Kwa nini nyumba za watu wa imani hazina sehemu za ibada?

Kwa nini nyumba za watu wa imani hazina sehemu za ibada?

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Watu wa imani sala ndio kila kitu. Yaani wakati wasio na imani wanajisifia nyumba ni choo, wao wanatakiwa kusema nyumba ni chumba cha sala.

Watu wengi wa kipato cha kati wakifikilia kujenga, ramani ni masterbedroom, chumba cha vijana wa kike, cha vijana wa kiume, choo cha ndani, sebule na dining, jiko na store. Muonekano wa nje ni mbwembwe tu ila ndani pataishia hivyo.
Akijitahidi ataweka kanyumba ka nje (servant quarter) ili asilale na wageni wenye hadhi ya Chini kwenye nyumba kubwa au ndugu ambao hawapendwi saana.

Huu mtego hadi watu wa imani wamenasa. Kulipaswa kuwa na chumba maalumu cha ibada ambacho sio cha mchezo wala masihara. Chumba hicho ni faragha hata baba mambo yakikusibu unajifungia humo ukiungurumisha dua kwa Mwenyezi Mungu.

Dunia ilipofikia inataka watu wenye misimamo kwenye wanachoamini na kuonyesha kwa vitendo.

Kqma unaimani na mazoezi, Weka chumba cha Gym.

Kama unaamini Mizimu, weka kilinge cha matambiko,

Kqma unaamini katika Uislam, weka kamsikiti kadogo nyumbani

Kama unaamini katika Yesu ambaye ni Mungu, weka chumba cha sala nyumbani tena kizuri kuliko vyumba vyote.

Ni hayo tu....

Kama umeelewa, fanyia kazi. Ishi kwa vitendo unavyoviamini.
 
Ukweli mtupu,tena ukiweka chumba kimoja kwa ajili ya Ibada,nyumba yako inapata baraka sana
 
Ndio sahihi,Nashukuru Mungu mimi hili nimelifanya,Kule India chumba cha sala wanaita PUJA
 
Watu wa imani sala ndio kila kitu. Yaani wakati wasio na imani wanajisifia nyumba ni choo, wao wanatakiwa kusema nyumba ni chumba cha sala.

Watu wengi wa kipato cha kati wakifikilia kujenga, ramani ni masterbedroom, chumba cha vijana wa kike, cha vijana wa kiume, choo cha ndani, sebule na dining, jiko na store. Muonekano wa nje ni mbwembwe tu ila ndani pataishia hivyo.
Akijitahidi ataweka kanyumba ka nje (servant quarter) ili asilale na wageni wenye hadhi ya Chini kwenye nyumba kubwa au ndugu ambao hawapendwi saana.

Huu mtego hadi watu wa imani wamenasa. Kulipaswa kuwa na chumba maalumu cha ibada ambacho sio cha mchezo wala masihara. Chumba hicho ni faragha hata baba mambo yakikusibu unajifungia humo ukiungurumisha dua kwa Mwenyezi Mungu.

Dunia ilipofikia inataka watu wenye misimamo kwenye wanachoamini na kuonyesha kwa vitendo.

Kqma unaimani na mazoezi, Weka chumba cha Gym.

Kama unaamini Mizimu, weka kilinge cha matambiko,

Kqma unaamini katika Uislam, weka kamsikiti kadogo nyumbani

Kama unaamini katika Yesu ambaye ni Mungu, weka chumba cha sala nyumbani tena kizuri kuliko vyumba vyote.

Ni hayo tu....

Kama umeelewa, fanyia kazi. Ishi kwa vitendo unavyoviamini.
Mkuu kwa wale wazee wa ulabu, wanaweza kuweka chumba maalum kwa ajili ya huo. Tatizo linakuja pale unapokuwa ni mtu mwenye vipaumbele vingi, hii inamaanisha nyumba yako itapaswa kuwa na utitiri wa vyumba vingi sana na maalum kwa ajili ya shighuli hizo maalum.

Kutakuwa ni kile chumba maalum kwa ajili ya mambo ya ibada, mazoezi, maktaba, kilaji, n.k. Kwa hiyo hii inathibitisha ukweli kwamba nyumba nyingi za kawaida hujengwa ili ku "accomodate" mahitaji ya jumla ya kifamilia ambayo ni mahususi kwa ajili ya chakula, malazi, na mavazi.

Mambo mengine kuhusu "work-life balance" hupaswa kufanyika katiia maeneo mengine maalum ambayo hutengwa kwa ajili ya shughuli hizo muhimu za kimaisha.
 
Back
Top Bottom