OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Wewe ungeweza? Hilo ni swali unalopaswa kujiuliza au kumuuliza shabiki wa soka au mdau anayehoji kuuzwa kwa waliokuwa nyota watatu kwenye Ligi Kuu Bara kina Luis Miquissone na Clatous Chama wa Simba na winga wa Yanga, Tuisila Kisinda.
Miquissone ameuzwa kwa mabingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri wakati Chama na Kisinda wamejiunga na RS Berkane ya Morocco.
Ni kweli nyota hao kila mmoja alikuwa na mchango mkubwa kwenye timu yake hususan msimu uliopita na tukianza na Chama ambaye licha ya kufunga mabao matano na kutoa pasi za mabao ‘asisti’ tatu kwenye mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika na kuifanya Simba ifike robo fainali ya michuano hiyo kwa msimu uliopita, pia aliibuka kinara wa asisti kwenye Ligi Kuu Bara akitoa pasi za mabao 15 na kupachika mabao manane.
Miquissone naye alikuwa moto akifunga mabao matatu na kuasisti mara tatu kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, huku akifunga mabao tisa na ku-asisti mara 10 Ligi Kuu Bara.
Kwa upande wa Kisinda alikuwa na msimu mzuri ndani ya Yanga akifunga mabao
matano na kutoa asisti tano kwenye Ligi Kuu Bara na kuisaidia timu yake kumaliza ligi katika nafasi ya pili.
Kila shabiki alitamani kuwaona nyota hao wakisalia katika vikosi vyao msimu ujao, lakini wameuzwa. Sio kuuzwa tu, bali wameuzwa kwa pesa ndefu ambazo Kibongo ni ngumu kwa kiongozi yeyote wa soka kuziacha
Nje ya kuuzwa kwao, ikumbukwe soka ni biashara na ndio kitu pekee wanachotegemea wachezaji kwa kiasi kikubwa kuendesha maisha na familia.
Kupitia makala hii, Mwanaspoti linakuletea uchambuzi wa mauzo ya wachezaji hao na faida zitakazopata pande zote tatu - kwa maana ya wachezaji, klabu walizotoka na wanakoenda kisha kupitia namba zilizopo hapa chini utatujibu kuwa wewe ungekuwa Yanga au Simba ungeweza kuwabakisha?
LUIS MIQUISONE
Taarifa lilizonazo Mwanaspoti ni kwamba, Miquissone ameuzwa kwa Al Ahly kwa Dola 1,000,000 ambazo ni zaidi ya Sh2.3 bilioni na atakuwa akipokea mshahara wa Dola 34,000 kwa mwezi sawa na Sh80 milioni - pesa ambazo kwa msimu uliopita zingeweza kulipa mishahara ya kikosi chote cha Simba.
Nje ya mkwanja huo, pia imeelezwa Miquissone atakuwa anapewa Dola 20,000 (sawa na Sh46.3 milioni) kama bonasi ya kufanya manunuzi yeye na familia yake. Hapo bado hayajatajwa marupurupu mengine atakayoyapata akiwa ndani ya Al Ahly. Hilo ndilo dili la thamani kubwa kufanywa na Simba tangu kuanzishwa kwake, je Simba wangekataa ofa hiyo?
CLATOUS CHAMA
Kabla ya kuonekana akiwa amevalia jezi ya RS Berkane sambamba na Kisinda, kiungo huyu fundi alikuwa kwenye mawindo ya Far Rabat ya nchini Morocco inayonolewa na kocha wa zamani wa Simba, Sven Vandenbroeck.
Inaelezwa kuwa Far Rabat ilikuwa tayari kutoa Dola 600,000 (sawa na takriban Sh1.3 bilioni) kama ada ya uhamisho, lakini dili hilo likapigwa chini na mabosi wa Simba na kuamua kumpiga bei RS Berkane.
Kwa mantiki hiyo huenda Simba imelipwa pesa zaidi ya Sh1.3 bilioni kumuachia Chama na taarifa za ndani ni kwamba, kambi ya Simba inayoendelea Morocco ni moja ya makubaliano yaliyofanywa na pande hizo mbili katika dili la Chama.
My Take
Nakuuliza wewe shabiki maandazi ungeweza kubaki Simba Sc?
Miquissone ameuzwa kwa mabingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri wakati Chama na Kisinda wamejiunga na RS Berkane ya Morocco.
Ni kweli nyota hao kila mmoja alikuwa na mchango mkubwa kwenye timu yake hususan msimu uliopita na tukianza na Chama ambaye licha ya kufunga mabao matano na kutoa pasi za mabao ‘asisti’ tatu kwenye mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika na kuifanya Simba ifike robo fainali ya michuano hiyo kwa msimu uliopita, pia aliibuka kinara wa asisti kwenye Ligi Kuu Bara akitoa pasi za mabao 15 na kupachika mabao manane.
Miquissone naye alikuwa moto akifunga mabao matatu na kuasisti mara tatu kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, huku akifunga mabao tisa na ku-asisti mara 10 Ligi Kuu Bara.
Kwa upande wa Kisinda alikuwa na msimu mzuri ndani ya Yanga akifunga mabao
matano na kutoa asisti tano kwenye Ligi Kuu Bara na kuisaidia timu yake kumaliza ligi katika nafasi ya pili.
Kila shabiki alitamani kuwaona nyota hao wakisalia katika vikosi vyao msimu ujao, lakini wameuzwa. Sio kuuzwa tu, bali wameuzwa kwa pesa ndefu ambazo Kibongo ni ngumu kwa kiongozi yeyote wa soka kuziacha
Nje ya kuuzwa kwao, ikumbukwe soka ni biashara na ndio kitu pekee wanachotegemea wachezaji kwa kiasi kikubwa kuendesha maisha na familia.
Kupitia makala hii, Mwanaspoti linakuletea uchambuzi wa mauzo ya wachezaji hao na faida zitakazopata pande zote tatu - kwa maana ya wachezaji, klabu walizotoka na wanakoenda kisha kupitia namba zilizopo hapa chini utatujibu kuwa wewe ungekuwa Yanga au Simba ungeweza kuwabakisha?
LUIS MIQUISONE
Taarifa lilizonazo Mwanaspoti ni kwamba, Miquissone ameuzwa kwa Al Ahly kwa Dola 1,000,000 ambazo ni zaidi ya Sh2.3 bilioni na atakuwa akipokea mshahara wa Dola 34,000 kwa mwezi sawa na Sh80 milioni - pesa ambazo kwa msimu uliopita zingeweza kulipa mishahara ya kikosi chote cha Simba.
Nje ya mkwanja huo, pia imeelezwa Miquissone atakuwa anapewa Dola 20,000 (sawa na Sh46.3 milioni) kama bonasi ya kufanya manunuzi yeye na familia yake. Hapo bado hayajatajwa marupurupu mengine atakayoyapata akiwa ndani ya Al Ahly. Hilo ndilo dili la thamani kubwa kufanywa na Simba tangu kuanzishwa kwake, je Simba wangekataa ofa hiyo?
CLATOUS CHAMA
Kabla ya kuonekana akiwa amevalia jezi ya RS Berkane sambamba na Kisinda, kiungo huyu fundi alikuwa kwenye mawindo ya Far Rabat ya nchini Morocco inayonolewa na kocha wa zamani wa Simba, Sven Vandenbroeck.
Inaelezwa kuwa Far Rabat ilikuwa tayari kutoa Dola 600,000 (sawa na takriban Sh1.3 bilioni) kama ada ya uhamisho, lakini dili hilo likapigwa chini na mabosi wa Simba na kuamua kumpiga bei RS Berkane.
Kwa mantiki hiyo huenda Simba imelipwa pesa zaidi ya Sh1.3 bilioni kumuachia Chama na taarifa za ndani ni kwamba, kambi ya Simba inayoendelea Morocco ni moja ya makubaliano yaliyofanywa na pande hizo mbili katika dili la Chama.
My Take
Nakuuliza wewe shabiki maandazi ungeweza kubaki Simba Sc?