Kongosho
JF-Expert Member
- Mar 21, 2011
- 35,991
- 24,211
mie niliwahi leta uzi hapa nikauliza maana ya kujirekodi ni nini, sikupata jibu hata moja nilililoelewa.
Lakini hata hawa wanawake wanafanya na wanamme, mie naona wote aibu iko pale pale.
Labda kama hao wanawake walikutwa wanafanya wao wenyewe vinginevyo aibu ya wote tu.
Lakini hata hawa wanawake wanafanya na wanamme, mie naona wote aibu iko pale pale.
Labda kama hao wanawake walikutwa wanafanya wao wenyewe vinginevyo aibu ya wote tu.
We mzee mwenzangu Mamndenyi , haya mambo tuwaachie vijana.
Sisi enzi zetu kupiga picha lazima uende studio na redio na maua unaweka juu ya stuli na pozi kuuubwa. Unajihakiki kama bugaluu na raizoni zimekaa vyema. Nywele unazipiga kwa kitanna cha mti. Shati vifungo kama ishirini hivi tena lazima liwe la kubana. Saa lazima ionekane na ilikuwa lazima iwe kubwa kama mita ya maji. Jamaa anakupiga black and white na unaambiwa uje uchukue picha baada ya wiki mbili! Ole wake asikupe negative ya picha....
Haya mambo kina RussianRoulette, gfsonwin Cantalisia, Erotica Bishanga na Rejao walikuwa bado kuzaliwa na kina Kongosho na AshaDii walikuwa bado hawajavunja manyungo.
Last edited by a moderator:
