Kwa nini Mikataba ya Wachezaji ina asili ya kikoloni nyakati hizi za uhuru wa Mwanadamu?

Kwa nini Mikataba ya Wachezaji ina asili ya kikoloni nyakati hizi za uhuru wa Mwanadamu?

Heart Wood.

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2014
Posts
982
Reaction score
1,179
Nijuavyo mie, kazi ya Mchezaji Mpira (Professional player) ni kazi ya ajira kama ilivyo kazi nyingine.

Sasa, kwa ushamba wangu na kutokujua kwangu huwa nashangaa mambo haya:

- Mikataba haiwapi wachezaji uhuru wa kuvunja mikataba yao wakati wowote kama ilivyo kwa waajiriwa wengine. Mikataba inapokuwa flexible, inampa room mchezaji kutafuta fursa sehemu nyingine yoyote kwa muda apendao yeye kama ilivyo kwa ajira nyingine. Yaani kama ajira nyingine zinaruusu mwajiriwa kuacha kazi na kuajiriwa sehemu nyingine wakati wowte, iweje iwe ngumu kwa ajira ya Mpira? Hatuoni kuwa huu ni ukoloni?

-Hakuna kanuni za wazi za kubainisha kiasi gani mchezaji alipwe kama ilivyo kwa ajira nyingine. Mfano ukiwa Daktari, inafahamika kabisa kuwa range za mishahara ni kiasi flani. Kutofahamika bayana mishahara ya wachezaji hupelekea sintofahamu kati ya timu husika na mchezaji pengine kutofikia maelewano.

Mie kwa mawazo yangu kazi ya mpira ilitakiwa itangazwe kwenye public na wachezaji waweze ku-apply. Inteview yao inakuwa ni uwanjani kwa muda kadhaa. CV zao zioneshe wazi experience yake na mfano kama ni striker aseme amefunga magoli mangapi kwa muda gani kwa ligi ipi... Sio mambo kuwa gizani gizani kama shughuli za Mganga wa Jadi..

Kwa sasa naomba kuishia hapo. Nitaendelea kubainisha ukoloni wa mikataba ya wachezaji..
 
Mkataba ni makubaliano ya pande mbili, kabla ya kusaini ama kuuandika mkataba kuna vitu mnajadili, kuanzia malipo, kusikitisha mkataba na chochote kile, kisha ndio mkataba unasainiwa.. Sasa kama mkataba wewe mchezaji hujajiwahi usitegemee timu itetee maslahi yako, pale kila mtu anaegama kwake.

Mfano mchezaji unaweza kuingia makubaliano, nasaini mkataba wa miaka mitatu mtanilipa kiasi fulani, ila nikiwa mfungaji bora nitapa hiki, nikiwa mchezaji bora nitapata hiki, nikicheza game fulani ndani ya msimu napewa nyongeza hii, na ikitokea timu niruhusiwe kuondoka, sasa timu nayo inangalia upande wake, inaweza kuja na sababu zake, mfano sawa timu ikija ndani ya mkataba tunakuuza ila isiwe ndani ya ligi tunayocheza sisi, n.k.. Baada ya hapo mkataba unaandikwa na kusainiwa.

Ila kama mchezaji hujielewi imekula kwako, we ukiambiwa tu utalipwa milioni 10 unapagawa, kisa umetoka timu ulikuwa unalipwa laki 7 kwa mwezi

Kuhusu malipo kwenye soka haiwezekani kuwa sawa na ajira maalum kama udaktari, sababu ndani ya timu umuhimu wa wachezaji hutofautiana, thaman zinapanda na kushuka.
 
Nijuavyo mie, kazi ya Mchezaji Mpira (Professional player) ni kazi ya ajira kama ilivyo kazi nyingine.

Sasa, kwa ushamba wangu na kutokujua kwangu huwa nashangaa mambo haya...
Siyo kweli. Isipokuwa kifo tu, mchezaji hawezi kuacha kazi katikati ya msimu kwa vile atasabibisha timu iwe na wachezaji pungufu.

Kuna kazi nyingi ambazo mfanyakazi hawezi kuacha kazi katikati ya msimu kienyeji tu; kwa mfano waalimu wote wa vyuo vikuu Marekani hawawezi kuacha kazi kinyeji katikati ya muhula.
 
kwanini wananchi wa tanzania tunaishi kama enzi za ukoloni na tulishapata uhuru na tukawasha mwenge kwa madai umulike mpka kwa majirani🤣🤣🤣
 
Siyo kweli. Isipokuwa kifo tu, mchezaji hawezi kuacha kazi katikati ya msimu kwa vile atasabibisha timu iwe na wachezaji pungufu.

Kuna kazi nyingi ambazo mfanyakazi hawezi kuacha kazi katikati ya msimu kienyeji tu; kwa mfano waalimu wote wa vyuo vikuu Marekani hawawezi kuacha kazi kinyeji katikati ya muhula.
Mchezaji awe huru kuacha kazi wakati wowote kama ilivyo ajira nyingine. Akitaka kuacha atoe notice ya muda kadhaa kama ilivyo kazi nyingine. Kwa muda ambao anakuwa ametoa notice, timu itafute mchezaji mwingine.
 
Mchezaji awe huru kuacha kazi wakati wowote kama ilivyo ajira nyingine. Akitaka kuacha atoe notice ya muda kadhaa kama ilivyo kazi nyingine. Kwa muda ambao anakuwa ametoa notice, timu itafute mchezaji mwingine.
Mchezaji siyo mfanyakazi huru ambaye nafasi yake inaweza kuzibwa na mtu yoyote wakati wowote, yeye ni sehemu ya timu.
 
Mchezaji siyo mfanyakazi huru ambaye nafasi yake inaweza kuzibwa na mtu yoyote wakati wowote, yeye ni sehemu ya timu.
Mkuu, unamanisha tuna uhaba sana wa vipaji vya SOKA kiasi kwamba, mfano: Nafasi ya Mzize au Aziz Ki haiwezi kuzibwa kabisa na vipaji vingine hapa Africa kwa haraka? Vipi kama huyo mtu unayedhani ni muhimu sana katika timu ataumia na kukaa benchi kwa muda mrefu, Je Timu hiyo itakosa kabisa kipaji kingine kuziba pengo hilo?
 
Siyo kweli. Isipokuwa kifo tu, mchezaji hawezi kuacha kazi katikati ya msimu kwa vile atasabibisha timu iwe na wachezaji pungufu.

Kuna kazi nyingi ambazo mfanyakazi hawezi kuacha kazi katikati ya msimu kienyeji tu; kwa mfano waalimu wote wa vyuo vikuu Marekani hawawezi kuacha kazi kinyeji katikati ya muhula.
Lakini Feisal aliondoka katikati ya msimu na baadhi ya mashabiki walisema anazo haki zote yeye Feisal si mtumwa.
Nita shangaa ikiwa Kibu atakataliwa kuondoka wakati mashabiki haohao walisema wachezaji wako huru kuondoka.
 
Kwa ulicho andika hapa unaonesha kabisa wewe ni sio shabiki wa mpira kabisa, ukielekezwa mikataba ya kimpira ilivyo sidhani kama utaelewa hata kidogo
JF ni kisiwa cha Maarifa. Tupo hapa kujifunza. Karibu utoe darasa Mkuu.
 
Nijuavyo mie, kazi ya Mchezaji Mpira (Professional player) ni kazi ya ajira kama ilivyo kazi nyingine.

Sasa, kwa ushamba wangu na kutokujua kwangu huwa nashangaa mambo haya:

- Mikataba haiwapi wachezaji uhuru wa kuvunja mikataba yao wakati wowote kama ilivyo kwa waajiriwa wengine. Mikataba inapokuwa flexible, inampa room mchezaji kutafuta fursa sehemu nyingine yoyote kwa muda apendao yeye kama ilivyo kwa ajira nyingine. Yaani kama ajira nyingine zinaruusu mwajiriwa kuacha kazi na kuajiriwa sehemu nyingine wakati wowte, iweje iwe ngumu kwa ajira ya Mpira? Hatuoni kuwa huu ni ukoloni?

-Hakuna kanuni za wazi za kubainisha kiasi gani mchezaji alipwe kama ilivyo kwa ajira nyingine. Mfano ukiwa Daktari, inafahamika kabisa kuwa range za mishahara ni kiasi flani. Kutofahamika bayana mishahara ya wachezaji hupelekea sintofahamu kati ya timu husika na mchezaji pengine kutofikia maelewano.

Mie kwa mawazo yangu kazi ya mpira ilitakiwa itangazwe kwenye public na wachezaji waweze ku-apply. Inteview yao inakuwa ni uwanjani kwa muda kadhaa. CV zao zioneshe wazi experience yake na mfano kama ni striker aseme amefunga magoli mangapi kwa muda gani kwa ligi ipi... Sio mambo kuwa gizani gizani kama shughuli za Mganga wa Jadi..

Kwa sasa naomba kuishia hapo. Nitaendelea kubainisha ukoloni wa mikataba ya wachezaji..
wewe hujui mpira hata kidogo kaa kwa kutulia
 
Karibu utoe darasa Mkuu ili ututoe tongotongo sie Washamba wa SOKA. JF ni kisiwa cha Maarifa ambapo wajuvi wa mambo kama nyie hupata fursa ya kutoa shule. Karibu Mkuu.
Ugumu kwenye Mpira huwezi kusajili mchezaji wakati wowote unaojisikia,Kuna dirisha maalum..

Mfano yanga imecheza na kaizer chief,Kaizer ikapenda wachezaji sita wa Yanga,wachezaji wakataka kuvunja mkataba,yanga Si itajifia??maana hawatoweza kusajili wachezaji wapya kwenye kikosi ..ndio maana Sheria hairuhusu kuvunja mkataba wakati ligi inaendelea..
 
Mkuu, unamanisha tuna uhaba sana wa vipaji vya SOKA kiasi kwamba, mfano: Nafasi ya Mzize au Aziz Ki haiwezi kuzibwa kabisa na vipaji vingine hapa Africa kwa haraka? Vipi kama huyo mtu unayedhani ni muhimu sana katika timu ataumia na kukaa benchi kwa muda mrefu, Je Timu hiyo itakosa kabisa kipaji kingine kuziba pengo hilo?
Wingi wa wachezaji wazuri siyo uzuri wa team. Na timu nzuri haina maana ya kuwa na wachezaji wazuri wengi. Msimu uliopita Simba ilikuwa na wachezaji wazuri sana kuliko wa Azam lakini sote tunajua matokeo.

Wachezaji wanafundishwa kuunda timu na kocha wao. Wakishauda timu halafu mmoja akaondoka ghafla itabidi kocha aanze upya kuunda timu nyingine
 
Lakini Feisal aliondoka katikati ya msimu na baadhi ya mashabiki walisema anazo haki zote yeye Feisal si mtumwa.
Nita shangaa ikiwa Kibu atakataliwa kuondoka wakati mashabiki haohao walisema wachezaji wako huru kuondoka.
Feisal hakuondoka kihalali; ndiyo maana alishindwa kesi zote huko TFF. Mamlaka ya raisi wa JMT ndiyo yaliyoingilia kati ( si unajua raisi wa JMT, Feisal, na Bakhresa)
 
Mchezaji awe huru kuacha kazi wakati wowote kama ilivyo ajira nyingine. Akitaka kuacha atoe notice ya muda kadhaa kama ilivyo kazi nyingine. Kwa muda ambao anakuwa ametoa notice, timu itafute mchezaji mwingine.
MKuu Field ya Mpira ni tofauti sana na ajira nyingine.

Kwenye mpira kuna mashindano.
Na kwenye ushindani lazima kuwe na sheria ambazo zitafanya ushindani uwe fair.

Moja wapo ya sheria ni kuwa na madirisha maalumu yanayoruhuru uhamisho wa wachezaji.
 
MKuu Field ya Mpira ni tofauti sana na ajira nyingine.

Kwenye mpira kuna mashindano.
Na kwenye ushindani lazima kuwe na sheria ambazo zitafanya ushindani uwe fair.

Moja wapo ya sheria ni kuwa na madirisha maalumu yanayoruhuru uhamisho wa wachezaji.
Mkuu, wewe sasa kwa maelezo haya angalau ndo umeanza kuelezea facts.
Ila kwa ufahamu wangu nadhani hizi sheria zina-favour zaidi Timu za Mpira na kuwanyima uhuru wachezaji.
 
Back
Top Bottom