Hilo ni pira ambalo wachezaji muda wote wanakimbia kimbia tu uwanjani kama nyumbu vile waliojeruhiwa na majangili!
Yaani timu inaweza ikashinda, lakini hata magoli hayaeleweki yameingiaje!! Hilo pira linachezwa kwa sasa na timu fulani hivi.
Algeria mchezo wake wa jana ni wa kukamilisha ratiba tu, tushukuru tumepata suluhu na kufuzu lakini bado kocha aweke mbinu mbadala katika ushambuliaji na umiliki wa mpira hasa wachezaji wa kati.
Simba haijawahi kuwa na takwimu kama za jana ila cha kushangaza hakuna mtu amesema Tanzania tumecheza mpira mbovu. Halafu kingine nilichogundua kina Mwamnyeto na Bacca hawakuwa wanapigiana hata pasi mbili kabla ya kuosha mpira, nimeukumbuka uzi wangu mwingine niliouleta majuzi ambao nilipouleta kuna watu wakaubeza.
Acha kuhararisha ujinga kwa kigezo Cha Taifa state kufuzu, Taifa Stars alikuwa hana namna na Wala kufuzu sio juhudi bali ni hisani ya Algeria .... Ukicheza vibaya utaambiwa. Taifa Stars hana uwezo wa kucheza Afcon hiyo hisan ya Algeria mkianza kula mkono huko ivory coast ndio mtajua.