Kwa sasa, kuokota simu si bahati tena bali ni balaa

Kwa sasa, kuokota simu si bahati tena bali ni balaa

sanalii

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2018
Posts
1,639
Reaction score
5,767
Kuna tukio limetokea Kibaha, Kwa Mfipa, familia imevamiwa, wameibiwa vitu ndani ikiwemo na gari, wamechukua na simu za uwakala wamelazimisha wapewe na PIN, wamepewa.

Kama haitoshi wamewafunga kamba mke na mume, wakawaweka kwenye mashimo ya choo tofauti, mtoto wa miezi saba hajulikani yuko wapi. Labda wameondoka nae, au nae wamemuweka shimo tofauti haieleweki. Mungu amuweke salama huko aliko, pole kwa familia.

Sasa najiuliza kama wakiamua kutupa hizo simu kisha mtu akajichanganya kuokota, atakumbana na kesho mbaya sana.

Kwasasa ukiokota simu ni bora uipeleke kituo cha polisi, matukio yamekuwa mengi na simu ya mhusika ni moja ya trace. Unaweza kudhani umepata kumbe ndio mlango wa gereza unaufungua.

Ni hatari sana.
 
Kuna tukio limetokea Kibaha, Kwa Mfipa, familia imevamiwa, wameibiwa vitu ndani ikiwemo na gari, wamechukua na simu za uwakala wamelazimisha wapewe na PIN, wamepewa.

Kama haitoshi wamewafunga kama mke na mume, wakawaweka kwenye mashimo ya choo tofauti, mtoto wa miezi saba hajulikani yuko wapi. Labda wameondoka nae, au nae wamemuweka shimo tofauti haieleweki. Mungu amuweke salama huko aliko, pole kwa familia.

Sasa najiuliza kama wakiamua kutuma hizo simu kisha mtu akajichanganya kuokota, atakumbana na kesho mbaya sana.
Kwasasa ukiokota simu ni bora uipeleke kituo cha polisi, matukio yamekua mengi na simu ya mhusika ni moja ya trace. Unaweza kudhan umepata kumbe ndio mlango wa gereza unaufungua. Ni hatari sana.
Kwasasa ukiokota simu ni bora uipeleke kituo cha polisi, matukio yamekua mengi na simu ya mhusika ni moja ya trace. Unaweza kudhan umepata kumbe ndio mlango wa gereza unaufungua. Ni hatari sana....

Never ever usije ukajaribu hilo kosa..unaweza kuangushiwa jumba bovu
 
Kuna tukio limetokea Kibaha, Kwa Mfipa, familia imevamiwa, wameibiwa vitu ndani ikiwemo na gari, wamechukua na simu za uwakala wamelazimisha wapewe na PIN, wamepewa.

Kama haitoshi wamewafunga kama mke na mume, wakawaweka kwenye mashimo ya choo tofauti, mtoto wa miezi saba hajulikani yuko wapi. Labda wameondoka nae, au nae wamemuweka shimo tofauti haieleweki. Mungu amuweke salama huko aliko, pole kwa familia.

Sasa najiuliza kama wakiamua kutuma hizo simu kisha mtu akajichanganya kuokota, atakumbana na kesho mbaya sana.
Kwasasa ukiokota simu ni bora uipeleke kituo cha polisi, matukio yamekua mengi na simu ya mhusika ni moja ya trace. Unaweza kudhan umepata kumbe ndio mlango wa gereza unaufungua. Ni hatari sana.
Kuliko upeleke polisi si bora uiache tu, mana polisi wenyewe hawachelewi kukung'ang'ania mwishowe kwa wema ukajikuta umekula mvua ya miaka 20 kimasihara
 
Kwasasa ukiokota simu ni bora uipeleke kituo cha polisi, matukio yamekua mengi na simu ya mhusika ni moja ya trace. Unaweza kudhan umepata kumbe ndio mlango wa gereza unaufungua. Ni hatari sana....

Never ever usije ukajaribu hilo kosa..unaweza kuangushiwa jumba bovu
Ni bora kuiacha tu kuliko kuipeleka polisi hawachelewi kukuonganisha na tukio lolote wale sio Salam kabisa bora usiokote uiache tu
 
Upo sahihi mkuu, kuna jamaa huko migombani alijiokotea simu smartphone akajua amepata kumbe kapatikana. Ile simu kuna tukio la wizi lilitokea na mwenye simu alijeruhiwa vibaya hali iliyopelekea kupoteza maisha siku chache baadae.

Ile simu ikafuatiliwa baada ya miezi 6 ya tukio kutokea wakamkuta nayo alieiokota, kufupisha kwa sasa yupo jela.
 
Kuliko upeleke polisi si bora uiache tu, mana polisi wenyewe hawachelewi kukung'ang'ania mwishowe kwa wema ukajikuta umekula mvua ya miaka 20 kimasihara
Huwa hawajishughulishi kutafuta ukweli kwa kutumia akili nyingi na utaalamu kutatua kesi.Wao hutafuta njia nyepesi kama ;-
-kutaka rushwa wamalize mambo
-kubambikiza kesi kwa yeyote atakayetokeza mbele yao.
-kuomba wapewe taarifa za uhalifu kutoka kwa watu wasio na ujuzi wowote wa kung'amua uhalifu.
-kutumia nguvu,vitisho,vipigo na mateso makali kulazimisha watakalo..
TAHADHARI;Usijipeleke kizembe polisi kwa nia ya kupeleka ushahidi au kitu ulichookota.Fikiri kabla.
 
Kuna tukio limetokea Kibaha, Kwa Mfipa, familia imevamiwa, wameibiwa vitu ndani ikiwemo na gari, wamechukua na simu za uwakala wamelazimisha wapewe na PIN, wamepewa.

Kama haitoshi wamewafunga kamba mke na mume, wakawaweka kwenye mashimo ya choo tofauti, mtoto wa miezi saba hajulikani yuko wapi. Labda wameondoka nae, au nae wamemuweka shimo tofauti haieleweki. Mungu amuweke salama huko aliko, pole kwa familia.

Sasa najiuliza kama wakiamua kutupa hizo simu kisha mtu akajichanganya kuokota, atakumbana na kesho mbaya sana.
Kwasasa ukiokota simu ni bora uipeleke kituo cha polisi, matukio yamekua mengi na simu ya mhusika ni moja ya trace. Unaweza kudhan umepata kumbe ndio mlango wa gereza unaufungua. Ni hatari sana.

Ukipata kitu ambacho si chako peleka mahali husika; kwa kifupi Kama huna tamaa wala hutaki vitu vya watu then Maisha sio magumu!
 
Kwasasa ukiokota simu ni bora uipeleke kituo cha polisi, matukio yamekua mengi na simu ya mhusika ni moja ya trace. Unaweza kudhan umepata kumbe ndio mlango wa gereza unaufungua. Ni hatari sana....

Never ever usije ukajaribu hilo kosa..unaweza kuangushiwa jumba bovu
Hata ukiipeleka polisi, bado wataanza na wewe..!! Yaani "UTAISAIDIA" polisi. Na polisi wetu, kwenye kuisadia polisi, wewe ndo unakuwa "MTUHUMIWA" wa kwanza. Ndiyo maana siku hizi mtu hata akiiona maiti, anakula kona. Polisi si rafiki tena kwenye mambo haya
 
Back
Top Bottom