Poppy Hatonn
JF-Expert Member
- Apr 9, 2021
- 3,095
- 4,632
Kwa sasa, tunaona mwanamke anayewania urais pamoja na chama cha siasa kinachotaka mgombea wao wa nafasi hiyo awe mwanamke.
Hata hivyo, dini inasema bila utata kwamba mwanamke haruhusiwi kuwa kiongozi mkuu wa nchi. Anaweza kuwa makamu wa rais, waziri, au kushika nafasi nyingine za uongozi, lakini si kuwa mkuu wa dola.
Kwa muktadha huo, tunaposema mwanamke anaweza kuwa rais, tunapingana na maandiko matakatifu tuliyo nayo.
Sasa tunafanyaje?
Katika Biblia, kuna hadithi ya mfalme aliyesema, "Siku nyingi hekalu halijakarabatiwa. Nataka hekalu likarabatiwe." Wakati wa ukarabati, walikuta kitabu cha Torati. Waliposoma maandiko yake, mfalme aligundua kuwa taifa lilikuwa linafanya mambo mengi yaliyokatazwa. Akauliza, "Tufanye nini sasa?"
Je, Watanzania tunapaswa kujiuliza swali hilo hilo?
Ikumbukwe kuwa Ikulu ilipojengwa awali, haikuwa nyumba ya mtawala; ilikuwa chuo cha dini ya Kiislamu. Sasa, tunajadili jambo ambalo limekatazwa katika Msahafu.
Tunasema mwanamke anaweza kuwa rais, lakini Msahafu unakataa.
Kwa mfano, hata Kanisa Katoliki limekataa kuwapa wanawake upadrisho, na suala la wanawake kuwa maimamu bado halijakubaliwa.
Pengine ni wakati wa kurudi kwenye misingi ya imani na historia ya taifa letu.
Hata hivyo, dini inasema bila utata kwamba mwanamke haruhusiwi kuwa kiongozi mkuu wa nchi. Anaweza kuwa makamu wa rais, waziri, au kushika nafasi nyingine za uongozi, lakini si kuwa mkuu wa dola.
Kwa muktadha huo, tunaposema mwanamke anaweza kuwa rais, tunapingana na maandiko matakatifu tuliyo nayo.
Sasa tunafanyaje?
Katika Biblia, kuna hadithi ya mfalme aliyesema, "Siku nyingi hekalu halijakarabatiwa. Nataka hekalu likarabatiwe." Wakati wa ukarabati, walikuta kitabu cha Torati. Waliposoma maandiko yake, mfalme aligundua kuwa taifa lilikuwa linafanya mambo mengi yaliyokatazwa. Akauliza, "Tufanye nini sasa?"
Je, Watanzania tunapaswa kujiuliza swali hilo hilo?
Ikumbukwe kuwa Ikulu ilipojengwa awali, haikuwa nyumba ya mtawala; ilikuwa chuo cha dini ya Kiislamu. Sasa, tunajadili jambo ambalo limekatazwa katika Msahafu.
Tunasema mwanamke anaweza kuwa rais, lakini Msahafu unakataa.
Kwa mfano, hata Kanisa Katoliki limekataa kuwapa wanawake upadrisho, na suala la wanawake kuwa maimamu bado halijakubaliwa.
Pengine ni wakati wa kurudi kwenye misingi ya imani na historia ya taifa letu.