Kwa nchi kama Tanzania mtu wa kijijini akifa kwa coronavirus kama hajaenda hospitali serikali inajuaje?

Hawana habari naye kabisa.
Wananchi watazika tu, na sababu ya umauti inaweza ikaandikwa kuwa ni malaria, kazi kwisha.
 
Mkuu hoja yako haina mashiko kabisa.
Kwahiyo unavyo3lewa nchi zote duniani zina nguvu sawa za kiuchumi kutekeleza hayo?
Pia kifo hakijifichi
Kama wewe hapo hujafa na uko unatype kwa simu wala yule hujamliripoti basi ujue bado maambukizi si mengi ikifika siku utawajua tu sio kwa vipimo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uingereza wenyewe wanakwambia idadi wanayotaja haihusishi watu ambao hawajafia hospitali, wao wanachukua figure za hospitalini tu, na hata kupima hovyohovyo wameacha, leo ije kuwa tanzania
Hii wameisemea wapi mkuu, ingependeza kama unayo 'source' ya tamko hilo.

Naona hapa unalisha watu matango pori, kama huna chanzo cha habari hiyo.
 
Inawezekana vijiji vya mbali wanafikiri korona ni mnyama fulani,au mdudu fulani, ebu waandishi watusaidie watembelee huko.
 
Mbona kijijini mbali sana mkuu,hata hapa Dar, intelligensia yetu inanusa Mambo ya siasa zaidi kuliko kitu chochote,si hatari kwa uchumi wetu,si ufisadi Wala hatari kwa mstakabari wa watanzania na Mali zao.Bali inanusa hatari zote dhidi ya ccm hata Kama bado unaziwazia kichwani watakudaka,muulize Yerrico Nyerere atakusimulia zaidi
 
Hii wameisemea wapi mkuu, ingependeza kama unayo 'source' ya tamko hilo.

Naona hapa unalisha watu matango pori, kama huna chanzo cha habari hiyo.
Angalia BBC ile ya Uk.
Mkuu wamedondosha vikaratasi vya NHS kila nyumba vina maelezo kwamba ukiwa na dalili Corona usiwapigie simu wewe Fanya self isolation fourteen days, simu wapigie ukifika hatua ya kupumua kwa Shida, kukupima hawaji ng'o, Kuna watu wengi wanaugua then wanarecover bila kupimwa.
 
Una hoja lakini uandishi wako una matatizo. Herufi ndogo badala ya kubwa, R badala L , hakuna nukta nk

Ukweli Africa bado sana kwenye maisha kuwa standard. Viongozi wa Africa ni kuwatanyia tu ubabe wananchi wao.

Odhis *
 
Umetia chumvi nyingi sana kwa malengo yako mwenyewe.

Kwanza hii uliyoweka hapa ni tofauti sana na ile uliyoweka mwanzo.

Na hata hivyo, katika hii uliyoweka sasa, bado unaionea aibu na kuweka ukweli kiasi kidogo usionekane mwongo wa kutupwa.

Tatizo ni moja. Watu kama wewe mpo huko serikalini; ndio mnaopindisha mambo kwa kushindwa kutoa huduma kwa waTanzania, halafu mnatafuta visingizio na sababu za kipuuzi na mifano ya kilaghai kama uliyoweka hapa.
 
Wewe endelea kutia sukari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…