Kwa nini Kenya ilihairisha kuivamia Tz kijeshi mwaka 1984??

Kwa nini Kenya ilihairisha kuivamia Tz kijeshi mwaka 1984??

nakumbuka nilikuwa darasa la 4 Arusha. baba lituaga akiwa kikosi 977 kj chekereni Arusha kuwa wanakwenda kulinda mipaka Namanga majeshi ya kenya yanavamia tz. Mama alikuwa akilia na hakula wiki nzima. Mh that year.
Mkuu hebu jazilishia nyama mkuu, ilikuaje??

Mzee alikaa mpakani kwa muda gani??

Alirudi na story zipi toka mpakani??
 
hadithi yako siyo sahihi sana. Kulikuwa na tension mpakani lakini siyo kwa sababu Kenya ilitaka kuvamia Tanzania ila ni kwa sababu Tanzania ilikuwa imefunga mpaka ule kusudi watalii wanaoingilia Kenya wasije kupumzikia Tanzania halafu malipo yaende Kenya. Wakati huo bado Tanzania ilikuwa na jeshi kali sana ambalo lingeweza kuisambaratisha nchi yoyote jirani, na Kenya walikuwa wanalijua hilo; kwa vile viongozi wa Kenya ni strategists sana, sidhani kama kweli wengejiingiza kupigana na Tanzania ilihali wakijua wangevurugwa sana. Matatizo ya kijeshi Tanzania nadhani yalianza kuharibika kuanzia muda huo huo lakini siyo kwa kasi kubwa vile ingawa sijui leo yakoje tena. Majuzi nilishangaa kusikia kuwa tunabadilishana ndege za zamani na China, yaani siyo kuwa tunanunua ndege za kisasa.
 
Wakuu kama mnakumbuka vizuri mwaka 1984 kulikua na vuguvugu kubwa sana la Kenya kuivamia kijeshi Tanzania.

Sababu kubwa ilikua ni mnyukano wa kugombea mali za JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI iliyovunjika mwaka 1978. Za kiintelijensia zinadai Kenya ilitaka kucheza rafu kubwa mno kwa kuchukua assets zote muhimu kitu ambacho mwalimu alipambana nacho mno.

Inadaiwa kuwa kuna baadhi ya mali kama meli na ndege kubwa kubwa ziliibwa na kufichwa Kenya, ikabidi Mwalimu atume vijana maalumu wa TISS ya wakati huo wakafanya yao, na baadhi ya mali zikatoroshwa kurudi Tanzania ikiwamo meli maarufu ya MV Victoria kitu ambacho wakenya kiliwaach midomo wazi.

Wakenya kwa kuwa na uchu wa mali hawakuwa na option zaidi ya kutaka kuivamia kijeshi Tanzania, na kama mnakumbuka mwaka 1984 Tanzania ilikua iko tayari tayari kwa vita nyingine na vuguvugu lilikua hot sana.

Ni nini kilipelekea Kenya wakaahirisha mkakati wao wa kuivamia Tanzania??

Walimwogopa Mwalimu ambaye alikua tayari kwa lolote pindi maslahi ya nchi yake yanapoguswa ikibidi hata kuingia vitani?

ulikotoa habari hii ndo kuna jibu la swali lako endelea kudadisi utajua tu mkuu
 
Kipindi hicho nilikuwa na miaka miwili toka nitoke Vitani Uganda na nilikuwa Lugalo,ni kweli kulitokea sintofahamu kati ya Serikali ya Tanzania na Kenya hivyo kufikia Serikali yetu kupeleka Majeshi yetu mpakani lakini hiyo ilikuwa ni Show of force tu ilikuwa tu kumuonyesha adui kuwa tuko vizuri kijeshi na tuko tayari kwa lolote pindi tukichokozwa.
Bahati nzuri sana Kenya walielea somo hawakuweza kuongeza msuguano uliokuwepo wakati huo na kufanya hali ya Tahadhali(Alert)kuondolewa,ki ukweli hata kama kungekuwa na Ulazima kupigana naamini serikali yetu ingeweza kutumia Diplomasia kumaliza fukuto hilo, sababu kubwa ni hali ya Uchumi wa nchi yetu kwa wakati huo pili jeshi letu wakati huo lilikuwa likijijenga upya(Re-Organisation)baada ya vita vya Kagera,maana Jeshini tulikua na watu engi toka sehemu mbali-mbali wengine walitoka Polisi wengine Magereza na pia tulikuwa na Wanamgambo ambao pia walichukuliwa katika JWTZ lakini wakati huo kulionekana si vizuri kuwa-ingiza Jeshini kama waajiriwa maana tungekuwa na Jeshi kubwa sana kiasi ambacho lingekuwa Mzigo kwa Taifa,Lakini kwa kudhamini mchango wao huko vitani Uganda wengine walihamishiwa kwenye majeshi yetu mengine ya Polisi na Magereza.
Mimi siamini kama Kenya ilitaka kuvamia nchi yetu 1984 ila najua kulikuwa na msuguano wa kisiasa kati ya nchi hizi mbili hivyo kupelekea mtafaruku mkubwa wa kijeshi kwenye mipaka.
 
Last edited by a moderator:
kipindihicho si ndicho cha uhujumu uchumi? hata ukikamatwa na chumvi unawekwa ndani. uchumiwetu ulikuwa vibaya tulinyimwa misaada kwa sababu ya kuivamia UGANDA. Nyelele akatumia njia ya kihuni kupata pesa. tungepigwa mbaya.huu ni ukweli japo mchungu
 
kipindihicho si ndicho cha uhujumu uchumi? hata ukikamatwa na chumvi unawekwa ndani. uchumiwetu ulikuwa vibaya tulinyimwa misaada kwa sababu ya kuivamia UGANDA. Nyelele akatumia njia ya kihuni kupata pesa. tungepigwa mbaya.huu ni ukweli japo mchungu

Mapolomoko

kwanza hakujawah kua na mtu anaeitwa NYELELE hapa tanzania..

pili sababu ya kunyimwa misaada ni baada ya nyerere kupinga masharti ya mkopo ya IMF na WB na sio kwasababu ya vita..
 
Last edited by a moderator:
Kenya walikaa wakatafakari kichapo alichopata Idd Amin mwaka 1978-79,wakafyata mkia.
 
Mapolomoko

kwanza hakujawah kua na mtu anaeitwa NYELELE hapa tanzania..

pili sababu ya kunyimwa misaada ni baada ya nyerere kupinga masharti ya mkopo ya IMF na WB na sio kwasababu ya vita..

Mkuu, muongeze kiroba kingine bili kwangu.
 
Last edited by a moderator:
hadithi yako siyo sahihi sana. Kulikuwa na tension mpakani lakiniyo kwa sababu Kenya ilitaka kuvamia Tanzania ila ni kwa sababu Tanzania ilikuwa imefunga mpaka ule kusudi watalii wanaoingilia Kenya wasije kupumzikia Tanzania halafu malipo yaende Kenya. Wakati huo bado Tanzania ilikuwa na jeshi kali sana ambalo lingeweza kuismbaratisha nchi yoyote jirani, na Kenya walikuwa wanalijua hilo; kwa vile viongozi wa kKenya ni strategists sana, sidfhani kama kweli wengijiingiza kupigana na Tanzania ilihali wakijua wangevurugwa sana. Matatizo ya kijesi Tanzania nadhani kuharibika kuanzia muda huo huo lakini siyo kwa kasi kubwa vile ingawa sijui leo yakoje tena. Majuzi nilishangaa kusikia kuwa tunabadilishana ndege za zamani na China, yaani siyo kuwa tunanunua ndege za kisasa.

Sijakuelewa! Yaani China Ndo Wanatupa Mpya C Tunawapa Za Zamani au? if xo ni vzur kwani CHINA Taifa Kubwa Sasa.
 
Ntuzu chukua like hiyo....Wakenya si watu wema kwetu kabisa. Wamejaa dharau, majigambo na kujitweza

nakumbuka umeme ulizimwa usiku mzima kupisha usafirishaji wa silaha na askari kuelekea mitelemko ya mlima kilimanjaro! magari ya jeshi yalikuwa yanapita jioni yakiwa na bendera nyekundu. Tangu siku hiyo hakupiti muda kabla majeshi yetu hayajafanya mazoezi mpakani na kenya
 
Mkuu tatizo vitu vingi sana hii nchi vinabaki kuwa siri za serikali wakati sheria ya classified information inadai miaka 30 ndio mwisho, inabidi mambo yamwagwe hadharani..

Mambo kama haya watawala wanabidi wayaweke kweupe yanasaidia sana kuongeza uzalendo hasa kwa kizazi hiki cha .com

mkuu i partly agree with you, ila kuna nyingi hua zinaachiwa kama tetesi tu kumbe ndio zenyewe, siri zikiwa yingi sana nayo inakua tatizo, si vibaya watu kujifunza historia na kujenga uzalendo kupitia simulizi, Mfano mzuri ni yale aliyoyasema mkuu kule bondeni kwenye mziko ya madiba, kwa kiasi kikubwa imani ilejengeka kwenye mioyo ya wakazi wa jamhuri
 
Sijakuelewa! Yaani China Ndo Wanatupa Mpya C Tunawapa Za Zamani au? if xo ni vzur kwani CHINA Taifa Kubwa Sasa.

Kama hukuelewa, nadhani katika ile post yangu ya kwanza kulikuwa na makosa mengi ya typing. Huwa natumia kidole kimoja kwenye keyboard, na madole yangu ni makubwa sana wakati macho yangu nayo hayaoni vizuri sana kwa karibu ingawa najivunga kukataa miwani.

Kuhusu kubadilishana ndege ni transaction inayoonyesha kuwa hatuko katika mwenendo wa kutafuta vitu vizuri kwa jeshi letu. Huwezi kumpa mtu kitu kikuu kuu eti yeye akupe kitu kipya ambacho ni bora kuliko vishindani; tunapata mpya ambazo siyo bora kwenye medani. Miaka tisa iliyopita, wakati Zimbabwe iko kwenye vigogo kweli kweli China waliiuzia nchi hiyo ndege za MA-6 ambazo ziliuzwa kwa mtindo wa buy one-get one free. Leo hii ndege hizo hazifanyi kazi kabisa, kwani zilifikia kuwa zinajulikana kama flying coffins. Kuna wakati mmoja injini ilizimikia angani, inabidi watue kwa dharura barabarani kwa kutumia injini moja. Kuna wakati ilishindwa kuruka kabisa kutoka uwanjani. Vya bure vina gharama zake, mchina siyo mjombwa wetu wa kutupa vya bure. Pamoja na kukua uchumi wake, nchi hiyo bado ina maskini wengi sana kwa wastani kama sisi tu.

Kwa hiyo pointi niliyokuwa nasema ni hiyo hatuwezi kuendeleza jeshi letu kwa kutumia vitu vya bure,, tunatakiwa kufanya investment kubwa sana.
 
Ntajiridhisha Ikiwa Kuna Mwenye Historia Yote Ya Sakata Hilo!
 
Bonge la story, wakenya wanatudharau sana, lakini hata kama tulikuwa tuna hali mbaya ya kiuchumi, tulikuwa na uzalendo. tungewatandika
 
Kipindi hicho nilikuwa na miaka miwili toka nitoke Vitani Uganda na nilikuwa Lugalo,ni kweli kulitokea sintofahamu kati ya Serikali ya Tanzania na Kenya hivyo kufikia Serikali yetu kupeleka Majeshi yetu mpakani lakini hiyo ilikuwa ni Show of force tu ilikuwa tu kumuonyesha adui kuwa tuko vizuri kijeshi na tuko tayari kwa lolote pindi tukichokozwa.
Bahati nzuri sana Kenya walielea somo hawakuweza kuongeza msuguano uliokuwepo wakati huo na kufanya hali ya Tahadhali(Alert)kuondolewa,ki ukweli hata kama kungekuwa na Ulazima kupigana naamini serikali yetu ingeweza kutumia Diplomasia kumaliza fukuto hilo, sababu kubwa ni hali ya Uchumi wa nchi yetu kwa wakati huo pili jeshi letu wakati huo lilikuwa likijijenga upya(Re-Organisation)baada ya vita vya Kagera,maana Jeshini tulikua na watu engi toka sehemu mbali-mbali wengine walitoka Polisi wengine Magereza na pia tulikuwa na Wanamgambo ambao pia walichukuliwa katika JWTZ lakini wakati huo kulionekana si vizuri kuwa-ingiza Jeshini kama waajiriwa maana tungekuwa na Jeshi kubwa sana kiasi ambacho lingekuwa Mzigo kwa Taifa,Lakini kwa kudhamini mchango wao huko vitani Uganda wengine walihamishiwa kwenye majeshi yetu mengine ya Polisi na Magereza.
Mimi siamini kama Kenya ilitaka kuvamia nchi yetu 1984 ila najua kulikuwa na msuguano wa kisiasa kati ya nchi hizi mbili hivyo kupelekea mtafaruku mkubwa wa kijeshi kwenye mipaka.

Mkuu we kweli veterani umetoa maelezo mazuti
 
Back
Top Bottom