Kwa mtazamo wangu naona Treni ya SGR haitachukua miaka 6 itakufa

Kwa mtazamo wangu naona Treni ya SGR haitachukua miaka 6 itakufa

Mkwawe

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2016
Posts
3,132
Reaction score
5,508
Niwapongeze watanzania (hususani watanganyika) kipekee zaidi watumishi wa umma kwa kufanikisha nchi yetu kuwa na moja ya miundombinu na usafiri wa kisasa nchini hakika pongezi ziende kwenu na naamini mtamsamehe magufuli kwa kutiwapandisha madaraja ili tunufaike tunu njema kama hii.

Lakini siku zote mbongo ni mbongo, Mimi siyo nabii ila ninaongea hili jambo kwa ujasiri na uhakika mkubwa mkubwa kuwa ndani ya miaka 6 chini ya serikali ya CCM hii reli inaenda KUFA kifo kibaya sana siyo cha mende ila cha vunjajungu dume. Vunjajungu dume akishampanda jike tu yeye anageuka chakula cha vunjajungu jike na hapo ndo umauti wake hufikia. Sasa hii SGR unaenda kuwa ni mradi wa hasara sana kw taifa hili sio kwa kuwa umetekelezwa kwa gharama! La! ila kwa kuwa utatalekezwa kwa gharama

Nawajua watanzania, hawajawahi kuwa dhahiri (serious) kila kitu kwao ni 10%

Naahidi kutoa sh 700k kwa yeyote atakayekuwa wa kwanza kuufufua huu uzi baada ya miaka 6 na kunionesha SGR ikifanya kazi

Nieleweke namaanisha ndani ya miaka 6 hii SGR haitakiwi kusitisha huduma zake ikitokea imesitisha huduma zake hata kwa wiki kadhaa au mwezi mmoja au miezi miwili au kadhaa tafsiri take utabiri wangu utakuwa umetimia, kwa maana ile integrity na durability iliyotegemewa si yenyewe

Nawasilisha
 
Uchawi sio mpaka upae au umroge mtu kwa madawa, hata Ile kumsema sema mtu kwa watu yale mabaya yake nao ni uchawi tosha, lengo lako ni nini?........lengo lako ni umuharibie Na watu wa muone kama kinyesi
 
Bufa kakimbilia marekani anajifanya haamin uchawi wakati huko kwao mbeya hajaaga na hatumi hata mia pamoja na hela zote anazipokea pale Alabama. Aliwah kulala ndan akaamka akajikuta juu ya mpapai.. Leo hii kawa mbishi kweli
🤣 🤣 🤣
 
🤣 🤣 🤣
Kijana anaongea fact huyu... mradi huo umejichanganya. Magari mengi makubwa ikiwemo kampuni ya buti la zungu kuna doni mmoja nchii hii anaziendesha na zinampa faida. Huu mradi lazima udororeshwe ili watu wapige pesa kama kawaida. Hiyo stigler yenyew mpaka mda huu tia maji tia maji
 
Roho za kichawi hizi na watu wachawi ni watu wasiopenda maendeleo ndio wana tabia hizi, treni itakuwepo sana tu hata miaka 60 ijayo
 
Kina bufa mnamiliki magar makubwa ya kusafirisha wateja mikoan ndo mmepew usimamiz wake. Kwa n. Msiiue ili umbakie wenyew sokoni

Mkuu, nchi zote zilizoendelea all means of transportation zinafanya kazi kwa ufanisi. Study shows ufanisi wa njia moja unavyoongezeka na njia zingine zinakua as well.

Kudhani reli itaua biashara ya malori is being short-sighted, realistically biashara ya malori itaongezeka zaidi. Wateja watakua na option na watu wengi wataitumia TZ maana usafiri utakua wa uhakika na ushindani wa nguvu.

Nchi kuendelea inahitaji reli bora, kilimo chenye tija na umeme wa kutosha na uhakika; the human capital goes without saying. That's it.
 
Back
Top Bottom