Kwa nini Simba na Yanga hawaweki hesabu zao za kifedha hadharani kwa wanachama wao kuondoa harufu na mizozo ya ulaji na upigaji?

Kwa nini Simba na Yanga hawaweki hesabu zao za kifedha hadharani kwa wanachama wao kuondoa harufu na mizozo ya ulaji na upigaji?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Hizi timu mbili zinazoitwa za wanachama kwa nini uongozi wao hawaweki hesabu zao za kifedha hadharani?

Ukirejea haya malalamiko ya huyu anayeitwa mzee wa Yanga, Magoma na Hamis Kigwangala wa Simba inaonyesha kuna ujanja mkubwa sana katika hizi timu. Hii yote ingeweza kuwekwa sawa kama masuala ya kifedha na biashara katika hizi timu yangekuwa wazi.

Kwenye hizi timu ilitakiwa ijulikane,
Nani ameweka shilingi ngapi kila mwaka, ionyeshe kama ni pesa za mkopo, udhamini au mtu amejitolea sadaka tu kwa kuipenda timu. Pia mapato mengine yote kuanzia ada za uanachama, viingilio vya mechi hadi na mapato ya kushiiki michuano au kuchukua makombe yalitakiwa yawe wazi. Gharama zote pia zilitakiwa kuwekwa wazi. Kwa kifupi hizi timu kila mwaka zinatakiwa kuandaa na kuchapisha hadharani financial statements.

Huyo mzee magoma anasema Yanga katika mauzo ya jezi moja wanapata Tsh 1,300 wakati jezi inauzwa 35,000. Tajiri anaagiza mzigo wa jezi mwenyewe, anafunga na kufungua kontena mwenyewe, anauza mwenyewe. Kwa mwaka wanaambiwa wanapata mapato zaidi ya bilioni 13 kutoka kwa tajiri na wadhamini tu ila mwisho wa siku wanaambiwa timu imepata hasara. Kuna mambo ya hovyo sana kwenye hizi timu.
 
Hizi timu mbili zinazoitwa za wanachama kwa nini uongozi wao hawaweki hesabu zao za kifedha hadharani?

Ukirejea haya malalamiko ya huyu anayeitwa mzee wa Yanga, Magoma na Hamis Kigwangala wa Simba inaonyesha kuna ujanja mkubwa sana katika hizi timu. Hii yote ingeweza kuwekwa sawa kama masuala ya kifedha na biashara katika hizi timu yangekuwa wazi.

Kwenye hizi timu ilitakiwa ijulikane,
Nani ameweka shilingi ngapi kila mwaka, ionyeshe kama ni pesa za mkopo, udhamini au mtu amejitolea sadaka tu kwa kuipenda timu. Pia mapato mengine yote kuanzia ada za uanachama, viingilio vya mechi hadi na mapato ya kushiiki michuano au kuchukua makombe yalitakiwa yawe wazi. Gharama zote pia zilitakiwa kuwekwa wazi. Kwa kifupi hizi timu kila mwaka zinatakiwa kuandaa na kuchapisha hadharani financial statements.

Huyo mzee magoma anasema Yanga katika mauzo ya jezi moja wanapata Tsh 1,300 wakati jezi inauzwa 35,000. Tajiri anaagiza mzigo wa jezi mwenyewe, anafunga na kufungua kontena mwenyewe, anauza mwenyewe. Kwa mwaka wanaambiwa wanapata mapato zaidi ya bilioni 13 kutoka kwa tajiri na wadhamini tu ila mwisho wa siku wanaambiwa timu imepata hasara. Kuna mambo ya hovyo sana kwenye hizi timu.
Wakati timu wanaendesha wanachama walifanya nini la maana?

Halafu wewe si mfuatiliaji wa mambo Simba na Yanga wameshatowa report zao za fedha za mapato na matumizi.

Nendeni kwenye timu za mikoa yenu mziongoze kupata mafanikio kama mnadhani ni kazi rahisi.

Msione vinaelea.
1720546266110.jpg
 
Hufuatilii. Kwenye mikutano mikuu ya timu hizo ya hivi karibuni hesabu zimewekwa hadharani tuliona. Kwa mfano Yanga wao walisema timu imepata hasara ya zaidi ya bilioni 1 kwenye gharama za uendeshaji.
 
Hufuatilii. Kwenye mikutano mikuu ya timu hizo ya hivi karibuni hesabu zimewekwa hadharani tuliona. Kwa mfano Yanga wao walisema timu imepata hasara ya zaidi ya bilioni 1 kwenye gharama za uendeshaji.
Weka hapa hizo financial statements, au mliandikiwa hesabu ubaoni kwa chaki tu kisha zikafutwa.
Sio wanachama, mashabiki na wapenzi wote wanaweza kuingia kwenye mkutano mkuu.
 
Weka hapa hizo financial statements, au mliandikiwa hesabu ubaoni kwa chaki tu kisha zikafutwa.
Sio wanachama, mashabiki na wapenzi wote wanaweza kuingia kwenye mkutano mkuu.
Kichwa cha uzi kinasema kuweka hesabu hadharani kwa wanachama. Kuweka hesabu hadharani kwa wanachama ndio kuchapisha kwenye mitandao kama hapa jamii forums?

Wanachama wamekwenda kwenye mkutano na hesabu wakawekewa hadharani huko kwenye mkutano. Kama wewe ni mwanachama hesabu utazipata kwenye mkutano. Timu ya mpira wa miguu hailazimishwi kisheria kuchapisha hesabu zake kwa umma. Ile sio taasisi ya fedha.
 
Weka hapa hizo financial statements, au mliandikiwa hesabu ubaoni kwa chaki tu kisha zikafutwa.
Sio wanachama, mashabiki na wapenzi wote wanaweza kuingia kwenye mkutano mkuu.
Tufanye assumption kuwa kuna wizi ama kuna uongo kwenye ripoti, naomba niambie kama hao wataiba pesa je wataiba hiyo pesa kutoka kwenye fungu lipi? Maana tukiongea tu uhalisia, ela ya viingilio haviwezi hata kuendesha timu mara ngapi tunatangaziwa mapato na TFF kwenye mechi kubwa za Simba vs Yanga na tunashuhudia mechi kubwa timu inapata ela kidogo. Embu weka wazi ela zinaibwa kwenye mapato yapi?
 
Ninachojua kunakuwa na FS ila shida ni kwenye hesabu hazina uhalisia. Kuna mdhamini au watu wanatoa hela zinasajili wachezaji halafu zinaingiwa ktk matumizi ya timu kana kwamba klabu imetoa hela yake. Hapa ndo kuna michezo inachezwa. Kuna mchezaji anataka labda Dola 50,000 klabu haina hela mtu anatoa zake mfukoni mchezaji anasajiliwa then jamaa anakuwa anaidai klabu pesa. Siku timu ikicheza mechi mapato ya mlangoni yakiiingia tuseme 200m jamaa anachukua chake plus interest. Ndio maana nyakati zote akaunti ya klabu huwezi kukuta salio hata mara moja. Na hawa jamaa ndo watu wa ndani kabisa.
 
Wakati timu wanaendesha wanachama walifanya nini la maana?

Halafu wewe si mfuatiliaji wa mambo Simba na Yanga wameshatowa report zao za fedha za mapato na matumizi.

Nendeni kwenye timu za mikoa yenu mziongoze kupata mafanikio kama mnadhani ni kazi rahisi.

Msione vinaelea.View attachment 3045313
Timua chama huyo ana gundu
 
Labda huko utopoloni, ila Mo anaweka mapato na matumizi. Ni hasara tuu anayopata ya mabilioni ya pesa ila kwa kuwa anaipenda timu basi anazidi tu kumwaga mabilioni wala hajali hasara anayopata 😀😀
 
Ninachojua kunakuwa na FS ila shida ni kwenye hesabu hazina uhalisia. Kuna mdhamini au watu wanatoa hela zinasajili wachezaji halafu zinaingiwa ktk matumizi ya timu kana kwamba klabu imetoa hela yake. Hapa ndo kuna michezo inachezwa. Kuna mchezaji anataka labda Dola 50,000 klabu haina hela mtu anatoa zake mfukoni mchezaji anasajiliwa then jamaa anakuwa anaidai klabu pesa. Siku timu ikicheza mechi mapato ya mlangoni yakiiingia tuseme 200m jamaa anachukua chake plus interest. Ndio maana nyakati zote akaunti ya klabu huwezi kukuta salio hata mara moja. Na hawa jamaa ndo watu wa ndani kabisa.
Kwa nini wasionyeshe wazi kwamba fulani katoa shilingi kadhaa kama mkopo kusaidia kununua mchezaji fulani na atarejeshewa kiasi kadhaa??
 
Tufanye assumption kuwa kuna wizi ama kuna uongo kwenye ripoti, naomba niambie kama hao wataiba pesa je wataiba hiyo pesa kutoka kwenye fungu lipi?
Kama katika mauzo ya jezi moja yanga inatakiwa kupata 5,000 halafu inapewa 1,300 huo ni wazi.
Upigaji uko wa aina nyingi katika klabu ya mpira.
 
Kama katika mauzo ya jezi moja yanga inatakiwa kupata 5,000 halafu inapewa 1,300 huo ni wazi.
Upigaji uko wa aina nyingi katika klabu ya mpira.
Mauzo ya jezi yanaweza kuendesha timu? Embu nipe vyanzo vya mapato vya hizi timu za kariakoo zinazoweza kufanya zijiendeshe zenyewe.
 
Umeongea Jambo la msingi, wanachama wengi wakiingia mkutanoni kazi yao ni kupiga makofi.
Pesa na hesabu zao zinatakiwa kukaguliwa na kuwekwa hadharani na sio kuja kusema tumepata hasara.
 
Mauzo ya jezi yanaweza kuendesha timu? Embu nipe vyanzo vya mapato vya hizi timu za kariakoo zinazoweza kufanya zijiendeshe zenyewe.
Kipi usichoelewa? Hesabu za mapato za klabu zinatakiwa zionyeshe kiasi cha
1. Ada za wanachama
2. Mapato ya viingilio vya mechi
3. Pesa za udhamini
4. Pesa za matangazo
5. Pesa za misaada
6. Pesa zitakanazo na ushiriki mashindano mbalimbali
 
Kipi usichoelewa? Hesabu za mapato za klabu zinatakiwa zionyeshe kiasi cha
1. Ada za wanachama
2. Mapato ya viingilio vya mechi
3. Pesa za udhamini
4. Pesa za matangazo
5. Pesa za misaada
6. Pesa zitakanazo na ushiriki mashindano mbalimbali

Hiyo namba 1 na namba 2 pekee haziwezi kuendesha timu, pesa za udhamini, pesa za ushiriki wa mashindano hizo ni matokeo ya uongozi bora unaobuni na kushawishi makampuni mbalimbali. Hizo kampuni zilikuwepo tangu na tangu lakini hapo zamani husikii kampuni imedhamini timu kwa milioni 500 au bilioni kadhaa ila ni swala la maono ya kiuongozi. Na pesa za mashindano, ukiachana na mashindano ya CAF hakuna mashindano mengine yanayolipa vizuri na utambue hadi upate hizo pesa lazima timu iwe imevuka hatua.

Ingekuwa ni rahisi hivyo kupata ela kuendesha vilabu basi tungeona hizi Simba na Yanga kipindi cha nyuma zikiyumba kiuchumi na kushindwa kusajili wachezaji bora nje ya mipaka ya Tanzania. Timu zinapata mafanikio kupitia utashi na akili za wenye pesa zao wanaojua namna kuendesha taasisi mnaanza ngebe za kuibiwa utafikiri hivi vilabu vilikuwa vinaukwasi wa kutosha hapo kabla.
 
Kipi usichoelewa? Hesabu za mapato za klabu zinatakiwa zionyeshe kiasi cha
1. Ada za wanachama
2. Mapato ya viingilio vya mechi
3. Pesa za udhamini
4. Pesa za matangazo
5. Pesa za misaada
6. Pesa zitakanazo na ushiriki mashindano mbalimbali

Nani aliyetoa pesa za msaada?
Chukua hizo pesa za ada jumlisha na pesa za viingilio kisha jumlisha na pesa matangazo ni sh ngapi kwa wastani kwa mwaka?

Kwenye hiyo pesa toa mishahara ya wachezaji wa Yanga princess, yanga timu ya wanaume, na timu ya vijana kwa mwaka. Kisha mishahara ya benchi la ufundi kwa timu zote tatu za yanga, kisha toa mishahara ya watendaji (wafanyakazi) kisha toa gharama ya mbalimbali kama safari, chakula na malazi.

N.b mchezaji mmoja akilipwa mshahara wa mil 25 kwa mwezi ina maana ndani ya miezi 10 anakunja mil 250 mtu mmoja pekee.
 
Kipi usichoelewa? Hesabu za mapato za klabu zinatakiwa zionyeshe kiasi cha
1. Ada za wanachama
2. Mapato ya viingilio vya mechi
3. Pesa za udhamini
4. Pesa za matangazo
5. Pesa za misaada
6. Pesa zitakanazo na ushiriki mashindano mbalimbali
Nimejiridhisha wewe huna akili kichwani, unaichosha shingo yako tu kwa kubeba empty kasha.
 
Back
Top Bottom