Uchaguzi 2020 Kwa namna gani chama imara kama CCM, kikubwa na chenye historia ndefu kinawezaje kusumbuliwa na vyama vidogo?

Uchaguzi 2020 Kwa namna gani chama imara kama CCM, kikubwa na chenye historia ndefu kinawezaje kusumbuliwa na vyama vidogo?

Sawa hayo madhabahu ata Kama yalijengwa kwa rushwa hapo tunazungumzia muda uliopita kwa Sasa hayo hayo madhabahu yanaweza kusafishika na ibada ikaendelea. Mimi binafsi naonelea kwenye Hili chama Kama chama kiangalie kwa umakini Sana majina mbayo watakayoyarudish yawe ya ushindani na Wala wasiangalie wakwanza kapata kura ngapi waangalie tu ubora wa watia Nia wote hizo idadi za kura zilizopigwa zitupwe kule au zibaki tu Kama kumbukumbu za yule aliyezinunua kwa wajumbe
Tujenge la Sasa huko nyuma tushapita vitabu vyetu vya dini vinasema tusamee
 
Hasa jimbo la Kibaha,rushwa kwa wajumbe ilikuwa waziwazi
Binafsi kwangu rushwa ndani ya CCM kwnye kura za maoni nimeiona ikitendeka waziwazi kwenye kata ya Azimio Jimbo la Temeke kiukweli mgombea mmoja kamwaga pesa utadhani anagombea ubunge kumbe ni udiwani tu,na matumizi ya pesa yameonekana maana sio kwa gape kubwa namna hile alilo waacha wenzake.
Takukuru waanze na kata ya Azimio
 
Hili tatizo ni kubwa kuliko linavyo jidhihirisha sasa.
Tatizo hili lianza tangu utawala wa mwalimu.
Mwl alijitahidi kushughulikia lakini lilijichipua. Kutumbuliwa kwa Jumbe ni mfano halisi. Lakini enzi hizo wakati ni mshiriki humu JF wa kusoma nyuzi za wengine na si member nilisoma mahali Sokoine eti alichapishaga kadi zake. Lakini Mwl yasemekana alinusurika kupinduliwa Mara kadhaa. Mimi naijua ya 1984, angalau ilikuwa wazi kiasi.

Tatizo lenyewe ni hili mtu/kikundi cha watu kinakuwa na masilahi yake, yaliyo jazwa na tamaa za kujinufaisha binafsi, wao, marafiki na jamaa zao si wananchi wote/taifa. Mbinu inayofanywa ni kuandaa mtandao ambao si rasimi hauko ndani ya chama kiundeshaji wake, lakini nje ya chama. Mtandao huu unawahusisha watu mbalimbali, kama kwa baadhi ya wafanyabiashara na watumishi wa serikali na mashirika wasio waaminifu. Kwenye chama ndio wanatumia wakati wa uchaguzi kama sasa kuweka mamluki wao kwa ajili ya kuandaa kuunda serikali ijayo ie awamu ya sita. Wafanyabiashara wanaahidiwa mambo yakifanikiwa mtandao ukishika serikali basi watapendelewa kwenye shughuli zao za kibiashara, hivyo wanatakiwa wawe wafadhili wa fedha wa kutekeleza mipango ya wanamtandao, kumbuka baadhi ya wanaotakiwa na mtandao hununuliwa kwa vipande vya fedha wakionekana ni wagumu kutoa ushirikiano.

Mwl alijaribu sana kupambana na hili tatizo, mfano halisi ni uchaguzi 1995. Mwl aliamua kama kawaida yake kuvaa uso usio na soni ila wakijasiri kwa maana halisi ya ujasiri. Mkapa akapata Urais na Mwl akaamini kuwa jamaa hata muangusha mengine ni historia jiongeze.... Ndio hii kauli mbiu ya kura hazikutosha. Lakini Mwl aliependa nchi kwa dhati na uzuri wenyewe wawili hawa walikuwa Marais. Kama ukweli huna hiyana ndani yako utajuwa who was the best president kati yao.

Watumishi wa umma wasio waaminifu wanaahidiwa kupandisha vyeo, si vyeo tu ila vyeo kwenye nafasi nyeti. Mfano Mkurugezi nssf au tass. Wako walio ahidiwa hivyo na wanajulikana. Wengine wakaambulia patu, yuko nguli mmoja wa kalamu na aliitumua vizuri kalamu yake kuwa uzia Watanzania mbuzi kwenye gunia yeye amebakia kumnunuia kila ajaye. Mtumishi akisha ahidiwa hivyo yeye kazi yake ni kuhujumu, kwa kuchelewesha mambo ofisni, kukatisha tamaa wenzake,kutafuta siri zitakazo saidia mtandao na kumhujumu kiongozi mkuu na wale wanaonekana ni wazuri na mahiri katika kumsaidia kazi. Ni rahisishe kwa kusema hivi wanamtandao wanaunda mfumo nje ya mfumo rasmi. Kazi ya huu mfumo ni kuhujumu mfumo rasmi kwanza usiwe na nguvu na lakini usiimarike. Kazi nyingine ni kumuandalia mazingira mtu wao kuwa Rais.

Wanamtandao hawa wakishafanya hivyo ndani ya nchi kama haitoshi hutafuta washirika nje ya nchi. Wanawapataje hawa? Nje ya nchi wako wenye masilahi ndani ya Tanzania. Masilahi haya mengi ni wingi wa raslimali lakini yako ya kisiasa na ya kijamii, mfano hai na halisi ni ushoga na yule mfalme aliyepinduliwa Zanzibar ana tamani arudi kwa mlango wa nyuma. Hawa nao wanapewa abadi zao stahiki kutokana na matamanio yao.
Pia kwa hili la nje ya nchi wanatumia propaganda zinazoichafua serikali iliopo madarakani kwa kutumia walewale wafanyakazi wasio waaminifu ambao wamewarecruit katika mtandao. Hili liko wazi mwenye akili atakuwa na mfano ya hivi karibu na inayo endelea.

Nitoe ushauri kwa matokeo haya ya kura za maoni CCM bado wana muda hawajachelewa, watume watu waaminifu kwenye majimbo yeye ukakasi wafanye kautafiti kwa random sampling ya maoni ya wapiga kura wananchi wa kawaida wakashangazwe na ukweli halisi. Na amini Mkt taifa na team yake ya uongozi wa juu ni watu makini na very serious hawatalipuuza hili.
Niishie hapo tusubiririe wachangiaji wengine.
 
Hili tatizo ni kubwa kuliko linavyo jidhihirisha sasa.
Tatizo hili lianza tangu utawala wa mwalimu.
Mwl alijitahidi kushughulikia lakini lilijichipua. Kutumbuliwa kwa Jumbe ni mfano halisi. Lakini enzi hizo wakati ni mshiriki humu JF wa kusoma nyuzi za wengine na si member nilisoma mahali Sokoine eti alichapishaga kadi zake. Lakini Mwl yasemekana alinusurika kupinduliwa Mara kadhaa. Mimi naijua ya 1984, angalau ilikuwa wazi kiasi.

Tatizo lenyewe ni hili mtu/kikundi cha watu kinakuwa na masilahi yake, yaliyo jazwa na tamaa za kujinufaisha binafsi, wao, marafiki na jamaa zao si wananchi wote/taifa. Mbinu inayofanywa ni kuandaa mtandao ambao si rasimi hauko ndani ya chama kiundeshaji wake, lakini nje ya chama. Mtandao huu unawahusisha watu mbalimbali, kama kwa baadhi ya wafanyabiashara na watumishi wa serikali na mashirika wasio waaminifu. Kwenye chama ndio wanatumia wakati wa uchaguzi kama sasa kuweka mamluki wao kwa ajili ya kuandaa kuunda serikali ijayo ie awamu ya sita. Wafanyabiashara wanaahidiwa mambo yakifanikiwa mtandao ukishika serikali basi watapendelewa kwenye shughuli zao za kibiashara, hivyo wanatakiwa wawe wafadhili wa fedha wa kutekeleza mipango ya wanamtandao, kumbuka baadhi ya wanaotakiwa na mtandao hununuliwa kwa vipande vya fedha wakionekana ni wagumu kutoa ushirikiano.

Mwl alijaribu sana kupambana na hili tatizo, mfano halisi ni uchaguzi 1995. Mwl aliamua kama kawaida yake kuvaa uso usio na soni ila wakijasiri kwa maana halisi ya ujasiri. Mkapa akapata Urais na Mwl akaamini kuwa jamaa hata muangusha mengine ni historia jiongeze.... Ndio hii kauli mbiu ya kura hazikutosha. Lakini Mwl aliependa nchi kwa dhati na uzuri wenyewe wawili hawa walikuwa Marais. Kama ukweli huna hiyana ndani yako utajuwa who was the best president kati yao.

Watumishi wa umma wasio waaminifu wanaahidiwa kupandisha vyeo, si vyeo tu ila vyeo kwenye nafasi nyeti. Mfano Mkurugezi nssf au tass. Wako walio ahidiwa hivyo na wanajulikana. Wengine wakaambulia patu, yuko nguli mmoja wa kalamu na aliitumua vizuri kalamu yake kuwa uzia Watanzania mbuzi kwenye gunia yeye amebakia kumnunuia kila ajaye. Mtumishi akisha ahidiwa hivyo yeye kazi yake ni kuhujumu, kwa kuchelewesha mambo ofisni, kukatisha tamaa wenzake,kutafuta siri zitakazo saidia mtandao na kumhujumu kiongozi mkuu na wale wanaonekana ni wazuri na mahiri katika kumsaidia kazi. Ni rahisishe kwa kusema hivi wanamtandao wanaunda mfumo nje ya mfumo rasmi. Kazi ya huu mfumo ni kuhujumu mfumo rasmi kwanza usiwe na nguvu na lakini usiimarike. Kazi nyingine ni kumuandalia mazingira mtu wao kuwa Rais.

Wanamtandao hawa wakishafanya hivyo ndani ya nchi kama haitoshi hutafuta washirika nje ya nchi. Wanawapataje hawa? Nje ya nchi wako wenye masilahi ndani ya Tanzania. Masilahi haya mengi ni wingi wa raslimali lakini yako ya kisiasa na ya kijamii, mfano hai na halisi ni ushoga na yule mfalme aliyepinduliwa Zanzibar ana tamani arudi kwa mlango wa nyuma. Hawa nao wanapewa abadi zao stahiki kutokana na matamanio yao.
Pia kwa hili la nje ya nchi wanatumia propaganda zinazoichafua serikali iliopo madarakani kwa kutumia walewale wafanyakazi wasio waaminifu ambao wamewarecruit katika mtandao. Hili liko wazi mwenye akili atakuwa na mfano ya hivi karibu na inayo endelea.

Nitoe ushauri kwa matokeo haya ya kura za maoni CCM bado wana muda hawajachelewa, watume watu waaminifu kwenye majimbo yeye ukakasi wafanye kautafiti kwa random sampling ya maoni ya wapiga kura wananchi wa kawaida wakashangazwe na ukweli halisi. Na amini Mkt taifa na team yake ya uongozi wa juu ni watu makini na very serious hawatalipuuza hili.
Niishie hapo tusubiririe wachangiaji wengine.
[emoji122][emoji122]
 
Kama ccm ni chama kubwa wakubali tume huru ya uchaguzi waone janja ya nyani kula indi bichi!
Ata Kama ikija tume huru bado mchezo wa rushwa utakuwepo tu na ndio maana sisi wadau tunaona kwanza ikomeshwe rushwa then haya mengine yatafata tu kiurasi
 
Wakuu habarini za kitambo kidogo na poleni sana kwa msiba mkubwa wa kuondokewa na mpendwa wetu Rais Mstaafu Mzee Benjamini Mkapa (R.I.P),

Kwa muda mrefu huko nyuma nilikuwa najiuliza inawezekanaje na ni kwanini CCM hujikuta wanatumia nguvu kubwa sana kuvuka na hatimaye kupata ushindi wa chaguzi mbalimbali,

nimekuwa nikijiuluza pia ni kwa namna gani chama imara kama hiki, kikubwa na chenye historia ndefu kinawezaje kusumbuliwa na vyama vidogo na wakati mwengine vyama vipya kabisa kama vilivyoibuka kama CHADEMA, ACT WAZALENDO na vinginevyo

NILICHOJIFUNZA
CCM
ni ama imelewa nguvu za madaraka au haihitaji kuendana na wakati nhususani mahitaji husika ya wananchi katika chaguzi zao za ndani wanapotaka kuchagua mwakilishi wao kwenda kushindana na wa vyama vingine.

chaguzi za ndani ya chama hiki kikubwa maarufu kama KURA ZA MAONI ni kichocheo kikuwa sana cha CCM kujikuta wanatumia nguvu kubwa kuwanadi wagombea wao katika chaguzi za kiserikali

nimejifunza kuwa chaguzi za kura za maoni CCM ni kielelezo namba moja cha chama hicho kujichimnbia kaburi la kupata washindani wabovu kulinganisha na vyama vingine, hii inatokana na ukweli wa namna michakato ya chaguzi hizo inavyopatikana ikwemo upigwaji wa kura, muda wa kujinadi, ufahamu wa wajumbe kuhusu wagombea, matumizi mabaya ya madaraka, upendeleo na mzizi mkuu RUSHWA

nimefuatilia chaguzi nyingi zilizopita namna wajumbe walivyowanyoa wagombea ambao walipewa chinin ya dakika 3 kujinadi ambapo kundi kubwa la wagombea hao waliambulia kura 0 na wengine namba za viatu

MTIHANI WA RUSHWA
sijui kama TAKUKURU wanaweza kunikosoa kwenye hili, lakini kwa dhahiri shairi na kwa macho tu ya kawaida, haikuwa rahisi kwa mgomea wa CCM akashinda kura za maoni kama hajatoa kiasi kikubwa cha pesa kulinganisha na wagombea wenzake.

tafiti zisizo rasmi zimeonyesha pasi na shaka namna Wabunge wanaotetea nafasi zao, wafanyaiashara wakubwa, na watu wengine wenye uchumi mkubwa walivyoweza kushinda kura za maoni bbila kujali uwezo wao wa kuchambua masuala yanayowahusu watu wanaotaka kuwawakilisha.

hii ndio kusema kwamba linapokuja swala la kura za maoni, wajumbe wa kura hizo wa CCM hufumba macho yao kuchagua kiongozi mwenye uwezo na badala yake huangalia nani amewapa nini kumzidi nani...HATARI SANA HII

MAJUNGU NA FITNA

katika somo kubwa lingine ni uwezo wa wagombea wengi walioshinda na kushindwa kura za maoni kutengeneza uwongo na majungu dhidi ya wagombea wenzao wanaohisi kuwazidi vigezo vya ushindi ama uteuzi katika vikao vya juu.

udhaifu wa vyombo vya ulinzi na usalama kwa ngazi za wilaya na mikoa umewafanya wagombea walioshinda ama kushindwa kufanikiwa kuwatengenezea tuhuma wenzao wanaohisi kuwa wanaweza kuwazidi sifa za kuteuliwa hivyo kuwatengenezea wakati mgumu.

MJADALA UMEFUNGULIWA
Sawa kabisa. Lakini hii ilikuqa zama hizo. Katikabzama hizi sijui, labda kwa nadra sana!

Nina imani na JPM, Dr Bashiru Ally, Mzee Mangula na Kijana wetu mzalendo namba Tatu Polepole.

Hawa hawana faces za ku tolerate rushwa. Kwanza sidhani kama wanajua jinsibya kutoa rushwa.

CCM huko juu kuko safi na salama. Tatizo liko hapo katikati na huku chini.

Ombi langu kwako! Fanya uchunguzi mahiri kwanza alafu ndiyo uje na fantasies zako.
"Ich glaube, du bist in einem falschen Dampfer!"
 
Katika hayo majimbo 27 yaliofanyiwa tafiti ambayo siyo rasmi kwamba wagombea ambao wameongoza kwa kura za maoni wameongoza kwa kutoa rushwa basi majimbo haya mawili na kata hazikosi

Jimbo la kibaha mjini rushwa ilikuwa wazi wazi
Jimbo la Temeke mpaka pesa zilikuwa zinagawiwa kwenye ukumbi

Kata ya Azimio kwenye Jimbo la Temeke mama aliye ongoza kura za maoni amemwaga rushwa Kama mvua mpaka siku ya kura za maoni kwenye ukumbi. Kuna kipindi mama aliyeongoza kwa kura alikuwa anatembea usiku na makatibu wa matawi kuwatishia mabalozi wasio muunga mkono kwamba kupitia makatibu wao wasinge weza kuchukua Tena fomu za ubalazi 2022

Kata ya mtoni Jimbo la temeke aliye ongoza naye kamwaga Sana mpunga

Kata ya kiburugwa aliye ongoza naye kamwaga rushwa si mchezo..

Kwa haraka haraka ukitaka kutambua Hili angalia uwiano wa kura ukichek mtu wa kwanza anamzidi wa tatu kwa asilimia Mia yani hapo ni dhaili hakuna aki iliyo tendeka.

Nafikilia chama kiwe Makin sana kwenye kurudisha majina ya wawakirishi kwenye majimbo na kata
 
Sawa kabisa. Lakini hii ilikuqa zama hizo. Katikabzama hizi sijui, labda kwa nadra sana!

Nina imani na JPM, Dr Bashiru Ally, Mzee Mangula na Kijana wetu mzalendo namba Tatu Polepole.

Hawa hawana faces za ku tolerate rushwa. Kwanza sidhani kama wanajua jinsibya kutoa rushwa.

CCM huko juu kuko safi na salama. Tatizo liko hapo katikati na huku chini.

Ombi langu kwako! Fanya uchunguzi mahiri kwanza alafu ndiyo uje na fantasies zako.
"Ich glaube, du bist in einem falschen Dampfer!"
Kweli kabisa mdau CCM juu ipo Safi ila kimbembe kwenye majimbo na kata Bora kidogo kwenye majimbo Raisi anaweza kuyafikia lakini huku kwenye kata huku ndio shida ilipo watu wanafanya wanavyotaka wakijua kabisa kwamba hakuna wa kuwafanya kitu Tena mtu akiwashika viongozi wa wilaya au mkoa basi ndio kamaliza kazi kabisa
 
Hili suala la wajumbe na kura rushwa ni pana kidogo, kwa kifupi tuu mimi ninaamini hiyo ni SLEEZY wala sio ( corruption) rushwa.

Mimi ni Mkazi wa Mwanga na Jimbo la uchaguzi la Mwanga kuna Tarafa 16 zinazo toa wajumbe, yaani tarafa za 1) Chomvu, 2) Jipe, 3) Kifula, 4) Kighare, 5) Kileo, 6) Kilomeni, 7) Kirongwe, 8) Kirya,9) Kwakoa, 10) Lang'ata,11) Lembeni, 12) Msangeni, 13) Mwaniko,14) Ngujini, 15) Shinghatini na tarafa ya 16) Mwanga MJINI.

Na katika Tarafa zote hizo ni tarafa 9 tuu ndio unaweza kufika makao makuu ya Jimbola uchaguzi kwa kusafiri kwa chini ya shillingi 10,000/= lakini tarafa 7 zilizo baki sio chini ya kilometa 40 mpaka 80 kufika makao makuu ya jimbo kwa hiyo gharama lazima itakuwa zaidi ya 10,000/=.

Kwa kata zote hizi ni kata tisa (9) pekee ndizo ambazo Mkutano wa uchaguzi mfano ukiisha saa 9 jioni ndio Mjumbe anaweza kurudi kwake mara baada ya kwisha Kikao cha uchaguzi kutokana na ratiba ya kawaida ya usafiri.

Kata zilizo baki inabidi uondoke leo ukalale mwanga mjini, upige kura asubuhi na ulale na kesho yake asubuhi ndio urudi nyumbani.

Hapa kuna mahitaji ya usafiri wa kwenda na kurudi kesho kutwa yake , upate malazi na chakula kwa siku wajumbe wakiwa Mwanga kwenye kikao, na nina amini hali ya kipesa kwa wajumbe haifanani , nikiwa na maana sio wajumbe wote wametimia kiuwezo. Sasa hapa ndio takrima inaanzia.

KWA HIYO SUALA LA RUSHWA LAZIMA LIANGALIWE KWA MAPANA KIDOGO NA CCM HAIWAWEZESHI WAJUMBE, UNATEGEMEA HILO OMBWE NA MAPUNGUFU YA PESA KUKIDHI MAHITAJI NANI ANALIZIBA.
 
Back
Top Bottom