke
Hayo mengine nikuamua.
Eti mtoto wa shangazi , wacha uvivu
 
Pale anasaidia kupitia kampuni ya WCB na pesa inatolewa na kampuni kama sehemu ya promo aka kujitangaza kwa kampuni yao. Pale wanatengeneza brand na kutengeneza brand kuna gharama sana na ni strategies za hali ya juu. Hapo ndio utaona tofauti ya WCB na makundi mengine wale wana strategies za kubaki juu kisanaa
 
Mkuu kumsaidia mtu hata kama ni nduguyo si lazima ni hiari sasa wote wa mwangalie yeye kwa nini na wao wasijitahidi angalau wakatoka ki vingine? Nitamlaumu tu kama atakuwa kasahau mama basi
Hapana Mkuu, siku zote Upendo wa Kweli huanzia Nyumbani.
 
Ni kweli mkuu...Mimi mwenyewe huyo
"Mayonnaise" ni mtoto wa shangazi lakini hajawahi kunipa hata mia mie nateseka hapa kijijini na biashara yangu ya majeneza.! Nilishamwambia anisaidie japo kupata masoko ya bidhaa zangu huko Dar lakn wapi.!
Yaani wewe huyo unayemuongelea bado hajatoka na hata nyumba hana halafu leo aje kukusaidia kwenye biashara zako?. Wewe binafsi una mchango gani kwake. utakufa masikini kwa mawazo yako hayo ya kipuuzi.
 
mkuu sidhani kama harmonize ana uwezo wa kugawa million 9. hiyo ni kiki am sure
Anao... kumbuka mama[muzungu] anapesa bado chalii analipwa na kampuni tarakimu 7+.
 
Mkuu hakuna aliye zaliwa kwaajili ya kuwaneemesha ndugu na kama unamtazamo wa kuufulahisha ukoo basi mafanikio utayasikia redioni tu
 
Inanekana mleta mada ni ndugu yake na harmonize ila hapewi pesa
 
yeye kasaidiwa na ndugu gani? hao ndugu kwanini wasipambane kama yeye, unaweza saidia mtu akaenda kuhonga, kulewa na upuuzi mwingine Adebayor alikuwa anasaidia ndugu zake ila ndio kwanzaa walikuwa wana msinitch ndugu sometimes mizinguo, zamani tulikuwa tukienda kwa ndugu zetu tunashiriki masuala ya uzalishaji mali, kilimo ila leo ndugu anataka akae tu na rimoti kwenye sofa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…