Kwa miaka 18 sijawahi kushudia ugumu wa biashara kama awamu hii ya Tano


Mwanangu pambana na hali yako. Siye mbele kwa mbele.
Kipindi hiki nimeweza kununua ndinga, kujenga house (siyo nyumba, namaanisha mjengo).
Nimepanda ndege
Nimefika uropa.

Hahahaha, awamu ya 5 ni zamu yetuuuuuuu
 
Unafanya biashara gani? Ni nini unachoona tofauti na wakati mwingine? eg. kodi imekuwa kubwa, wateja wamepungua etc..
Biashara karibu zote tu, mi nipo kkoo mtu unawahi unafungua duka saa moja asubuhi, mpaka inafika saa nne hata mteja kuja angalau kuuliza bei tu hamna!
kwa kifupi uwezo wa watu kununua bidhaa umeshuka kwa kiasi kikubwa sana, tunasinzia tu madukani.

007 james Bond
 
Muoneni huyu bank teller!!!

Tafadhali tusitafutiane BAN zisizokuwa za lazima,tafwadhali sana!

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
Achana nae mpuuzi huyo, hata ma bank teller wenyewe wanachezea simu tu.
Atakuwa anakaa kwa shemeji! ndio akili zao zinakuwaga hivyo.

007 james Bond
 
ukizoea kunyonga,kuchinja huwezi
Sasa ni kulipa kodi tu,kwa kua ulizoea kulipalaki tano kwa mwaka,lazima hali uone ngumu
Mtoa mada hajalalamika kulipa kodi!
rudi ukasome tena.

007 james Bond
 
pole sana!

007 james Bond
 
Mkuu unatushauri nini tunaotaka anzisha biashara kwa sasa?
 
Kuna kitu kimoja ambacho wanaojiita wafanyabiashara hasa wa Dar ambacho hawakioni. Utitiri wa biashara za aina moja kwenye kila sehemu ya Dar nayo unachangia. Huwezi kuwa na jiji ambalo kila mtaa nyumba za barabarani wamejenga vibanda vidogo vidogo vinavyoita fremu na kwenye kila frem bidhaa ni za aina moja halafu utegemee biashara isifikie kwenye ''turning point'' siku moja. Jamani kama hiyo Kariakoo unayosema kila nyumba imegezwa ya biashara. Na mbaya zaidi nyumba moja imeganywa ''vichochoro'' vidogo vidogo vingi vinavyoitwa frem. Na kuweka chumvi kwenye kidonda bidhaa karibu zinafanana fanana. Hata Magufuli asingeingia madarakani nakuhakikishia hii hali lazima ingetokea tu.
 
Tatizo kubwa kuliko yote linayoigharimu Tanzania ni kwenye maamuzi yani mtu anaeamua hatma ya wafanyabiashara sio mfanyabiashara mfano Kenya wao viongozi wao wengi ni wafanyabiashara hivyo wanaweka mazingira mazuri na marahisi ili biashara zao ziweze kushamiri vizuri lakini huku unamkuta mtu amekaa ofisini na tai shingoni anaamka anasema kuanzia kesho tupandishe tozo fulani, ongeza tozo hii serikali itapata mapato yani sehemu kubwa yenye tatizo ni hio, awamu iliopita ilikua inaunafuu sababu yule jamaa alietoka alikua na elements na michakato ya kibiashara sasa hivi yupo mtu katoka bush huko lakini anaamua mambo mpaka unashangaa..
 
Mkuu unatushauri nini tunaotaka anzisha biashara kwa sasa?

Usithubutu mkuu,Afadhali huyo mtaji ukaweke fixed account then ubangaize mpaka siku mambo yakibadilika ndio ufikirie kuhusu biashara ya kununua na kuuza. Ukianzisha biashara sasa nakupa miezi 3 tu mtaji utakuwa umeteketea.Hali ni mbaya mno, Nguvu ya manunuzi imeshuka mpaka kwenye vyakula. Bajeti za nyumbani hazipangiki,Na ukipanga bajeti nyumbani lazima nyama na samaki iwe kwa wiki mara moja. Hali ni mbaya mno!
 
Nilishafunga biashara zangu mbili ya printing na stationery na vifaa vya umeme na solar baada ya kuona biashara mauzo yameshuka kwa 50% unajikuta kila wakati unatakiwa kuiboost kwa kuongeza mtaji ukiangalia mikopo kibao.

Nimengia kwenye kilimo na mazao huku sikutani na TRA wala kodi ya pango wala kumlipa mfanyakazi baada ya miaka 2 mungu akitupa uhai basi huko mjini nitakuja kuulizia ni gari gani mpya inatamba mjini nimunue.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwakweli ukifanikiwa kutoboa awamu hii,hutakaa ufilisike tena kibiashara.Mambo yamekua hovyo biashara haipo kabsa,Wengi wamepoteza mitaji yao.Wafanyabiashara tuna hali ngumu sana[emoji22]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…