Kwa nini Kanda ya Ziwa ina Kiwango kikubwa cha Ugonjwa wa Cancer kuliko Maeneo mengine?

Kwa nini Kanda ya Ziwa ina Kiwango kikubwa cha Ugonjwa wa Cancer kuliko Maeneo mengine?

Naona wengi wanataja samaki. Lakini samaki hao hao wanaoliwa Kanda ya ziwa, wanaliwa pia nchi nzima
 
Kanda hii imezungukwa na migodi mingi na bahati mbaya wachimbaji wadogowadogo wanatumia Chemikali hatarishi kama zebaki ambapo katika uoshaji wa dhahabu hutiririsha maji yenye mchanganyiko wa kemikali/Contaminants kwenye mikondo ya maji pia tahadhari ni ndogo kwa watumiaji wa hizo kumikali
Pia hii kanda kuna matumizi makubwa sana ya viuatilifu kwenye mashamba ya pamba na mazao ya bustani na tahadhali ni ndogo kwa watumiaji
Ninamfano mmoja wakulima wa bustani huwa wana tabia moja isiyofaa ya kupiga dawa nyanya na kupeleka sokoni kesho ya yake ili isioze
Wito kwa Sereilikali tunaomba ifanye jitihada za kiutafiti wa kubaini tatizo
Kwakweli hivi ni moja ya visababishi vikubwa vya kansa maeneo ya kanda ya ziwa.

Kuna matumizi makubwa sana ya kemikali na viuatirifu kuanzia migodini na kwenye mashamba..ambavyo huingia kwenye ziwa na huathiri samaki ambao ni kitoweo kikuu cha watu wa kanda ya ziwa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Naona wengi wanataja samaki. Lakini samaki hao hao wanaoliwa Kanda ya ziwa, wanaliwa pia nchi nzima
Sio kwa kiwango sawa na kanda ya ziwa..kwamfano kigoma wanakula sana samaki wanao patikana ziwa Tanganyika..tukija pwani wanakula sana samaki wanao vuliwa baharini kuliko hao wa kanda ya ziwa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Hospitali itapunguzaje tatizo wakati mfumo wetu wa afya upo kusubiri kutibu wagonjwa?

Suala hapa ni wataalamu wa afya watoke mahospitalini wakatafute chanzo hasa kisababishi cha hizo kansa sio kusubiri wagonjwa.

#MaendeleoHayanaChama
Nakubaliana na wewe mkuu, wakati watafiti wanafanya utafiti ni vizuri pia na hospitali zijengwe kusaidia wagonjwa
 
Wakuu hili swali nauliza kwa wema kabisa. Kuna kiwango kukubwa cha wagonjwa wa Cancer kwa upande wa kando kando ya Ziwa Victoria kuliko maeneo mengine nchini. Mtakumbuka hata Mama Samia alieleza nia ya Serikali kujenga kituo kikubwa Mwanza chenye kutoa matibabu ya Cancer
Sasa najiuliza:
1. Kwa nini kanda hii inaandamwa sana na Cancer?
2. Kitu gani wananchi wafanye kujiepusha na cancer
3. Je Serikali ifanye nini kupunguza tatizo la cancer nchini na hasa kwa kanda ya Ziwa?

Nawakaribisha wenye mawazo na nia njema na wenye kuguswa na hili tatizo tupeane mawazo wakuu ili kupunguza hili tatizo

Kulingana na matatizo ya kansa, mara nyingi kila kansa ina visababishi vyake. Na ukiangalia hili linatokana na muunganiko wa kansa aina tofauti ndani ya jamii husika. Pia, hili ni swali la tafiti nyingi na unaweza kuandika vitabu vingi vikubwa sana kulingana na maisha ya watu husika.

Ila ni kujitahidi kutoa ufupisho/summary. Kwa mfano:
1: Kansa ya kibofu cha mkojo vs ini: kuna aina ya konokono walioko kwenye ziwa Victoria, ambao ni sehemu ya mzunguko wa minyoo isababishayo kichocho. Hii baadaye inakuja kusababisha kansa ya kibofu cha mkojo na ini.
Matumizi ya maji ya ziwa bila kuchemsha: kunywa vs kuogelea ni tatizo.

2: Kansa ya kizazi
A: Human papilloma virus
B: Wake wengi/patners
C: Ndoa za mapema/umri mdogo
D: Kuzaa watoto wengi etc.

3: Kansa ya njia ya chakula
A: Namba moja hapo juu
B: Viwanda na mazao yake
C: Viwanda na taka zake
D: Matumizi ya mbolea ya chumvichumvi/mbolea za viwandani kwenye kilimo, ambayo baadaye huenda kwenye vyanzo vya maji.

4: Kansa ya koo
A: Migodi na vumbi lake lililo na chemikali.
B: Matumizi ya dawa za kuua wadudu kwenye pamba vs kahawa.

Ili kupata suluhisho, inabidi kuvunja chain/mzunguko kulingana na kila kisababishi kwa kuwa na matumizi sahihi pamoja na elimu au kusitisha matumizi au kwenda kwenye mbadala usio na madhara husika.

Kuwa na utaratibu wa mandatory/lazima wa ku-screen watu wote ambao wako kwenye risk kulingana na aina ya kansa ili wasifike hospitali wakiwa wamechelewa.

Kwani, kwa mfano: Tunayoyaona leo ni madhira ya miaka mingi labda 10-50 iliyopita. Pia likely, gharama za screening na elimu ni rahisi kuliko kutibia pamoja na matokeo ya tiba kama watu wakichelewa kufika kwenye bituo vya afya.
 
Kulingana na matatizo ya kansa, mara nyingi kila kansa ina visababishi vyake. Na ukiangalia hili linatokana na muunhaniko wa kansa aina tofauti nfani ya jamii husika.

Kwa mfano:
1: Kansa ya kibofu cha mkojo vs ini: kuna aina ya konokono walioko kwenye ziwa Victoria, ambao ni sehemu ya mzunguko wa minyoo isababishayo kichocho. Hii baadaye inakuja kusababisha kansa ya kibofu cha mkojo.
Matumizi ya maji ya ziwa bila kuchemsha: kunywa vs kuogelea.

2: Kansa ya kizazi
A: Human papilloma virus
B: Wake wengi/patners
C: Ndoa za mapema/umri mdogo
D: Kuzaa watoto wengi etc.

3: Kansa ya njia ya chakula
A: Namba moja hapo juu
B: Viwanda na mazao yake
C: Viwanda na taka zake
D: Matumizi ya mbolea ya chumvichumvi/mbolea za viwandani kwenye kilimo, ambayo baadaye huenda kwenye vyanzo vya maji

4: Kansa ya koo
A: Migodi na vumbi lake lililo na chemikali.
B: Matumizi ya dawa za kuua wadudu kwenye pamba

Ili kupata suluhisho, inabidi kuvunja chain/mzunguko kulingana na kila kisababishi.
Shida mfumo wa afya upo kusubiri watu waugue ili iwatibu na wala sio kupambana kuilinda jamii dhidi ya haya matatizo ya kiafya.

Umenena vyema sana..twende kwenye visababishi tuweke nguvu huko ili kuondoa kama sio kumaliza kabisa haya matatizo kwa jamii zet.

#MaendeleoHayanaChama
 
Sioni mtu akitoa wazo kuwe na tume ya muda maalumu ya watafiti watakao kwenda kutafiti sababu na visababishi vya hiyo cancer wakazi wa huko pahala.

Tukikaa kimya ndugu zetu watakufa na kudhurika kwa wingi. Uchunguzi ufanyie na report ziwe published. Mfano lile tukio la juzi la samaki kufa sijasikia ripoti yake ya ukweli zaidi ya wale matapeli kusema ni mafuta sijui tope sijui mikojo ya ng'ombe.

Hawa wahusika wa ile kamati wanatakiwa kutafutwa na kuwekwa ndani kama wauwaji.

Na ule mgodi ufungwe mara moja na kulipa fidia kwa serikali , na raia wa eneo lile.

Na waziri husika naona wizara inamshinda.
Si kuna mbunge alishawahi kusema bungeni wazazi wake wote wamekufa na cancer wakati ile ripoti ya samaki kukutwa wamekufa kwa hyo chanzo kikubwa akasema ni ziwa Victoria ile migodi ina discharge maji yenye heavy metal halafu ile report ikaingiliwa na wanasiasa mpaka Leo ukweli haujulikani ila migodi ndo chanzo.
 
Wakuu hili swali nauliza kwa wema kabisa.

Kuna kiwango kukubwa cha wagonjwa wa Cancer kwa upande wa kando kando ya Ziwa Victoria kuliko maeneo mengine nchini.

Mtakumbuka hata Mama Samia alieleza nia ya Serikali kujenga kituo kikubwa Mwanza chenye kutoa matibabu ya Cancer
Sasa najiuliza:

1. Kwa nini kanda hii inaandamwa sana na Cancer?

2. Kitu gani wananchi wafanye kujiepusha na cancer.

3. Je Serikali ifanye nini kupunguza tatizo la cancer nchini na hasa kwa kanda ya Ziwa?

Nawakaribisha wenye mawazo na nia njema na wenye kuguswa na hili tatizo tupeane mawazo wakuu ili kupunguza hili tatizo
KANSA
Sababu: Ingawa kansa katika baadhi ya sehemu za mwili ni
kuongezeka kwa kasi ya kutisha, katika maeneo mengine, kama vile
tumbo na uterasi, matukio ya saratani yanapungua.
Aina fulani zinaweza kuzuiwa kwa kiwango kikubwa, na ni hivyo
.Inakadiriwa kuwa zaidi ya nusu ya saratani zote zinatokana na
tabia mbaya ya maisha na ulaji ikifuatiwa na wengi Kupitia ulevi sugu, kuvimbiwa, na
-
kutofanya kazi kwa viungo vya kuondoa uchafu kama mapafu, ini, figo,.ngozi, na matumbo - mfumo unakuwa na sumu na sumu hujilimbikiza karibu na viungo dhaifu au mahali
amejeruhiwa na kipigo, kuanguka, au michubuko.
Sumu ya mwili
mwili husababishwa na matumizi ya vyakula visivyofaa, kama chai, kahawa,
.vinywaji baridi, vileo, tumbaku za aina zote, nyama za kila aina (zwnye magonjwa) , hasa nyama ya nguruwe, sukari ya miwa na bidhaa za sukari ya miwa, nyeupe ,bidhaa za unga, mchele mweupe, na vyakula vyote vya denatured, ambavyo kusababisha taka katika mfumo (costipation).. Saratani itakuwa nadra ikiwa
vyakula na nyama zisizo na afya hazitaliwa damu itakuwa safi.
Izingatiwe pia kansa husababishwa pia na virus kama EBV, HPV MCv
Iz
 
chanzo cha utafiti n nini mkuu? Au ni experience yako binafsi
Kwa kweli ni experience binafsi tu nimekutana na hizi case mara nyingi ni watu wa kutokea kanda hiyo. Pia kwa takwimu zilizopo inaonesha kuna ukubwa wa hili tatizo kwa wenzetu wa maeneo hayo
 
Back
Top Bottom