3 Lakini fahamu jambo hili: kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu. 2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, watukanaji, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio na utakatifu;
3 wasio na ubinadamu, wasiopenda kusuluhishwa, wachonganishi, walafi, wakatili, wasiopenda mema;
4 wasaliti, wasiojali kitu, waliojaa majivuno, wapendao anasa badala ya kumpenda Mungu.
5 Hao ni watu ambao kwa nje wataonekana kuwa wana dini, huku wakikana nguvu ya imani yao. Jiepushe na watu wa jinsi hiyo.Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu. Watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu; watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema; watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu. Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake.
Hizi ndiyo sifa za watu wa kizazi Cha mwisho; kulingana na biblia
Tegemea kusalitiwa
Tegemea mke au mume kukosa shukrani hata kama umemtendea makubwa
Tegemea watu kuwa wakatili,tumeona watu wakiuana kinyama
Tegemea watu kuwa na tamaa ya fedha,mke kumsaliti mume Kwa hiyo
Tegemea wanandoa kukosa upendo
Watu watachukia mema,ndoa ni njema ila watu watachukia.
Ukisalitiwa na mke au mume fahamu ya kwamba unabii wa maandiko unatumia.