Kwa maisha wanayoishi ndugu zake Harmonize halafu nikimuona anatoa mil 9 kwa wengine, inaniuma sana

Hakuna watu wanafki kama ndg, afadhali kidoogo wa tumbo moja, ngd wengi watakuona wa maana ukiwa nacho ukiwa huna hawana muda na ww utapigwa majungu mpaka basi yan, ndg mkubwa ni mama yako tuu alafu wengine ata ukiwasaidia hawasaidiki
 
Mtoa mada umenigusa sana, mimi napafahamu anapoishi mama yake mzazi njia ya kwenda Kijichi kutokea mbagala mission, tena ni bondeni kwenye mkondo wa maji. Watu wanatafuta umaarufu kwa nje wakati nyumbani shida ziko hadi mlangoni. Mungu atusaidie tujitambuwe.
 
Ywewe ndugu zako walivyo na shida hivi yaani unanunua bundle na kumsema huyu kijana. Bora hiyo pesa ya bundle ungewasaidia nduguzo.


Kweli, hii pesa ya bundle bora angewanunulia kandambili wadogo zake kijijini wanatembea pekupeku.
 
Hujui wanasaidiana vipii na shilole mpaka kaamua kutoa zawadi ya gari
 
Ni kweli mkuu...Mimi mwenyewe huyo
"Mayonnaise" ni mtoto wa shangazi lakini hajawahi kunipa hata mia mie nateseka hapa kijijini na biashara yangu ya majeneza.! Nilishamwambia anisaidie japo kupata masoko ya bidhaa zangu huko Dar lakn wapi.!
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] Nimecheka balaa.!
 
Si juzi tu hapa alitoa msaada wa fimbo nyeupe kwa watu wenye ulemavu wa macho au sio huyu unaemzungumzia
 
Daaah, thanks my mama. Matatizo kibao yamenikuta lkn mama yupo upande wangu. Naumwa hadi demu wangu na ndugu hawataki kuja kunitembelea. Nikipona utaskia ndugu ushuzi wanaanza unajua yule kijana wangu kamaliza form six ila hana mkopo. Tusaidie basi hata ada. Ndugu ni Wanafiki wakubwa. Yule aliye pembeni yako kwenye matatizo msaidie, ila wengine Piga chini.
 

Wewe ndiyo mjinga, wazungu wanasema charity begins at home.
 
Hao ndugu zake kijijini ni walemavu??? kwanini wasipambane na hali zao

Umeambiwa wanalima NA wako hai, inamaanisha wanajitahidi. Huyu ndugu H angeweza kuwasaidi kuwekeza kwenye hicho kilimo chao, kuwanunulia trekta NA kuongeza mashamba, hiyo familia ingebadilika kimaisha.
 
Unaweza kuta hao ndugu zake walikuwa wanapambana usiku na mchana asifanikiwe
 
Kama umetoboa kimaisha,ukitaka ndugu nao wafanikiwe uwatie hasira ya kupambana na maisha,ukianza kuwagawia hela kaa ukijua unawatengenezea umaskini
 
Wakati mwingine watu maarufu hufanya hivyo(kutoa pesa au misaada) kwa ajili ya kujenga majina yao. Sio kama wana upendo wa kweli kwa hao wanaowasaidia, bali ni kwa kuangalia jinsi inavyoweza kuwatangaza.
They call it STUNTS
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…