Kwa sasa huenda 90% ya Degree hazina tena maana, hazikupi ajira wala maarifa ya kupata kipato

Kwa sasa huenda 90% ya Degree hazina tena maana, hazikupi ajira wala maarifa ya kupata kipato

Mimi nimesema, usomi wa degree kwa sasa 90% umeshindwa kufikia malengo (ajira au kipato).

Kama kwa 100% ya vijana walikwenda kusoma degree ili ziwasaidie kirahisi kupata ajira na kipato cha uhakika, halafu baada ya wao kuhitimu 90% wameshindwa kupata ajira au kipato kupitia degree zao, hapo utasemaje?
Kama msingi wa elimu ya digrii ni kuajiriwa lazima tukae chini tuangalie ni wapi hasa katika jamii yetu ni muajibikaji wa ajira. Sekta ya uchumi lazima itupe majibu

Na iwe na uwezo wa kubeba watu wengi zaidi kila mwaka mana waafrika kwa kuzaana hatujambo. Any way Kuna marifa unatakiwa uyapate. Tafuta kitabu kimoja ameandika Adam jamrozik 1998
 
ndio tulikofika, cha kufanya sasa ni kuwa na altenative ways/plan A, B, C yaani wakati unasomea kuajiriwa pia unasoma na kujifunza mambo mengine mengine interested. Ukifeli kuajiriwa tayari una ujuzi wa kujiajiri na maisha yanaendelea kama kawaida. Tusisahau ukulima, ufugaji, biashara/ujasiriamali na ufundi
Kuliko kupoteza pesa, muda na nguvu kusoma degree ambayo mtaani kwa 90% haiwezi kuajirika, kwanini asijikite kujifunza ujuzi mahususi ambao elimu ya darasa la saba inatosha sana kuweza kuumudu na moja kwa moja aingie mtaani kupambana kuitumia.
 
Kama msingi wa elimu ya digrii ni kuajiriwa lazima tukae chini tuangalie ni wapi hasa katika jamii yetu ni muajibikaji wa ajira. Sekta ya uchumi lazima itupe majibu

Na iwe na uwezo wa kubeba watu wengi zaidi kila mwaka mana waafrika kwa kuzaana hatujambo. Any way Kuna marifa unatakiwa uyapate. Tafuta kitabu kimoja ameandika Adam jamrozik 1998
Maisha ya watanzania wengi yamejengwa kwenye uchumi mdogo mdogo na Uchumi mdogo mdogo wa Tanzania kwa 80% sio rasmi, hauhitaji hata cheti, huo ndio tunapaswa tuongelee na kuupambania. Hatuna sababu ya kusaka degree ili kushinda hiyo vita, ni suala la Elimu ya darasa la saba mpaka fomu four, kisha moja kwa moja watu wakajifunze fani husika. Kama ni kilimo, basi tukutane shambani, kama ni biashara tukutane sokoni, kama ni ufundi basi tukutane kwenye karakana, vyuo pekee labda ni VETA tu.
 
Nadhani elimu ya ufundi hasa vyuo vya VETA vingeboreshwa zaidi kuanzia mitaala na aina ya wanafunzi.

Magari yameongezeka,ujenzi wa nyumba umekuwa mkubwa sana.Taifa linahitaji vijana wenye skills ufundi umeme,ujenzi,bomba,ufundi magari ya kisasa (utumiaji wa diagnosis) ili tuache kudanganya watu Dualis zinaungua kumbe mafundi wa chini ya Mwembe hawana ujuzi wa kuzitengeneza.

Hizi degree za Procurement,Accounting,Library,Banking,Geography,History ........ kazi zake ni chache sana.
 
Ndugu yangu, soma mada utanielewa.
Nimerudia kusema, kwa hali ilivyo sasa, kwa 90% ya wahitimu wa chuo kikuu wa level ya degree, hawajaweza kuajiriwa kwa degree zao na wala hawajaweza kutengeneza kipato cha kueleweka kutumia degree zao.

Sasa mtu alimaliza degree ya Political science miaka minne iliyopita, akasaka ajira kwa miaka mitatu bila mafanikio Dar, Dodoma na Mwanza, akatupa degree yake kabatini, ndugu wakamchangia mtaji wa milioni tatu akaenda zake huko Mbeya vijijini kujumuika na wanakijiji walioishia darasa la saba, wakamfundisha kulima mpunga, mwaka huu kavuna na kuuza mpunga gunia kama 20, vipi hapo Degree yake ya political science imemsaidiaje kutoboa?
Tatizo lipo katika mindset na sio degree
 
Maisha ya watanzania wengi yamejengwa kwenye uchumi mdogo mdogo na Uchumi mdogo mdogo wa Tanzania kwa 80% sio rasmi, hauhitaji hata cheti, huo ndio tunapaswa tuongelee na kuupambania. Hatuna sababu ya kusaka degree ili kushinda hiyo vita, ni suala la Elimu ya darasa la saba mpaka fomu four, kisha moja kwa moja watu wakajifunze fani husika. Kama ni kilimo, basi tukutane shambani, kama ni biashara tukutane sokoni, kama ni ufundi basi tukutane kwenye karakana, vyuo pekee labda ni VETA tu.
Do you know anything about social force?
 
Ndugu yangu, soma mada utanielewa.
Nimerudia kusema, kwa hali ilivyo sasa, kwa 90% ya wahitimu wa chuo kikuu wa level ya degree, hawajaweza kuajiriwa kwa degree zao na wala hawajaweza kutengeneza kipato cha kueleweka kutumia degree zao.

Sasa mtu alimaliza degree ya Political science miaka minne iliyopita, akasaka ajira kwa miaka mitatu bila mafanikio Dar, Dodoma na Mwanza, akatupa degree yake kabatini, ndugu wakamchangia mtaji wa milioni tatu akaenda zake huko Mbeya vijijini kujumuika na wanakijiji walioishia darasa la saba, wakamfundisha kulima mpunga, mwaka huu kavuna na kuuza mpunga gunia kama 20, vipi hapo Degree yake ya political science imemsaidiaje kutoboa?
Mimi nakuelewa mkuu, ni kweli kundi kubwa la wahitimu wengi wa degree hawana ajira na ukizingatia mitaala yetu imeshindwa kumuandaa mhitimu kujiajiri pia serikali bado haijaweka mazingira wezeshi kwa mtu kujiajiri na pia sekta binafsi kukua kwa ujumla.

Ajira za sasa kwa uchache wake kama huna connection inakuwa ngumu kupata ni wachache sana wanao zingatia ufaulu na uwezo wa mtu.
 
Hivyo tunarudi pale pale, kwa 90% hakuna tena ulazima wa watu kusoma mpaka chuo kikuu ili kupata degree. Ni kupoteza rasimali tu. Maana mwisho wa siku hupati ajira wala huwezi kutumia degree yako kutengeneza kipato.
Tatizo ni wenge la wazazi na vijana wenyewe, huwezi kuwaeleza kitu kwamba wasisome degree.......na hii yote ni kutaka wawe kama waliowatangulia bila kujua mambo huwa yanabadilika kuendana na nyakati.

Jambo jingine lilitokea wimbi hapo kati la kuua vyuo vya kati na kuvifanya kuwa vyuo vikuu na baada ya bodi ya mikopo kuanza kufadhili hadi kwenye vyuo binafsi mtifuano wa kuongeza idadi ya vyuo, kozi na idadi ya wanafunzi ukawa mkubwa.

Mimi naona serikali ingejikita kufadhili masomo ya degree kwenye vyuo vikuu vya umma kulingana na bajeti na uhitaji na kupanua zaidi elimu ya vyuo vya awali na kati (certicate, diploma, VETA).​
 
Nadhani elimu ya ufundi hasa vyuo vya VETA vingeboreshwa zaidi kuanzia mitaala na aina ya wanafunzi.

Magari yameongezeka,ujenzi wa nyumba umekuwa mkubwa sana.Taifa linahitaji vijana wenye skills ufundi umeme,ujenzi,bomba,ufundi magari ya kisasa (utumiaji wa diagnosis) ili tuache kudanganya watu Dualis zinaungua kumbe mafundi wa chini ya Mwembe hawana ujuzi wa kuzitengeneza.

Hizi degree za Procurement,Accounting,Library,Banking,Geography,History ........ kazi zake ni chache sana.
Kama kazi ni chache je, hizo digrii hazina maana?
 
Tatizo ni wenge la wazazi na vijana wenyewe, huwezi kuwaeleza kitu kwamba wasisome degree.......na hii yote ni kutaka wawe kama waliowatangulia bila kujua mambo huwa yanabadilika kuendana na nyakati.​
Mkuu mfano ukisema vijana waache wenge la kusoma degree je ndio solution naona vilevile tu kimsingi hakuna tofauti ya aliyesoma na asiyesoma endapo aliyesoma hakupata kazi so kutokwenda degree si solution mimi niliowaacha mtaani hadi sasa wote tuna maisha sawa tu hawana Steps zozote kiuchumi

Jambo jingine lilitokea wimbi hapo kati la kuua vyuo vya kati na kuvifanya kuwa vyuo vikuu na baada ya bodi ya mikopo kuanza kufadhili hadi kwenye vyuo binafsi mtifuano wa kuongeza idadi ya vyuo, kozi na idadi ya wanafunzi ukawa mkubwa.

Mimi naona serikali ingejikita kufadhili masomo ya degree kwenye vyuo vikuu vya umma kulingana na bajeti na uhitaji na kupanua zaidi elimu ya vyuo vya awali na kati (certicate, diploma, VETA).​
 
Ukweli usemwe na usemwe wazi ili kila mtu aujue. Wigo wa watanzania kusoma mpaka chuo kikuu ili kupata degree umekuwa mkubwa lakini huo mfumo umekuwa ni hasara na upotevu wa rasimali (muda, pesa na nguvu) kwa 90%.

Ajira mtaani kwa 90% hakuna kwa fani nyingi, ni sawa na kucheza kamili, na elimu ya vyeti vya chuo kikuu haina mchango wowote wa mhitimu wa level ya degree kuweza kujiajiri moja kwa moja. Hapa chini ni baadhi ya fani zinazoangukia kwenye kundi hilo.

1. Public administration
2. Political science
3. Business administration
4. Procurement and supply
5. Human resource
6. Sociology
7. Environment
8. Language
9. Mass communication
10. Tourism
11. Banking
12. Accounting
13. Economy
14. Finance
15. History
16. Insurance
17. Tax
18. Cooperative
19. Marketing
20.

Kama wewe ni mhitimu wa hizo fani kwa miaka ya karibuni utaelewa hicho nilichokiandika, na kama wewe ni mwanafunzi wa hizo fani anza kujiandaa kisaikolojia, hali ni mbaya mtaani. Wahitimu ni wengi na hawana ajira yoyote, wamechoka vibaya, wameshazunguka na mabahasha mpaka soli za viatu kuchakaa, wamejitolea mpaka basi, wameshikiza mpaka wamedondoka na wengi wamekata tamaa kabisa, vyeti vyao wamesahau hata vipo wapi, havina msaada. Bado wanakula, kulala na kutunzwa na wazazi wao, mashemeji au wajomba. Wengine wameamua kujiajiri katika fani zingine ambazo hazina uhusiano wowote wa fani walizosomea na zenye kuhitaji elimu ya darasa la nne tu.
Wajanja wengine wameamua kurudi chuo, hususani kwa ngazi ya Diploma kusoma fani za ualimu au afya ili kuingia kwenye mkondo wa kuja kupata ajira hapo baadaye.

Jamani hali ni mbaya na tete.
Ukweli usemwe!
Ukweli mtupu
mtaani kwa sasa hatujivunii digree bali kipato
 
sio kweli, ni uwezo mdogo tu wa kufikiria wa watu tuliowapa mamlaka ya kutuongoza.

Tanzania bado ni nchi masikini yenye opportunities nyingi ambazo zinahitaji hao watu, shida ni uwezo mdogo wa watu kutengeza fursa zitakazotanua uwanja na kutoa ajira nyingi.

Taifa lolote linalojengwa katika stage za mwanzo, halipaswi kuwa na shida ya ajira.
 
Tunarudi pale pale.
Kwa sasa Degree pekee kwa 90% ya wahitimu haina mchango wowote wa kukupa ajira au kipato.

Kumbe mtaani watu wanataka connection na ujuzi mahususi ili utoboe kwenye ajira, sio degree yako.
Degree inakupa knowledge Ila haikupi skills za kuitumia hiyo knowledge Ila kwa sasa kuna initiatives nyingi kama incubators ambazo zinawasaidia hawa vijana kuwa na vitu vyote viwili.. Ubaya hizi initiatives ni za hiyari na wengi hawazichukui

Kwanza tutoke huko kwenye kusubiria degree ikufanyie kitu badala ya wewe kuitumia ikufanikishie mambo yako. Degree haikutumii Ila wewe ndiye mwenye jukumu la kuitumia,

Kama ulichagua course flani for the wrong reasons na hukuweka plan ya kuitumia, usilaumu pale unapofeli maana kufaulu ni responsibility yako

Tunachoweza kulaumu ni hiyo job market kutokukua kiasi cha kuitegemea serikali kama muajiri mkuu, only that
 
🤣🤣🤣🤣 Nina jamaa yangu tulimaliza wote IFm alikua na GPA ya 4.6 now yupo shinyanga anapambana kupata madini. Kuna ajira Tena nyingi zilitoka za bank assurance na walibana kweli kweli kwenye GPA. Cha ajabu Kuna jamaa nilikua napambana naye mtaani kutafuta just wateja tu ili tupate vikamishen vya bima na alikua na GPa ya 2.9 akatoboa na hakua na connection yoyote. Mi naungana na wadau wengine kwamba vyuo vibadilike. Mitaala ibadilishwe. Nenda kasomee insurance au actuarial science Kenya then linganisha na WA TZ utashawashangaa sana Watz. Ni aibu. Mi pia Niko mtaani almost 4 yrs now lakini nilijiongeza na Nina wateja wa bima kibao tu na napata ela ambayo hata doctor hospitalin mwajiriwa hapati na sitaki kusikia mambo ya kuajiriwa. Japo Kuna time kazi zinakata lakini ni kupambana na vibiashara vingine vidogo dogo. Si muda naingia kwenye kilimo
Hongera mkuu,

Na ukweli ni kuwa skills hazihitaji GPA ndio maana nikawashauri watumie hiyo gap maana kampuni ikihitaji videographer, photographer au graphic designer, hawaangalii cheti bali portfolio ya kazi mtu alizowahi kuzifanya..na kama ni extremely corporate,wanaweza omba kujua kiingereza kama qualification

Ila pia kama mtu anaona course yake haimpi maslahi, hakuna gap lililo wazi kama sales kwenye makampuni makubwa

Uzuri hiyo ni game of numbers, anaeweza kuleta mapato mengi zaidi ndio anapata opportunities zaidi kwenye hizo kampuni.. Sema wengi huwa tunazidharau kwa sababu lazma uvuje jasho na damu hadi uwe good salesman unless iwe ni inborn character yako kuweza kushawishi watu kununua bidhaa na ile aggressiveness bhasi

Na hivyo ndivyo wakenya wametuzidi "wapo aggressive".

Hongera mkuu
 
Tunahitaji mapinduzi halisi ya viwanda(industrial revolution), hatuhitaji kuwa na wahitimu wa vyuo vikuu kwa wingi huo, tunahitaji wahitimu wa vyuo vya kati wafanye kazi kwenye viwanda.

Engineer mwenye shahada na mwenye fani yake kwa level ya diploma au cheti, atakayeleta thamani ni mwenye diploma.

Tunahitaji viwanda, otherwise tuna bomb kubwa.
Bomu limeshalipuka tayari....matapeli wa mtandao wengi ni graduates. We are slowly becoming a second Nigeria kwa idadi ya matapeli wasomi!
 
Nadhani elimu ya ufundi hasa vyuo vya VETA vingeboreshwa zaidi kuanzia mitaala na aina ya wanafunzi.

Magari yameongezeka,ujenzi wa nyumba umekuwa mkubwa sana.Taifa linahitaji vijana wenye skills ufundi umeme,ujenzi,bomba,ufundi magari ya kisasa (utumiaji wa diagnosis) ili tuache kudanganya watu Dualis zinaungua kumbe mafundi wa chini ya Mwembe hawana ujuzi wa kuzitengeneza.

Hizi degree za Procurement,Accounting,Library,Banking,Geography,History ........ kazi zake ni chache sana.
Hapa umemaliza kila kitu.
Umekuja na majibu kamili namna ya kukabiliana na hii hali.
Huo ushauri kuanzia serikali, taasisi na mtu mmoja mmoja tunapaswa kuufuata.

VETA, vyuo vya kati na elimu ya ufundi na stadi za maisha ndio mkombozi wetu wa hii hali ya sasa.

Vyuo vikuu tuviache kwa wataalamu wachache sana hususani watafiti.
 
Ukweli usemwe na usemwe wazi ili kila mtu aujue. Wigo wa watanzania kusoma mpaka chuo kikuu ili kupata degree umekuwa mkubwa lakini huo mfumo umekuwa ni hasara na upotevu wa rasimali (muda, pesa na nguvu) kwa 90%.

Ajira mtaani kwa 90% hakuna kwa fani nyingi, ni sawa na kucheza kamili, na elimu ya vyeti vya chuo kikuu haina mchango wowote wa mhitimu wa level ya degree kuweza kujiajiri moja kwa moja. Hapa chini ni baadhi ya fani zinazoangukia kwenye kundi hilo.

1. Public administration
2. Political science
3. Business administration
4. Procurement and supply
5. Human resource
6. Sociology
7. Environment
8. Language
9. Mass communication
10. Tourism
11. Banking
12. Accounting
13. Economy
14. Finance
15. History
16. Insurance
17. Tax
18. Cooperative
19. Marketing
20.

Kama wewe ni mhitimu wa hizo fani kwa miaka ya karibuni utaelewa hicho nilichokiandika, na kama wewe ni mwanafunzi wa hizo fani anza kujiandaa kisaikolojia, hali ni mbaya mtaani. Wahitimu ni wengi na hawana ajira yoyote, wamechoka vibaya, wameshazunguka na mabahasha mpaka soli za viatu kuchakaa, wamejitolea mpaka basi, wameshikiza mpaka wamedondoka na wengi wamekata tamaa kabisa, vyeti vyao wamesahau hata vipo wapi, havina msaada. Bado wanakula, kulala na kutunzwa na wazazi wao, mashemeji au wajomba. Wengine wameamua kujiajiri katika fani zingine ambazo hazina uhusiano wowote wa fani walizosomea na zenye kuhitaji elimu ya darasa la nne tu.
Wajanja wengine wameamua kurudi chuo, hususani kwa ngazi ya Diploma kusoma fani za ualimu au afya ili kuingia kwenye mkondo wa kuja kupata ajira hapo baadaye.

Jamani hali ni mbaya na tete.
Ukweli usemwe!
Siyo kweli. Ukisoma literature kuhusu 'the work of the future' kuna msisitizo kwamba besides technical skills (na siyo without technical skills - ambazo mtu hupata wakati wa kusomea taaluma fulani) mfanyakazi anatakiwa awe na soft skills (employability, 21st century, transferable skills). Yaani waajiri wanataka mtu mwenye both types of skills kuliko mwenye aina moja tu.
 
Mimi siamini kama civil engineer atakosa cha kufanya, siamini kabisa.
Our Engineers are mostly administrators...sasa projects zinahitaji administrators wangapi...only a few ndiyo maana wapo na wanakosa ajira.

Fundi mwashi wa VETA au fundi mchundo mwenye FTC can easily get a job kuliko engineer.

Kosa lilifanyika kuua mfumo wa elimu wa tabaka la kati la watendaji: Diploma na FTC holders ambao ndiyo wanashinda na kulala sites...tumezalisha administrators wengi(degree holders) na sasa hatuna pa kuwapeleka.

Na hakuna miujiza wala maombi...we just need to go back, restructure and ensure we do the basics right!
 
Hongera mkuu,

Na ukweli ni kuwa skills hazihitaji GPA ndio maana nikawashauri watumie hiyo gap maana kampuni ikihitaji videographer, photographer au graphic designer, hawaangalii cheti bali portfolio ya kazi mtu alizowahi kuzifanya..na kama ni extremely corporate,wanaweza omba kujua kiingereza kama qualification

Ila pia kama mtu anaona course yake haimpi maslahi, hakuna gap lililo wazi kama sales kwenye makampuni makubwa

Uzuri hiyo ni game of numbers, anaeweza kuleta mapato mengi zaidi ndio anapata opportunities zaidi kwenye hizo kampuni.. Sema wengi huwa tunazidharau kwa sababu lazma uvuje jasho na damu hadi uwe good salesman unless iwe ni inborn character yako kuweza kushawishi watu kununua bidhaa na ile aggressiveness bhasi

Na hivyo ndivyo wakenya wametuzidi "wapo aggressive".

Hongera mkuu
Well said and ahsante sana mkuu jitihada,bidii,displine na kutokata tamaa hulipa daima
 
Back
Top Bottom