Kwa msimamo wa sasa wa kundi la Yanga, kuna matumaini kiasi gani watafuzu robo fainali ?

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
EDIT: Asanteni kwa ufafanuzi, Nimepitwa na sheria za mpira, sikuhizi hawaangalii GD mkifanana point, wanaangalia nani kamfunga mwenzake nyingi



1. AL AHLY - point 9 (goli +4)
2. YANGA - point 8 (goli +4)
3. CR BELOUZDAD point 5 - (goli -2)
4. MEDEAMA point 5 - (goli -4)

Mechi za kumalizia

Al Ahly vs Yanga - Misr
Belouzdad vs Medeama - Algeria

Medeama ni kibonde wa kundi si ajabu akapigwa hata nne, Yanga na Al Ahly washajipigia za kutosha wakiwa nyumbani

IKIWA YANGA ATAPIGWA TATU KAMA ALIZOPIGWA NA BELOUZDAD UGENINI, KISHA MEDEAME APIGWE NNE NA BELOUZDAD, SAFARI ITAENDELEA ?
 
Yanga kafuzu. Kikubwa asifungwe nyingi kule misri
 
Yanga ameshafuzu anaenda tu kukamilisha ratiba
 
YANGA kashaenda robo fainali hata kama belouzdad ashinde goli 10 kwa madema. Head to head ya belouzdad na Yanga ndio inaangaliwa nani kamfunga mwenzake goli nyingi.
 
YANGA kashaenda robo fainali hata kama belouzdad ashinde goli 10 kwa madema. Head to head ya belouzdad na Yanga ndio inaangaliwa nani kamfunga mwenzake goli nyingi.
Ikiwa Yanga atafungwa goli tatu huko Misri na Belouzdad amfunge Medeama goli nne ?
 
Aibu sana yaani umeumbuka vibaya sana mpaka unatafuta pa kutokea. Si ulikuja na uzi kuwa Yanga kaaga rasmi mashindano. Maumivu ni makali sana uliyonayo kwa sasa. Yanga hata akufungwa magoli 100 kafuzu tayari.

 
Mjinga wewe(samahani lakini)

Yanga hata afugwe mia na Al ahly

Belouizad ashinde mia nae , bado yanga anafuzu...

Yanga ashaingia robo Hio imeisha tayari😃😃
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…