Kwa Milioni 30, UTT amis na nyumba ya kupangisha kipi bora?

Kwa Milioni 30, UTT amis na nyumba ya kupangisha kipi bora?

Nyumba ya kupanga siyo mradi wa kutegemea. Payback period yake ni kubwa, kuwadai Wapangaji Kodi ni stress. Kuna kipindi wapangaji wanaadimika, Gharama za uchakavu nk.

Miradi mizuri ni kama kilimo Cha kisasa, ufugaji wa kisasa, biashara ya vipuli vya magari na pikipiki NK
Uko sahihi,akijenga nyumba asitegemee kupata hela kwa wakati labda ajenge kwa ajili ya kulala yeye na watoto wake.
 
Tunaweza kutofautiana kimtazamo lakini ukweli unabakia pale pale, kwa Tanzania yetu hii, ukiondoa uwekezaji kama wa UTT, karibu biashara zingine zote ni pasua kichwa. Usipoibiwa na watu, utafirisiwa na Serikali. Utitiri wa makodi, matozo na blah blah kibao.
Vipi hiyo uwekezaji wa UTT kwamba unataka kusema serikali hawana access nayo?yaani serikali wakihitaji kukopa huko itashindikana?
 
Milioni 30 utajenga nyumba ambayo utakuwa unapata si zaidi ya 250,000 kwa mwezi.

Itachukua miaka 10 ku breakeven hiyo milioni 30 yako. Ila thamani ya eneo pia itakuwa imeongezeka.
 
Uko sahihi,akijenga nyumba asitegemee kupata hela kwa wakati labda ajenge kwa ajili ya kulala yeye na watoto wake.
Ushauri wangu wa dhati.
Chukua iyo 30m ununue government bonds za 20 or 25 years. Utapata between 15.5 to 16% annual interest ambayo ulipwa kila miezi 6. Yaani hii ni clean money no longo longo.
Ukishapata iyo bond ombea mkopo ambao unawezapata up to 80% ya thamani ya bonds zako. Ukiwa na bonds banks wanatoa mkopo chap yaani no many questions. Mapato yako ya bonds ndio yanaenda kulipa mkopo. No stress za marejesho. Na ukimaliza mkopo 30m zako zipo palepale na utakula faida.
Then ukipata iyo cash jenga nyumba upangishe hapa utapata Mapato kila mwezi.
Yaani in short iyo 30m inaweza kukuzalishia cash na nyumba juu na ni guarantee utaipata baada ya miaka 20 au 25 kulingana na utakavyochagua. Na hata mambo yakikuendea vibaya ukaitaka hela yako kabla ya maturity unaweiza iuza kwenye secondary markert tena if you are lucky with interest.
Bonds unanunua kupitia kwa ma agent kama crdb Bank etc, wapo wengine wengi tu but make sure they are genuine.
Hope umeelewa.. Fene
 
Ushauri wangu wa dhati.
Chukua iyo 30m ununue government bonds za 20 or 25 years. Utapata between 15.5 to 16% annual interest ambayo ulipwa kila miezi 6. Yaani hii ni clean money no longo longo.
Ukishapata iyo bond ombea mkopo ambao unawezapata up to 80% ya thamani ya bonds zako. Ukiwa na bonds banks wanatoa mkopo chap yaani no many questions. Mapato yako ya bonds ndio yanaenda kulipa mkopo. No stress za marejesho. Na ukimaliza mkopo 30m zako zipo palepale na utakula faida.
Then ukipata iyo cash jenga nyumba upangishe hapa utapata Mapato kila mwezi.
Yaani in short iyo 30m inaweza kukuzalishia cash na nyumba juu na ni guarantee utaipata baada ya miaka 20 au 25 kulingana na utakavyochagua. Na hata mambo yakikuendea vibaya ukaitaka hela yako kabla ya maturity unaweiza iuza kwenye secondary markert tena if you are lucky with interest.
Bonds unanunua kupitia kwa ma agent kama crdb Bank etc, wapo wengine wengi tu but make sure they are genuine.
Hope umeelewa.. Fene

Hii ina utofauti gani na UTT AMIS? (kiusalama wa pesa za mteja).

Ufafanuzi tafadhari.

-Kaveli-
 
Salaaam Wachumi

Rejea mada hapo juu
Je upi ni uwekezaji ulio bora endapo katika harakat zako za utafutaji ukajaaliwa umeishika 30Mil cash
Na option ukawa umeweka ni hizo mbili kati ya kuwekeza utt amis ambapo kwa utafiti niliofanya humu return yake yaweza kuwa 250k-300k per month
Na kujenga nyumba ya kupangisha ambapo return yake kwa uwekezaji wa 30Mil naamin pia wazoefu watatoa muangaza
Nb/ katika ujenzi wa nyumba tuna assume kiwanja bado

JE NI UPI UWEKEZAJI ULIO BORA KATI YA HIVYO KWA MTAZAMO WAKO?
Nyumba ya kupanga ya nn jenga lodge hata ya vyumba 5 tu
 
Wastani wa gawio kwa miaka 5/10 nyuma upoje? Maana hii assumption uliyoweka factor lazima ibase katika miaka 5/10 iliyopita ndo "with other factors remain constant" unaweza kuassume kuwa utapokea same rate kwa 5 years mbeleni.

Halafu ukumbuke sisemi kuwekeza katika vipande vya hisa si sawa, nasema sio option ambayo binafsi ningeichukua sababu naamini katika biashara ya real estate na naifanya.

Faida naweza peleka huko ila si mtaji. M 30 nikitulia vizuri napata eneo zuri nje ya mji linalokuwa kwa kasi jirani na maeneo ambayo yana majina.

Nilitoa mfano kerege ni pwani ila ni jirani na mbweni na linakua kwa kasi, nanunua, nazungusha fensi ya wiremesh, naweka geti la kawaida navuta maji au nachimba kisima kama itawezekana isipowezekana naacha, naweka kibanda cha mbao na kachoo simple, nampa mtu akae bure atunze mazingira kisha natulia nikisubiri simu za madalali. Kama eneo ni zuri na watu wanajenga kwa kasi in 3 years naweza pata karibu mara mbili hata na zaidi ya nilichowekaza. Nina uzoefu.

Hapo sina mawazo kuwa bidhaa itaoza, hisa zitaanguka, sijui serikali imekopa fedha za UTT haijarudisha. Ila huyo ni mimi, wewe una mtazamo tofauti na upo sahihi.
Ndugu unaongelea Kerege katika kitongoji gani kati ya hivi? Kitonga, Kwa Manofu, Amani, Nyakahamba, Matumbini, Kwakiwete au Kibemela?
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Ila basi Tu tumetofautiana akili ila 30M ukiwa na biashara Una uhakika hata 500k daily profit...hata ukipata 1% bado ni faida kuliko utt unapata uzoefu
Sasa sijui ulipataje hiyo 30M
 
Ila basi Tu tumetofautiana akili ila 30M ukiwa na biashara Una uhakika at minimum kupata at 3% daily profit ambayo ni kama 900k daily...
Sasa sijui ulipataje hiyo 30M
Mzee 😂😂
3% daily? Biashara gani hio?
 
Ningepeleka UTT hiyo Mil30, then naenda kukopa kupitia hiyo investment ya UTT ningepata kitu kama Mil 21 hapo sasa ndio naanzisha biashara au kilimo ambapo faida itakayopatikana ndio itakayokuja kujenga
 
Ningepeleka UTT hiyo Mil30, then naenda kukopa kupitia hiyo investment ya UTT ningepata kitu kama Mil 21 hapo sasa ndio naanzisha biashara au kilimo ambapo faida itakayopatikana ndio itakayokuja kujenga

Ukikopa 21m riba yake ikoje? Faida ya UTT ikoje.

Ukitoa FAIDA YA UTT toa Riba ya bank unabakiwa na nini?
 
Ndugu unaongelea Kerege katika kitongoji gani kati ya hivi? Kitonga, Kwa Manofu, Amani, Nyakahamba, Matumbini, Kwakiwete au Kibemela?
Boss, hii mada muda kama umepita hivi, nilitoa mfano tu.
 
Nyumba ya kupanga siyo mradi wa kutegemea. Payback period yake ni kubwa, kuwadai Wapangaji Kodi ni stress. Kuna kipindi wapangaji wanaadimika, Gharama za uchakavu nk.

Miradi mizuri ni kama kilimo Cha kisasa, ufugaji wa kisasa, biashara ya vipuli vya magari na pikipiki NK
Mil30 kilimo, vipuri vya magar!? Utaua watu na kihalusi.
 
Back
Top Bottom