Kwa miaka 5 Magufuli alikopa Trilioni 36, kwa miezi 6 Mama amekopa Trilioni 10, Ndugai yuko sahihi, spidi ya kukopa ni kubwa sana.

Mkuu tunaongelea mikopo ya 36T na 10T katika kipindi cha miaka 5 na kile cha miezi 10. Ni vema tukajua fedha hizo zilitumikaje ili tujue nani kakopa kwa tija na nani katuingiza mkenge.
 

Nikukumbushe kidogo, JPM hakukopa 36tr bali alikopa 28tr.hiyo ni kwa mujibu wa Taarifa za BOT
 
Uongo Mtupu,Mama fedha alizokopa ni zile T1.3 ambazo matumizi yake tumeyaona.Rais aliekopa kuliko Marais wote ni Jiwe na hilo liko wazi.

Mama kakopa 10tr ila 1.3tr ndio matumizi yake yapo wazi hizo zingine matumizi yake yapo kapuni bado.

Jiwe kwa wakati wake alikopa 28tr kwa ajili ya miradi ambayo itarudisha pesa , mfano bwawa la nyerere litajilipia,sgr itajilipia,stand na masoko vitajilipia .
 
Tatizo sio Kukopa bali unakopa aina ipi ya mikopo.

Pili kwa uchumi wa Nchi wa Sasa si rahisi kukamilisha miradi kwa kutegemea vikodi,Kodi zikiongezwa na kuporana pesa kwa staili ya awali ,Nchii hii itaanguka kiuchumi..

Hakuna popote ambapo soft loans ziliwahi kuleta shida hata zingepita ukomo wa 55%.

Serikali isisikilize hizi ujinga,wachumi wote tunamkubali hii njia ni afya kwa uchumi kuliko njia nyingine,tukope hadi kufikia ukomo kwa ajili ya miradi ya miundombinu.
 
Kukopa kuna utaratibu wake na timing, ndo maana wakopaji wengi hujikuta wameishiwa bila kutarajia na kuhisi hiyo pesa haijafanya jambo la maana. Ndo maana ukiendesha nchi ukiwa na kipaumbele sana cha kukopa utaleta majanga makubwa kwa viongozi watakaokuja. Huwezi kukopa trilioni 1.3 ukajenge madarasa na vituo vya afya ambavyo vinakuwa budgeted kwenye matumizi ya maendeleo na huna huo uhitaji kwa kiwango hicho. Bora hata ingetupwa kwenye reli, barabara au stiglaz.......jambo jingine ni kama kuna double allocation, tozo zimeenda kujenga madarasa na vituo vya afya, mkopo wa covid nao umepelekwa kujenga madarasa na vituo vya afya, hili jambo linaingiaje akilini.​
 
Deni la taifa bado ni himilivu....

Profesa Luoga amefafanua kitaalamu kuwa hatujafika hata nusu ya asilimia 70 ya "cap" ya kukopa.....

#Siempre JMT๐Ÿ™
#Siempre SSH๐Ÿ™
Ndio maana mimi kama Mchumi na tafuta mchumi yoyote anaunga mkono njia hii ya ku finance miundombinu..

Ukweli ni kwamba hatuna uchumi wa ndani kuweza kujenga miundombinu na Nchi zote zinatumia mikopo.

Sijui ni wapi madeni laini yaliwahi kuleta shida.

Kiuchumi tunashauri serikali iendelee Kukopa kwa ajili ya miundombinu ya msingi,ila tuu wakope soft loans na wasikope ndani ,Kukopa ndani hakufai kabisa ila kutoa nafasi kwa liquidity iweze kuchochea uchumi.

Mwisho bado kuna tatizo kubwa la kusimamia watu walipe risiti,mara mia Serikali ianzishe kikosi Kazi cha TRA kwa ajili ya kuhakikosha kila muuzaji anatoa risiti na kila mnunuzi anadai risiti.

Kwa observation niliyofanya ,watu hawafai risiti na wauzaji hawatoi risiti,, serikali iweke adhabu kali kwa raia na muuzaji yeyote,hapa kuna udhaifu mkubwa Sana..
 
Mkuu tunaongelea mikopo ya 36T na 10T katika kipindi cha miaka 5 na kile cha miezi 10. Ni vema tukajua fedha hizo zilitumikaje ili tujue nani kakopa kwa tija na nani katuingiza mkenge.
Hiyo 36T over 5 years olmost 90% yote ni commercial na hiyo ya 10T olmost 80% ni grants na soft loans ..

Mikopo yote ya Samia iko wazi na imekopwa kwa ajili ya kujenga barabara,kuzalisha umeme na kusambaza,elimu nk na mchanganuo wake huu hapa ๐Ÿ‘‡









 
Punguza jazba mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Tunawasaidia na kama alivyosema mh.Rais ,,hii ni mikopo ambayo unapewa grace period ya miaka 5 na repayment period ya miaka 20..

Kwamba ukijenga reli leo ikamalizika mapema unatumia sehemu ya faida unayopata kulipia sasa hapo kuna shida gani?

Kwamba Hawa waliokopa sasa wameuzwa au umesikia kuna shida ๐Ÿ‘‡



 
Inawezekana tangu mwaka 2018 ulikuwa umelala ndio umezinduka leo.
Acha bangi mapato yalisomwa miezi kama 6 had 7 ya mwaka 2016 baada ya kupokea kijiti hapo hatukusikia tena habari za kusomewa mapato TRA baadae wakaanza kusoma kwa mwaka usijisahahulishe bwashee hata kama unamahaba malihemu.
 
Wewe huna akili, grant inakuaje tena mkopo? Hivi unaelewa unachokiandika?

Wewe hizo details za kwamba 36T ni commercial terms na hizo 10T ni concessions loan umezitoa wapi kama huwezi kutofautisha kati ya grant na loan?

Rudi shule acha kudandia dandia mada.
 
Wewe taahira unalinganisha Japan na Tanzania? Hivi una akili timamu kweli?
 
Deni la taifa bado ni himilivu....

Profesa Luoga amefafanua kitaalamu kuwa hatujafika hata nusu ya asilimia 70 ya "cap" ya kukopa.....

#Siempre JMT๐Ÿ™
#Siempre SSH๐Ÿ™
Tusipofika huko Tutapungukiwa nini ?

Tangu lini madeni ikawa sifa..., kama wengine wanakopa na sisi ndio tukope ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ