lee Vladimir cleef
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 9,571
- 35,475
Nawaomba sana NEC na Vyombo vyote vya Dola, chondechonde kwa idadi ya Watanzania wanaojitokeza kumpokea na kumsikiliza Lissu kwa furaha na mapenzi yao ya dhati kwake na kwa chama chake nawaomba sana enyi watumishi wa NEC na Majeshi yetu, ruhusuni Haki ichukue mkondo wake, msiwanyime Watanzania haki yao ya kuongozwa na mtu wanaemtaka. Msiwanyime maelfu kwa mamilioni ya Watanzania furaha kwa kuwabadilishia mtu wanaemtaka na kumweka mtu wasiyemtaka.
Hata kikiingia chama kingine madarakani stahiki zenu mtapata tu, tena yaweza kuwa zaidi. Na mtu akishashindwa kihalali hawezi kuwafanya lolote,msiogope. Umati wote unaojitokeza kumlaki Lissu kuwakosesha Raha Mungu hata kaa kimya nasema.
Au maafa yakitokea kwa umati huo kuona umedhulumiwa, nyie mtapata faida gani kiuchumi na kiroho? Tazameni mapokezi ya Lissu tangu anarudi nchini na hata sasa wakati wa Kampeni,tazama Kawe,Arusha na leo Mwanza.
Kama atashindwa kihalali sawa, nyie simamieni Haki, lakini kama atashinda, mpeni Haki yake nanyi mtapata heshima ya milele na tuzo huko kwa Mungu.
Najua hata sasa hivi hatendewi Haki mtu huyu, kwa sababu hujuma juu yake Ni kubwa mno, kuliko Uchaguzi wowote uliowahi kutokea,ingawa bado watu wengi sana wanamuunga mkono.
Enyi NEC na Vyombo vya dola ruhusuni Haki itendeke.
Ni gharama nafuu mno kuruhusu Haki itendeke, lakini Ni gharama kubwa mno kuzuia Haki isitendeke.
Mkiruhusu Haki ikatendeka, mtakumbukwa Kama mashujaa wa Haki. Nayo majina yenu yataandikwa kwa wino wa dhahabu.
Vizazi vijavyo vitapenda kusoma habari zenu kwa furaha na majigambo,nayo mataifa yataja jifunza juu ya maamuzi yenu ya haki, nanyi mkiendelea kuheshimika.
Hata kikiingia chama kingine madarakani stahiki zenu mtapata tu, tena yaweza kuwa zaidi. Na mtu akishashindwa kihalali hawezi kuwafanya lolote,msiogope. Umati wote unaojitokeza kumlaki Lissu kuwakosesha Raha Mungu hata kaa kimya nasema.
Au maafa yakitokea kwa umati huo kuona umedhulumiwa, nyie mtapata faida gani kiuchumi na kiroho? Tazameni mapokezi ya Lissu tangu anarudi nchini na hata sasa wakati wa Kampeni,tazama Kawe,Arusha na leo Mwanza.
Kama atashindwa kihalali sawa, nyie simamieni Haki, lakini kama atashinda, mpeni Haki yake nanyi mtapata heshima ya milele na tuzo huko kwa Mungu.
Najua hata sasa hivi hatendewi Haki mtu huyu, kwa sababu hujuma juu yake Ni kubwa mno, kuliko Uchaguzi wowote uliowahi kutokea,ingawa bado watu wengi sana wanamuunga mkono.
Enyi NEC na Vyombo vya dola ruhusuni Haki itendeke.
Ni gharama nafuu mno kuruhusu Haki itendeke, lakini Ni gharama kubwa mno kuzuia Haki isitendeke.
Mkiruhusu Haki ikatendeka, mtakumbukwa Kama mashujaa wa Haki. Nayo majina yenu yataandikwa kwa wino wa dhahabu.
Vizazi vijavyo vitapenda kusoma habari zenu kwa furaha na majigambo,nayo mataifa yataja jifunza juu ya maamuzi yenu ya haki, nanyi mkiendelea kuheshimika.