Kwa sasa huenda 90% ya Degree hazina tena maana, hazikupi ajira wala maarifa ya kupata kipato

Kwa sasa huenda 90% ya Degree hazina tena maana, hazikupi ajira wala maarifa ya kupata kipato

Naona ile dhana ya division na gpa inajifia yenyewe itabaki kusoma na kupata ujuzi tu hata usipopata ufaulu huo inatosha kwenda kujiajiri kwenye mambo yako. Hayo ma divisheni na gpa tuwaachie serikali wachague wafanyakazi wao sie wengine tunajijua wenyewe akili zetu namna ya kutengeneza uchumi.
 
Unachosema nikweli, ajira zimekua ngumu Sana kupatikana, nataman kama nchi ingejikita zaidi kwenye elimu ya vitendo Kwa zaidi ya 70%.
Hakuna cha elimu ya vitendo wala nini ,suala ni kwamba ajira hamna na mitaji na mazingira ni mabovu kitaani kwa hao wahitimu kujiajiri kupitia fani zao .
Mbona kuna lundo la watu wana certificates na diploma zao za technical courses na bado hawana ajira na hawajaweza kujiajiri ?
Hili suala watu wasioelewa uhalisia ndio wataishia kuponda tu ukosefu wa ajira kwa hao wa degree ,
Hao wa diploma na certificates nao mbona wako wanaranda randa kitaa kama machokoraa ?
Uchumi duni wa nchi na fursa kuwa duni ,result ndio hicho mnachokiona
Na hali itaendelea kuwa mbaya tu
 
Wanamaliza wahitimu zaidi elfu 20 wa Accounting kwa level ya degree hapa Tanzania kila mwaka, lakini ajira rasmi za kudumu za kuwaajiri (tena za mchongo balaa) hazifiki hata 300 kwa mwaka, hao wengine wanakwenda wapi?

Serikali haajiri wengi na wala haajiri kila mwaka, na taasisi binafsi zenye kuajiri ni chache, kwa uchache sana huajiri, tena huajiri wenye uzoefu mkubwa na mzuri. Sasa mhitimu mpya anavukaje hapo?

Big four Auditing firms zenyewe siku hizi zinakwepa kuajiri graduates wenye degree za accounts.

Zinaajiri graduates wenye degree za engineering ama acturial science. Kisha kazini wanaenda msomesha ACCA na CPA.

Wanadai watu wanaojua hesabu ngumu ( advance mathematics) ndio wana attention to small details kwenye kazi zao za audit.

kuajiri wenye degree za accounts ni ujinga huku engineers wanaweza kufanya kazi za accounts kwa ubora zaidi wakielekezwa siku chache tu
 
Ungekuwa mhitimu wa fani yoyote ya uhandisi ungeamini vizuri mbona ?
Ungekula msoto na kupata first hand experience soon baada ya kugraduate
Hali ni mbaya kwa fani zote ,ni kama soko la ajira lipo kwenye" standstill "mode
Mimi ni mhandisi wa fani moja wapo ya uhandisi ,ila ninafanya issue tofauti kabisa na fani yangu
 
Maarifa yasiyo na mtaji ni sawa na kazi bure.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Kumbe basi tusilaumu mfumo wa elimu yetu. Kuna tatizo zaidi ya mfumo wa elimu.

Binafsi nadhani ni siasa mbovu na uongozi wa hovyo ndivyo vinavyopelekea ajira kukosekana katika taifa letu lenye baraka tele.

Hakuna sera na mipango inayotabirika na kufanya taasisi za fedha, wawekezaji na vyuo kushindwa kuandaa programu na mipango ya kifedha kulingana na mwelekeo wa kisera na mipango ya serikali.

Kila awamu inakuja na mipango yake"kilimo kwanza, Tanzania ya viwanda, Royal tour",
 
Mimi mwenyewe ni mhanga wa kozi mojawapo hapo, sema nilisoma zamani nikapata ajira ambayo haiendani na nilichosomea ndo inaniweka mjini.

Wenye ahueni ni wale waliosomea Bachelor of Science in/with education hao kwa masomo hayo ya PCM wana ajira, ila wale waliosoma Bachelor of science in Maths, phys au chem pamoja na hao wa engr wengi hakuna rangi wanaacha kuiona mtaani.
Kumbe hadi mainjinia wanakosa kazi?
 
Hamna haja ya kulalamika wakati mnafurahia kufaulisha 100%. Mitihani inatakiwa iwe migumu ili tupate wahitimu wachache wanaohitajika.

Dunia haihitaji watu wengi wenye degree.. inahitaji watendaji, mafundi wengi ambao ni certificate.. na wasimamizi wachache wa kati ambao ni diploma.. degree holders wanaandaliwa kuwa wasimamizi wakuu.. ambao ni wachache zaidi


Tuamshe veta, tuzisurport na kuzichangamkia tutaongea lugha nyingine kabisa
Kama huna industrial base / sekta ya viwanda na technology iliyokomaa ,hicho unachoandika na kudhani ndio solution ni kazi bure .
Supply and demand ,hii mizania ndio wengi mmeshindwa kuelewa , hamna sekta wala uchumi komavu na demand ya kubeba hao mafundi na technicians nchi hii ,hata leo hii vyuo vyote vya degree vifutwe na hao wanafunzi wapelekwe veta na technical colleges ni kazi bure .
Supply should be in line with the demand
 
Mkuu hakuna degree nzuri au mbaya. Hata medicine wapo kitaa wanaendesha bodaboda.

Tatizo kubwa in lipo kwenye mtazamo (mindset) wa wasomi. Wengi mmejengwa na kuandaliwa kupewa ajira. Hapa ndipo penye kosa kubwa.

Lengo la degree siyo kuajiriwa kwenye fani uliyosomea kama mleta mada unavyotaka kutuaminisha. Lengo la degree ni kupanua mawanda ya kufikiri ili msomi aweze kuyakabili mazingira yake kwa namna toauti na asiyesoma.

Kwahiyo ktk nchi kama Tanzania iliyobarikiwa ardhi kubwa yenye rutuba na imezungukwa na mito, maziwa na bahati ni aibu kwa wasomi kuleta mada za kulalamikikia kukosa kuajiriwa. Mlienda chuo kudanga, kubet na kuvuta shisha badala ya kujielimisha. Shubamiti, ndengeleki ninyi!
Alaf unakakuta haka kajamaa kanasubiri mshahara laki 6 mwisho wa mwezi.
 
20. Mineral processing engr
21. Bachelor of art with education
22. Fine art and design
23. Statistics
24.Mathematics
25.Physics
26. Civil engr
27. Chemistry
28. Agroeconomy
29. Biochemistry
30. French
31. Arabic
32.
33.
34.

Hapo kwenye civil eng nakataa. Niko kwenye hiyo game for long time bado zinauhitaj but lazima ujue sector ipi inauhitaj currently

Ila hizo zingine Mungu saidia aisee ni vilio
 
Ukweli usemwe na usemwe wazi ili kila mtu aujue. Wigo wa watanzania kusoma mpaka chuo kikuu ili kupata degree umekuwa mkubwa lakini huo mfumo umekuwa ni hasara na upotevu wa rasimali (muda, pesa na nguvu) kwa 90%.

Ajira mtaani kwa 90% hakuna kwa fani nyingi, ni sawa na kucheza kamili, na elimu ya vyeti vya chuo kikuu haina mchango wowote wa mhitimu wa level ya degree kuweza kujiajiri moja kwa moja. Hapa chini ni baadhi ya fani zinazoangukia kwenye kundi hilo.

1. Public administration
2. Political science
3. Business administration
4. Procurement and supply
5. Human resource
6. Sociology
7. Environment
8. Language
9. Mass communication
10. Tourism
11. Banking
12. Accounting
13. Economy
14. Finance
15. History
16. Insurance
17. Tax
18. Cooperative
19. Marketing
20.

Kama wewe ni mhitimu wa hizo fani kwa miaka ya karibuni utaelewa hicho nilichokiandika, na kama wewe ni mwanafunzi wa hizo fani anza kujiandaa kisaikolojia, hali ni mbaya mtaani. Wahitimu ni wengi na hawana ajira yoyote, wamechoka vibaya, wameshazunguka na mabahasha mpaka soli za viatu kuchakaa, wamejitolea mpaka basi, wameshikiza mpaka wamedondoka na wengi wamekata tamaa kabisa, vyeti vyao wamesahau hata vipo wapi, havina msaada. Bado wanakula, kulala na kutunzwa na wazazi wao, mashemeji au wajomba. Wengine wameamua kujiajiri katika fani zingine ambazo hazina uhusiano wowote wa fani walizosomea na zenye kuhitaji elimu ya darasa la nne tu.
Wajanja wengine wameamua kurudi chuo, hususani kwa ngazi ya Diploma kusoma fani za ualimu au afya ili kuingia kwenye mkondo wa kuja kupata ajira hapo baadaye.

Jamani hali ni mbaya na tete.
Ukweli usemwe!
Sasa braza au sisita,kumbuka nyingine za mchongo.
-enzi hizo wazazi wa leo walikuwa wakisoma kweli kweli. Humu tu kwenyewe ukiangalia waliokula matunda kimasihala,ni wanachuo, na walikuwa wanakula wenzao humo humo. Eti baada ya hapo,ikawa ndo kila nikitaka najilia vyangu. Na mwenzie ndo hivo hivo akitakwa analiwa. Hao wanachuo au wanandoa? Wanawaza tu kugegedana,masomo saa ngapi?

-Elimu na maadili vinaenda sambamba. Wakati mwingine unakuta muajiri na yeye anaangalia na chuo chenyewe. Mkisema Mabibo Hostel wanaliwa kwa buku 2, mwajiri unategemea atachukuliaje hicho chuo?

-Unaenda kutafuta kazi umevaa mlegezo, mwingine mikucha ya bandia unategemea nini? Unaanza kuomba kazi, Boss mtarajiwa anaanza kutongoza. Ulivyoingia, ndo hivo hivo utakavyopokelewa.

-Mwenzenu katokea Kigoma huko Kasuru,tena siyo Kigoma mjini,akimaliza anarudi kwao. Kwenye ajira ni miji mikubwa. Haijui huenda na nauli hupata kwa shida.
Wakienda Dar kwa ndugu zao, ndo hao mnawavizia stendi na kuwagegeda,wanaondoka na mimba. Wanaofanya hivyo,utasikia toka siku hio hata namba hatukupeana. Huyu akishakuwa na msongo wa mawazo au kurudishwa alikotoka,ile degree haina msaada tena.

Kwenye maarifa ya kipato,na kwenyewe changamoto.
Hakuna kazi isiyolipa. Lakini,unawaza,mi na elimu yangu nikawe konda kwenye basi la mikoani? Je,nikikutana na Asha nilokuwa namuaminisha kwamba mi nikimaliza kazi ipo ni uhakika?
Vitu kama hivyo. Au mbona kazi hii haina hadhi ya elimu yangu? Changamoto zinakua nyingi. Sema tu labda yangeongezwa masomo practical,na wahitimu wakaweza kupata hata mikopo kuendesha biashara zao kwa watakaokosa ajira,lakini wakawa na uhakika wa soko.
Hayo ni badhi,ila mambo ni mengi. Af cha ajabu,unakuta kuna watu wengine wapo hata nje,wanazijua fursa lakini hawastui wenzao. Wengine hawajui wawapate wapi.
 
Wanamaliza wahitimu zaidi elfu 20 wa Accounting kwa level ya degree hapa Tanzania kila mwaka, lakini ajira rasmi za kudumu za kuwaajiri (tena za mchongo balaa) hazifiki hata 300 kwa mwaka, hao wengine wanakwenda wapi?

Serikali haajiri wengi na wala haajiri kila mwaka, na taasisi binafsi zenye kuajiri ni chache, kwa uchache sana huajiri, tena huajiri wenye uzoefu mkubwa na mzuri. Sasa mhitimu mpya anavukaje hapo?
Taasisi haziajiri wenye uzoefu bali wenye connection.
 
Ajira zipo kwa fani zote, na hazipo kwa fani zote kutegemeana na mhusika anayeitafuta, una connection?

Kama connection unayo hata kama una ufaulu mbaya ajira utapata, lakini kama una pass mark nzuri connection hauna umeumia.

So hizo kozi ulizoweka hapo zina ajira na hazina ajira pia kutegemeana na situation ya mhitimu na wazazi wake, au kama akiwa mtoto wa kike akakutana na boss anamemuelewa ajira ataipata, bahati mbaya ukiwa wa kiume....

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Yale yale mkuu. Boss akishakuchungulia, ujue umeisha. Usipokubali,kazi huna. Ukikubali, hukai mda mrefu. Ukishaliwa tu,utajiona unawazidi wenzako. Akimtaka mwenzio,anakula, kuepuka lawama,unapumzishwa
 
Back
Top Bottom