Kwa mpira wa jana (Taifa Stars VS Tunisia); Kuna haja ya mabadiliko makubwa katika soka letu

Kwa mpira wa jana (Taifa Stars VS Tunisia); Kuna haja ya mabadiliko makubwa katika soka letu

kasenene

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2008
Posts
1,632
Reaction score
2,413
Hakuna ubishi jana tumeionyesha Afrika na Dunia kuwa sisi soka bado saana. Mambo machache niliyoyaona mimi kweny emchezo wa jana na ambayo yamekuwa yakijirudia rudia:

1. Wachezaji hawana kabisa misingi muhimu ya uchezaji mpira mfano jinsi ya kumiliki mpira, kufanya maamuzi yenye tija na malengo pamoja na kuwa na kuwa wengine wanacheza nje ya nchi .

2. Nina wasi wasi na walimu wa soka letu kuanzia vilabu mpaka timu ya Taifa sijui wanawafundishaga nini hawa wachezaji wetu...sawa kuna vitu vingine ni '"basic" mchezaji anatakiwa kuvijua mapema lakini swala la malengo ya mchezo hiyo ni kazi ya mwalimu.

3. Lishe bado ni tatizo kubwa saana kwa wachezaji hasa wa ukanda huu wa Africa Mashariki .Wapo wanaolalamikia maumbile ya wachezaji wetu kwamba madogo lakini hili sio tatizo kuna tofauti kati ya maumbile na lishe .Angalia wachezaji wa Korea na Japan au Mexico wengi wao tunafanana maumbile au tunawazidi kimo lakini bado wana stamina. Sisi chips kavu zinawamaliza wanamichezo wetu!

4. Haya matitizo bahati mbaya hayawezi kurekebishika au kutatuliwa kwa wachezaji tulionao sasa, tayari mda umewakimbia. Kazi kwetu kama tunataka kusonga mbele tuanze upya kwa kuwekeza kwenye vijana lakini pia na kutafuta walimu wanaolijua soka na waliotutangulia kwenye mpira na sio kupeana nafasi za ukocha kisiasa. Nimeambiwa "under 20" eti mwalimu ni Julio! Maweeeeee!!

5.Mwisho kabisa tunatakiwa kuwa na viongozi wa soka sio wenye nidhamu tu kama ilivyo sasa bali wawe wanalijua soka na misingi yake vinginevyo ni aibu tu.

Ngoja nisubiri kuwasikiliza wachambuzi wetu wa soka kuona jinsi watakavyofunguka kuhusu "performance" ya timu yetu kama wanavyofungukaga kwenye mechi za Simba na Mtibwa au Yanga na Gwambina.
 
Tanzania tumewekeza mpira mdomoni sio kwenye vitendo. Jana wale jamaa walikuwa wa kawaida ila tatizo kubwa lilikuwa kwenye viungo wachezeshaji na mbinu za mwalimu.

Mfano ukiachana na beki wa kati Erasto Nyoni viungo wengine walikuwa wanapiga mipira isiyosonga mbele au wanawaza kupiga vyenga badala ya kutoa pass mapema kwa mwenzake.

Suala la ukosefu wa stamina ni ngumu kwa wachezaji wetu kulitatua maana watanzania tumedumaa na hatuna lishe tangu utoto wetu ktk hilo tutawalaumu bure wachezaji wetu.

Tuache ushabiki wa Usimba na Uyanga wa kusifia vibovu wanavyomiliki huku wakilazimisha vionekane vizuri badala yake tuwekeze kwenye timu za vijana huko mbeleni tutafanikiwa ila kwa sasa tutalaumiana na majibu hayatapatikana.

N.B Kocha wa Simba ana kitu cha kuwaambia washabiki Nyoni alimkosea nini?
 
Hiyo point namba 1 ni muhimu sana, pia tunahitaji kuwekeza katika mpira kuanzia umri mdogo kabisa kama chini ya miaka 5 na kuendelea.

Tunahitaji kuwa na soccer academy angalau katika kila mkoa, ikiwezekana kila wilaya ili tuwaandae vijana kutoka umri mdogo.
Hakika tusipofanya hivyo, tutakuwa washiriki tu kwenye mashindano yote tutakayo kuwa tunashiriki.

Michezo inahitaji uwekezaji na sio maneno matupu. Watanzania tupo zaidi ya milioni 55 lakini tunazidiwa katika michezo na nchi ndogo ndogo zenye population hata chini ya milioni 20. Ni aibu kubwa.

Natamani siku moja hii nchi ipate kiongozi ambaye atajitoa kwa 100% kuwekeza kwenye michezo.
 
Tanzania tumewekeza mpira mdomoni sio kwenye vitendo. Jana wale jamaa walikuwa wa kawaida ila tatizo kubwa lilikuwa kwenye viungo wachezeshaji na mbinu za mwalimu...
Hapo kwenye N.B : Mimi kuna mapungufu mengi nilishayaona kwa yule kocha wa Simba Sven Vandernbroek, mwenye macho kama ana utitiri wa kuku machoni mwake, jamaa si kocha yule.
 
Tanzania tumewekeza mpira mdomoni sio kwenye vitendo. Jana wale jamaa walikuwa wa kawaida ila tatizo kubwa lilikuwa kwenye viungo wachezeshaji na mbinu za mwalimu...
Hapo kwenye N.B : Mimi kuna mapungufu mengi nilishayaona kwa yule kocha wa Simba Sven Vandernbroek, mwenye macho kama na utitiri wa kuku machoni mwake, jamaa si kocha yule.
 
Hapo kwenye N.B : Mimi kuna mapungufu mengi nilishayaona kwa yule kocha wa Simba Sven Vandernbroek, mwenye macho kama ana utitiri wa kuku machoni mwake, jamaa si kocha yule
Sijui anawapa nini wenye Simba kiasi cha kutoguswa kwa lolote wakati hana jipya zaidi ya kuwaongezea msongo wa mawazo wapenzi wa Simba?
 
Tanzania tumewekeza mpira mdomoni sio kwenye vitendo. Jana wale jamaa walikuwa wa kawaida ila tatizo kubwa lilikuwa kwenye viungo wachezeshaji na mbinu za mwalimu...
Erasto Nyoii amemprove wrong kocha wa Simba nadhani. Ila mimi nahisi itakuwa sio kocha tu bali lazima kuna baadhi ya viongozi hawako nae sawa kwani siamini kwa matatizo ya beki tuliyonayo Simba kwa sasa kama wanegekubali kuona anamuweka benchi.

Ila subirini muone baada ya mechi ya jana kama hajacheza mechi ya Simba inayofuata...Watasingizia oho Onyango Mgonjwa kumbe kelele zetu mashabiki ukichukulia na boko la juzi la Onyango ndio kabisa...
 
TFF wako busy na simba/yanga huku timu yao ikizidi tu kuporomoka.

wangeandaa mpango kazi wa miaka mitatu hata miwili wa kukuza vijana talented ambao wangekaa kambini muda wote wa mwaka na wangekua wanasoma soka darasani na mazoez ya uwanjani huku wakisimamiwa na football specialists mbalimbal.

hao vijana wangeweza na kufika mbali..tuachane na hawa vpl players, wameshapitwa na wakati na hawawezi kutupa jambo zuri.
 
Wabongo mafundi wa kuongea sana, usikute hata familia yako imekushinda kuiendesha ila unalazimisha kutaka kukosoa wataalam wa soka.
Mh..sio kila andiko ulisomalo lazima kuchangia...mdomo unapozungumza bila kuwasiliana na ubungo ndio madhara yake haya. Waswahili wanasema "kuropoka"
 
Tutafika tu siku hata mbuyu ulianza kama mchicha
 
hakuna mchezaji anaeweza kufosi yaani kutumia uwezo binafsi kuwachachafya mabeki wa timu pinzani na kufunga goli,yan hata shot on target sidhani kama walipata
 
Hakuna ubishi jana tumeionyesha Afrika na Dunia kuwa sisi soka bado saana. Mambo machache niliyoyaona mimi kweny emchezo wa jana na ambayo yamekuwa yakijirudia rudia...
Mkuu wekeza kwenye viwanja amini nakuambia utapata iyo cream unayoitaka wewe.
 
Kuna haja pia kuangalia wachezaji kutoka timu zingine ambao kwenye timu zao wanacheza katika mechi zote.

Naamini wapo wachezaji mtibwa, kmc, polisi Tanzania nk. Ambao ni wazuri.

Hii kasumba ya kuchezesha wachezaji wa simba, yanga na Azam pekee ambao wengi uwezo wao unaonekana kwa sababu ya wachezaji wa nje, inaweza inaweza ikawa si kipimo sahihi kuhusu uwezo wao
 
Kama wachezaji wenyewe ni kina Tshabalala na Mkude unategemea lipi la maana?
 
Back
Top Bottom