Kwa mshahara wa laki saba naweza kujenga nyumba?

Kwa mshahara wa laki saba naweza kujenga nyumba?

Cementi mfuko 18000
Nondo ya bei ya chini 22000
Mchanga lori 120000
Kumtizama fundi millioni.
Anyway nisikukatishe tamaa
 
Mkuu hata mshahara wa laki nne unaweza kujenga, mm nina nyumba 2 na viwanja 2 havijajengwa na nina mshahara kama wako, natembelea gari pia
Hapana mkuu labda uwe na marupurupu mengine. Miaka 9 iliopita niliwahi kulipwa hio laki saba baada ya matumizi yote nilikua nabaki na kama na laki moja hivi.
 
Cementi mfuko 18000
Nondo ya bei ya chini 22000
Mchanga lori 120000
Kumtizama fundi millioni.
Anyway nisikukatishe tamaa
Wapi huko..
Nilipo mimi cement 16,500 wanakuletea hadi unakojengea hatakama ni moja..

Lori kubwa la mchanga ni 70,000

Uwanja mita 25 Kwa 18 mil 2.5 kilomita 9 kutoka main road mjini kabisa..

Jamani tusing'ang'ane kujenga mjini daslaam tujenge hata mikoani tunapotoka, ukijenga unaweza pangisha nyumba yako then ikakulipa kodi huko unakofanya shughuli zako..

Lengo ukipata majanga msiba waweza kwenda kufanyika kwako kuondokana na viaibu vidogo vidogo Kwa familia na pengine angalau kuwaachia wanao baadae sio kuja kuteseka wakati we haupo.
 
mtaani kuna fundi viatu anajenga nyumba..... kuna jamaa angu alikuwa anauza viwanja vyake, nikawa namsaidia kuvitangaza... kuna siku nilienda kumsaidia zoezi la mauziano... mmoja wa wateja wake ni mshkaji dereva wa bajaj kituo cha mtaani.... kuna siku ktk dala dala ya STESHENI - MAKUMBUSHO nilimskia konda anamfokea engineer (mi nilielewa fundi wake) baada ya engineer kumwambia siku hiyo hawatafanya kazi, vibarua hawajatokea site! Nimejifunza Mjini Mipango na usithubutu kujua mipango ya watu!

Kaka Slim5 nilipokuwa nnafanya kazi dar dereva wa kampuni (mshahara 350,000) alikuwa na nyumba moja na anahangaika kumaliza ya pili. Kigamboni nilimuona mama mmoja wa makamo muuza matunda kwenye mabeseni posta anajenga banda zuri la vyumba vitatu. Mjini mipango kweli.
 
Habari za majukumu wakuu,

Naomba mwenye ujuzi na uzoefu juu ya masuala ya ujenzi anisaidie. Nahtaji kujenga nyumba ya vyumba vitatu kiwanja tayari ninacho na mshahara wangu ni laki 7 kwa mwezi.

Asante na karibuni
Utajenga nyingi mno+maisha mazuri sana...kama ukiapply hii theory

the state to be a rich is not what you gain,but what you save


Y=C+S
 
Pamoja na ushauri wote wa mapato na matumizi, kibongobongo wengi wetu tumejenga kwa kuangalia hitaji la wakati husika.

Ushauri wangu ni kuwa Ujenzi wetu wa kipato cha chini huo tunaufanya kwa kugawanya hatua za ujenzi katika awamu kama ifuatavyo:

1. Anza kununua mabati.
Hii ni muhimu sana maana nyumba ikisha pauliwa inatakiwa iezekwe haraka vinginevyo mbao za paa zitapinda.

2. Uliza gharama za kusafisha uwanja. Ukipata changa pesa au mlipe kidogo kidogo msafishaji hadi una maliza.

3. Uliza gharama za mawe, mchanga na cement pamoja na kujenga msingi. Anza kuweka mawe kulingana na kipato. Kisha mchanga na baadae nunua cement. Vikikamilika tafuta hela ya fundi fanya mambo.

4. Uliza matofali kiasi gani. Shuhulika na matofali mpaka yakamilike. Tafuta cement yake ya kujengea na hela ya fundi fanya mambo.

5. Nenda kwenye lenta nayo fanya hivyohivyo.

Hapo ni kwa ufupi naamini utanielewa. Ila kama unaweza, jichange ununue cement nyingi kwa wakati mmoja kwa maana ya msingi na kujengea maana cement inapanda bei kila uchao.

Mie nilijenga wakati kipato changu kikiwa laki 4 kwa mwezi. Toka kipande zaidi ya milioni sijafanikiwa hata kununua baiskeli.

Kwahiyo pamoja na kuwa kipato ni muhimu ktk ujenzi, lakini malengo na nia ndio muhimu zaidi. Na mara nyingi ukishaanza ujenzi, raha na faraja unazopata hakuna mtu atakushauri ubane matumizi. Kila ukipata hela utakua unakimbilia kutimiza kitu fulani kwy ujenzi.

Jinsi nyumba inavyopiga hatua...ndivyo hata mashavu yataanza kunona kutokana na amani na furaha unayoipata.

Kila la kheri!
mkuu nimekuelewa mnoo
 
Habari za majukumu wakuu,

Naomba mwenye ujuzi na uzoefu juu ya masuala ya ujenzi anisaidie. Nahtaji kujenga nyumba ya vyumba vitatu kiwanja tayari ninacho na mshahara wangu ni laki 7 kwa mwezi.

Asante na karibuni
Unaweza.
Kila mwezi, nunua matofali mia mbili ambayo ni kama Tsh laki mbili na nusu kisha peleka site. Mpaka mwaka mmoja unaisha utakuwa na matofali 2400.
Hayo yanatosha sana kujenga nyumba ndogo ya vyumba vitatu. Yasipotosha, utahitajika kuongezea kidogo...
 
anzisha mradi kwanza faida unayoipata ingiza kwenye ujenzu, usikope kwa ajili ya kujenga
Hiii sitosahau mkuu, nilikurupuka kufanya hivi nikashindwa kumaliza nyumba, ikabidi niishi ivoIvo
 
Ninamfahamu secretary mmoja serikalini analipwa 390,000/ sijui ni kabla au baada ya makato amejenga nyumba japo ametumia km miaka minne mitano hivi. Kamaliza, na alinambia hajajengewa na mtu.

So ni wewe tu namna ya kujipanga!
Unawajua masekretari wewe? Bosi kachangia hapo.
 
Back
Top Bottom