Kwa mshahara wa laki saba naweza kujenga nyumba?

Kwa mshahara wa laki saba naweza kujenga nyumba?

MKUU WAPE SAVING YAKO BAADA YA MATUMIZ?MAHITAJIO YAKO YA MWEZI NDIO TUTAJUA ACCUMULATION YAKO KWA MWEZI
 
Hakuna kinachoshindikana as long as mtu ana nia ya dhati kufanya kile anachotaka na kwa bahati nzuri tayari ana sehemu ya kuanzia habari ya matumizi hiyo ni personal case ishu ni NATAKA KUFANYA NINI NA KWA WAKATI GANI, mengine nyongeza mzee
 
Habar za majukumu wakuu , naomba mwenye ujuz na uzoefu juu ya maswala ya ujenzi , nahtaji kujenga nyumba ya vyumba vitatu kiwanja tayari ninacho, na mshahara wangu ni laki 7 kwa mwez. asante na karibun
Waweza kabisa kujenga nyumba, cha msingi chunga matumizi yako.
 
Habar za majukumu wakuu , naomba mwenye ujuz na uzoefu juu ya maswala ya ujenzi , nahtaji kujenga nyumba ya vyumba vitatu kiwanja tayari ninacho, na mshahara wangu ni laki 7 kwa mwez. asante na karibun
Hongera kwa wazo la kujenga, kwa tulio wengi, fedha ya kujenga either hutokana na faida itokanayo katika biashara ama mkopo, mshahara ama kazi yako husimama kama "security" ktk kukuwezesha kuwa na reliable cash flow endapo utakuwa umekopa. Aitha, wengine huanza ujenzi kwa kutumia mshahara kwa kiwango fulani then hulazimika kutafuta namna nyingine ya kuendelea na ujenzi, mathalani, hatua ya lenta na kuendelea huhitaji fesha nyingi kwa mkupuo nakadhalika! Laki 7 ni bando 1 tu ya bati kwa bati za Alaf geji 30 kwani huuzwa 450k, nyumba ya aina yako ni lazima ianzie walau bando 5 kwa makadirio.
Katika kufanya maendeleo usiwazie sana fedha yako kidogo, mind u, kuna watu wana fedha na either hawana matumizi ama hawajui namna bora ya matumizi, chukua fedha husika na kupiga hatua, tumia fedha kwa usahihi na kwa malengo kusudiwa utafanikiwa. Shalom.
 
mtaani kuna fundi viatu anajenga nyumba..... kuna jamaa angu alikuwa anauza viwanja vyake, nikawa namsaidia kuvitangaza... kuna siku nilienda kumsaidia zoezi la mauziano... mmoja wa wateja wake ni mshkaji dereva wa bajaj kituo cha mtaani.... kuna siku ktk dala dala ya STESHENI - MAKUMBUSHO nilimskia konda anamfokea engineer (mi nilielewa fundi wake) baada ya engineer kumwambia siku hiyo hawatafanya kazi, vibarua hawajatokea site! Nimejifunza Mjini Mipango na usithubutu kujua mipango ya watu!
 
Unajenga vizuri tu. Anza na kununua tofari kidogo kidogo kila mwezi nunua tofari 200. Tofari 2,000 zinatosha nyumba kubwa tu. Utakavyoanza kununua tofari 200 kila mwezi utajikuta unahamasika kuna miezi mingine utajikuta unanunua mpaka tofari 300. Pia itakusaidia kubana matumizi yasiyokua ya lazima. Nakushauri kwa sasa kama umeamua kujenga achana kabisa na habari za kununua sofa, makabati ya nguo, dressing table nk. focus ktk kujenga. Marafiki zako wakikutembelea watakua wanakucheka kwa kukaa chini lakini ipo siku utakuja kuwaonyesha mjengo wako watabaki wanashangaa
 
Pamoja na ushauri wote wa mapato na matumizi, kibongobongo wengi wetu tumejenga kwa kuangalia hitaji la wakati husika.

Ushauri wangu ni kuwa Ujenzi wetu wa kipato cha chini huo tunaufanya kwa kugawanya hatua za ujenzi katika awamu kama ifuatavyo:

1. Anza kununua mabati.
Hii ni muhimu sana maana nyumba ikisha pauliwa inatakiwa iezekwe haraka vinginevyo mbao za paa zitapinda.

2. Uliza gharama za kusafisha uwanja. Ukipata changa pesa au mlipe kidogo kidogo msafishaji hadi una maliza.

3. Uliza gharama za mawe, mchanga na cement pamoja na kujenga msingi. Anza kuweka mawe kulingana na kipato. Kisha mchanga na baadae nunua cement. Vikikamilika tafuta hela ya fundi fanya mambo.

4. Uliza matofali kiasi gani. Shuhulika na matofali mpaka yakamilike. Tafuta cement yake ya kujengea na hela ya fundi fanya mambo.

5. Nenda kwenye lenta nayo fanya hivyohivyo.

Hapo ni kwa ufupi naamini utanielewa. Ila kama unaweza, jichange ununue cement nyingi kwa wakati mmoja kwa maana ya msingi na kujengea maana cement inapanda bei kila uchao.

Mie nilijenga wakati kipato changu kikiwa laki 4 kwa mwezi. Toka kipande zaidi ya milioni sijafanikiwa hata kununua baiskeli.

Kwahiyo pamoja na kuwa kipato ni muhimu ktk ujenzi, lakini malengo na nia ndio muhimu zaidi. Na mara nyingi ukishaanza ujenzi, raha na faraja unazopata hakuna mtu atakushauri ubane matumizi. Kila ukipata hela utakua unakimbilia kutimiza kitu fulani kwy ujenzi.

Jinsi nyumba inavyopiga hatua...ndivyo hata mashavu yataanza kunona kutokana na amani na furaha unayoipata.

Kila la kheri!
 
Habar za majukumu wakuu , naomba mwenye ujuz na uzoefu juu ya maswala ya ujenzi , nahtaji kujenga nyumba ya vyumba vitatu kiwanja tayari ninacho, na mshahara wangu ni laki 7 kwa mwez. asante na karibun
Hata mshahara ungekuwa laki moja,kujenga inawezekana,weka utaratibu wa kutenga kiasi kidogo kwenye kipato chako,nunua vitu kidogo kidogo,nyumba inajengeka mekuuu!!
 
Una jenga kama una kiwanja tayari. Itabidi mwaka mzima upotezee asikubane mtu majukumu hasa mabinti wazuri, na tegemezi watulie. Pandisha room 2 halafu hamia humo. Ile kodi uliokuwa unalipa itaanza kujenga hapo pia. Inabidi Uwe una pika.
 
KAZI YAKO NI GANI!?

Kuna jamaa alikua anaomba ushauri wa jinsi ya kuacha pombe, watu wakampa ushauri mwingi sana, lkn walisahau kumuuliza kazi yake kwanza,

KUMBE kazi yake ilikua BARMAN ( Muuza pombe mjuzi)
 
Wakati nasubiri matokeo ya kidato cha nne niliomba kazi ya utunzaji bustani restaurant ya Khana Khazana.

Pale nililipwa 90,000/=

Mtu mwenye mshahara mkubwa kabisa kwa wasio mameneja alilipwa 250,000/= alikua ni mpishi.

Aliyenipokea kazini na kunionyesha mambo yanavyoenda alikua analipwa 130,000/=

Huyu mpishi mpaka mimi matokeo yanatoka alikua kanunua Suzuki Swift.
Aliyenipokea alijenga nyumba Kinondoni nahisi alianza muda mrefu kwasababu mpaka mimi nafika alikua hatua ya madirisha na milango.

Mwaka mbele nakutana naye ananiambia mjengo uliisha.
 
Back
Top Bottom