Kwa sasa hakuna Mpinzani wa kuipigania Tume Huru ya Uchaguzi waliopo wanategemea huruma ya CCM

Kwa sasa hakuna Mpinzani wa kuipigania Tume Huru ya Uchaguzi waliopo wanategemea huruma ya CCM

Kiongozi wewe kwa ufupi hujielewi

Tunapoongelea Tume huru, Tunaongelea maisha ya watoto na wajukuu zetu baadae

Tunaongelea siku ukiwa haupo hapa duniani ungependa watoto wako waishi vipi kisiasa na kiuchumi

Hili la Tume huru ni la kila mtu,
Wengine Tume iliyopo wanaiamini bwashee....... Usikariri!
 
Kiukweli kwa hawa wapinzani tulionao Tume Huru ya Uchaguzi itaendelea kuwa ndoto hadi pale CCM itakapotupa JK mwingine wa kuanzisha mchakato wa kutengeneza Katiba mpya.

Hakuna namna vyama vya upinzani vitaweza kushinda uchaguzi bila kuwa na Tume huru.

Sidhani kama CCM bado ina huruma au bado inaogopa Wafadhili kwani nijuavyo ni kwamba kwa sasa taifa letu linajitegemea.

Kwa NEC hii sitashangaa kuona Wapinzani wakikosa mbunge na diwani hata mmoja katika uchaguzi mkuu wa mwezi Octoba.

Na hapa asitafutwe mchawi bali wachawini wapinzani wenyewe.

Maendeleo hayana vyama!
Kati ya wanaJF wengi hapa, ni wewe unayenipa wakati mgumu kujua hasa unasimamia wapi; Tanzania au CCM.

Mfano mzuri ni mada hii.

Umeandika ukweli mtupu usioweza kupingwa kirahisi.

Ingekuwa ni CCM kama CCM yenyewe, pengine pangekuwepo na mategemeo kwamba pamoja na udhaifu walionao vyama vya upinzani wangeweza wakajitutumua na wananchi wakawaonea huruma kwa baadhi ya maeneo.

Lakini hapa sio CCM tena, ni mtu mwenye mabavu ambaye hata CCM yenyewe haifurukuti mbele yake. Na kutokana na vifaa alivyonavyo, hakuna yeyote atakayezuia lolote analotaka yeye lifanyike.
Wapinzani, sijui kama safari hii watapona.

Na ukifikiri kwa undani wake, pengine ni bora kutokuwepo na upinzani katika hali hii, maana utakuwa unatia tu matumaini yasiyokuwepo. Upinzani usiokuwa na uwezo wa kubadili chochote hapo hakuna upinzani tena.

Ni bora uondoke tujue letu moja tu! Kwamba tunae mtu anayejua kila jambo na anayejua mahitaji yetu yote ya maendeleo yanayotakiwa kuwepo ndani ya nchi hii. Mtu anayejua kwamba wananchi hawahitaji kuwa na haki ya kuchagua viongozi wao, ila yeye anajua viongozi wanaohitajiwa na wananchi.
 
Sasa why mpinzani au chadema ndo waipiganie na wanaipigania toka kwa nani na anatunyima hiyo tume kwa faida ya nani?
Kati ya wanaJF wengi hapa, ni wewe unayenipa wakati mgumu kujua hasa unasimamia wapi; Tanzania au CCM.

Mfano mzuri ni mada hii.

Umeandika ukweli mtupu usioweza kupingwa kirahisi.

Ingekuwa ni CCM kama CCM yenyewe, pengine pangekuwepo na mategemeo kwamba pamoja na udhaifu walionao vyama vya upinzani wangeweza wakajitutumua na wananchi wakawaonea huruma kwa baadhi ya maeneo.

Lakini hapa sio CCM tena, ni mtu mwenye mabavu ambaye hata CCM yenyewe haifurukuti mbele yake. Na kutokana na vifaa alivyonavyo, hakuna yeyote atakayezuia lolote analotaka yeye lifanyike.
Wapinzani, sijui kama safari hii watapona.

Na ukifikiri kwa undani wake, pengine ni bora kutokuwepo na upinzani katika hali hii, maana utakuwa unatia tu matumaini yasiyokuwepo. Upinzani usiokuwa na uwezo wa kubadili chochote hapo hakuna upinzani tena.

Ni bora uondoke tujue letu moja tu! Kwamba tunae mtu anayejua kila jambo na anayejua mahitaji yetu yote ya maendeleo yanayotakiwa kuwepo ndani ya nchi hii. Mtu anayejua kwamba wananchi hawahitaji kuwa na haki ya kuchagua viongozi wao, ila yeye anajua viongozi wanaohitajiwa na wananchi.
Kila siku unashindwa kutimiza wajibu wako kwa sababu ibilisi anakuzidi nguvu na maarifa, je, kwa sababu ibilisi anakuzidi nguvu utajisalimisha kwake na kumkufuru Mungu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mara nyingine kumbe una akili, hoja yako naikubali 100%, ni kipofu tu atakayeweza kukubali kwamba upinzani watapata hata kiti kimoja kwa tume iliyopo. Badala ya kukimbizana na mambo ya kijinga afadhali wangepambana kupata tume huru ya uchaguzi, hilo liwe ndo lengo lao kubwa.

Hayo mengine wanajipotezea tu muda.
 
Kuna shida sana. Hivi bado tunafikiria uwepo wa tume huru ni kwa manufaa ya "wapinzani"? Kama hivyo ndivyo, hata hiyo demokrasia haina maana kabisa.

Nafikiri uwepo wa tume huru (soma demokrasia ya kweli) ni kwa manufaa ya watanzania na Tanzania yao. Watanzania ndio wanapaswa kupigania uwepo wa demokrasia ya kweli (ikiwapo tume huru) ili wapate viongozi wanaowataka kweli na kujiletea maendeleo.
 
Kila siku unashindwa kutimiza wajibu wako kwa sababu ibilisi anakuzidi nguvu na maarifa,
Jibu umekwishaliweka hapa mkuu 'infinix'.

Isingekuwa hivyo pasingekuwepo na sehemu inayoitwa jehenamu.

Kama umepangiwa huko, ni lazima utakwenda tu, hata ufanye nini!

'On a serious note':
Hapana sipendekezi iwe hivyo. Ninalosema mimi ni kuwa kwa upinzani tulionao sasa hivi hakuna njia.

Bila shaka kuna siku patainuka viongozi walio imara zaidi ya tulionao sasa hivi huko kwenye upinzani. Viongozi ambao 'conviction' yao kwa wanachokipigania ni kila kitu, na kama inalazimu hata maisha wanayaweka rehani.

Tuna jua viongozi hao wapo, ila hawajajitokeza mbele wawaongoze wananchi.

Nani aliyejua kuwepo kwa akina Martin Luther King Jr. hadi walipojitokeza mbele na wananchi kuwaunga mkono.

Nasi tunao viongozi hao Tanzania yetu hii; ni jinsi tu ya kuwatambua na kuwapa nafasi ya kutuongoza.
 
Kuna shida sana. Hivi bado tunafikiria uwepo wa tume huru ni kwa manufaa ya "wapinzani"? Kama hivyo ndivyo, hata hiyo demokrasia haina maana kabisa.

Nafikiri uwepo wa tume huru (soma demokrasia ya kweli) ni kwa manufaa ya watanzania na Tanzania yao. Watanzania ndio wanapaswa kupigania uwepo wa demokrasia ya kweli (ikiwapo tume huru) ili wapate viongozi wanaowataka kweli na kujiletea maendeleo.
Hapana.

Upinzani unatajwa tu kama uongozi kwa wananchi waliotayari kutafuta mabadiliko. Wananchi bila uongozi inakuwa shida kuendesha shughuli za kuleta mabadiliko.

Ni lazima pawepo na mipango na uratibu wa mipango ya kuyaleta mabadiliko hayo, ikiwa ni pamoja na ajenda ya kuwa na 'Tume Huru'.
 
Hapana.

Upinzani unatajwa tu kama uongozi kwa wananchi waliotayari kutafuta mabadiliko. Wananchi bila uongozi inakuwa shida kuendesha shughuli za kuleta mabadiliko.

Ni lazima pawepo na mipango na uratibu wa mipango ya kuyaleta mabadiliko hayo, ikiwa ni pamoja na ajenda ya kuwa na 'Tume Huru'.
Sawa. lakini kusema tume huru ya uchaguzi ni kwa manufaa ya wapinzani hiyo si sawa. Ukiona mtu anafurahia bunge au mbaraza ya madiwani kukosa wapinzani ujue kuna tatizo. Uwepo wa demokrasia ni kwa manufaa yetu sote....watanzania.
 
Kiukweli kwa hawa wapinzani tulionao Tume Huru ya Uchaguzi itaendelea kuwa ndoto hadi pale CCM itakapotupa JK mwingine wa kuanzisha mchakato wa kutengeneza Katiba mpya.

Hakuna namna vyama vya upinzani vitaweza kushinda uchaguzi bila kuwa na Tume huru.

Sidhani kama CCM bado ina huruma au bado inaogopa Wafadhili kwani nijuavyo ni kwamba kwa sasa taifa letu linajitegemea.

Kwa NEC hii sitashangaa kuona Wapinzani wakikosa mbunge na diwani hata mmoja katika uchaguzi mkuu wa mwezi Octoba.

Na hapa asitafutwe mchawi bali wachawini wapinzani wenyewe.

Maendeleo hayana vyama!
Nchi hii haina upinzani, imejaa ma opportunist tuu ! Absolutely no credible opposition party ! Viongozi wabinafsi, wapigaji hela acha kabisa !
 
Nchi hii haina upinzani, imejaa ma opportunist tuu ! Absolutely no credible opposition party ! Viongozi wabinafsi, wapigaji hela acha kabisa !
Mkuu wapinzani wa kweli huwa unawaona nchi gani na wana tofauti gani na hawa wa kwetu?
 
Sawa. lakini kusema tume huru ya uchaguzi ni kwa manufaa ya wapinzani hiyo si sawa. Ukiona mtu anafurahia bunge au mbaraza ya madiwani kukosa wapinzani ujue kuna tatizo. Uwepo wa demokrasia ni kwa manufaa yetu sote....watanzania.
uwepo wa tume huru ya uchaguzi si utu utafanya democrasia itamalaki bali pia itatuongezea probability ya kupata viongozi wazuri na competent na hivyo kutuepusha na taifa kuwa na viongozi wa aina ya magufuli
 
Back
Top Bottom