Kwa mtazamo wa Kidini. Je, mwanamke anaweza kuwa Rais?

Kwa mtazamo wa Kidini. Je, mwanamke anaweza kuwa Rais?

Kwa sasa, tunaona mwanamke anayewania urais pamoja na chama cha siasa kinachotaka mgombea wao wa nafasi hiyo awe mwanamke.

Hata hivyo, dini inasema bila utata kwamba mwanamke haruhusiwi kuwa kiongozi mkuu wa nchi. Anaweza kuwa makamu wa rais, waziri, au kushika nafasi nyingine za uongozi, lakini si kuwa mkuu wa dola.

Kwa muktadha huo, tunaposema mwanamke anaweza kuwa rais, tunapingana na maandiko matakatifu tuliyo nayo.

Sasa tunafanyaje?

Katika Biblia, kuna hadithi ya mfalme aliyesema, "Siku nyingi hekalu halijakarabatiwa. Nataka hekalu likarabatiwe." Wakati wa ukarabati, walikuta kitabu cha Torati. Waliposoma maandiko yake, mfalme aligundua kuwa taifa lilikuwa linafanya mambo mengi yaliyokatazwa. Akauliza, "Tufanye nini sasa?"

Je, Watanzania tunapaswa kujiuliza swali hilo hilo?

Ikumbukwe kuwa Ikulu ilipojengwa awali, haikuwa nyumba ya mtawala; ilikuwa chuo cha dini ya Kiislamu. Sasa, tunajadili jambo ambalo limekatazwa katika Msahafu.

Tunasema mwanamke anaweza kuwa rais, lakini Msahafu unakataa.

Kwa mfano, hata Kanisa Katoliki limekataa kuwapa wanawake upadrisho, na suala la wanawake kuwa maimamu bado halijakubaliwa.

Pengine ni wakati wa kurudi kwenye misingi ya imani na historia ya taifa letu.
Hamku liona hilo mlipoweka Katiba kwamba ikitokea maradhi au kifo Makamu wa Raisi anachukua Madaraka. Kwani hakuna viongozi wakubwa Ndani ya Serikali na kwenye chama hakuna aliye muislamu au mkristo wa Torati.

Na walioabdika Katiba ni wanasiasa au wanasheria , hawa kufanya rejea ya vitabu vya dini . Viongozi wa Dini zetu hawakuhusishwa. Walidharauliwa.


Hivi viongozi wetu wa chama na sirikali, hawaombi ushauri toka Kwa Bagonza au Kitime au Ponda.

Nini matumizi ya kamati ya Amani, ni kusamehe na kuwadanganya raia wawasamehe viongozi waongo na wezi ili watuibie vizuri na sio kutenda haki.
 
Kwa sasa, tunaona mwanamke anayewania urais pamoja na chama cha siasa kinachotaka mgombea wao wa nafasi hiyo awe mwanamke.

Hata hivyo, dini inasema bila utata kwamba mwanamke haruhusiwi kuwa kiongozi mkuu wa nchi. Anaweza kuwa makamu wa rais, waziri, au kushika nafasi nyingine za uongozi, lakini si kuwa mkuu wa dola.

Kwa muktadha huo, tunaposema mwanamke anaweza kuwa rais, tunapingana na maandiko matakatifu tuliyo nayo.

Sasa tunafanyaje?

Katika Biblia, kuna hadithi ya mfalme aliyesema, "Siku nyingi hekalu halijakarabatiwa. Nataka hekalu likarabatiwe." Wakati wa ukarabati, walikuta kitabu cha Torati. Waliposoma maandiko yake, mfalme aligundua kuwa taifa lilikuwa linafanya mambo mengi yaliyokatazwa. Akauliza, "Tufanye nini sasa?"

Je, Watanzania tunapaswa kujiuliza swali hilo hilo?

Ikumbukwe kuwa Ikulu ilipojengwa awali, haikuwa nyumba ya mtawala; ilikuwa chuo cha dini ya Kiislamu. Sasa, tunajadili jambo ambalo limekatazwa katika Msahafu.

Tunasema mwanamke anaweza kuwa rais, lakini Msahafu unakataa.

Kwa mfano, hata Kanisa Katoliki limekataa kuwapa wanawake upadrisho, na suala la wanawake kuwa maimamu bado halijakubaliwa.

Pengine ni wakati wa kurudi kwenye misingi ya imani na historia ya taifa letu.
Ushaambiwa serikali haina dini
 
Sio tu mtazamo wa kidini hata kijamii,kibinadamu,kiuchumi,kisiasa mwanamke hayupo equiped kupambana wala kuwezana na mikiki ya nje ya ulimwengu wa nyumbani.

Hata huyu anafanya kazi kwa kuzungukwa na wanaume kwa asilimia kubwa. Wanawake uongozi sio jukumu lao hiyo ipo wazi kabisa wala sio jambo la kutengeneza.

Mataifa ya ulaya na Marekani wenyewe tazama nafasi nyeti kama wameweka wanawake.

Nenda Asia na Uarabuni utakutana na jambo hilo hilo.

Wanawake kutokuwa na sifa ya uongozi ni sawa na swala kutokuwa na sifa za kumuwinda na kumla Simba, sio ulemavu wala ugonjwa ni asili.

Shida ni hawa wasomi wa kisasa wenye mitazamo ya "eurocentric feminist agenda" wanakazia sana ajenda ya ufanano wa mwanamke na mwanaume kinadharia. Ila kiuhalisia wanajua kuwa ni akili za kichaa cha mbwa tu hizo sio uhalisia.
 
Tumia akili,uraisi sio mambo ya dini.Mama ako aliongoza,nyumba yenu,hata baba ako,anajua hilo.
Upumbavu wa fikra huo haujui wewe wanaume waliyoyapitia shangilia tu ufisadi huu wa leo kutegemea pesa na elimu dunia kufilisi ustawi wa jamii.
 
Kuwa rais wa nchi inawezekana, kwa upande wa dini inategemea na hiyo dini!!!
 
Sio tu mtazamo wa kidini hata kijamii,kibinadamu,kiuchumi,kisiasa mwanamke hayupo equiped kupambana wala kuwezana na mikiki ya nje ya ulimwengu wa nyumbani.

Hata huyu anafanya kazi kwa kuzungukwa na wanaume kwa asilimia kubwa. Wanawake uongozi sio jukumu lao hiyo ipo wazi kabisa wala sio jambo la kutengeneza.

Mataifa ya ulaya na Marekani wenyewe tazama nafasi nyeti kama wameweka wanawake.

Nenda Asia na Uarabuni utakutana na jambo hilo hilo.

Wanawake kutokuwa na sifa ya uongozi ni sawa na swala kutokuwa na sifa za kumuwinda na kumla Simba, sio ulemavu wala ugonjwa ni asili.

Shida ni hawa wasomi wa kisasa wenye mitazamo ya "eurocentric feminist agenda" wanakazia sana ajenda ya ufanano wa mwanamke na mwanaume kinadharia. Ila kiuhalisia wanajua kuwa ni akili za kichaa cha mbwa tu hizo sio uhalisia.
Asante kwa ufafanuzi mzuri.
 
Back
Top Bottom